Je! Inawezekana mtu akawa anafanya miujiza na bado asinyakuliwe?

0
6K

SWALI: Naomba kuelewa kwanini mtu atoe pepo, aombee wagonjwa wapone, asikie sauti ya Mungu Ikimwambia hiki na kile kuhusu watu na yeye mwenyewe kufunua siri za mioyo yao, halafu bado asiende mbinguni au asinyakuliwe? Hili linawezekanikaje?


JIBU: Ni sababu ile ile ya Mungu kumpa mwovu afya, chakula, miaka mingi ya kuishi, mvua, uzao, ujuzi, akili, utashi,n.k. vipawa hivi vyote vinatolewa na Mungu, kwasababu yeye anawanyeshea mvua yake waovu na wema. sasa kwa kupewa baraka zote hizo haimpi uhakika mtu huyo kupata uthibitisho ya kuwa Mungu yupo na yeye,

Kwasababu hivi vitu vyote hata mchawi anapewa kitendo cha kuwa tu mwanadamu tayari vinaambatana na wewe, kuna vitu Mungu akikupa haviondoi hata uwe mbaya kiasi gani kama ilivyo kwa shetani Mungu hakumnyang’anya nguvu zake zote japokuwa ni muasi, lakini sababu ya Mungu kuruhusu hayo yote ni kuonyesha uwepo wake dhahiri ili mtu asiwe na udhuru katika siku ya hukumu kwamba hakuuona utukufu wake…

Siku zote Mungu anabaki katika NENO lake, mtu anayempendeza ni yule anayelishika NENO lake kwa kuishi maisha matakatifu yampendezayo, HILO TU! na ndio maana Bwana Yesu aliwaambia wanafunzi wake katika Luka 10:20″

Lakini, msifurahi kwa vile pepo wanavyowatii; bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni. “

Unaona tunapaswa tufurahie pale majina yetu yanapoandikwa mbinguni na sio pale pepo wanapotutii kwasababu kuna watakao toa pepo, watakaoona maono, watakao ponya wagonjwa, watakaotabiri na bado watakuwepo kuzimu.

Soma mistari ifuatayo;

Kumbukumbu 13:1 Kukizuka katikati yako nabii, au mwotaji wa ndoto, akikutolea ishara au ajabu, 2 ikatukia hiyo ishara au hiyo ajabu aliyokuambia akisema, Na tuifuate miungu mingine usiyoijua, tuitumikie hiyo; 3 wewe usiyasikize maneno ya nabii yule, au yule mwotaji wa ndoto, kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yuawajaribu, apate kujua kwamba mwampenda Bwana, Mungu wenu, kwa mioyo yenu yote na roho zenu zote. 4 Tembeeni kwa kumfuata Bwana, Mungu wenu; mcheni na kushika maagizo yake na kuisikia sauti yake, nanyi mtumikieni na kushikamana naye. 5 Na yule nabii, au yule mwotaji wa ndoto, na auawe, kwa kuwa amesema yaliyopotoka juu ya Bwana, Mungu wenu, aliyewatoa katika nchi ya Misri, akakukomboa katika nyumba ya utumwa, apate yule mtu kukupotoa katika njia aliyokuamuru Bwana, Mungu wako, uiendee. Ndivyo utakavyouondoa uovu utoke katikati yako.

Na ndio maana Bwana alimalizia na kusema….

Mathayo 7:21-27 ” Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni. 22 Wengi wataniambia siku ile, Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? 23 Ndipo nitawaambia dhahiri, Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu. 24 Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba; 25 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba. 26 Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga; 27 mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.”

Hivyo usipumbazwe na karama yoyote ile uliyonayo au mtu aliyonayo, Dumu katika Neno la Mungu na utakatifu. Hilo tu.

‘bali furahini kwa sababu majina yenu yameandikwa mbinguni’.

Ubarikiwe.

Căutare
Categorii
Citeste mai mult
MAHUSIANO KIBIBLIA
KANUNI YA MUDA KATIKA MAHUSIANO
Muda hupima upendo wangu kwako.Kama kweli nakupenda, nita tumia kiasi kikubwa cha Muda wangu kwa...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-06 15:03:16 0 5K
NDOA KIBIBLIA
MWANAUME UKIKOSA UNYENYEKEVU MKE ATAKUSHINDA
Unyenyekevu ni tabia ya kujishusha na kuvaa kiatu cha aliye chini yako; unavua heshima na utukufu...
By GOSPEL PREACHER 2021-11-08 00:12:34 3 6K
Networking
WELCOME TO PROSHABO.COM, LET US PREACH TOGETHER
Welcome to PROSHABO.COM, together we can preach the gospel of Christ Jesus and harvest many...
By PROSHABO NETWORK 2021-09-04 10:37:15 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
Je, Nina wezaje kupokea msamaha wa dhambi toka kwa Mungu?
Matendo ya Mitume 13:38 yasema, “Basi naijulikane kwenu, ndugu zangu ya kuwa kwa huyo...
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:42:55 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
Hekima yao ikapate kuwa ubatili na maarifa yao yawe ujinga!
2Samuel 15:30-31 “Daudi akapanda akishika njia ya kuupandia mlima wa Mizeituni, akilia...
By GOSPEL PREACHER 2022-04-01 09:26:31 4 7K