YESU NI MWANA WA MUNGU MAANA YAKE NINI?

0
5KB

Wanadhuoni wa Kiislam pamoja na waumini wa dini ya Kiislam huwa wanauliza na kusema kwa Wakristo yafuatayo:

1. Kivipi Yesu ni Mwana wa Mungu?
2. Mungu atakuwaje na Mwana bila ya Mke?
 
KIVIPI YESU NI MWANA WA MUNGU?

Yesu Kristo si Mwana wa Mungu kulingana na ubaba wa kawaida wa binadamu, nikimaanisha kuwa Mungu hakuoa na kupata mwana wa kiume. Nikiwa na maanisha kuwa, Mungu hakufanya tendo la ndoa na Mariamu, na pamoja naye kuzaa mtoto wa kiume ambaye anaitwa Yesu, la hasha.
 
 
MUNGU ATAKUWAJE NA MWANA BILA YA MKE?

Yesu ni Mungu katika hali kwamba ni Mungu anajithirihisha kama mwili. (Yohana 1:1, 14) Yesu ni mwana wa Mungu kwa dhana kwamba Mariamu alipata mimba kupitia Roho Mtakatifu ambaye ni Mungu. Luka 1:35 yasema, “Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, MWANA WA MUNGU.”
Mariamu aliambiwa na Malaika kuwa, Mtoto atakaye zaliwa atakuwa Matakatifu na ataitwa MWANA WA MUNGU. Huu ushahidi upo kwenye Luka 1:35.
 
YESU AKUBALI KUWA YEYE NI MWANA WA MUNGU MBELE YA KUHANI MKUU

Wakati wa kujaribiwa kwake mbele ya viongozi wa Kiyahudi, kuhani mkuu alimtaka Yesu, “Nakuapisha kwa Mungu aliye hai, utuambie kama wewe ndiwe Kristo, MWANA WA MUNGU” (Mathayo 26:63). [NOTE: YESU HAKUKATAA ALIPO ITWA MWANA WA MUNGU NA KUHANI MKUU, SOMA JIBU LAKE] “Yesu akamwambia wewe umesema,’ Yesu akamwambia, wewe umesema; lakini nawaambieni, Tangu sasa mtamwona Mwana wa Adamu ameketi mkono wa kuume wa nguvu, akija juu ya mawingu ya mbinguni” (Mathayo 26:64) viongozi wa Kiyahudi walimdhania kwa kukufuru (Mathayo 26:65-66).
 
WAYAHUDI WANAKIRI KUWA YESU AMEKUBALI KUWA YEYE NI MWANA WA MUNGU
Baadaye mbele ya Pilato, “Wayahudi wakamjibu, Sisi tunayo sheria, na kwa sheria hiyo amestahili kufa, kwa sababu alijifanya kuwa Mwana wa Mungu” Yohana 19:7) [KWENYE HIYO AYA YA YOHANA 19:7, WAYAHUDI WANAKIRI KUWA YESU AMEKUBALI KUWA YEYE NI MWANA WA MUNGU] ni kwa nini makisio yake kuwa Mwana wa Mungu yachukuliwe kuwa kufuru na astahili hukumu ya kifo?
 
Wayahudi wilielewa vizuri sana chenye Yesu alimaanisha kwa maneno haya “Mwana wa Mungu” kuwa Mwana wa Mungu ni kuwa hali moja na Mungu. Mwana wa Mungu “wa Mungu” kusema uko katika hali sawa na Mungu-hakika kuwa Mungu- kulikuwa sawa na kukufuru kwa viongozi wa Kiyahudi; kwa hivyo walimtaka Yesu auwawe, kulingana na Mambo ya Nyakati 24:15. Waebrania 1:3 inadhihirisha haya wazi, “Yeye kwa kuwa ni mng’ao wa utukufu wake, akiisha kufanya utakaso wa dhambi, aliketi mkono wa kuume wa Ukuu huko juu.”
 
Mfano mwingine unaweza patikana katika Yohana 17:12 mahali Yuda anaelezwa kama mwana wa “upotevu”? jina upotevu lamaanisha “uharibivu” Yuda hakuwa mwana wa uharibivu, lakini mambo hayo ndio ya kutambulisha maisha ya Yuda. Yuda anadhihirisha upotevu. Vile vile Yesu mwana wa Mungu. Ni Mungu anajidhihirisha (Yohana 1:1,14).
 
Hii mada iatufundisha maana ya Yesu ni Mwana wa Mungu, SWALI ambalo limekuwa likiulizwa na Waislam kila siku. Leo wamesha pata jibu thabiti tena lenye ushahidi wa aya za Biblia.
 
Hakika Yesu ni Mwana wa Mungu
Pesquisar
Categorias
Leia mais
OTHERS
MAGUGU "WAISLAMU" WATATUPWA KWENYE TANURI LA MOTO
Kwenye somo letu, tutajifunza kuhusu Magugu "Wapinga Kristo = Waislamu" ambayo yanaota kwenye...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-25 11:35:17 0 5KB
Injili Ya Yesu Kristo
Kujengwa kwa Hekalu bila kelele!
1Wafalme 6:7. “Na nyumba ilipokuwa ikijengwa, ikajengwa kwa mawe yaliokwisha kuchongwa...
Por GOSPEL PREACHER 2022-04-01 08:26:15 0 5KB
DEUTERONOMY
Verse by verse explanation of Deuteronomy 31
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 31 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-25 07:03:32 0 5KB
1 SAMUEL
Verse by verse explanation of 1 Samuel 27
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 23 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-26 04:26:05 0 5KB
HOLY BIBLE
JIFUNZE MAANA YA MAJINA YA MUNGU (YEHOVA)
Mungu ni mmoja tu, lakini katika umoja wake amekuwa akijifunua katika majina mengi, kulingana...
Por GOSPEL PREACHER 2021-10-30 08:26:51 0 6KB