ATHARI ZA MAHUSIANO YA UCHUMBA YA MUDA MREFU KUPITA KIASI (Miaka 2 au zaidi)

0
6KB

1. Huweza Kufungua Milango ya uasherati kwa Wachumba
Inaweza kupelekea kwenye maisha ya uasherati kati yenu kwasababu mtakuwa mmetumia muda mwingi kuwa pamoja na kujihalalishia uhalali wa kushiriki tendo la ndoa na kujiona tayari mmeshazoenana na kujihisi ni kama mke na mume tayari.

2. Inaweza kupunguza kasi na kiwango chenu katika mambo ya Mungu.
Kukaa sana katika uchumba kupita kiasi kutaweza kushushaa kiwango chenu cha mambo ya kimungu kwasababu mtapeleka nguvu kubwa ya vipaumbele vyenu na muda wenu kwenye mambo ya mahusiano kuliko kupeleka kwa Mungu.

3. Inanyonya kwa kiwango kikubwa sana nguvu za kihisia kati yenu. (It is emotionally demanding).

  • Muda mwingi unakuwa unamuwaza mchumba wako.
  • Huna uhakika huko aliko kama yupo salama?
  • Hakuna wengine walio msogelea na kutaka kukupindua.
  • Kutaka kujua yupo wapi sasa, anafanya nini, nk.
  • Inachukua mawazo yako kwa sehemu kubwa sana na wakati mwingine hata kazi zako hauzifanyi vuzuri.
  • Sasa inapokuwa ni kwa muda mrefu inaweza kukunyonya sana kiwango cha hisia zako.


4. Inaweza kupelekea mawazo yasiyofaa na ya upinzani kutoka kwa ndugu zenu, jamaa na marafiki.

  • Uchumba unapokaa kwa muda mrefu sana kupita kiasi unawafanya wanandugu kuanzisha maneno maneno ambayo yanaweza kuharibu na kila kitu katika mahusiano hayo.
  • Kuna msemo wa kiswahili unasema kuwa "bata ukimchunguza sana huwezi kumla" kama mmekaa katika uchumba kwa muda mrefu sana, inaweza kuwafanya wanandugu kumfuatilia mchumba wako kwa ukaribu kwa muda mrefu na kuanza kugundua vikasoro vidogo vidogo ambavyo hata kama vilikuwa vinaweza kurekebishika wao wanavishikia bando na kusema huwezi kuoana na yule kwasababu ya hivyo vikasoro kasoro,


5. Inaweza kusababisha uchumba kuvunjika kabla ya kuoana.

  • Kukaa katika mahusiano ya uchumba kwa muda mrefu kunaweza kupelekea hata uchumba wenyewe kuvynjika.
  • Kukaa katika uchumba muda mrefu kunaweza kuwafanya hata ile shauku mliyokuwa nayo ya kuoana iweze kwisha kabisa na kuwafanya mjikute mkivunja na uchumba wenyewe.


6. Italeta majeraha makubwa sana baina yenu hasa baada ya uchumba kuvunjika kutakuwa na majuto na maumivu sana kwasababu Zifuatazo:

  • Kupotezeana muda miongoni mwenu.
  • Kupoteza pesa na vitu mbalimabli mlivyopeana wakati wa uchumba (loss of resources).
  • Maumivu ya kumwaga siri zako hata zile za ndani kabisa ambazo usingependa mtu mwingine azijue, sasa unakuwa huna uhakika kama hatamweleza mtu mwingine huko nje.
  • Aibu kwa ndugu, jamaa na marafiki na jamii kwa ujumla na kujiona kuwa wameshindwa (failure to the public image).
  • Hupelekea historia mbaya (bad records) kwa wachumba watakao fuata na hasa kama uchumba ujao hautafanikiwa pia.


7. Kuendesha Uchumba Wa Muda Mrefu Ni Gharama Kubwa.

  • Safari za mara kwa mara kwaajili ya kuonana na mchumba wako.
  • Mitoko "outing" za mara kwa mara pamoja na mchumba wako.
  • Mawasiliano ya kila dakika na mchumba wako.
  • Kutumiana zawadi za mara kwa mara na mchumba wako.
Suche
Kategorien
Mehr lesen
Networking
How to build trust in your marketplace
One of the biggest problems marketplace businesses need to tackle is fear. Whenever customers...
Von Business Academy 2022-09-17 03:58:52 0 11KB
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 26
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-26 04:24:39 0 6KB
OTHERS
Islam offers HELL and that is all
Allah Promised hell for his followers:  Sura 3:185, "Every soul shall have a taste of...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:08:53 0 5KB
DANIEL
DANIELI 1
Jina la Bwana wetu YESU KRISTO na MKUU wa Dunia yote libarikiwe, Karibu katika kujifunza...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-05 23:20:59 0 7KB
OTHERS
THERE IS A GOD How the World’s Most Notorious Atheist Changed His Mind
In the parable of the lost sheep, in the Gospel of Luke, Jesus says there shall be more joy in...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:00:09 0 6KB