Biblia inasema nini juu ya kushirikiana katika ngono kabla kuoana?
Pamoja na matendo mengine ya uchafu, kufanya kitendo cha mapenzi kabla kuoana kumekatazwa katika maandiko (matendo 15:20; warumi 1:29; wakorintho wa kwanza 5:1; 6:13, 7:2; 10;8; wakorintho wa pili 12:21; wagalatia 5:19; waefeso 5:3; wakolosai 3:5; wathesalonike 4:3; yuda7). Biblia inasisitiza kuepuka kitendo hicho kabla ya ndoa.hii ina maana ya kuwa ni dhambi kama ya uzinifu kwa kuwa hujaunganishwa na unayefanya naye kitendo hicho. Mapenzi baina ya mume na mke waliooana ndiyo mapenzi...
NAFASI YA MWANAMKE KIBIBLIA
Mwanzo 1:27 ‘Mungu akaumba mtu kwa mfano wake,kwa mfano wa Mungu alimwumba,mwanaume na mwanamke aliwaumba. Sikiliza mahali popote pale mwanamke ni mtu mwenye nguvu na ushawishi mkubwa katika kufanya mambo kuliko hata mwanaume.Ikiwa ushawishi huu utatumiwa katika mpango wa Mungu basi kusudi la Mungu litatekelezwa.
Mungu hakumwumba mwanamke kwa bahati mbaya au makosa,kila ambacho Mungu alikifanya ,alikifanya kwa kusudi.kwa lugha nyingine kila ambacho Mungu alikifanya...
NIFANYE NINI ILI KUSHINDA TAMAA ZA MWILI?
Septemba mwaka 2011, Mwanafunzi mmoja wa shule ya Sekondari alinitembelea nyumbani kwangu hapa Dodoma. Alipofika nilimkaribisha ndani nikajua amekuja kunisalimia tu. Baada ya muda akaniambia kaka Sanga nina swali nahitaji msaada wako sana. Tukatoka nje mahala penye utulivu ndipo akaniambia tamaa za mwili kwa maana ya uasherati/zinaaa zinanitesa nifanye nini ili kushinda? Jambo hili linanitesa kiasi kwamba nahisi kama vile sijaokoka kutokana na vita niliyonayo katika fahamu zangu na mwilini...
MAKOSA WANAYOFANYA VIJANA KATIKA KUTAFUTA MWENZI WA MAISHA.
KWA NINI VIJANA WENGI WANAKOSEA KATIKA KUTAFUTA MWENZI WA MAISHA?
Maamuzi ya kuoa au kuolewa, si maamuzi madogo, ni moja ya maamuzi makubwa ambayo vijana wengi wa kike na wa kiume wana kutana nayo kila siku. Sasa katika kufanya maamuzi haya ukweli ni kwamba sehemu kubwa ya vijana mpaka wafike mahali pa kumpata kijana au binti wa kusema huyu ndiye haswa wa kutoka kwa Bwana, basi ujue tayari wengi wanakuwa walishakosea mara nyingi mpaka kufikia hapo. Wapo ambao wakikosea husema, yule wa kwanza...
NAMNA YA KUKABILIANA NA CHANGAMOTO ZA UJANA
Shalom, neno changamoto linaweza kuwa na maana kadhaa, katika somo hili nimefafanua changamoto kama ushindani au mashindano baina ya pande mbili au zaidi, kila upande ukidai uhalali wa kile unachokiamini na hivyo kushawishi upande wa pili ukubaliane na kukifuata kile unachokiamini. Kutoka kwenye dhana ya vita vya kiroho (Waefeso 6:10), Shetani kama mfalme wa giza ndiye mwenye kuzileta changamoto mbalimbali dhidi ya wana wa Mungu kwa nia ya kuwaondoa kwenye nafasi zao za ki-Mungu na hivyo...
VIJANA MSIYACHOCHEE MAPENZI HATA YATAKAPOONA VEMA YENYEWE
Shalom, leo katika ukurasa huu wa maswali na majibu nataka kujibu swali kuhusu mwenendo wa vijana wakati wa uchumba ambalo limekuwa likiulizwa na wasomaji mbalimbali wa blogu hii kwa namna tofauti.
Swali: Bwana Yesu asifiwe Sanga, naomba kuuliza, je mimi na mchumba wangu kufanya michezo ya mapenzi bila kufanya tendo la ndoa ni dhambi? Mfano; kumbusu, kushikana shikana mwilini, kutekenyana, kunyonyana ndimi na yale yanayofanana na hayo? ni mimi James (James siyo jina halisi la aliyeuliza...
JINSI YA KUISHINDA DHAMBI YA TAMAA ZA MWILI
WAGALATIA 5:16-17:-"Basi nasema, ENENDENI KWA ROHO, WALA HAMTAZITIMIZA KAMWE TAMAA ZA MWILI. Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka."〰〰〰〰〰〰〰〰〰〰Maadamu bado tumeuvaa mwili huu, basi sio kwamba kutamani hakutakuwepo kabisa. Kunaweza kuwepo! Lakini neno limetupa siri ya kuzishinda hizo tamaa za mwili kwa kuenenda kwa Roho Mtakatifu.Neno la Mungu limeatuambia hapo mtu anayeenenda kwa Roho hataweza...
UMEHESABU GHARAMA?
Mahusiano ya uchumba hadi ndoa yanajengwa. Na kama yanajengwa, basi yana gharama na yanachukua muda, si jambo la mara moja au ghafula. Kuna gharama za ujenzi wa msingi, kuna gharama za kuinua, kuna gharama za kuendeleza, na kuna gharama za matengenezo (repairs).Kwa kifupi, mahusiano ya uchumba hadi ndoa ni gharama. Pasipo kulipa gharama hakuna mahusiano, iwe ni uchumba na hasa ndoa. Kushindwa kulipa gharama ni kushindwa ndoa, kwa wale ambao wako kwenye uchumba ni kushindwa uchumba.Kwa sababu...
MWANAMKE NA NGUVU YA USHAWISHI (UBEMBELEZI)
Mwanamke aliumbwa na nguvu ya ushawishi ndani yake kwa kusudi la kuweza kutimiliza jukumu lake katika familia la Kujenga na Kulinda nyumba yake. Lakini kwa bahati mbaya, nguvu hii ya ushawishi ambayo hufanya kazi yake kupitia uwezo wa ubembelezi alionao mwanamke, mara nyingi imekuwa ikitumika vibaya. Mwanamke mwenye hekima hujenga nyumba yake kwa mikono yake mwenyewe akitumia hazina ya uwezo aliowekewa ndani yake, na mojawapo ni nguvu ya ushawishi na ubembelezi alionao ndani yake.Ushawishi...
HATARI ZA KUWA NA MAHUSIANO YASIYO SAHIHI
UTANGULIZIMahusiano yasiyo sahihi ni mahusiano ya namna gani? Haya ni mahusiano kwanza kabisa ambayo mtu unaoa au unaolewa na mtu ambaye kusudi lake au nia yake ya kukuoa si sahihi. Pengine labda anakuoa au anakubali kuolewa na wewe sana sana kwa ajili ya kutimiza matamanio au matakwa yake.Pili ni mahusiano ambayo aliyekuchumbia au uliyemchumbia ni mtu ambaye hana lengo la kuolewa na wewe au kukuoa wewe. Pengine kuna kitu anafukuzia kwako na akiisha kukipata basi atavunja mahusiano hayo.Tatu,...
UNA HOFU YA KUTOKUOLEWA, AU KUACHIKA? SOMA HII ITAKUSAIDIA
Kama wewe ni mwanamke na bado hujaolewa, na sasa kitu kama hofu ndani yako ya kutokuolewa kimeingia, somo hili linakuhusu sana tu. Lakini pia labda una hofu ya kupoteza mchumba wako, au mume wako, somo hili pia linakuhusu.Leo japo nitazungumza kwa kirefu kidogo lakini kwa kina nataka nizungumzie tatizo linalowakumba wanawake wengi wa sasa katika mahusiano yao, HOFU YA KUTOKUOLEWA, KUACHIKA AU KUPOTEZA MCHUMBA (AU MUME). Naomba usome mpaka mwisho, ITAKUSAIDIAUzoefu unaonyesha wazi kuwa,...
HIZI NI TABIA HATARISHI KWA MWANAMKE KATIKA MAHUSIANO: UCHUMBA HADI NDOA
KWELI KUU: Tabia ni msingi na kielelezo cha mahusiano bora ya aina yoyote na hasa yale ya uchumba hadi ndoa.Mithali 31:30:
Upendeleo hudanganya, na uzuri (wa sura au umbo au rangi) ni ubatili; Bali mwanamke amchaye Bwana, ndiye atakayesifiwa.
Somo hili ni kwa ajili ya wanaume lakini pia ni kwa ajili ya wanawake. Kwa wanaume linawasaidia kujua mwanamke wa tabia gani ni wa kuoa na wa tabia gani si wa kuoa. Kwa wanawake linawasaidia kujichunguza na kubadilika kitabia ili kujiweka katika...
Статьи пользователей
Sub-Categories
Больше
Verse by verse explanation of 2 Kings 20
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
UNATEKELEZA WAZO LA NANI UNAPOKUWA NDANI YA JARIBU?
Andiko la msingi ni Matahayo 27:11-20.
Mpenzi msomaji ninakusalimu katika jina la Bwana...
NAFASI YA MAWAZO KATIKA KUVIPIGA VITA VYA KIROHO
Vita vya kiroho, ni vita ambayo inapigwa katika ulimwengu wa roho, kwa jinsi ya rohoni baina ya...
Mtu ambaye amemwamini Yesu lakini akafa bila kubatizwa je! atenda mbinguni?
JIBU: Inategemea kama hapo kabla alishausikia ukweli au la, kwa mfano kama mtu alishaufahamu...
FORM 6
List of all subjects for the form 6 class
ACCOUNTANCY
ADVANCED MATHEMATICS
AGRICULTURE
BASIC...