LEO TUTAMTAZAMA BWANA YESU NA MUHAMAD NI NANI MWENYE MATUMAINI YENYE UHAKIKA KATI YAO

0
5كيلو بايت
Tutapitia kauli zao walizozisema wakiwa Duniani, na kila mmoja atahukumu ni yupi mbora wa kufwata kati ya Bwana Yesu na Muhamad.

BWANA YESU ANASEMA
Yohana 8:12 Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
Yohana 10:9 Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho.

Yohana 10:11 Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo.
Yohana 10:14 Mimi ndimi mchungaji mwema; nao walio wangu nawajua; nao walio wangu wanijua mimi;
Yohana 11:25 Yesu akamwambia, Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi, ajapokufa, atakuwa anaishi;
Yohana 14:6 Yesu akamwambia, Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi.


Yohana 6:40 Kwa kuwa mapenzi yake Baba yangu ni haya, ya kwamba kila amtazamaye Mwana na kumwamini yeye, awe na uzima wa milele; nami nitamfufua siku ya mwisho.


Yohana 8:14 Yesu akajibu, akawaambia, Mimi ningawa ninajishuhudia mwenyewe, ushuhuda wangu ndio kweli; kwa sababu najua nilikotoka na niendako; lakini ninyi hamjui nilikotoka wala niendako.


Yohana 14: 2 Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi; kama sivyo, ningaliwaambia; maana naenda kuwaandalia mahali.3 Basi mimi nikienda na kuwaandalia mahali, nitakuja tena niwakaribishe kwangu; ili nilipo mimi, nanyi mwepo. 4 Nami niendako mwaijua njia.


Ufunuo 1:17… Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,18 na aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama, ni hai hata milele na milele. Nami ninazo funguo za mauti, na za kuzimu.

MUHAMAD ANASEMA
Q 46:9. Sema: Mimi si kiroja miongoni mwa Mitume. Wala sijui nitakavyo fanywa wala nyinyi. Mimi nafuata niliyo funuliwa tu kwa Wahyi, wala mimi si chochote ila ni mwonyaji mwenye kudhihirisha wazi.


Q19:71. Wala hakuna yeyote katika nyinyi ila ni mwenye kuifikia(hiyo Jehanam). Ni wajibu wa Mola wako uliokwisha hukumiwa.


Na ktk Sahihi Al-Bukhari IV, Hadith Na. 728, na VI, Hadith Na. 294. Muhamad anasema Eeh ndugu zangu Abdul Manaf, Abbas bin Abdul bin Mutalib, Safiyyah(shangazi) na binti yangu Fatima mimi sina uwezo wa kuwaokoa dhidi ya ghazabu ya Mungu.


Q 10:102. Basi, je! Wanangojea jingine ila (kuwajia) mfano wa siku za (adhabu zilizowafika) watu walio pita kabla yao? Basi Ngojeni! Mimi pia ni pamoja nanyi katika wanao ngojea.


Fafanuzi yake: Ukimwone mwenzio amenyolewa kwa jambo hilo hilo unalolifanya, basi kitie maji upesi kichwa chako kwani na wewe utanyolewa km alivyonyolewa.


Quran 40: 60. Na Mola wenu Mlezi anasema: Niombeni nitakuitikieni. Kwa hakika wale ambao wanajivuna na kuniabudu Mimi wataingia Jahannamu wadhalilike.


"Mwenye kubadili dini yake (ya kiislamu, muueni" (A) Bhukari 6922, Abu Dawuwd 4329, At - Tirmidhiy 1483
O Khadija, Ninaona Mwanga, na nasikia Masautisauti, nina hofu kuwa mimi nina Wazimu. "Kitab al-Tabaqat al-Kabir", by Ibn Sad, , ukurasa wa 225

Ndugu msomaji(Mkristo na Mwislam) tukiacha yote ni nani hapo anamatumaini ya uhakika ya kumfuata kati ya Bwana Yesu na Muhamad????.

Bwana Yesu apewe sifa.
البحث
الأقسام
إقرأ المزيد
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 17
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 26 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-02-05 15:52:21 0 5كيلو بايت
1 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 1 Chronicles 26
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 27 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-03-20 05:20:12 0 6كيلو بايت
JOSHUA
Verse by verse explanation of Joshua 13
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
بواسطة THE HOLY BIBLE 2022-01-25 08:09:48 0 5كيلو بايت
Injili Ya Yesu Kristo
NI NINI MAANA YA “ROHO”?
Hebu tuzungumzie jinsi Biblia inavyotumia neno “roho.” Watu fulani hufikiri kwamba...
بواسطة MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 19:51:05 0 6كيلو بايت
JONAH
YONA 2
Jina la mwokozi wetu YESU KRISTO libarikiwe. Karibu katika mwendelezo wetu wa kitabu cha...
بواسطة GOSPEL PREACHER 2022-01-20 03:04:34 0 5كيلو بايت