Malaika Waliofanya Dhambi

0
5KB
Biblia inafundisha kwamba Mungu ni Roho na kwamba viumbe wake wa kwanza walikuwa roho. (Yohana 4:24; Waebrania 1:13, 14) Isitoshe, Biblia pia inataja kwamba kuna roho waovu. (1 Wakorintho 10:20, 21; Yakobo 2:19) Lakini haifundishi kwamba Mungu ndiye aliyewaumba roho waovu. Basi wao ni nani, na walitokea jinsi gani?

Katika Biblia tunasoma kuwa, kuna Malaika walitenda dhambi na kufukuzwa Mbiguni. Mungu mwenye upendo, alipowaumba viumbe wa roho, viumbe hawa, aliwaumba wakiwa na uhuru wa kuchagua ikiwa watatende mema au mabaya.

Roho wa kwanza kuasi na mwenye sifa mbaya zaidi alikuwa Lucifer ambaye anajulikana sasa kwa jina la Shetani.

Ni nini kilichomchochea Shetani kumwasi Mungu?
Shetani alianza kutamani ibada ambayo ilikuwa hasa ya Muumba-Mungu, kisha akajikweza kutokana na tamaa hiyo na kujifanya kuwa mungu. Isaya 14: 11Fahari yako yote imeshushwa mpaka kuzimu, pamoja na kelele ya vinubi vyako, mafunza yametanda chini yako na minyoo imekufunika. 12Tazama jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe nyota ya asubuhi, mwana wa mapambazuko! Umetupwa chini duniani, wewe uliyepata kuangusha mataifa! 1 3Ulisema moyoni mwako, “Nitapanda juu hadi mbinguni, nitakiinua kiti changu cha enzi juu ya nyota za Mungu, ataketi nimetawazwa juu ya mlima wa kusanyiko, kwenye vimo vya juu sana vya mlima Mtakatifu.

Biblia inamfafanua Shetani kuwa kiumbe halisi ambaye yuko katika makao ya roho. (Ayubu 1:6) Inatueleza kuhusu sifa zake za ukatili kutia ndani matendo yake ya uovu. (Ayubu 1:13-19; 2:7, 8; 2 Timotheo 2:26) Pia inasimulia mazungumzo kati ya Shetani na Mungu na pia kati yake na Yesu.—Ayubu 1:7-12; Mathayo 4:1-11.

Kiumbe huyo mwovu alitoka wapi? Mungu aliumba viumbe “roho” wanaoitwa malaika. (Ayubu 38:4-7) Wote walikuwa wakamilifu na waadilifu. Hata hivyo, mmoja kati ya malaika hao akaja kuwa Shetani.

Malaika huyo hakuitwa Shetani alipoumbwa kama nilivyo sema hapo mwanzo na/au hakuumbwa akiwa Shetani, kama imani zingine zinavyo sema, bali alikuwa Malaika muadilifu mbele za Mungu. Jina hilo Shetani ni la kumfafanua, na linamaanisha “Mpinzani; Adui; Mshtaki.” Alikuja kuitwa Shetani kwa sababu alichagua kumpinga Mungu.



Kiumbe huyo wa roho akaanza kukuza hisia za kiburi na za kushindana na Mungu. Alitaka wengine wamwabudu yeye. Mwana mzaliwa wa kwanza wa Mungu alipokuwa hapa duniani, Shetani alimtaka Yesu ‘amfanyie tendo la ibada.’—Mathayo 4:9.

Katika Bustani ya Edeni, Shetani amdanganya Hawa:
Shetani “hakusimama imara katika kweli.” (Yohana 8:44) Alidai kwamba Mungu alikuwa mwongo, ilhali kwa kweli, yeye ndiye alikuwa mwongo. Alimwambia Hawa kwamba angekuwa kama Mungu, lakini ni yeye hasa aliyetaka kuwa kama Mungu. Na kupitia mbinu zake za ujanja, alitosheleza tamaa yake yenye ubinafsi. Alimfanya Hawa amwone kuwa mkuu kuliko Mungu. Kwa kumtii Shetani, Hawa alimkubali kuwa mungu wake.—Mwanzo 3:1-7.

Kwa kuchochea uasi, malaika huyo ambaye awali alikuwa mwenye kuaminika akawa Shetani, yaani, mpinzani na adui ya Mungu na wanadamu. Neno “Ibilisi,” linalomaanisha “Mchongezi,” likawa pia jina la malaika huyo mwovu. Malaika huyo ambaye aliongoza katika kutenda dhambi mwishowe aliwachochea malaika wengine wakose kumtii Mungu na wamwasi kama yeye. (Mwanzo 6:1, 2; 1 Petro 3:19, 20) Kwa kufanya hivyo malaika hao waliwaongezea wanadamu shida. Kwa sababu ya kuiga njia za Shetani zenye ubinafsi, “dunia ikajaa jeuri. Na uovu”—Mwanzo 6:11; Mathayo 12:24.

Ingawa ni wazi kwamba roho waovu wamezuiwa wasijigeuze kuwa wanadamu, bado wana nguvu na uvutano mwingi juu ya akili na maisha ya watu. Kwa kweli, Shetani, na roho wake waovu, ‘anaipotosha dunia nzima inayokaliwa.’ (Ufunuo 12:9; 16:14) Kwa njia gani? Hasa kupitia “mafundisho ya roho waovu.” (1 Timotheo 4:1) Mafundisho hayo ya uwongo, ambayo mengi ni ya kidini, yamepofusha akili za mamilioni ya watu wasitambue ukweli kumhusu Mungu. (2 Wakorintho 4:4) Fikiria mifano kadhaa.

Unaweza kujilinda jinsi gani dhidi ya roho waovu?
Biblia inajibu hivi: “Jitiisheni kwa Mungu; lakini mpingeni Ibilisi, naye atawakimbia ninyi.” (Yakobo 4:7) Tunatii agizo hilo tunapoishi kupatana na mafundisho yaliyo katika Biblia, kitabu pekee kitakatifu ambacho kinamfichua Shetani, roho waovu, na “hila” zao. (Waefeso 6:11; 2 Wakorintho 2:11) Pia, Biblia inatuambia kwamba roho waovu pamoja na wote wanaompinga Mungu, hawatakuwapo milele. (Waroma 16:20) “Wanyoofu ndio watakaokaa duniani, na wasio na lawama ndio watakaobaki ndani yake,” inasema Methali 2:21.
Pesquisar
Categorias
Leia mais
MASWALI & MAJIBU
Mitume Wote Waliopita Walikuwa Ni Watu Weupe Hata Manabii Wote Waliopita Hadi Ma-Papa Ni Ngozi Nyeupe. Ni Kweli Ngozi Nyeusi Ililaaniwa ?
JIBU: Hakuna ngozi yoyote iliyolaaniwa, watu wote kwa Mungu ni sawa, Mungu hana upendeleo...
Por GOSPEL PREACHER 2022-06-13 08:37:18 0 5KB
SPIRITUAL EDUCATION
SELF DELIVERANCE
NO DEMONS ALLOWED SELF DELIVERANCE PROVERBS 6:5 "...DELIVER THYSELF..." If you want to get...
Por MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 19:28:32 0 5KB
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 28
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-01-21 06:39:38 0 5KB
PSALMS
Verse by verse explanation of Psalm 2
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-04-04 22:55:04 0 5KB
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 3
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 29 questions at the...
Por THE HOLY BIBLE 2022-02-05 12:25:19 0 5KB