JIFUNZE MAANA YA MAJINA YA MUNGU (YEHOVA)

0
6K

Mungu ni mmoja tu, lakini katika umoja wake amekuwa akijifunua katika majina mengi, kulingana na  uweza wake alionao, au majira Fulani yaliyopita, au matukio ya namna tofauti tofauti  yaliyotokea. Ni sawa, ni raisi Fulani aitwe JOHN, lakini huyo huyo anaweza akaitwa baba sehemu fulani, akaitwa mjomba sehemu nyingine, mhandisi kwa watu fulani, amiri jeshi mkuu eneo Fulani, babu sehemu nyingine n.k.

Unaona utaona vyeo vyote hivyo vimekuja aidha kulingana na wakati, au matukio, au nafasi aliyopo au ujuzi alionao n.k. Na vivyo hivyo Mungu wetu , alijifunua katika  majina mengi, ambayo leo hii tutayatazama kwa ufupi.

  1. ADONAI: Mungu Mwenye enzi yote, kimbilio imara Mwa 15:2‐8, Kut 6:2‐3
  2. ELOHIMU: Mungu mwenye uweza, muumbaji  wa milele, mwenye nguvu (Mwanzo 1: 1, 17:7, Yeremia 31:33)
  3. EL-ELOHE-ISREAL: Mungu wa Israel, Mwanzoh 33:20
  4. EL-OHEEKA: Bwana Mungu Wako Kut 20:2 , 5, 7
  5. EL-ELYONI:  Mungu Aliye juu zaidi ‐Mwa14:18, Dan 4:34
  6. YEHOVA  EL- GIBBOR: Mungu Mwenye Nguvu ( Isaya 9:6-9)
  7. YEHOVA EL-OHEENU: Bwana Mungu Wetu (Zaburi 99:5,8,9
  8. YEHOVA EL – SHADAI: Mungu Ututoshelezaye/ Mungu Mtoshelezi (Mwanzo 17:1) 
  9. YEHOVA HOSEENU: Bwana Aliyetuumba Zaburi 95:6
  10. YEHOVA-MEKADISHKEMU: Bwana atutakasaye (Kutoka 31:13)
  11. YEHOVA-NISI: Mungu ni Bendera yetu (Berani ya vita) (Kutoka 15:26).
  12. YEHOVA OLAMU: Mungu wa milele Zaburi 90:1-3
  13. YEHOVA-RAFA: Mungu-Atuponyaye. (Kutoka 15:26).
  14. YEHOVA-ROHI: Bwana ndiye mchungaji wangu (Zab 23)
  15. YEHOVAH SABAOTHI: Bwana wa Majeshi (1 Samweli 1:3)
  16. YEHOVA SHAMA: Bwana Yupo Hapa (Ezekiel 48:35).
  17. YEHOVA SHALOM: Bwana ni Amani Yangu (Waamuzi 6:24)
  18. YEHOVA TSIDKEMU: Bwana ni Haki Yetu (Yeremia 23:6)
  19. YEHOVA-YIRE: Mungu atupaye (Mwanzo 22:14)..
  20. YE-SHUA (YESU): Mungu utuokoaye.(Mathayo 1:21)

Jina Hili la YESU ndio jina tulilonalo mpaka sasa. Kwa kupitia hili ndio tunapata wokovu, kwa jina hili ndio tunamshinda adui, kwa jina hili ndilo tunapata Baraka, na kwa jina hili ndio tunaishi.

Lakini biblia inatuonyesha pia jina hili sio la kudumu, Upo wakati Kristo atakuja na jina jipya,(Ufunuo 19:12 ) jina hilo wakati huo litakuwa sio la Ukombozi tena, sio la kurehemu tena, bali litakuwa ni jina la kifalme. Na ndio maana wakati huu ambao angali bado neema ipo, usiruhusu, ikupite ikiwa wewe ni bado mwenye dhambi, Leo hii Kristo bado yupo kama kuhani mkuu akitupatanisha sisi na Mungu, ikiwa na maana kuwa mlango wa rehema bado upo wazi kwa kila mtu atakayetaka kuuingia, Lakini hautakuwa wazi sikuzote. Kwani dalili za kurudi kwa Yesu mara ya pili zimeshatimia zote, tunachongojea ni unyakuo tu.

Pesquisar
Categorias
Leia Mais
HOLY BIBLE
What are the keys of the kingdom?
The biblical passage that makes reference to the “keys of the kingdom” isMatthew...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:23:00 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
Kujengwa kwa Hekalu bila kelele!
1Wafalme 6:7. “Na nyumba ilipokuwa ikijengwa, ikajengwa kwa mawe yaliokwisha kuchongwa...
Por GOSPEL PREACHER 2022-04-01 08:26:15 0 6K
SPIRITUAL EDUCATION
SIRI YA MUNGU
Shalom Mwana wa Mungu, karibu tujifunze biblia, chakula cha uzima, kitupacho afya rohoni, leo...
Por GOSPEL PREACHER 2021-10-30 10:57:25 0 5K
OTHERS
YEHOVA KWA KIARABU NI YAHUH ( يهوه ) NA SIO ALLAH
Ndugu msomaji, Ninaendelea kuweka ukweli kuhusu Allah ambaye sio Yehova na wala hajawai sema yeye...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:09:27 0 6K
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-24 19:18:10 0 5K