ATHARI ZA MAHUSIANO YA UCHUMBA YA MUDA MREFU KUPITA KIASI (Miaka 2 au zaidi)

0
6K

1. Huweza Kufungua Milango ya uasherati kwa Wachumba
Inaweza kupelekea kwenye maisha ya uasherati kati yenu kwasababu mtakuwa mmetumia muda mwingi kuwa pamoja na kujihalalishia uhalali wa kushiriki tendo la ndoa na kujiona tayari mmeshazoenana na kujihisi ni kama mke na mume tayari.

2. Inaweza kupunguza kasi na kiwango chenu katika mambo ya Mungu.
Kukaa sana katika uchumba kupita kiasi kutaweza kushushaa kiwango chenu cha mambo ya kimungu kwasababu mtapeleka nguvu kubwa ya vipaumbele vyenu na muda wenu kwenye mambo ya mahusiano kuliko kupeleka kwa Mungu.

3. Inanyonya kwa kiwango kikubwa sana nguvu za kihisia kati yenu. (It is emotionally demanding).

  • Muda mwingi unakuwa unamuwaza mchumba wako.
  • Huna uhakika huko aliko kama yupo salama?
  • Hakuna wengine walio msogelea na kutaka kukupindua.
  • Kutaka kujua yupo wapi sasa, anafanya nini, nk.
  • Inachukua mawazo yako kwa sehemu kubwa sana na wakati mwingine hata kazi zako hauzifanyi vuzuri.
  • Sasa inapokuwa ni kwa muda mrefu inaweza kukunyonya sana kiwango cha hisia zako.


4. Inaweza kupelekea mawazo yasiyofaa na ya upinzani kutoka kwa ndugu zenu, jamaa na marafiki.

  • Uchumba unapokaa kwa muda mrefu sana kupita kiasi unawafanya wanandugu kuanzisha maneno maneno ambayo yanaweza kuharibu na kila kitu katika mahusiano hayo.
  • Kuna msemo wa kiswahili unasema kuwa "bata ukimchunguza sana huwezi kumla" kama mmekaa katika uchumba kwa muda mrefu sana, inaweza kuwafanya wanandugu kumfuatilia mchumba wako kwa ukaribu kwa muda mrefu na kuanza kugundua vikasoro vidogo vidogo ambavyo hata kama vilikuwa vinaweza kurekebishika wao wanavishikia bando na kusema huwezi kuoana na yule kwasababu ya hivyo vikasoro kasoro,


5. Inaweza kusababisha uchumba kuvunjika kabla ya kuoana.

  • Kukaa katika mahusiano ya uchumba kwa muda mrefu kunaweza kupelekea hata uchumba wenyewe kuvynjika.
  • Kukaa katika uchumba muda mrefu kunaweza kuwafanya hata ile shauku mliyokuwa nayo ya kuoana iweze kwisha kabisa na kuwafanya mjikute mkivunja na uchumba wenyewe.


6. Italeta majeraha makubwa sana baina yenu hasa baada ya uchumba kuvunjika kutakuwa na majuto na maumivu sana kwasababu Zifuatazo:

  • Kupotezeana muda miongoni mwenu.
  • Kupoteza pesa na vitu mbalimabli mlivyopeana wakati wa uchumba (loss of resources).
  • Maumivu ya kumwaga siri zako hata zile za ndani kabisa ambazo usingependa mtu mwingine azijue, sasa unakuwa huna uhakika kama hatamweleza mtu mwingine huko nje.
  • Aibu kwa ndugu, jamaa na marafiki na jamii kwa ujumla na kujiona kuwa wameshindwa (failure to the public image).
  • Hupelekea historia mbaya (bad records) kwa wachumba watakao fuata na hasa kama uchumba ujao hautafanikiwa pia.


7. Kuendesha Uchumba Wa Muda Mrefu Ni Gharama Kubwa.

  • Safari za mara kwa mara kwaajili ya kuonana na mchumba wako.
  • Mitoko "outing" za mara kwa mara pamoja na mchumba wako.
  • Mawasiliano ya kila dakika na mchumba wako.
  • Kutumiana zawadi za mara kwa mara na mchumba wako.
Căutare
Categorii
Citeste mai mult
OTHERS
UTATA MKUMBWA NDANI YA KORAN: Nini kitaingia PEPONI: Roho/Nafsi au Mwili au zote mbili?
Somo letu la leo ni la swali kwa Allah ambaye ameshindwa kujieleza, kuwa ni kipi kinaingia Peponi...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:30:26 0 5K
OTHERS
ATHARI YA MKRISTO KUOANA NA MUISLAMU
Imeletwa kwenu na Abel Suleim Shiriwa Imekuwa ni jambo la kawaida kushuhudia Wakristo na...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 06:04:02 0 9K
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
By THE HOLY BIBLE 2022-04-01 21:57:06 0 5K
OTHERS
Bible Verses about Honoring Parents
The New Testament binds a great responsibility on children when it says in Ephesians 6, verses...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 10:58:36 0 7K
OTHERS
Kwanini Mkristo anauhakika wa kwenda Paradiso zaidi ya Muislamu?
1. Je, Kurani inatoa uhakika kwa Waislamu? Kurani inatengeneza tu mazingira ya mashaka kuhusiana...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 06:26:41 0 5K