MWANAMKE WA KIISLAM HANA HAKI MBELE YA MUMEWE

0
5KB
Leo nitawapa hadith kadhaa kuhusu Wanawake wa Kiislam na jinsi wanavyo onewa na Mtume Muhammad.
 
NGONO NI LAZIMA HATA KAMA MWANAMKE ANAUMWAKutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mume atakapomwita mkewe kwenye kitanda chake [kwa tendo la ndoa] na yule mke akakataa kumuitika, Malaika humlaani mpaka kupambazuke”[Imepokelewa na Al-Bukhaariy, kitabu cha Nikaah, mlango wa atakapolala mwanamke hali ya kuwa amekihama kitanda cha mumewe. Hadiyth namba 4821 na namba 4822; Muslim, kitabu cha Nikaah, mlango uharamu wa mwanamke kujizuilia [kujitenga] na kitanda cha mumewe, Hadiyth namba 2602 na Hadiyth namba 2603 na 2604.]
 
MWANAMKE KABLA YA KUFUNGA LAZIMA APEWE RUHUSA NA MUMEWE. HUU NI MSIBAImepokelewa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Asifunge mwanamke [Swawm ya Sunnah] na huku mumewe yuko pamoja nae isipokuwa kwa idhini yake huyo mume na wala asimruhusu mtu katika nyumba ikiwa mumewe yuko isipokuwa kwa idhini yake huyo mume” [Imepokelewa na Al-Bukhaariy, kitabu cha Nikaah, mlango wa Swamw ya Sunnah ya mwanamke kwa idhini ya mumewe, Hadiyth namba 4820; na katika Kitabu cha Tafsiri Qur aan, Suuratul Qul A’uwdhu birabbil Falaq, Hadiyth namba 4823; na Muslim, katika Kitabu cha Zakaah, mlango wa atachotoa mtumishi katika mali ya tajiri wake, Hadiyth namba 1710].
 
MWANAMKE WA KIISLAM HARUHUSIWI KUSAIDIA NDUGU ZAKEImepokelewa kutoka kwa Abu Umaamah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Asitoe mwanamke kitu chochote kutoka katika nyumba ya mumewe isipokuwa kwa idhini ya mumewe.” [Imepokelewa na Al-Bukhaariy, kitabu cha Nikaah, mlango wa Swawm ya Sunnah ya mwanamke kwa idhini ya mumewe, Hadiyth namba 4823; na Muslim, katika Kitabu cha Zakaah, mlango wa atachotoa mtumishi katika mali ya tajiri wake, Hadiyth namba 1710].
 
MWANAMKE WA KIISLAM KAZI YAKE NI KUMFURAISHA MUMEWE NA NGONO TU.Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allahu ‘anhu) amesema kwamba aliulizwa Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wanawake gani bora? Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: “Ambae humfurahisha [humpendezesha]anapomtazama, na humtii anapomwamrisha, mke humhifadhi katika nafsi yake na mali ya mumewe” [Imepokelewa na Ahmad, katika Musnad ya Kumi waliobashiriwa Jannah, Musnad waliobakia katika Mukthiriyna katika Swahaabah (Radhiya Allahu ‘anhum), Musnad Abi Hurayrah (Radhiya Allahu ‘anhu), Hadiyth namba 7245 na 9377 na 9445].
 
MWANAMKE WA KIISLAM HARUHUSIWI KUOMBA TALAKAKatazo La Kudai Talaka Bila Ya Sababu Inayokubalika
Ndoa ni katika mambo Aliyoyaamrishwa Allaah na kuyahimizaMjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), ndoa ni mafungamano ya kishari’ah baina ya mwanamme na mwanamke yenye mipaka, nidhamu, vidhibiti na kanuni maalumu; na inaathiri mengi; ima kujenga na kusimamisha familia ya Kiislamu yenye kuongozwa na kuongoka kwa uongofu wa Qur-aan na Sunnah za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na kuwa miongoni mwa tofali la kuijenga jamiirabbaaniy [yenye kumuabudu Allaah pekee Mola wa viumbe vyote na yenye kufundisha Kitabu, kukisoma na kukifuata]; na ima kuvunja na kubomoa familia kwa kuivuruga vuruga na kuisambaratisha na kusababisha athari mbaya kwa jamii na watoto kwa kuachana kwa mume na mke.
 
Na katika yaliyokatazwa ambayo yameenea na kuzagaa kwa wenye kupenda dunia na kuiweka kando Aakhirah ni kwa mwanamke kumtaka au kumghilibu mumewe; iwe kwa kumhadaa au vinginevyo kwa kumshurutisha amuache mkewe ili apate kuolewa yeye au abakie yeye pekee yake [kama ni mke mwenza] hili limekatazwa kama ilivyothibiti katika Hadiythi kuwa Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mwanamke asitake (katika Riwayah: Si halali kwa mwanamke kudai kuachwa ukhti wake [mwanamke mwenzake] ili aichukue nafasi yake na kuolewa yeye; kwani hatopata isipokuwa yale aliyoandikiwa.” [Imepokelewa na Al-Bukhaariy, kitabu cha tafsiyr ya Qur-aan, Surat Qul A’uwdhu Birabbil Falaq, Hadiyth namba 6141 na 4782; na Muslim, katika Kitabu cha ndoa, mlango wa Uharamu wa kuwakusanya mwanamke na Shangazi yake, Hadiyth namba 2527; na Abu Daawuud, katika Kitabu cha atw-Twalaaq, mlango katika mwanamke anamtaka mumewe talaka ya mke wake, Hadiyth namba1865].
Suche
Kategorien
Mehr lesen
MAHUSIANO KIBIBLIA
SEHEMU YA 5: MISINGI YA KIIMANI KATIKA MAHUSIANO YA UCHUMBA HADI NDOA
Bwana asifiwe!! Unaweza kusoma SEHEMU YA 1, SEHEMU YA 2, SEHEMU YA 3, SEHEMU YA 4 ya somo hili,...
Von GOSPEL PREACHER 2021-11-06 11:49:18 0 5KB
OTHERS
UTATA KATIKA KORAN: ADAM ALIUMBWAJE?
Binadamu aliumbwa kutoka nini? Tone la Damu? Maji? Udongo? Vumbi?Jamani huu nao ni Msiba Mkubwa...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:20:59 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
DEMONS - WHAT ARE THEY?
Demons are NOT human. They are invisible evil spirits with various sizes and shapes.God did in...
Von MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 19:04:18 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
MSHINDE GOLIATHI.
Bwana Yesu asifiwe… Kwa ufupi; Goliathi alikuwa ni mtu wa vita wa kifilisti. Habari za mtu...
Von GOSPEL PREACHER 2022-03-30 05:03:54 0 5KB
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 24
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
Von THE HOLY BIBLE 2022-01-25 06:40:04 0 6KB