Yesu Kristo hajaumbwa bali alikuwepo tangu milele yote

0
5Кб

Ni kweli kabisa kwamba Yesu alikuwepo tangu milele yote kabla ya kuumbwa kitu cho chote kile. Bwana Yesu kwa kauli ya kinywa chake mwenyewe anasema kwamba:

“Na sasa, Baba, unitukuze Mimi pamoja Nawe, kwa utukufu ule Mimi niliokuwa nao pamoja Nawe kabla ya ulimwengu kuwako.” (Yohana 17:5)

Neno “UTUKUFU” maana yake ni heshima, uweza, uzuri, umaarufu, nguvu, sifa na mamlaka. Mambo hayo yote Yesu alikuwa nayo kabla hata ulimwengu haujaumbwa. Yesu Kristo alikuwapo hata kabla ya kuzaliwa na Mariamu; jambo hili pia Yesu Kristo kwa kinywa Chake Yeye mwenyewe ametuthibitishia alipokuwa akiwaambia Wayahudi kwamba:

 

“Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.

 

Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Je! Sisi hatusemi vema ya kwamba wewe u Msamaria, nawe una pepo?

 

Yesu akajibu, Mimi sina pepo; lakini Mimi namheshimu Baba yangu, na ninyi mwanivunjia heshima Yangu. Wala mimi siutafuti utukufu Wangu; Yuko mwenye kutafuta na kuhukumu. Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele. Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akuilishika neno langu, hataonja mauti milele. Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani? Yesu akajibu, Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si situ; anitukuzaye ni Baba Yangu, ambaye ninyi mwanena kuwa ni Mungu wenu. Wala ninyi hamkumjua; lakini mimi namjua. Nikisema ya kwamba simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi; lakini namjua, na neno lake nalishika. Ibrahimu baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.

 

Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe haujapata bado miaka hamsini, nawe umemona Ibrahimu? Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, Mimi niko.” (Yohana 8:47-58)

 

Katika kisa tulichokisoma katika maandiko hayo (Yohana 8:47-57) tunajifunza mambo kadhaa hapo. Tumeona dhahiri jinsi ambavyo hata baadhi ya Wayahudi ilivyo wawia vigumu sana kumwelewa huyu Yesu ni nani; hata wakadiriki kusema kuwa Yesu anayo mapepo (mashetani). Hawakumwelewa kwa sababu walimtazama Yesu kibinadamu kama jinsi wao walivyo, lakini hawakujua kuwa Yesu ni alikuwepo hata kabla ya Yeye kuzaliwa na Mariamu. Huyo Ibrahimu anayeongelewa hapo ni yule ambaye habari zake tunazisoma katika kitabu cha MWANZO cha Biblia (Ibrahimu baba yake Isaka na Ishmaili). Wayahudi walishangaa; Inawezekanaje huyu Yesu aseme alimwona Ibrahimu aliyeishi na kufa miaka mingi tena zaidi ya elfu moja iliyopita, wakati huyu Yesu tumemwona utotoni mwake na hata sasa bado hajatimiza umri wa miaka hamsini? Hayo yalikuwa ni mawazo ya kibinadamu; tena inaezekana hata wewe ukawa ni miongoni mwa waliokuwa wanawaza hivyo; lakini, Yesu mwenyewe anatuthibitishia kwa kinywa Chake kwa kusema:

“...Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, Mimi niko.” (Yohana 8:58)

Pia Yesu amewaambia Wayahudi kuwa huyo ambaye wao wanamwita Mungu (YEHOVA), Yeye ndiye Baba wa Yesu; tena Yesu anamjua ingawa hao Wayahudi hawamju (Yohana 8:54,55). Vile vile tusomapo kitabu cha MITHALI tunaona habari zinazo mhusu huyu Yesu; imeandikwa kwamba:

 

“BWANA alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake. Kabla ya matendo Yake ya kale. Nalitukuka tokea milele, tangu awali, Kabla haijawako dunia. Wakati visipokuwapo vilindi nalijidhihirisha... (...I was brought forth... – NKJV)...” (Mithali 8:22-24)

Usomapo Biblia ya Kiswahili; hapo nilipoandika “...Wakati visipokuwapo vilindi NALIJIDHIHIRISHA...” utaona baadhi ya Biblia za Kiswahili zimeandika “...NALIZALIWA...” lakini maana halisi hapo ni “...I was brought forth...” ambayo tafsiri yake ni “...NALIJITOKEZA...” au “...NALIJIDHIHIRISHA...”

 

Kumbuka kuwa Wayahudi walimtambua Mungu kwa jina "YEHOVA" ambalo mara nyingi walitamka kwa kusema "BWANA." Hapo Biblia Takatifu inamtaja huyu Yesu likuwa pamoja na YEHOVA katika mwanzo wa njia za YEHOVA. Kabla ya YEHOVA kuumba cho chote (...matendo ya kale...) huyu Yesu alikuwepo. Hivyo basi; huyu Yesu alikuwapo “...tokea milele, tangu awali, Kabla haijawako dunia.” (Mithali 8:23) Neno “MILELE” maana yake ni wakati ambao hauna mwanzo wala mwisho; ni wakati usioweza kuhesabika.

 

Upo ushahidi mwingi sana ndani ya Biblia Takatifu unaotuthibitishia kuwa Yesu alikuwepo hata kabla ya kuumbwa kitu cho chote kile; kwani nao manabii pia walitabiri ujio wa Yesu ambaye alikuwepo tangu milele yote, na tena manabii hao walisema wazi wazi kuwa huyu Yesu ni Mungu. 

Поиск
Категории
Больше
OTHERS
How an Atheist Found God
A personal account from an atheist who was convinced no god exists, and what facts led to God....
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 09:43:58 0 6Кб
Religion
JE CHANJO YA KORONA NI ALAMA YA MNYAMA?
  Jina la Bwana na Mwokozi wetu Yesu, libarikiwe, karibu katika kujifunza maandiko. Leo...
От PROSPER HABONA 2021-08-24 02:14:52 0 7Кб
Injili Ya Yesu Kristo
Ubatizo wa Rohoho Mtakatifu ni nini?
Ubatizo wa Roho mtakatifu unaweza kufafanuliwa/kuelezwa kuwa ile kazi ambayo Roho Mtakatifu wa...
От MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 04:05:10 0 4Кб
REVELATION
MAJIRA YA KANISA LA SARDI
(1) MLENGWA WA KANISAUFUNUO 3:1Na kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika; Haya ndiyo anenayo...
От GOSPEL PREACHER 2021-09-24 10:07:38 0 5Кб
SPIRITUAL EDUCATION
RECEIVE JESUS CHRIST AS YOUR LORD AND SAVIOUR
Romans 10:9-10.  “That if thou shalt confess with thy mouth the Lord Jesus, and shalt...
От GOSPEL PREACHER 2021-11-19 07:45:34 0 5Кб