ETI ALLAH AMEKUBALI KUTOA USHAIDI KWA VIUMBE VYAKE?

0
5KB

Je, nani atakuwa Hakimu wakati Allah anatoa Ushaidi?

NDUGU WASOMAJI, Hivi Allah anaweza kuwa shaidi wakati yeye ndie anadai kuwa alitoa Utume kwa Muhammad? Hivi Mungu anaweza kwenda kutoa Ushaidi kwa viumbe vyake? Nani atakuwa Hakimu wa hiyo Kesi?

Katika hii aya hapa chini, mhukumiwa ni Allah aliyedai katoa Utume kwa Muhammad, kivipi na tokea lini Mhukumiwa akawa shaidi katika Kesi yake ya jinai?

Quran 4:72 Surat Annisa inasema "wema uliokufikia unatoka kwa Mwenyenzi Mungu na baya lililokufikia linatoka nafsini mwako nasi tumekupeleka kwa watu kuwa Mtume na Mwenyenzi Mungu ni shahid wa kutosha wala hapaitajiwa shaid mwingine ila yeye"

Allah anadai kuwa yeye ndie aliye mpa Utume Muhammad na hapo hapo ALLAH anajihami kuwa mkibisha na au kuwa na shaka na utume wa Muhammad basi yeye ni Shaidi yake. Hivi, MFANO: Rais akimpa Mtu uwaziri, umesha wai sikia Rais anajihami kwa kusema kama wakikukataa mimi nitakuwa Shaidi yako? Kwani Allah ana mshindani mpaka atoe maneno ya kujihami? Je, Allah ni Mungu? Mbona anakubali kuchukia nafasi ya chini ya kuwa Shaidi kwa viumbe vyake? Au kuna Mungu mwingine ambaye ni zaidi ya Allah ndio maana Allah anajihami kwa kusema yeye atakuwa shaidi wa Muhammad?

Ndugu zanguni, tukisoma Biblia, hakuna hata sehemue moja na au aya yeyote ile inayo sema kuwa Yehovah alijihami kwa Mitume wake kuwa, kama wakikataliwa basi Yehovah atakuwa shaidi yao. Allah anadai kuwa yeye ni shaidi lakini ameshindwa kutuambia wapi hiyo kesi itakuwa na nani ni Hakimu!

Binadamu/Sisi labda ndio tunaweza kuwa Mashaidi wa Neno la Mungu lakini si Mungu mwenye Mamlaka yote awe shaid katika viumbe vyake na neno lake. Mungu huwa halizimishi mambo kama Allah wa Uislam. Yesu anasema kuwa yeye Ndie Mwanzo na Mwisho, Alfa na Omega. Hakuna zaidi yake, lakini Allah amekiri kuwa yeye anaweza kuwa shaidi pale mambo yanapokuwa magumu. Hakika Allah hana Mamlaka yeyote yake, ndio maana yeye ni shaidi na sio Mungu mwenye Mamlaka. Sijui nani atakuwa Hakimu wakati Allah amesimama kutoa Ushaidi?

Suche
Kategorien
Mehr lesen
Injili Ya Yesu Kristo
BORA KUTESEKA MIKONONI MWA MUNGU,KULIKO KUPATA RAHA MIKONONI MWA SHETANI.
Bwana Yesu asifiwe … Kwa ufupi. Kuwa mikononi mwa Mungu haina maana hakuna mateso. Mateso...
Von GOSPEL PREACHER 2022-03-30 05:02:30 0 6KB
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-04-02 01:23:16 0 5KB
OTHERS
KORAN INAKIRI KUWA UISLAMU NI DINI YA WAARABU PEKEE
Katika hii mada ninawaletea ushaidi kuwa Uislam ni dini ya Waarabu peke yao. Waislamu bila...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:44:35 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
KAZI ZA IMANI KWA MUAMINI KATIKA KRISTO
KAZI KUU 5 ZA IMANI KATIKA MAOMBIA YA MUAMINI
Von Martin Laizer 2023-09-28 07:48:51 0 11KB
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 15
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 34 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-03-20 04:59:24 0 5KB