HAWA NI WATU WALIOMDHIHAKI MUNGU NA KUPATWA NA SHIDA

0
5χλμ.

1. JOHN LENNON (MUIMBAJI)

Wakati alipokuwa akihojiwa na mwandishi wa habari wa gazeti la American alinukuliwa akisema hivi "Ukristo utakufa na kutoweka duniani, siwezi kuwa na wasiwasi na hilo kwa kuwa nina uhakika nalo. Mafundisho ya Yesu yalikuwa sahihi na wala sipingi hilo ila mafundisho yale yalikuwa mepesi sana ambayo mtu yeyote anaweza kuyafundisha. Hebu angalia leo, tumekuwa maarufu hata zaidi yake (Hapo alilitaja kundi lake la The Bettle). Ilikuwa mwaka 1966. Wiki moja baada ya kutamba kwamba yeye na kundi lake lilikuwa maarufu hata zaidi ya Yesu, akapigwa risasi sita na kufariki..

2. TANCREDO NEVES (RAIS WA BRAZIL)

Alisema kwamba endapo angepata kura laki tano kutoka katika uchaguzi mkuu wa Brazil na kuwa rais, hata MUNGU asingeweza kumtoa katika urais huo. Akafanikiwa, akapata kura zaidi ya hizo, akashinda uchaguzi, siku moja kabla ya kuapishwa, akafariki dunia.

3. CAZUZA (MWANAMUZIKI WA BRAZIL)

Alipokuwa katika shoo yake ndani ya jiji la Rio De Janeiro, alichukua sigara, akaanza kuivuta, akachukua nyingine na kisha kuirusha juu na kusema "Mungu, hiyo yako, chukua nawe uvute" Alifariki akiwa na miaka 32 kwa ugonjwa wa kansa ya mapafu ambayo iliyaharibu sana mapafu yake kuliko mgonjwa yeyote yule.

4. MTENGENEZAJI WA MELI YA TITANIC.

Baada ya kutengeneza meli ya Titanic, mwanahabari akamuuliza ni kwa kiasi gani ilikuwa salama nae akajibu "Ni salama sana, haiwezi kuzama na hata Mungu hawezi kuizamisha" Nafikiri unajua kilichotokea kuhusu Titanic.

5. BON SCOTT (MUIMBAJI)

Mwimbaji huyu ambaye alitamba miaka ya 70 alitoa wimbo wake mmoja mwaka 1979 wenye maneno haya "Don't stop me; I'm going down all the way, down the highway to hell'. Tarehe 19 February mwaka 1980, alikutwa amekufa baada ya kupaliwa na matapishi yake.

6. BINTI ALIYEMKUFURU MUNGU.

Mwanamke mmoja alikuwa akihofia sana kuhusu ulevi wa marafiki wa mtoto wake. Wakati wanataka kuondoka na gari, akamshika mtoto wake mkono garini na kumwambia "Binti yangu, Mungu awatangulie katika safari yenu" Yule binti akajibu "Gari imejaa mama, huyo Mungu labda akae kwenye boneti (buti) la gari". Baada ya masafa fulani ya safari yao, gari lile lilipata ajali kiasi ambacho hata polisi hawakujua ni aina gani ya gari lilikuwa. Lilikuwa limebondeka sana na watu wote walikutwa wamekufa. Kilichowashangaza polisi, trey la mayai wala halikuonekana kuguswa na hakuna hata yai moja lililokuwa limevunjika na wakati gari lilibondeka mpaka kutokutambulika. Bila shaka Mungu aliyalinda mayai yale tu, kwa kuwa kule ndiko ambako watoto walipotaka Mungu akae.

7. CHRISTINA HEWITT (MWANDISHI WA HABARI)

Huyu alikaririwa akisema hivi "Nimesoma vitabu vyote duniani, ila hakuna kitabu kibaya...kibaya na kibaya kama Biblia" Siku chache baada ya kusema maneno hayo, mwili wake ulikutwa umeunguzwa na moto ambao haikujulikana mpaka leo ule moto ulisababishwa na nini.

8. MARILYN MONROE (MUIGIZAJI)

Huyu alifuatwa na Bill Graham na kumwambia kwamba alitumwa na Roho wa Mungu kwa ajili ya kumhubiria. Alimkaribisha ndani, akamsikiliza kwa makini, alipomaliza akasema "Simuhitaji Yesu wako, unaweza kuondoka nae". Wiki moja baadae, alikutwa amekufa katika makazi yake. Polisi walijaribu kuchunguza kipi kilimuua, mpaka leo hawajapata jibu

Αναζήτηση
Κατηγορίες
Διαβάζω περισσότερα
OTHERS
KUMBE SHETANI ANAISHI MAKKA
Ndugu zanguni huu ni Msiba mwingine kwa ndugu zetu. Amini usi amini habari ndio hii na ukweli...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 05:02:41 0 5χλμ.
Injili Ya Yesu Kristo
AGIZO LA KUTAWADHANA
Neno la Uzima kutoka kwa  Askofu Zachary Kakobe        ...
από GOSPEL PREACHER 2022-01-12 00:56:05 0 9χλμ.
OTHERS
JE, ISA NI JINA SAHIHI LA YESU WA BIBLIA?
Katika somo letu hili tutajifunza kuhusu jina sahihi la Yesu/Yashua na tafsiri yake katika...
από MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-23 08:28:15 0 5χλμ.
1 KINGS
Verse by verse explanation of 1 Kings 1
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 60 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-02-05 12:14:55 0 5χλμ.
2 CHRONICLES
Verse by verse explanation of 2 Chronicles 18
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 30 questions at the...
από THE HOLY BIBLE 2022-04-02 01:40:16 0 5χλμ.