FAHAMU KUHUSU JINA LA FARAO

0
5KB

Kwa ufupi…

Bwana Yesu asifiwe…

Je unafahamu nini kuhusu jina hili la farao? Basi ngoja nikujuze kidogo kuhusu jina la Farao.

Farao sio jina kama majina mengine bali ni cheo kilichotumika kwa wafalme wa Misri. Hivyo Farao ni cheo cha kifalme wa kimisri, yaani ni sawa na kusema jina linalotumika kumuelezea kiongozi wa juu katika nchi katika nchi zetu leo; tunatumia neno “ raisi”. Kwa hiyo tuna “ raisi fulani, raisi fulani.n.k”Kulikuwa na baadhi ya wafalme waliotawala Misri,wapo kama kumi na mbili au kumi na tatu,wale waliotajwa katika maandiko,ambao hao wote waliitwa kwa jina la Farao.

Miongoni mwa cheo hiki,Wafalme wengine wawili walikuwa na majina yao tofauti na jina hili,Wafalme hao ni Necho and Hophra.
Bali wengine walibakia na cheo hicho cha Farao.Mtililiko ufuatao unatupa picha nzuri ya Farao kama walivyotajwa katika maandiko matakatifu;

  1. FARAO (Mwanzo 12:14-15,)Huu ulikuwa ni wakati wa Abrahamu kama B.C.1920
  2. FARAO(mwingine) Alikuwa ni Farao ambaye akida wake alikuwa ni Potifa Mwanzo 37 :39 39 :1,Matendo 7:10,13. Ilikuwa ni kabla ya Kristo, kamaB. C. 1728. Hata hivyo wengine husema kwamba FARAO huyu ni mtoto wa FARAO Yule wa katika Mwanzo 37:36
  3. FARAO(mwingine) *Huyu ni Farao mwingine aliyeinuka juu ya Misri asiyemfahamu Yusufu Matendo 7 :18,Kutoka 1 :8,Soma tena Waebrania 11 :23,Hata hivyo,kuna FARAO mwingine aliyeinuka katika kipindi cha Musa alipokimbilia Midiani na ndio Farao ambaye alikufa kabla ya Musa kufikisha umri wa miaka themanini aliporudi kutoka Midiani kwenda Misri,Soma Kutoka 2:11-23,Kutoka 4:19,na Matendo 7:23
  4.  FARAO(mwingine)Huyu ni Farao ambapo aliwazuia Waisraeli wasitoke Misri.Soma Kutoka 5:1-14,Kutoka sura ya 31,2Wafalme17 :7,Nehemia 9:10,Zaburi 135:9
    Rumi 9:17; Waebrania 11:27, alitawala kama B. C. 1491.(Kabla ya Kristo)
  5. FARAO(mwingine)Huyu alikuwa ni Farao katika kipindi cha Daudi 1Wafalme 11:18-22; B. C. 1030.
  6.  FARAO(mwingine)
    Huyu alikuwa ni Farao ambaye ni baba mkwe wake Selemani, 1Wafalme 3:1; 7:8; 9:16,24, B. C. 1010.

     

    PAMOJA NA FARAO HAO,WAPO WENGINE KAMA VILE;

  7. SHISHAKI-B. C. 975, 1Wafalme 11:40; 1Wafalme 14:25; 2 Nyakati12:2

  8. ZERAH,-Alikuwa ni mfalme wa Misri na pia alikuwa ni mfalme a Ethiopia katika kipindi cha Asa , B. C. 930;

  9. SO,
    -Huyu alikuwa akiitwa SO hivyo hivyo na ndilo jina lake.Ilikuwa Katika kipindi cha Ahazi, B. C. 730,Soma 2 Wafalme 17:4.
  10. TIRHAKA( Tirhakah,)
    *Huyu alikuwa ni mfalme wa Ethiopia na Misri(KUSHI)Katika muda wa Hezekia B. C. 720, Soma2 Wafalme 19:9; Isaya 37:9.

  11. FARAO-NEKO
    *Alikua ni mfalme wa Misri katika kipindi cha Yosia B. C. 612, Soma 2 Wfalme23:29-30; 2 Nyakati35:20-24, etc.

     

    MWISHO .
    UBARIKIWE.  

Rechercher
Catégories
Lire la suite
OTHERS
Juhudi za Kupinga Ukristo za Mwanaharakati wa Kundi la Ahmadiah Kutoka Pakistani Zamfanya Aachane na Uislamu
Nusrat Aman alikuwa ni mwanaharakati wa kiislamu wa kundi la Ahmadiah kule Pakistani. Siku moja...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:31:32 0 4KB
HOLY BIBLE
If Jesus is God, then why did He not know the time of His return?
In Matt. 24:35-37 Jesus said, "Heaven and earth will pass away, but My words shall...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 06:01:47 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
TENGENEZA MAMBO YA NYUMB YAKO
TENGENEZA MAMBO YA NYUMBA YAKO
Par Martin Laizer 2023-12-19 18:47:21 0 5KB
MASWALI & MAJIBU
Kwanini Mungu Hakumuua Nyoka, Akamwacha Hawa Ajaribiwe Katika Bustani Ya Edeni?
JIBU: Hili ni swali watu wengi wanajiuliza ni Kwanini Mungu hakumuua Nyoka, badala yake akamwacha...
Par GOSPEL PREACHER 2022-06-13 09:19:01 0 6KB
2 SAMUEL
Verse by verse explanation of 2 Samuel 7
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-02-05 09:26:36 0 5KB