Mungu Alikuwa Anaongea Na Nani Aliposema Na “Tumfanye Mtu Kwa Mfano Wetu”,(Mwanzo 1:26)?

0
5KB

Mwanzo 1:26 Mungu akasema, Na tumfanye mtu kwa mfano wetu, kwa sura yetu; wakatawale samaki wa baharini, na ndege wa angani, na wanyama, na nchi yote pia, na kila chenye kutambaa kitambaacho juu ya nchi

JIBU: Mara nyingi Mungu alikuwa anatumia neno “sisi” kama wingi kuashiria kuwa hakufanya mambo yote peke yake, bali alikuwa na wengine aliowashirikisha mawazo yake, Kumbuka kuumba aliumba yeye peke yake lakini mawazo yake ya kufanya baadhi ya mambo aliwashirikisha wengine, hivyo hapo aliposema na tumfanye mtu kwa mfano wetu alikuwa anaongea na malaika zake, na hakuwa anazungumza na nafsi ya tatu katika uungu wake,kama wengi tunavyodhani Mungu ni mmoja tu na hana nafsi tatu, neno “TUMFANYE” halimaanishi ni watatu tu! bali linaweza likamaanisha wawili, au watano, au mia au milioni n.k.

Hivyo tukisema Mungu ana nafsi tatu kwa kuusimamia mstari huu sio kweli, pale Bwana alikuwa anazungumza na malaika zake ambao walikuwa wameshaumbwa kabla yetu sisi, Tunaona pia jambo hili linajirudia sehemu nyingine nyingi katika biblia Bwana akizungumza na malaika zake, Ukisoma

Mwanzo 3:22″Bwana Mungu akasema basi huyu mtu amekuwa kama MMOJA WETU, kwa kujua mema na mabaya”…,

pia,

Mwanzo 11:6 “Bwana akasema, Tazama, watu hawa ni taifa moja, na lugha yao ni moja; na haya ndiyo wanayoanza kuyafanya, wala sasa hawatazuiliwa neno wanalokusudia kulifanya. 7 Haya, na tushuke huko, tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao. 8 Basi Bwana akawatawanya kutoka huko waende usoni pa nchi yote; wakaacha kuujenga ule mji.”

Unaona hapo sehemu zote hizi mbili Bwana alionekana akijadiliana na malaika zake. Mungu huwa anatenda kazi na malaika zake. Tukisoma pia

Isaya 6:8 Kisha nikasikia sauti ya Bwana ikisema, nimtume nani? naye ni nani atakayekwenda KWA AJILI YETU? Ndipo niliposema mimi hapa nitume mimi. Naye akaniambia enenda ukawaambie watu hawa fulizeni kusikia lakini msifahamu; fulizeni kutazama lakini msione…”

Unaona tena hapo Bwana alimuuliza nabii Isaya ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu (yaani Mungu na jeshi lake la mbinguni)?. Kwahiyo Mungu kujadiliana na malaika zake sio jambo jipya tunaweza tukaliona pia kwenye ile habari ya mfalme Ahabu na nabii Mikaya ukisoma

2 nyakati 18:15-22” utaona jinsi Bwana alivyokuwa anashauriana na malaika zake juu ya hatma ya mfalme Ahabu.

Kwahiyo pale katika mwanzo 1:26 aliposema Na tumfanye mtu kwa mfano wetu Mungu alikuwa hazungumzi na YESU wala Roho Mtakatifu bali na malaika zake waliokuwepo kabla yetu sisi. (Lakini kumbuka sio kwamba malaika ndio waliokuwa wanaumba, hapana Mungu peke yake ndiye aliyekuwa muumbaji.)

Ubarikiwe sana.

Suche
Kategorien
Mehr lesen
OTHERS
If Jesus is God, then why did He say the Father was greater than He?
  "You heard that I said to you, ‘I go away, and I will come to you.’...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:47:05 0 5KB
UCHUMBA KIBIBLIA
UCHUMBA NI NINI? NA NDOA NI NINI?
Shalom, wapendwa,Katika somo letu leo nataka tuangalie vitu hivi viwili, mahusiano ya uchumba na...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-06 13:06:36 0 7KB
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 106 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-24 10:08:20 0 5KB
OTHERS
UTATU UNATHIBITISHWA KWA KUTUMIA HESABU/HISABATI
Kumekuwa na madai na hoja nyingi sana kuhusu hili swala la UTATU. Wengine wanasema kuwa...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:58:07 0 4KB
Injili Ya Yesu Kristo
Ngazi ya Yakobo
Mwanzo 28:10-19 “Yakobo akatoka Beer-sheba, kwenda Harani. Akafika mahali fulani...
Von GOSPEL PREACHER 2022-03-31 14:40:12 0 6KB