Je! Bikira Maria Ni MALKIA WA MBINGUNI?

0
7كيلو بايت

JIBU: Neno Malkia wa mbinguni limeonekana mara mbili katika biblia

Sehemu ya kwanza ni katika Yeremia 7:18-20

18 Watoto huokota kuni, na baba zao huwasha moto, na wanawake hukanda unga, ili kumfanyizia mikate malkia wa mbinguni, na kuwamiminia miungu mingine sadaka za kinywaji, wapate kunikasirisha mimi. 19 Je! Watu hawa wanikasirisha mimi? Asema Bwana; hawajikasirishi nafsi zao, na kuzitia haya nyuso zao wenyewe? 20 Kwa hiyo, Bwana MUNGU asema hivi, Tazama, hasira yangu na ghadhabu yangu zitamwagwa juu ya mahali hapa, juu ya wanadamu, na juu ya wanyama, na juu ya miti ya mashamba, na juu ya mazao ya nchi; nayo itateketea, isizimike.

Na pia ukisoma sehemu nyingine katika kitabu cha Yeremia utamwona akitajwa tena..  

Yeremia 44:17-23 ” Lakini bila shaka tutalitimiza kila neno lililotoka katika vinywa vyetu, kumfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, kama tulivyotenda sisi, na baba zetu, na wafalme wetu, na wakuu wetu, katika miji ya Yuda, na katika njia kuu za Yerusalemu; maana wakati huo tulikuwa na chakula tele, na kufanikiwa, wala hatukuona mabaya. 18 Lakini tulipoacha kumfukizia uvumba MALKIA WA MBINGUNI, na kummiminia sadaka za kinywaji, tumepungukiwa na vitu vyote; na kuangamizwa kwa upanga, na kwa njaa. 19 Nasi tulipomfukizia uvumba malkia wa mbinguni, na kummiminia sadaka za kinywaji, je! Tulimfanyizia mikate, ili kumwabudu, na kummiminia mamiminiko, waume zetu wasipokuwapo? 20 Ndipo Yeremia akawaambia watu wote, wanaume na wanawake, yaani, watu wote waliompa jibu lile, akisema, 21 Uvumba mliofukiza katika miji ya Yuda, na katika njia kuu za Yerusalemu, ninyi, na baba zenu, wafalme wenu, na wakuu wenu, na watu wa nchi, je! Bwana hakuwakumbuka watu hao? Je! Jambo hili halikuingia moyoni mwake? 22 Hata Bwana asiweze kuvumilia tena, kwa sababu ya uovu wa matendo yenu, na kwa sababu ya machukizo mliyoyafanya; kwa sababu hiyo nchi yenu imekuwa ukiwa, na ajabu, na laana, isikaliwe na mtu kama ilivyo leo. 23 Kwa sababu mmefukiza uvumba, na kwa sababu mmetenda dhambi juu ya Bwana, wala hamkuitii sauti ya Bwana, wala hamkwenda katika torati yake, wala katika amri zake, wala katika shuhuda yake; ndiyo maana mabaya haya yamewapata kama ilivyo leo. ”

Tunaona habari hizo zote mbili zinaelezea juu ya miungu ya kipagani iliyowasababishia Israeli kuingia matatizoni kwa kwenda kuifukizia uvumba, na kumbuka haina uhusiano wowote na ukristo, kwahiyo mbinguni Mungu anapoishi hakuna malkia, biblia inamtaja MFALME TU!, Naye ni mmoja na si mwingine zaidi ya BWANA wetu YESU KRISTO, MFALME WA WAFALME NA BWANA WA MABWANA yeye peke yake.

Hivyo Mariamu sio malkia wa mbinguni, alikuwa ni mwanamke kama wanawake wengine waliokuwa wanamcha Mungu na kupewa neema ya kipekee ya kumzaa Bwana wetu Yesu, lakini hilo halina uhusiano wowote na yeye kuwa malkia, desturi za kuabudu miungu wake ni za kipagani na zilikuwepo tangu zamani AShtorethi/Semiramisi/Artemi mungu mke alikuwa anaabudiwa zamani zile na ndiye aliyekuwa anajulikana kama malkia wa mbinguni.   Kanisa katoliki ndilo lililobeba tamaduni hizi za kipagani kumwabudu Mariamu na kuwa kama kipatanishi kati yetu na Mungu ambayo ni machukizo makubwa mbele za Mungu.   Kwahiyo mkristo yoyote hapaswi kujihusisha na ibada potofu zinazotaja kuabudu miungu “wake”. Ni YESU KRISTO pekee ndiye anayestahili kuabudiwa.  

Ubarikiwe sana.

البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
DARASA LA 2
DARASA LA 2
Orodha ya masomo yote ya darasa la 1
بواسطة PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-09 10:14:30 0 6كيلو بايت
أخرى
THE ROCKFELLER FAMILY
This is the Rockefeller family. it is one of the wealthiest families in America, and their...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-12-22 00:53:20 0 6كيلو بايت
SPIRITUAL EDUCATION
VITA INAYOENDELEA JUU MBINGUNI
Zipo vita mbili kuu zinazowahusu shetani na Malaika watakatifu. Vita ya kwanza: Ni ile...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2021-10-30 11:35:03 0 6كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
UTHIBITISHO KUWA YESU NI MUNGU
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:47:09 0 6كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
YESU ALIBADILI MWENENDO WA HISTORIA YOTE
Tembea sehemu yoyote ulimwenguni. Ongea na watu wa dini yoyote. Haijalishi jinsi walivyoshikilia...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 21:16:46 0 5كيلو بايت