Yesu alikuwa wapi katika siku tatu toka siku ile ya kufa mpaka kufufuka?

0
5KB
Kama Yesu alivyotabiri, alisalitiwa na mmoja wa wafuasi wake, Yuda Iscariot, na alikamatwa. Katika shitaka la kufedhehesha chini ya Gavana wa Kirumi, Pontio Pilato, alitiwa hatia ya uhaini na alilaaniwa kufa kwenye msalaba wa mbao. Kabla ya kupigiliwa misumari msalabani, Yesu alipigwa kwa ukatili kwa mjeledi wenye mifupa vyuma ambao ulinyofoa nyama. Alisukumwasukumwa, alipigwa mateke, na alitemewa mate.
Yesu akamwambia (mwizi aliyetubu) Amini nakwambia, leo utakuwa pamoja paradiso .
.
Luka 23:39 Mmoja wa wale wahalifu waliotundikwa msalabani, alimtukana akisema: "Je, si kweli kwamba wewe ndiwe Kristo? Basi, jiokoe mwenyewe, utuokoe na sisi pia." 40 Lakini yule mhalifu mwingine akamkemea mwenzake akisema: "Wewe humwogopi Mungu hata kidogo? Wewe umepata adhabu hiyohiyo. 41 Wewe na mimi tunastahili, maana haya ni malipo ya yale tuliyotenda. Lakini mtu huyu hakufanya chochote kibaya." 42 Kisha akasema, "Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako." 43 Yesu akamwambia, "Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi."
Hii inathibitisha kuwa roho ya Yesu na yule Mwizi aliyetubu hazikukoma kuishi bali zilikwenda Paradiso . Je, huko ndipo alipo kuwa Yesu kwa siku tatu?
Petro wa kwanza 3:18-19 inaeleza, “kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi zetu, mwenye haki kwa ajili yao wasiohaki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake ukauawa, bali roho yake ikahuishwa, ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokuwa kifungoni akawahubiri.”
Siku tatu kuu za Pasaka ndizo kiini cha mwaka wa Kanisa.
Zinamuadhimisha Yesu mteswa, mzikwa na mfufuka, yaani siku ya kwanza (Alhamisi kuu jioni hadi Ijumaa kuu jioni) inaadhimisha mateso yake kuanzia karamu ya mwisho hadi kifo cha msalaba; siku ya pili (Ijumaa kuu jioni hadi Jumamosi kuu jioni) inaadhimisha maiti yake kubaki kaburini na roho yake kushukia kuzimu; siku ya tatu (kuanzia Jumamosi kuu jioni hadi Jumapili ya Pasaka jioni) inaadhimisha ufufuko wake mtukufu.
Petro wa Kwanza 3:18-22 inaeleza ushikamano wa kuteswa kwake Kristo (fungu la 18) na kutukuzwa kwake (fungu la 22). Petro ndiye anayefafanua yaliyotokea katikati ya matukio haya mawili. Neno “alihubiri’ katika fungu la 19 lina maana ya kuwa aliwasilisha ujumbe. Yesu aliteswa na kufa msalabani, mwili ukiuawa na roho yake pia kufa kwa kufanywa dhambi. Lakini roho yake ilifufuliwa naye akaikakabidhi Baba. Kulengana na Petro, muda huo baada ya kufa mpaka kufufuka Yesu aliwasilisha hali Fulani ya ujumbe kwa “roho waliokuwa kifungoni.”
Bwana wetu aliikabidhi roho yake kwa Baba, akafa na wakati Fulani toka kufa mpaka kufufuka, akatembelea kuzimu alikowasilisha ujumbe kwa viumbe vya kiroho 9 pengine ni malaika waasi tazama yuda 6) waliokuwa na uhusiano na nyakati za kabla gharika la wakati wa Nuhu. Kifungu cha 20 kinafafanua zaidi. Petro hakutuambia kilichoambiwa roho hawa waliokuwa kifungoni lakini haiwezi kuwa ilikuwa habari ya wokovu kwa kuwa malaika hawaokolewi (Waebrania 2:16). Pengine ilikuwa ni kutangazwa kwa kushindwa kwa shetani na milki yake (Petro wa kwanza 3:22; Wakolosai 2:15). Waefeso 4:8-10 pia inajaribu kueleza kuwa Kristo alienda “paradise” (Luka 16:20; 23:43) na akawachukua mpaka mbinguni wale waliokuwa wamemuamini kabla kufa kwake.
Biblia haifafanui wazi wazi kilichotendeka ndani ya muda wa siku tatu hizi toka kufa mpaka kufufuka. Haiwezi kueleweka ya kuwa alikuwa ameenda kuwapa watu nafasi ya pili ya kuokolewa kwa kuwa biblia inatuambia ya kuwa tunakutana na hukumu punde tu baada ya kufa (Waebrania 9:27).
Shalom
Max Shimba mtumwa wa Yesu Kristo.
Rechercher
Catégories
Lire la suite
NDOA KIBIBLIA
UNATAKA KUOLEWA NA MTU SAHIHI??
Leo napenda nizungumze na akina dada ambao bado hawajaolewa na wanataka kuolewa.Mtu sahihi kwako...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-07 23:26:13 0 5KB
ESTHER
Verse by verse explanation of Esther 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 25 questions at the...
Par THE HOLY BIBLE 2022-04-02 12:48:38 0 5KB
OTHERS
MUHAMMAD ALIKUWA NA DHAMBI KUBWA KIASI CHA KUOMBA MSAMAHA MARA MIA KWA SIKU
Dhambi kubwa Katika "Sahih Muslim, Kitabu 35, 6522 Idadi" inasema kwamba Muhammad alikuwa...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:14:15 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
DINI YA KIISLAM ILIANZISHWA SIKU YA JUMATATU MWEZI WA 17, SAWA SAWA NA TAREHE 27 DESEMBA MKWA 610 B.K.
KUMBE UISLAM NI DINI YA KUTENGEZA TU, TENA CHANGA SANA NA HAIKUWEPO KABLA YA MUHAMMAD  ...
Par MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:13:31 0 5KB
MAHUSIANO KIBIBLIA
HIZI NI TABIA HATARISHI KWA MWANAMKE KATIKA MAHUSIANO: UCHUMBA HADI NDOA
KWELI KUU: Tabia ni msingi na kielelezo cha mahusiano bora ya aina yoyote na hasa yale ya uchumba...
Par GOSPEL PREACHER 2021-11-07 23:18:56 0 10KB