JINSI YA KUMJUA MWENZI WAKO ALIYEKUSUDIWA NA MUNGU

0
6KB

Leo napenda tuangalie mambo yatakayokufanya umjue mwenzi wako wa ndoa uliyekusudiwa na Mungu. Wanaume wapo wengi na si kila mwanaume anafaa kuwa mume wako. Wanawake wapo wengi lkn si kila mwanamke anafaa kuwa mke wako. Anayefaa kuwa mume wa mwingine hafai kuwa mume wako, anayefaa kuwa mke wa mwingine hafai kuwa mke wako. Kumbuka, wewe mwanamke hufanani na kila mwanaume, na wala wewe mwanamume hufanani na kila Mwanamke, Mungu anakupa wa kufanana na wewe, tofauti na hapo mwingine unayemtaka anatoka kwa wanadamu au shetani. Na huyo atakutesa kwa sababu hamfanani. Ndege warukao pamoja ni wale wanaofanana. Na kufanana huku ni kule kupatana ktk utu watu wa ndani, ni kufanana kunakupelekea kufaana. Kama hamfanani hamtapatana, na kama hampatani hamtafaana. Ukioa au kuolewa na usiyefanana naye umekwisha.

Sasa tuangalie namna gani unaweza mpata wa kufanana nawe, yaani aliyekusudiwa na Mungu:

1. Mtegemee na umtangulize Mungu kwa kila hatua ktk jambo hili.

Mungu hamtupi kamwe mtu anayemtegemea yeye. Kwa kuwa unamtegemea Mungu, basi, utaomba kwa ajili ya kutaka mwongozo wa Mungu ktk jambo hili. Mungu atakachofanya ni kuuelekeza moyo wako umuelekee mtu aliyekusudia awe mwenzi wako wa ndoa maisha yako yote. Mungu husema nasi kupitia mioyo yetu. Huweka nia na mawazo, au hali ya upendo mioyoni mwetu ktk yale makusudi yake tuliyomuomba. Kwa hiyo ukimtegenea ukamwomba atafanya hivyo.

2. Usiwe na haraka ya maisha {ya ndoa}, kuwa mtulivu na ukubali kusubiri.
Mtu mwenye haraka ya maisha hutapatapa kwa kutaka mafanikio ya haraka, hawezi kusubiri na kwa sababu hiyo ataangukia ktk mtego wa shetani. Maombi yatafanya kazi iwapo hutakuwa na haraka. Mara nyingi wa kwanza kukujibu maombi yako huwa ni shetani ili aharibu mpango na kusudi la Mungu ktk maisha yako. Kama utakuwa na haraka ya ndoa shetani atakupa mume au mke ili aharibu maisha yako. Kwa hiyo ni vyema kuwa muangalifu sana. Kubali kusubiri hata kama unaona umechelewa. Uhakika wa safari sio kuwahi kufika bali ni usalama wa safari. Haraka inaweza kusababisha ajali njiani hatimaye ukafa na usifike mwisho wa safari yako.

3. Tumia Akili yako Vizuri.
Mungu amekataza kuzitegemea akili zetu lkn ameamuru kuzitumia akili zetu kwa jinsi ipasavyo. Kwa hiyo tumia akili yako kufanya hukumu {judgement} ili kupambanua mwema na mbaya. Hata kama unaasilimia 100 kuwa huyo anayetaka au unayemtaka kuwa mwenzi wako anatoka kwa Mungu bado tumia akili yako kabla, wakati, na baada ya kufanya maamuzi.

Chunguza familia yao na ukoo anaotoka, hapa huitaji maombi, unahitaji akili. Chunguza tabia yake, tafuta kujua mahusiano yake na jamii inayomzunguka. Tabia ni muhimu kuliko vitu alivyonavyo, hautaishi naye kwa sababu ya mali, elimu au uzuri alionao, utaishi naye kwa sababu ya tabia njema aliyonayo. Usiwe mvivu wa kufikiri, usiwe mvivu wa kutumia akili yako kupambanua mambo.

4. Upendo wake kwako.

Si kila anayekuja kukuchumbia anakupenda, na wala si kila anayekukubali umuoe anakupenda. Kwa hiyo ni vyema kuhakikisha upendo wake kwake.

Upendo si vitu anavyokupa upendo ni namna yeye anavyojitoa kwako si kwa manufaa na faida yake, bali kwa faida yako. Upendo ni nia yake juu yako, haujajengwa ktk vitu au mali alizonazo mtu, umejengwa ktk utu wa mtu ktk hali yoyote. Muda tu ndio kipimo cha upendo. Pia anayetaka tendo la ndoa kabla ya ndoa hakupendi. Anayekupenda atakulinda.

5. Utayari wake kwako.

Ukiona mtu amekuchumbia halafu hayuko tayari kukuoa huyo si wako, anatafuta kukuharibia. Ukiona umemchumbia mtu halafu hayuko tayari kuolewa na wewe, hakupendi ila kuna kitu anatafuta. Lkn ukichumbiwa au kuchumbia mtu asiyekuwa tayari kuweka bayana mahusiano yenu kwa wazazi wa pande mbili au kwa viongozi wenu wa dini, au walezi wenu jua kabisa umeliwa. Haiwezekani muwe kwenye mahusiano miaka miwili, hata mmoja hakuna anayefahamu tena hata bila sababu za msingi. Ukiona unapozungumzia swala la ndoa na mwenzi wako hajali, anapotezea au kukasirika jua umeliwa.

Rechercher
Catégories
Lire la suite
SPIRITUAL EDUCATION
RECEIVE JESUS CHRIST AS YOUR LORD AND SAVIOUR
Romans 10:9-10.  “That if thou shalt confess with thy mouth the Lord Jesus, and shalt...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-19 07:45:34 0 5KB
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 62 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-01-01 10:29:14 0 5KB
JOB
Verse by verse explanation of Job 30
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-03 04:07:11 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
KWA NINI VIJANA WENGI HAWAJAKA KWENYE NAFASI ZAO KI-MUNGU?
1 Yohana 2:14  Kila kundi katika kanisa, jamii na hata nchi Mungu amelipa nafasi na wajibu...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:30:49 0 9KB
Networking
How to turn your marketplace into a community
As we have learned in the earlier chapters of the Practical guide for building a...
Par Business Academy 2022-09-17 03:49:25 0 9KB