KILA ATAKAYELIITIA JINA LA BWANA ATAOKOKA.

0
6K

Kwa ufupi..

Bwana Yesu asifiwe…

`` Kwa kuwa,kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka” Warumi 10:13

Ukihitaji kuokoka huna budi kilihitaji Jina la Bwana. Nabii Yoeli anasema,mtu yeyote atakayeliitia Jina la Bwana “ataponywa” Kumbe huna budi kushuka kwa Bwana kwa habari ya uponyaji na kuokoka kwako.

Tunaposema “ kuliitia Jina la Bwana” tunamaana ya kuomba kwa Jina Bwana Yesu kwenye kila eneo. Ingawa Bwana Mungu ajua shida zako, lakini bado unalo jukumu la kuomba ndipo utendewe sawa sawa na hitaji lako. Inawezakana ukawa kweli umeokoka, lakini bado hata hivyo unahitaji kuomba ili usaidiwe. 

Leo nataka tujifunze kwa Petro yeye aliyekuwa mtume wa Bwana,na kupitia andiko hili tunaweza kujifunza kitu hapa ;

Petro akamjibu, akasema, Bwana, ikiwa ni wewe, niamuru nije kwako juu ya maji.  Akasema, Njoo. Petro akashuka chomboni, akaenda kwa miguu juu ya maji, ili kumwendea Yesu. Lakini alipouona upepo, akaogopa; akaanza kuzama, akapiga yowe, akisema, Bwana, niokoeMara Yesu akanyosha mkono wake, akamshika, akamwambia, Ewe mwenye imani haba, mbona uliona shaka?” Mathayo 14:28-31

Tunaweza kujifunza mengi kutoka katika maandiko hayo hapo juu. Lakini nataka kujifunza neno moja tu,nalo ni “kuomba katika Jina la Bwana, wakati wa kuzama kwako” Petro anatufundisha njia nzuri ya kuokoka kutoka katika hali mbaya ya kuzama maji. Yeye Petro hakuwa na msaada mwingine isipokuwa ni kumuomba Bwana kwa kupiga yowe! Laiti kama Petro asingeliomba yamkini angelizama ndani ya yale maji.

Kumbuka Petro alikuwa na uzoefu mkubwa wa mambo ya baharini na uvuvi. Lakini safari hii uzoefu wake haukumsaidia isipokuwa ni Bwana tu ndiye aliyemsaidia asife maji, na huku ndiko kuokoka na kupona mauti. Leo inawezekana wewe nawe ukawa na uzoefu mwingi juu ya elimu fulani, lakini nataka nikuambie ukikamatwa kwenye kona mbaya, uzoefu wako kamwe hautakusaidia bali atakayekusaidia ni Bwana Yesu tu.

Petro hakuona tashwishwi kuliitia Jina la Bwana akihitaji msaada. Hata kwako,usione shida kuomba tena kuenda kuombewa na mchungaji aliye karibu nawe kusudi tatizo ulilokuwa nalo ni kama kuzama kwenye maji mengi. Wapo watumishi ambao wanagugumia na magonjwa yao,na shida zao wakiwa wameshikilia taratibu za kidini,na dini zao zimewakinga wakatae kuombewa.! nakushauri ikiwa unahitaji kuombewa fungua moyo wako na nenda kaombewe, Bwana naye atakuponya tu,uwe na imani hiyo ndugu yangu.

Căutare
Categorii
Citeste mai mult
Injili Ya Yesu Kristo
Jinsi ya kuzidi kuwa Hodari.
Utangulizi: Tunasoma Katika maandiko ya kwamba watu wengi wanaotajwa kama mashujaa wa Imani...
By GOSPEL PREACHER 2022-03-31 14:49:05 0 7K
Networking
What you need to know to plan your marketplace business
Online marketplaces are hot. The success of platforms like Airbnb, Etsy,...
By Business Academy 2022-09-17 03:36:39 0 6K
FORM 1
KISWAHILI : KIDATO CHA 1
Orodha ya mada zote za somo la Kiswahili kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha 1: BONYEZA HAPA...
By PROSHABO ONLINE SCHOOLS 2021-10-31 17:17:30 0 7K
CHRISTIAN EDUCATION
WEWE NI HEKALU LA MUNGU
WEWE NI HEKALU LA MUNGU 
By Martin Laizer 2023-12-23 16:13:51 0 7K
OTHERS
JE, WAGANGA WA KIENYEJI WANAWEZA KUKUPA ULINZI NA MAFANIKIO KATIKA MAISHA YAKO?
Naamini umeshasikia mara kadhaa watu wakitaja kile kinachoitwa “sayansi ya kiafrika”....
By MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:19:31 0 6K