• JE, KUNATOFAUTI KATI YA KUPUNGA PEPO NA KUTOA PEPO?

    Katika nyakati hizi za mwisho kumekuwa na roho nyingi zidanganyazo binadamu. Roho hizi za mpinga Kristo zinawadanganya wengi na kuwafanya wengi wajione kana kwamba wako na Mungu, kumbe Mungu hayupo kati yao na/au ndani ya maisha yao.

    Katika soma hili, tutajifunza tofauti iliyopo kati ya Kupunga Pepo na Kutoa Pepo kwa ushaidi wa aya takatifu za Biblia.
    ( TIMOTHEO 4:1 ).
    “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza  roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani”. Miongoni mwa mambo ya siku hizi za mwisho ni roho hizo kuwafanya watu wadanganyike na kufuata mafundisho ya uongo. Hao ni wale wanaoikataa ile kweli.

    (2 TIMOTHEO 4:3-5 )
    “Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia walimu makundi makundi kwa kuwa wana masikio ya utafiti; nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo”.

    (2 WATHESALONIKE 2:7-12 )
    Watu ambao hawataki mafundisho ya utakatifu lakini wanataka kuona nguvu za Mungu maishani mwao, watadanganywa kwa ishara na ajabu za uongo.
    Katika nyakati hizi tunaweza kuona jinsi watu wanavyofanyiwa maombezi kwa kuangushwa chini na hatimaye kusimama bila kupokea muujiza wa uponyaji. Utaweza kuona watu wamejazana madhabahuni wakigaagaa chini na baadaye husimama na kuondoka lakini wakati mwingine huchukua muda mrefu kwao kusimama na kuondoka.

    Jambo la kushangaza ni siku zote kuonekana watu haohao , mapepo yao hayatoki. Miujiza hii imeenea kote duniani, uatakuta watu wanapiga kelele lakini pepo hawawatoki watu hao. Miujiza ya kimungu huondoa pepo kabisa ndani ya mtu tena kwa mamlaka na kumwacha akiwa mzima. Watu hawa hawafanyi miujiza ya uponyaji bali wanapunga pepo.

    Ni muhimu kujua kuwa  hata wapagani wanaweza kupunga pepo na kuwafanya wapige kelele. Waganga wa kienyeji wanaweza kupunga pepo lakini hawawezi kuwatoa. Tunawaona wapunga pepo wakitaka kutoa pepo lakini wanashindwa  ( MATENDO 19:13-16 ). Watu hawa walikuwa wa kawaida lakini leo tungewaita walokole kwa kuwa walikuwa watu wa dini.

    Jina jingine linalotumika kwa wapunga pepo ni” wapandisha pepo”. Mungu anasema kila anayepandisha pepo ni chukizo mbele zake ( KUMBUKUMBU LA TORATI 18:9-14 ). Waganga wa kienyeji ni wapandisha pepo au wapunga pepo. Kuna mazingira fulani  yanaandaliwa ili pepo wajidhihirishe kwao. Wanaimba na kuchezacheza ili nguvu hiyo ya shetani  iwe dhahiri kwa mfano  wetu tunavyofanya  katika kusifu au kuabudu ili nguvu ya Mungu ionekane  au idhihirike. Mfano Paulo na Sila gerezani walimsifu Mungu na nguvu za Mungu zikashuka milango ya gereza ikafunguka.

    Kazi tuliyoitiwa  ni ya kutoa pepo na siyo kupunga au kupandisha pepo ( MARKO 16:17 ‘Na ishara hizi zitafuatana nao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo”. MATHAYO 12:22-28 ). Kazi ya kupunga pepo ni ya shetani. Yesu aliuliza,” je, wana wenu huwatoa kwa nani?”. Swali hili la Yesu lilielekezwa kwa afarisayo walioishangazwa na mamlaka yake ya kuponya wagonjwa na kutoa pepo. Kimsingi hapo alikuwa akiuliza kuhusiana na wapunga pepo au wapandisha  pepo, kwamba wao wanatumia nguvu gain?

    Kuna madaraja katika majeshi ya pepo. Katika kutoa kafara tofautitofauti kubwa au ndogo ndipo Mganga anapoweza  kupata pepo wa daraja la juu au la chini. Huyo anayelipa  leseni kubwa yaani kafara , anapewa uwezo mkubwa wa kipepo. Anakuwa na mamlaka makuu kama kamanda wa Jeshi hivyo anaweza kuwaamuru pepo kumwingia mtu na kunyamanzisha pepo wadogo waliomo ndani ya mtu lakini hatimaye hari ya huyo mtu baadaye inakuwa mbaya zaidi kwa sababu idadi yao ( pepo ) imeongezeka.


    (MARKO 6:7 )
    “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu”. Pepo wachafu wanakaa ndani ya mtu mchafu. Ni mfano wa Inzi, hukaa katika uchafu. Kwa hiyo pepo wachafu hukaa ndani ya mtu mwenye dhambi. Dhambi ni uchafu ( ZEKARIA 3:3-4 ). Baba ( mwanzilishi ) wa maovu yote ni Ibilisi ( Shetani ) na huyo ndiye baba yao watendao dhambi ( YOHANA 8:44 ).

    (YAKOBO 4:4 )
    “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu” Shetani ni mungu wa dunia hii ( 2 WAKORINTHO 4:4 ). Kuwa rafiki wa dunia ni kufanya yaleyale wanayoyafanya watu wa dunia hii ambao hawajaokolewa kwa kiumwamini Yesu Kristo. Watu wa dunui maisha yao ni maisha ya dhambi tu maana wao wanayafanya mapenzi ya mungu wa dunia ( baba yao ). Tukianza kuiga kuvaa kwao, kuongea kwao,  kucheza kwao, na mambo mengine mengi yasiyompendeza Mungu, Tutamfungulia Shetani mlango wa kuingia na kufanya maskani ndani yetu. Machizo yote tuwe mbali nayo ( YEREMIA 32:33-34; KUMBUKUMBU 7:26 ). Machukizo yanamfanya Mungu kutuacha kabisa ( 2 NYAKATI 36:14-16 ).

    Uweza wa Mungu wa kuponya unaweza usiwepo mahali kwa sababu ya kuwepo kwa machukizo. Makuhani nao wanaweza kutenda dhambi na kuingiza machukizo ndani ya nyumba ya Mungu kama tunavyoona katika andiko hilo juu. Watumishi wengi wanatamani kuziona nguvu za Mungu katika huduma zao kama wakati wa Mitume lakini gharama zake zinawashinda. Mungu hawezi kumtumia mtu mchafu ambaye siyo mtakatifu ( WAEBRANIA 1:9 ).

    Hivyo basi, vitu vyote tunavyovaa katika miili yetu ambavyo siyo vya mwili kwa asili yake  ni machukizo kwa Bwana. Kuvaa Mapambo na nywele za bandia ni machkizo kwa Bwana. Kama ingekuwa ni mapenzi ya Mungu tuvae Kwa mfano Heleni, Mungu angeweka tundu kwenye masikio yetu ili kutuandaa kwa ajili ya mapambo. (  1 TIMOTHEO 2:9-10; 1 PETRO 3;3-5;  ISAYA 29:16; WARUMI 9:19-21 ).

    Hatutaweza kuziona nguvu za Mungu katika maisha yetu kama nyakati za Mitume ni mpaka kanisa la sasa litakapotambua kuwa msingi wa Mitume na Manabii ulishaachwa ( WAEFESO 2:20 ). Mitume waliwafundisha watu kutokufuata fasheni ( namna ) za ulimwengu huu lakini leo hii mafundisho yamna hii ni dadra sana kuyasikia ( WARUMI 12:2 ).

    Pia waliweka msisitizo juu ya kutokufuata mataifa kufanya hili au lile wafanyalo kwa sababu nia za Mataifa ni batiri ( WAEFESO 4:17 ). Kati ya mataifa kuna makahaba ambao kazi yao ya ukahaba inawafanya kutafuta mavazi ya kuvaa ambayo yatawafanya hao wanaotafutwa kuvutika na kuwafuata katika uchafu. Biblia yetu imetaja mavazi ya kikahaba ( MITHALI 7:10 ). Fasheni nyingi za kidunia zinadizainiwa  na mkuuwa dunia na mfalme wa uwezo wa anga  ( WAEFESO 2:1-3 ).
    JE, KUNATOFAUTI KATI YA KUPUNGA PEPO NA KUTOA PEPO? Katika nyakati hizi za mwisho kumekuwa na roho nyingi zidanganyazo binadamu. Roho hizi za mpinga Kristo zinawadanganya wengi na kuwafanya wengi wajione kana kwamba wako na Mungu, kumbe Mungu hayupo kati yao na/au ndani ya maisha yao. Katika soma hili, tutajifunza tofauti iliyopo kati ya Kupunga Pepo na Kutoa Pepo kwa ushaidi wa aya takatifu za Biblia. ( TIMOTHEO 4:1 ). “Basi Roho anena waziwazi ya kwamba nyakati za mwisho wengine watajitenga na imani, wakisikiliza  roho zidanganyazo, na mafundisho ya mashetani”. Miongoni mwa mambo ya siku hizi za mwisho ni roho hizo kuwafanya watu wadanganyike na kufuata mafundisho ya uongo. Hao ni wale wanaoikataa ile kweli. (2 TIMOTHEO 4:3-5 ) “Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima; ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia walimu makundi makundi kwa kuwa wana masikio ya utafiti; nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo”. (2 WATHESALONIKE 2:7-12 ) Watu ambao hawataki mafundisho ya utakatifu lakini wanataka kuona nguvu za Mungu maishani mwao, watadanganywa kwa ishara na ajabu za uongo. Katika nyakati hizi tunaweza kuona jinsi watu wanavyofanyiwa maombezi kwa kuangushwa chini na hatimaye kusimama bila kupokea muujiza wa uponyaji. Utaweza kuona watu wamejazana madhabahuni wakigaagaa chini na baadaye husimama na kuondoka lakini wakati mwingine huchukua muda mrefu kwao kusimama na kuondoka. Jambo la kushangaza ni siku zote kuonekana watu haohao , mapepo yao hayatoki. Miujiza hii imeenea kote duniani, uatakuta watu wanapiga kelele lakini pepo hawawatoki watu hao. Miujiza ya kimungu huondoa pepo kabisa ndani ya mtu tena kwa mamlaka na kumwacha akiwa mzima. Watu hawa hawafanyi miujiza ya uponyaji bali wanapunga pepo. Ni muhimu kujua kuwa  hata wapagani wanaweza kupunga pepo na kuwafanya wapige kelele. Waganga wa kienyeji wanaweza kupunga pepo lakini hawawezi kuwatoa. Tunawaona wapunga pepo wakitaka kutoa pepo lakini wanashindwa  ( MATENDO 19:13-16 ). Watu hawa walikuwa wa kawaida lakini leo tungewaita walokole kwa kuwa walikuwa watu wa dini. Jina jingine linalotumika kwa wapunga pepo ni” wapandisha pepo”. Mungu anasema kila anayepandisha pepo ni chukizo mbele zake ( KUMBUKUMBU LA TORATI 18:9-14 ). Waganga wa kienyeji ni wapandisha pepo au wapunga pepo. Kuna mazingira fulani  yanaandaliwa ili pepo wajidhihirishe kwao. Wanaimba na kuchezacheza ili nguvu hiyo ya shetani  iwe dhahiri kwa mfano  wetu tunavyofanya  katika kusifu au kuabudu ili nguvu ya Mungu ionekane  au idhihirike. Mfano Paulo na Sila gerezani walimsifu Mungu na nguvu za Mungu zikashuka milango ya gereza ikafunguka. Kazi tuliyoitiwa  ni ya kutoa pepo na siyo kupunga au kupandisha pepo ( MARKO 16:17 ‘Na ishara hizi zitafuatana nao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo”. MATHAYO 12:22-28 ). Kazi ya kupunga pepo ni ya shetani. Yesu aliuliza,” je, wana wenu huwatoa kwa nani?”. Swali hili la Yesu lilielekezwa kwa afarisayo walioishangazwa na mamlaka yake ya kuponya wagonjwa na kutoa pepo. Kimsingi hapo alikuwa akiuliza kuhusiana na wapunga pepo au wapandisha  pepo, kwamba wao wanatumia nguvu gain? Kuna madaraja katika majeshi ya pepo. Katika kutoa kafara tofautitofauti kubwa au ndogo ndipo Mganga anapoweza  kupata pepo wa daraja la juu au la chini. Huyo anayelipa  leseni kubwa yaani kafara , anapewa uwezo mkubwa wa kipepo. Anakuwa na mamlaka makuu kama kamanda wa Jeshi hivyo anaweza kuwaamuru pepo kumwingia mtu na kunyamanzisha pepo wadogo waliomo ndani ya mtu lakini hatimaye hari ya huyo mtu baadaye inakuwa mbaya zaidi kwa sababu idadi yao ( pepo ) imeongezeka. (MARKO 6:7 ) “Akawaita wale Thenashara, akaanza kuwatuma wawili wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu”. Pepo wachafu wanakaa ndani ya mtu mchafu. Ni mfano wa Inzi, hukaa katika uchafu. Kwa hiyo pepo wachafu hukaa ndani ya mtu mwenye dhambi. Dhambi ni uchafu ( ZEKARIA 3:3-4 ). Baba ( mwanzilishi ) wa maovu yote ni Ibilisi ( Shetani ) na huyo ndiye baba yao watendao dhambi ( YOHANA 8:44 ). (YAKOBO 4:4 ) “Enyi wazinzi, hamjui ya kwamba kuwa rafiki wa dunia ni kuwa adui wa Mungu” Shetani ni mungu wa dunia hii ( 2 WAKORINTHO 4:4 ). Kuwa rafiki wa dunia ni kufanya yaleyale wanayoyafanya watu wa dunia hii ambao hawajaokolewa kwa kiumwamini Yesu Kristo. Watu wa dunui maisha yao ni maisha ya dhambi tu maana wao wanayafanya mapenzi ya mungu wa dunia ( baba yao ). Tukianza kuiga kuvaa kwao, kuongea kwao,  kucheza kwao, na mambo mengine mengi yasiyompendeza Mungu, Tutamfungulia Shetani mlango wa kuingia na kufanya maskani ndani yetu. Machizo yote tuwe mbali nayo ( YEREMIA 32:33-34; KUMBUKUMBU 7:26 ). Machukizo yanamfanya Mungu kutuacha kabisa ( 2 NYAKATI 36:14-16 ). Uweza wa Mungu wa kuponya unaweza usiwepo mahali kwa sababu ya kuwepo kwa machukizo. Makuhani nao wanaweza kutenda dhambi na kuingiza machukizo ndani ya nyumba ya Mungu kama tunavyoona katika andiko hilo juu. Watumishi wengi wanatamani kuziona nguvu za Mungu katika huduma zao kama wakati wa Mitume lakini gharama zake zinawashinda. Mungu hawezi kumtumia mtu mchafu ambaye siyo mtakatifu ( WAEBRANIA 1:9 ). Hivyo basi, vitu vyote tunavyovaa katika miili yetu ambavyo siyo vya mwili kwa asili yake  ni machukizo kwa Bwana. Kuvaa Mapambo na nywele za bandia ni machkizo kwa Bwana. Kama ingekuwa ni mapenzi ya Mungu tuvae Kwa mfano Heleni, Mungu angeweka tundu kwenye masikio yetu ili kutuandaa kwa ajili ya mapambo. (  1 TIMOTHEO 2:9-10; 1 PETRO 3;3-5;  ISAYA 29:16; WARUMI 9:19-21 ). Hatutaweza kuziona nguvu za Mungu katika maisha yetu kama nyakati za Mitume ni mpaka kanisa la sasa litakapotambua kuwa msingi wa Mitume na Manabii ulishaachwa ( WAEFESO 2:20 ). Mitume waliwafundisha watu kutokufuata fasheni ( namna ) za ulimwengu huu lakini leo hii mafundisho yamna hii ni dadra sana kuyasikia ( WARUMI 12:2 ). Pia waliweka msisitizo juu ya kutokufuata mataifa kufanya hili au lile wafanyalo kwa sababu nia za Mataifa ni batiri ( WAEFESO 4:17 ). Kati ya mataifa kuna makahaba ambao kazi yao ya ukahaba inawafanya kutafuta mavazi ya kuvaa ambayo yatawafanya hao wanaotafutwa kuvutika na kuwafuata katika uchafu. Biblia yetu imetaja mavazi ya kikahaba ( MITHALI 7:10 ). Fasheni nyingi za kidunia zinadizainiwa  na mkuuwa dunia na mfalme wa uwezo wa anga  ( WAEFESO 2:1-3 ).
    0 Comments 0 Shares 5K Views 0 Reviews
  • UPONYAJI WA MAGONJWA.

    Chanzo cha magonjwa: Magonjwa yanatokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya mtu aliyekuwa mngonjwa alimwonya akisema, “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi” Yn 5:14. Mtu akiwa amefanya dhambi anapoumwa na kupimwa ugonjwa unaonekana. Iwapo akipimwa vipomo vyote na ugonjwa hauonekani yamkini ni pepo wachafu wamemwingia. “Mara huenda akachukua pamoja naye pepo wengine walio waovu kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya” Mt 12:45.

    Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili, unaotokana kukosa lishe ya mlo wa kila siku (Utapia mlo). Mapungufu katika mwili wa mwanadamu yanaweza yakawa ni kusudi la Mungu, ijapokuwa si yote. “Bwana akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani amfanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, Bwana? Kut 4:11.

    Kuponywa kwa dawa.

    Kwa kawaida kuna njia ambayo imekuwa ikitumika ya kutibu mangonjwa ambayo ni kutibu kwa kutumia dawa. Tiba za dawa zimekuwapo kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali. Mtu anapokuwa mgonjwa kuna hatua ya kuchukua, kwanza anaenda hospitali au kupelekwa kutona na hali yake hajiwezi. Daktari anampima na kufahamu ugonjwa alio nao, halafu anamwandikia dawa na maelekezo ya kuzitumia. Kama hatazingatia maelekezo na kuzitumia haiwezekani akapona. Hapa tunaweza kuona mgonjwa ili apone ni lazima azingatie maelekezo aliyopewa na daktari. Lakini baadhi ya magonjwa hayana tiba kama UKIMWI (HIV Aids). Hata hivyo usikate tamaa mwamini Mungu anaweza kukuponya kwa njia ya kumwomba. Atakuponya kwa neema, na rehema, kwa uwezo na nguvu zake.VIlevile kuna kanuni na maelekezo ya kufuata ili Mungu akuponye

    UPONYAJI WA MUNGU. Una maelekezo na kanuni za kufuata:

    1. Kutubu na kuziacha dhambi: “Azifichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema” Mit 28:13. “Twajua ya kwamba Mungu hawasikii wenye dhambi;bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake huyo humsikia” Yn 9:31.

    2. Kuishi maisha ya utakatifu: Ndio maana Mungu amesema; “Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako. Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote…” Kumb 7:12, 15. Katika maandiko haya tunaona Mungu alisema na baba zetu ya kwamba kwa upande wetu tunapozishika na kuzitenda hukumu zake (Sheria zake). Na kwa upande wake yeye ndipo hutuondolea ugonjwa wote. Kwa sababu Mungu aliwaapia baba zetu akisema, nitakutimizia agano na rehema. Kwa kiapo chake anathibitisha atafanya yale aliyoahidi katika Agano alilolifanya na baba zetu. Mahali pengine tunasoma:

    “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote,…Mche Bwana, ukajiepushe na uovu, Itakuwa afya mwilini pako. Na mafuta mifupani mwako. Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzishike kauli zangu. Kwa maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote”Mit 3:5,7,8.

    3.Kumwamini Mungu na neno lake: Ndiyo maana Mungu alisema “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita roho yangu haina furaha naye.” Ebr 10:38. Kutokana na andiko hili, linaonyesha lazima mtu awe mwenye haki ndipo aweze kuishi kwa imani. Pia lazima kwanza kuamini moyoni na kuwa na uhakika Mungu atakuponya kama neno linavyosema,“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana (wazi) ya mambo yasiyoonekana” Ebr 11:1
    4. Kuishi maisha ya unyenyekevu: “Dhabihu za Mungu ni mioyo iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka Ee Mungu hutaudharau. “Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuwaganga jeraha zao” Zab 51:17; 147:3. Mungu anahitaji watu waliovunjika na kupondeka moyo ili awaponye. Maana ya kuvunjika na kupondeka moyo ni kunyenyekea chini ya Mungu na kujua yeye ni mwenye uwezo na nguvu zote; kutokuwa na kiburi na kujiona wewe ni bora kuliko wengine, kutokuonee na kunyanyasa wengine, kutokujivunia ulivyo nayo na kujisifia kwa yale unayoyafanya na kutokudharau wengine au kuwapuuza. “Amdharauye mwenzake afanya dhambi;…” Mit 14:21. Yesu Kristo yeye ni mfano kwetu, alikuwa ni mnyenyekevu aliacha enzi na mamlaka aliyokuwa nayo mbinguni akaja duniani kwa namna ya mtumwa hakutaka makuu na fahari, alimtii Mungu.

    5. Kuomba kwa imani: “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa , tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba”Yoh 5:14-15. Haya maandiko yanafundisha ni muhimu kujua kwamba tunapomwomba Mungu anatuskia, tunapoomba sawaswa na mapenzi yake (neno lake). Pia kujua tulichoomba tunacho tayari. Kama umemwomba Mungu akuponye unajua umepona, hii ni imani katika Mungu. Ndiyo maana Yesu alifundisha akisema, “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaoombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” Mk 11:24.

    6. Kuomba kwa bidii: Kuomba kwa bidii bila kukata tamaa hadi Bwana akuponye kabisa. Iwapo umeomba lakini bado Bwana hajakuponya, endelea kunyenyeke na kumlilia tena na tena mpaka Bwana akuponye. Kuomba kwa bidii ni mfano wa mwanariadha anayeshindana na wanariadha kwa kukimbia. Mwanariada anayeshinda ni kwa sababu amekimbia kwa bidii na kupewa zawadi. Kuna mifano ya kufuata ya watumishi wa Mungu waliomwomba Mungu kwa bidii tena na tena wakajibiwa, mmojapo ni Eliya;
    “Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi; akainama uso mpaka magotini. Akamwambia mtumishi wake, kwea sasa ukatazame upande wa bahari. Akakwea na kutazama, akasema, hakuna kitu. Naye akanena, enenda tena mara saba. Ikawa mara ya saba akasema, tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. … Ikawa muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikawa mvua nyingi…” 1Fal 18:42-45. Hapa maandiko yanaonyesha jinsi Eliya alimwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili, wingu la mvua halikutokea lakini hakukata tamaa aliendelea kuomba mpaka mara ya saba wingu likaonekana na mvua ikanyesha. Na mwingine aliyeomba kwa bidii na kujibiwa ni Elisha baada ya kumtuma Gehazi mtumishi wake kumfufua mtoto.

    “Na Gehazi akawatagulia, akaiweka ile fimbo juu ya mtoto; lakini hapakuwa na sauti wala majibu. Basi Elisha alipofika nyumbani, tazama, mtoto amekwisha kufa, amelazwa kitandani pake. Basi akaingia ndani akajifungia mlango, yeye na Yule mtoto wote wawili, akamwomba Bwana... Kisha akarudi, akatembea nyumbani, huko Na huko mara moja; akapanda akajinyoosha juu yake; Na Yule mtoto akapiga chafya mara Saba, Na mtoto akafumbua macho yake.” 2 Fal 4:31-35. Elisha naye alimtuma mtumishi wake Gehazi akaiweke fimbo juu mtoto abaye alikuwa amekufa ili afufuke, wala hakufufuka, lakini Elisha hakukata tamaa alikwenda mwenyewe akamwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili na mtoto akafufuka.

    7. Kumshukuru Mungu: “Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” 1The 5:18. Katika maisha yetu ni muhimu tumshukuru Mungu kwa ajili ya mema yote anayotutende kila siku.

    Mungu ni mwaminifu.
    Yale yote aliyoyaahidi katika neno lake hakika atayafanya kama alivyosema; “Mimi sitalihalifu agano langu, sitalibadili Neno lililotoka midomoni mwangu.” Zab 89:34. “Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu” Kut 20:6. “Maana Kama vile mvua ishukavyo, Na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; Bali huinywesha ardhi, Na kuizalisha Na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, Na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure Bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma” Isa 55:10-11.

    USHUHUDA. Hapa ninatoa ushuhuda wa mtu ambaye Bwana amemponya mara nyingi kwa magonjwa tofauti. Siri ya uponyaji wake ni kwamba yeye ni mtakatifu amejilinda na kuepuka dhambi. kumbuka dhambi ni kizuizi cha uponyaji wa Mungu kwako. Amekuwa ni mwenye imani na unyenyekevu, amevunjika na kupondeka moyo. Wakati mwingine anapomwomba Mungu huanguka kifulifuli akimsihi Mungu. Hakika mtu kama huyu atasikilizwa kwa sababu anao ujasiri, hana dhambi inayomhukumu ndani ya moyo wake.

    Ndio maana imeandikwa “Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri (bila dhambi), ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.” Ebr 4:16. Mtu anapodumu katika maisha ya kumpendeza Mungu anapata neema au upendeleo kujibiwa maombi. Wakati mwingine hata kabla ya kuomba hujibiwa. “Na itakuwa kwamba, kabla ya kuomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.” Isa 65:24. “….maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.” Mt 6:8.
    UPONYAJI WA MAGONJWA. Chanzo cha magonjwa: Magonjwa yanatokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya mtu aliyekuwa mngonjwa alimwonya akisema, “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi” Yn 5:14. Mtu akiwa amefanya dhambi anapoumwa na kupimwa ugonjwa unaonekana. Iwapo akipimwa vipomo vyote na ugonjwa hauonekani yamkini ni pepo wachafu wamemwingia. “Mara huenda akachukua pamoja naye pepo wengine walio waovu kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya” Mt 12:45. Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili, unaotokana kukosa lishe ya mlo wa kila siku (Utapia mlo). Mapungufu katika mwili wa mwanadamu yanaweza yakawa ni kusudi la Mungu, ijapokuwa si yote. “Bwana akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani amfanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, Bwana? Kut 4:11. Kuponywa kwa dawa. Kwa kawaida kuna njia ambayo imekuwa ikitumika ya kutibu mangonjwa ambayo ni kutibu kwa kutumia dawa. Tiba za dawa zimekuwapo kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali. Mtu anapokuwa mgonjwa kuna hatua ya kuchukua, kwanza anaenda hospitali au kupelekwa kutona na hali yake hajiwezi. Daktari anampima na kufahamu ugonjwa alio nao, halafu anamwandikia dawa na maelekezo ya kuzitumia. Kama hatazingatia maelekezo na kuzitumia haiwezekani akapona. Hapa tunaweza kuona mgonjwa ili apone ni lazima azingatie maelekezo aliyopewa na daktari. Lakini baadhi ya magonjwa hayana tiba kama UKIMWI (HIV Aids). Hata hivyo usikate tamaa mwamini Mungu anaweza kukuponya kwa njia ya kumwomba. Atakuponya kwa neema, na rehema, kwa uwezo na nguvu zake.VIlevile kuna kanuni na maelekezo ya kufuata ili Mungu akuponye UPONYAJI WA MUNGU. Una maelekezo na kanuni za kufuata: 1. Kutubu na kuziacha dhambi: “Azifichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema” Mit 28:13. “Twajua ya kwamba Mungu hawasikii wenye dhambi;bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake huyo humsikia” Yn 9:31. 2. Kuishi maisha ya utakatifu: Ndio maana Mungu amesema; “Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako. Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote…” Kumb 7:12, 15. Katika maandiko haya tunaona Mungu alisema na baba zetu ya kwamba kwa upande wetu tunapozishika na kuzitenda hukumu zake (Sheria zake). Na kwa upande wake yeye ndipo hutuondolea ugonjwa wote. Kwa sababu Mungu aliwaapia baba zetu akisema, nitakutimizia agano na rehema. Kwa kiapo chake anathibitisha atafanya yale aliyoahidi katika Agano alilolifanya na baba zetu. Mahali pengine tunasoma: “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote,…Mche Bwana, ukajiepushe na uovu, Itakuwa afya mwilini pako. Na mafuta mifupani mwako. Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzishike kauli zangu. Kwa maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote”Mit 3:5,7,8. 3.Kumwamini Mungu na neno lake: Ndiyo maana Mungu alisema “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita roho yangu haina furaha naye.” Ebr 10:38. Kutokana na andiko hili, linaonyesha lazima mtu awe mwenye haki ndipo aweze kuishi kwa imani. Pia lazima kwanza kuamini moyoni na kuwa na uhakika Mungu atakuponya kama neno linavyosema,“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana (wazi) ya mambo yasiyoonekana” Ebr 11:1 4. Kuishi maisha ya unyenyekevu: “Dhabihu za Mungu ni mioyo iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka Ee Mungu hutaudharau. “Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuwaganga jeraha zao” Zab 51:17; 147:3. Mungu anahitaji watu waliovunjika na kupondeka moyo ili awaponye. Maana ya kuvunjika na kupondeka moyo ni kunyenyekea chini ya Mungu na kujua yeye ni mwenye uwezo na nguvu zote; kutokuwa na kiburi na kujiona wewe ni bora kuliko wengine, kutokuonee na kunyanyasa wengine, kutokujivunia ulivyo nayo na kujisifia kwa yale unayoyafanya na kutokudharau wengine au kuwapuuza. “Amdharauye mwenzake afanya dhambi;…” Mit 14:21. Yesu Kristo yeye ni mfano kwetu, alikuwa ni mnyenyekevu aliacha enzi na mamlaka aliyokuwa nayo mbinguni akaja duniani kwa namna ya mtumwa hakutaka makuu na fahari, alimtii Mungu. 5. Kuomba kwa imani: “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa , tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba”Yoh 5:14-15. Haya maandiko yanafundisha ni muhimu kujua kwamba tunapomwomba Mungu anatuskia, tunapoomba sawaswa na mapenzi yake (neno lake). Pia kujua tulichoomba tunacho tayari. Kama umemwomba Mungu akuponye unajua umepona, hii ni imani katika Mungu. Ndiyo maana Yesu alifundisha akisema, “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaoombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” Mk 11:24. 6. Kuomba kwa bidii: Kuomba kwa bidii bila kukata tamaa hadi Bwana akuponye kabisa. Iwapo umeomba lakini bado Bwana hajakuponya, endelea kunyenyeke na kumlilia tena na tena mpaka Bwana akuponye. Kuomba kwa bidii ni mfano wa mwanariadha anayeshindana na wanariadha kwa kukimbia. Mwanariada anayeshinda ni kwa sababu amekimbia kwa bidii na kupewa zawadi. Kuna mifano ya kufuata ya watumishi wa Mungu waliomwomba Mungu kwa bidii tena na tena wakajibiwa, mmojapo ni Eliya; “Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi; akainama uso mpaka magotini. Akamwambia mtumishi wake, kwea sasa ukatazame upande wa bahari. Akakwea na kutazama, akasema, hakuna kitu. Naye akanena, enenda tena mara saba. Ikawa mara ya saba akasema, tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. … Ikawa muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikawa mvua nyingi…” 1Fal 18:42-45. Hapa maandiko yanaonyesha jinsi Eliya alimwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili, wingu la mvua halikutokea lakini hakukata tamaa aliendelea kuomba mpaka mara ya saba wingu likaonekana na mvua ikanyesha. Na mwingine aliyeomba kwa bidii na kujibiwa ni Elisha baada ya kumtuma Gehazi mtumishi wake kumfufua mtoto. “Na Gehazi akawatagulia, akaiweka ile fimbo juu ya mtoto; lakini hapakuwa na sauti wala majibu. Basi Elisha alipofika nyumbani, tazama, mtoto amekwisha kufa, amelazwa kitandani pake. Basi akaingia ndani akajifungia mlango, yeye na Yule mtoto wote wawili, akamwomba Bwana... Kisha akarudi, akatembea nyumbani, huko Na huko mara moja; akapanda akajinyoosha juu yake; Na Yule mtoto akapiga chafya mara Saba, Na mtoto akafumbua macho yake.” 2 Fal 4:31-35. Elisha naye alimtuma mtumishi wake Gehazi akaiweke fimbo juu mtoto abaye alikuwa amekufa ili afufuke, wala hakufufuka, lakini Elisha hakukata tamaa alikwenda mwenyewe akamwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili na mtoto akafufuka. 7. Kumshukuru Mungu: “Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” 1The 5:18. Katika maisha yetu ni muhimu tumshukuru Mungu kwa ajili ya mema yote anayotutende kila siku. Mungu ni mwaminifu. Yale yote aliyoyaahidi katika neno lake hakika atayafanya kama alivyosema; “Mimi sitalihalifu agano langu, sitalibadili Neno lililotoka midomoni mwangu.” Zab 89:34. “Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu” Kut 20:6. “Maana Kama vile mvua ishukavyo, Na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; Bali huinywesha ardhi, Na kuizalisha Na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, Na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure Bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma” Isa 55:10-11. USHUHUDA. Hapa ninatoa ushuhuda wa mtu ambaye Bwana amemponya mara nyingi kwa magonjwa tofauti. Siri ya uponyaji wake ni kwamba yeye ni mtakatifu amejilinda na kuepuka dhambi. kumbuka dhambi ni kizuizi cha uponyaji wa Mungu kwako. Amekuwa ni mwenye imani na unyenyekevu, amevunjika na kupondeka moyo. Wakati mwingine anapomwomba Mungu huanguka kifulifuli akimsihi Mungu. Hakika mtu kama huyu atasikilizwa kwa sababu anao ujasiri, hana dhambi inayomhukumu ndani ya moyo wake. Ndio maana imeandikwa “Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri (bila dhambi), ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.” Ebr 4:16. Mtu anapodumu katika maisha ya kumpendeza Mungu anapata neema au upendeleo kujibiwa maombi. Wakati mwingine hata kabla ya kuomba hujibiwa. “Na itakuwa kwamba, kabla ya kuomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.” Isa 65:24. “….maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.” Mt 6:8.
    Love
    1
    0 Comments 2 Shares 9K Views 0 Reviews
Sponsored
[Repenting + Holiness = Entering Heaven / Kutubu + Utakatifu = Kuingia Mbinguni].