• Wanyama wanne wa Danieli 7

    Karibu tujifunze kitabu hiki cha Daniel sura ya 7 ili tupate kujua BWANA ALIMFUNULIA NINI DANIEL KATIKA NDOTO NA KWETU SISI INATUFUNULIA NINI.Basi andaa moyo wako kujifunza karibu sana

    Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danieli aliona ndoto na maono kuhusu wanyama wanne ambao ni falme au mataifa manne. Aliona pepo nne za mbinguni zikivuma juu ya bahari kubwa, kisha wanyama wanne wakubwa wenye sifa tofauti tofauti walitokea juu bahari. Baadaye, Danieli alitamani sana kujua maono hayo yalimaanisha nini, hivyo alimkaribia malaika Gabrieli aliyekuwa amesimama karibu naye ili amfahamishe ukweli wa maono hayo. Naye malaika akamfahamisha.

    Danieli 7:2 “Danieli akanena, akisema, Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa.”

    “Pepo” katika unabii hutumika kuwakirisha vita, tufani, au ghasia. Yeremia 25:32 inasema, “BWANA wa majeshi asema hivi, Tazama, uovu utatokea toka taifa hata taifa, na tufani kuu itainuliwa toka pande za mwisho wa dunia.” Katika Ufunuo 7:1-3 tunaona malaika wameamuriwa kuzishikilia “pepo” nne; yaani kuzuia vita hata Mungu atakapomaliza kuwatia mhuri watu wake. Hivyo upepo katika unabii = vita, tufani au dhoruba.

    “Bahari” au maji katika unabii hutumika kuwakilisha mataifa na watu, Ufunuo 7:15 inasema, “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.” [angalia pia Isaya 8:7].

    Danieli 7:3 “Ndipo wanyama wanne wakatokea baharini wote wa namna mbalimbali.”

    “Mnyama” katika unabii hutumika kuwakilisha taifa au ufalme, malaika katika Danieli 7:17 alipomfahamisha Danieli kuhusu maono haya, alisema, “Wanyama hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani.” Hivyo, wale wanyama wanne wa Danieli 7:3 wanaotokea baharini ni wafalme wanne watakaotokea miongoni mwa mataifa na watu (duniani). Bahari = watu.

    Danieli 7:4 “Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu.”

    Mnyama wa kwanza aliye kama simba kwa hakika ni ufalme wa Babeli, ambao ulikuwa ukitawala wakati wa nabii Danieli. Sifa za mnyama huyo za kuwa kama simba, na kuwa na mabawa kama ya tai, zinawakilisha kuwa ufalme huo ungekuwa na nguvu nyingi na mwepesi katika kufanya vita, hii ni sawa na ufalme wa Babeli wakati wa mfalme Nebukandreza. Yeremia alipotabiri juu ya Yerusalemu kuhusuliwa na Babeli, alitaja sifa za Babeli kama tai. Yeremia 4:7, 13 inasema, “Simba ametoka katika kichaka chake, ndiye aangamizaye mataifa;…Tazama atapanda juu kama mawingu, na magari yake ya vita yatakuwa kama kisulisuli; farasi zake ni wepesi kuliko tai…” Pia Habakuki 1:6, 8 inasema, “Kwa maana, angalieni, nawaondokeshea Wakalidayo, taifa lile kali, lenye haraka kupita kiasi; wapitao katikati ya dunia, ili wayamiliki makao yasiyo yao…wapanda farasi wao watoka mbali sana; huruka kama tai afanyaye haraka ale.” Hivyo, yule mnyama wa kwanza anawakilisha ufalme wa Babeli.

    Danieli 7:4 juu ya mnyama wa kwanza inasema, “…naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi…naye akapewa moyo wa kibinadamu.” Badiliko hili lililotokea la mabawa yake kufutuka manyoya na kupewa roho ya kibinaadamu, linawakilisha kupungua kwa nguvu na wepesi wa ufalme wa Babeli, kitu ambacho kilitokea baada ya mfalme Nebukandreza kupita, na ufalme ukawa dhaifu na usio na nguvu wakati wa utawala wa wafalme; Nabonadius and Belshaza.

    Danieli 7:5 “Na tazama, mnyama mwingine, wa pili, kama dubu, naye aliinuliwa upande mmoja, na mifupa mitatu ya mbavu ilikuwamo kinywani mwake katika meno yake; wakamwambia mnyama huyo hivi, Inuka, ule nyama tele.”

    Mnyama wa pili kwa hakika anawakilisha ufalme wa Umedi na Uajemi, ambao ulifuata baada ya ufalme wa Babeli kuanguka. Mnyama huyu aliye kama dubu, tena ameinuliwa upande mmoja, kwa hakika, ni ufalme uliokuwa na pande mbili “Umedi na Uajemi” ambapo upande mmoja wa Uajemi uliinuliwa zaidi kwa ukuu kuliko upande mwingine wa uamedi katika ufalme wa “Umedi&Uajemi. Zile mbavu tatu zilizo katika kinywa cha dubu, zinawakilisha nchi tatu Babeli, Lydia, na Misri ambazo zilihusuliwa na ufalme wa Umedi na uajemi.

    Danieli 7:6 “Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.”

    Mnyama wa tatu anawakilisha ufalme wa Ugiriki/Uyunani, ambao ulifuata baada ya ufalme wa Umedi na Uajemi kuanguka. Tafadhari kumbuka kuwa mnyama huyu wa tatu aliye kama chui, tena ana mabawa manne; angewakilisha taifa ambalo ni jepesi na la haraka zaidi kuliko taifa la Babeli ambalo lilikuwa na mabawa mawili pekee. Hii inawakilisha vizuri zaidi ufalme wa Ugiriki wakati ulipokuwa chini ya utawala wa Alexander, ufalme huo ulikuwa mwepesi na wa haraka sana katika kuhusuru miji, na uliyapanga majeshi yake kwa jinsi ambayo kamwe haifanani na nyakati zilizokuwa zimepita. Vile vichwa vinne vinawakilisha sehemu nne ambazo ufalme huo uligawanyika baada ya mfalme Alexander.

    Danieli 7:7 “Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.”

    Malaika Gabrieli katika Danieli 7:23 akimfafanulia Danieli ukweli kuhusu mnyama huyu wa nne alisema, “…Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia, utakaokuwa mbali na falme zile zote, nao utakula dunia yote, na kuikanyaga, na kuivunja vipande vipande.” Mnyama huyu wa nne anawakilisha ufalme wa Roma, uliofuta baada ya ufalme wa Ugiriki kuanguka. Ufalme huu unafananishwa na “chuma” ikimaanisha Jeshi lake ni katili na lenye nguvu nyingi sana. Danieli 7:7 inasema kuwa, ufalme huu wa Roma uko mbali/tofauti na falme zile tatu za Babeli, Umedi na Uajemi, na Ugiriki; Utofauti huo ni kwamba falme zile tatu zilikuwa falme za kipagani tu, lakini ufalme huu wa Roma ni mchanganyiko wa upagani na ukristo kwa wakati mmoja: yaan, upapa.

    Mnyama huyu wa nne ana pembe kumi kama Danieli 7:7 inavyomwelezea. Pembe katika unabii pia hutumika kuwakilisha ufalme au taifa, malaika Gabrieli katika Danieli 7:24 alipokuwa anamfahamisha Danieli ukweli kuhusu zile pembe kumi za yule mnyama wa nne, alisema, “Na habali za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.” Hivyo, zile pembe kumi za yule mnyama wa nne ambaye tumegundua kuwa ni Roma, pembe hizo ni mataifa kumi ambayo yapo katika ufalme wa Roma. Baada ya ufalme wa Roma ya kipagani kuanguka, katika mwaka 351 hadi 476 BK uligawanyika katika mataifa(pembe) kumi ambayo katika historia yamekuwa yakijulikana kama mataifa kumi ya Ulaya ya magharibi.

    Danieli 7:8 “Nikaziangalia sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang’olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu.”

    Malaika Gabrieli akifafanua kuhusu pembe hiyo ndogo itakayoinuka katika zile pembe kumi, katika Danieli 7:24 alisema, “Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.” Huko nyuma tumegundua kuwa zile pembe kumi za mnyama wa nne, zilizoorodheshwa katika Danieli 7:7 ni mataifa kumi ya Ulaya ya magharibi ambayo yaligawanyika katika ufalme wa Roma. Sasa katika Danieli 7:8 pembe nyingine ndogo ikainuka na ikang’oa pembe tatu katika zile pembe kumi.

    Katika Danieli 7:24 malaika akafafanua kuwa, ile pembe ndogo ni ufalme au taifa jingine dogo ambalo litatokea ndani ya ufalme huo wa Roma katika mataifa yale kumi au pembe kumi. Kisha taifa hilo dogo au pembe ndogo baada ya kutokea litaangusha mataifa matatu katika yale mataifa kumi ya mwanzo. Kwa hakika taifa hili dogo (au pembe ndogo) ni taifa dogo la Vatican(upapa) ambalo liliinuka baada ya mataifa yale kumi. Taifa dogo la Vatican(upapa) liliinuka kutoka katika taifa la Italia, na taifa la Italia ni moja wapo katika yale mataifa kumi ( pembe 10). Baada ya taifa la Vatican kuinuka liliyaondoa mataifa matatu katika yale mataifa kumi ya mwanzo, hii inaweza kufananishwa vizuri na ile pembe ndogo inayong’oa pembe tatu katika zile pembe kumi za mwanzo.

    Sababu ya taifa dogo la Vatican kuyaondoa mataifa matatu katika yale kumi ya mwanzo ni kwamba, taifa la Upapa(vatican) lilitaka kuyatawala yale mataifa kumi yote, lakini mataifa matatu yalikataa kujiweka chini ya utawala wa upapa, hivyo upapa ukafanya vita juu ya mataifa hayo matatu na kuyaondoa kabisa hata yasiwepo. Mataifa matatu yaliyoondolewa ni Heruli, liling’olewa na
    upapa mwaka 493 B.K.
    Vandal, liling’olewa na
    upapa mwaka 534 B.K.
    Ostrogoth, liling’olewa upapa mwaka 538 B.K.

    Ifuatayo ni orodha ya mataifa 10 ya ufalme wa Roma (au pembe 10 za mnyama), huku mataifa mataifa 3 yakiwa yameondolewa (au pembe tatu zikiwa zimeng’olewa) na utawala wa upapa (pembe ndogo).

    Saxon, kwa sasa ni
    taifa la Uingereza.

    Frank, kwa sasa ni
    taifa la Ufaransa.

    Alamanni, kwa sasa ni
    taifa la Ujerumani.

    Visigoth, kwa sasa ni
    taifa la Uhispania.

    Suevi, kwa sasa ni taifa
    la Ureno.

    Lombard, kwa sasa ni
    taifa la Italia.

    Burgundia, kwa sasa
    ni taifa la Uswidi.

    Heruli, liling’olewa na
    pembe ndogo 493 B.K.

    Vandal, liling’olewa na
    pembe ndogo 534 B.K.

    Ostrogoth,
    liling’olewa na pembe
    ndogo 538 B.K

    Ushahidi mwingine unaothibitisha kuwa ile pembe ndogo ya Daniel 7:8 ni utawala upapa, ni ushahidi unaopatikana katika Danieli 7:25 ambapo inasema,

    Danieli 7:25 “Naye (pembe ndogo) atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.”

    Hapa ushahidi usioweza kupingika ni swala la kubadili majira na sheria za Mungu, ni mamlaka ya upapa pekee ndiyo iliyobadili sheria za Mungu, Sabato kutoka siku ya saba(Jumamosi) kwenda siku ya kwanza (Jumapili).

    “Bila shaka kanisa la katoliki hudai kuwa badiliko, (la Sabato Jumamosi kwenda Jumapili) ilikuwa ni kitendo chake…na kitendo hicho ni ALAMA ya mamlaka yake katika mambo ya kidini.” –-H.F. Thomas, Chancellor of Cardinal Gibbons

    “Jumapili ni ALAMA yetu ya mamlaka…kanisa liko juu ya Biblia, na uhamishaji huu wa utunzaji wa Sabato ni ushahidi wa jambo hilo la ukweli.” -–Catholic Record of London, Ontario Sept 1, 1923.

    Pia Danieli 7:25 inasema, pembe ndogo atawadhoofisha watakatifu wa Mungu, nao watatiwa mikononi mwake kwa muda wa wakati mmoja, na nyakati mbili, na nusu wakati. Wakati mmoja = mwaka 1, nyakati mbili = miaka 2, na nusu wakati = nusu mwaka, (hivyo, 1+2+05=3.5 miaka 3 na nusu). Miaka 3 na nusu = miezi 42 au siku 1260.

    Katika unabii siku moja = mwaka 1, Ezekieli 4:6 inasema, “…siku arobaini, siku moja kwa mwaka mmoja, nimekuagiza.” Hesabu 14:34 pia inasema, “…siku arobaini kila siku kuhesabiwa mwaka…” Hivyo, kutokana na Ezekieli 4:6 na Hesabu 14:34, ni hakika kwamba siku 1260 ni sawa na miaka 1260 ambayo Upapa ungetawala na kuwadhofisha watakatifu.

    Historia inathibitisha kuwa Upapa ulipata nguvu kabisa kuanzia mwaka 538BK, baada ya kumaliza kuyang’oa mataifa 3, hivyo utawala rasmi wa upapa ulianza mwaka 538.

    “Vigillius…alikalia kiti cha upapa (538 B.K.) chini ya ulinzi wa jeshi la Belisarius.” –History of the Christian Church, Vol. 3, p. 327

    Hivyo, ukijumlisha ile miaka 1260 ambayo upapa ungewadhoofisha watakatifu katika mwaka 538BK, utapata mwaka 1798BK (538+1260=1798). Kwa hiyo upapa ungewadhoofisha watakatifu kuanzia mwaka 538BK, hadi 1798BK. Historia inathibitisha kabisa kuwa upapa uliwadhoofisha watakatifu tangu mwaka 538bk hadi 1798bk ambapo upapa ulipata jeraha la mauti.

    “Katika mwaka 1798 Jemedari Berthier aliingia Roma, akauondoa kabisa utawala wa upapa, na kuanzisha mwingine.” –Encyclopedia Britannica 1941 edition

    Upapa ulipoondolewa madarakani katika mwaka 1798BK, hapo ndipo mateso ya wakristo yalikoma vile vile kama Danieli 7:25 inavyosema. Kwa hakika hii ni miaka halisi 1260 au miaka ya kiunabii 3.5, au wakati, nyakati mbili, na nusu wakati ya Danieli 7:25.

    Historia inasema wazi kuwa Upapa uliwadhoofisha watakatifu kwa miaka 1260, hata kanisa la Romani Katoliki linakubali kuwa liliwatesa wakristo wakati huo wa zama za giza, na papa Yohane II mwaka 2000 alitubu dhambi ya kanisa ya kuua Wakristo zaidi ya milioni 100. Kifuatacho ni baadhi ya ushahidi unaothibitisha kuwa kanisa Katoliki liliua wtakatifu kama Danieli 7:25 inavyosema.

    “Kwa sababu ya kufundisha imani kinyume na mafundisho ya Roma, historia inaonyesha vifo vya wafia dini zaidi ya milioni 100” –Brief Bible Readings, p 16.

    “Katoliki ana baadhi ya sababu kwa upande wake wakati anapotoa adhabu kwa waasi wa kidini, kwa maana anajidaia jina la Ukristo kwake mwenyewe kwa kuzuia, na anajidai kufundisha kwamba uwepo wa Roho wa Mungu kamwe hautaondoka kwake…Siyo kosa zaidi kumuua mtu kwa sababu ya uasi wa kidini, kuliko kwa sababu ya uuaji,…[na] katika mambo mengi mateso kwa maoni ya kidini siyo tu kwamba yanaruhusiwa, lakini ni ya busara na ya lazima.” –The Lawfulnees of Persecution” in the Rambler, 4, June, 1849, pp 119, 126. (“The Rambler” lilikuwa ni gazeti la kila siku la Romani Katoliki lililochapishwa kuanzia mwaka 1848 hadi 1862).

    “Chini ya mawazo na desturi za kijerumani, mateso yalitumiwa kidogo kuanzia karne ya 9 hadi karne ya 12, lakini kwa uhuikaji wa sheria ya Romani mateso yalianzishwa tena katika karne ya 12…Katika mwaka 1252 (Papa) Innocent IV aliruhusu adhabu ya mateso juu ya waasi wa kidini kwa kutumia mamlaka ya kiserikali, na mateso yakaja kuwa na mahali palipojulikana katika utaribu wa mahakama ya kiuchunguzi.” –New Catholic Encyclopedia, arts. “Inquisition”, “Auto-da-Fe’,” na “Massacre of St Bartholomew’s Day.”

    Hukumu na ufalme wa watakatifu.

    Danieli 7:9 “Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mmoja wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao.”

    Danieli 7:10 “Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.”

    Hukumu ambayo inatajwa hapo ni hukumu ya upelelezi ambayo ilianza tarehe 22 Octoba 1844 mwishoni mwa Siku 2300 za kiunabii za Danieli 8:14. Katika mwaka 1844 ambapo Yesu alimaliza kazi yake ya Ukuhani katika chumba cha Patakatifu, na akahamia chumba cha Patakatifu mno kwa ajili ya kazi yake ya Upatanisho, vitabu vilifunuliwa kwa ajili ya kuanza hukumu. Na hukumu hiyo ilianza kwa waliokufa na itaendelea hata kwa walio hai ambao wamekuwa na nuru kuu lakini wakashindwa kuenenda katika nuru. Ukisoma vizuri katika Danieli 7:11, 26 utaona kuwa hukumu imethibitishwa juu ya mfumo wa Upapa na utawala wake wote wa Roma.

    Danieli 7:11 “Nikatazama wakati huo; kwa sababu ya sauti ya yale maneno makubwa iliyoyasema ile pembe(upapa); nalitazama hata mnyama(Roma) yule akauawa, mwili wake ukaharibiwa, akatolewa ateketezwe kwa moto.”

    Wakati malaika akimfahamisha Danieli juu ya hukumu itakayokuja juu ya upapa na juu ya dola na ufalme wote wa Roma, katika Danieli 7:26 alisema, “Lakini hukumu itawekwa, nao watamwondolea(pembe ndogo[upapa]) mamlaka yake, kuipoteza na kuiangamiza, hata milele.” Lakini kuhusu wale wanyama wengine watatu unabii unasema,

    Danieli 7:12 “Na kwa habari za wale wanyama wengine, walinyang’anywa mamlaka yao; walakini maisha yao yalidumishwa kwa wakati na majira.”

    Wanyama wale watatu walinyang’anywa mamlaka yao na mnyama wa nne ambaye ni ufalme wa Roma, lakini maisha yao yaliendelea kuwepo; kwa mfano, taifa la Babeli liliendelea kuishi mpaka sasa linajulikana kama taifa la Irak (Al Hillah), vile vile kwa Umedi na Uajemi, na Ugiriki. Mataifa haya yanaishi hata sasa lakini mamlaka yao walinyanganywa na dola la Roma.

    Tukiangalia wanyama wote wanne tunaona kama ifuatavyo:

    Mnyama=Ufalme.1.Babeli.2.Umedi/Uajemi.3.Ugiriki.4.Roma

    Mnyama wa nne ni ufalme wa nne na wa mwisho katika historia ya dunia, na ufalme huo ni Roma, una pembe kumi ambazo ni mataifa yake kumi, pia una pembe ndogo ambayo ni upapa. Je unapita muda mrefu kabla dunia haijaisha? Tuko katika nyakati za mwishoni kabisa za mnyama wa nne na wa mwisho. Na hivi karibuni Yesu atakuja na kuziangamiza falme zote na upapa, na kisha ataanzisha ufalme wake pamoja na watakatifu katika ulimwengu mpya, ambao hautakuwa na mwisho. Ni Yerusalemu mpya utakaoshuka kutoka juu mbinguni.

    Danieli 7:13 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu(Mwana wa Adamu) akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye.”

    Danieli 7:14 “Naye(Mwana wa Adam) akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.”

    Wakati umekaribia, naam, wakati umefika ambao Yesu atarudi duniani kuwachukua watakatifu wake, nao watatawala katika ufalme wake wa amani ambao uzuri wake hakuna mtu anayeweza kuuelezea, ni ufalme ambao si wa dunia hii bali wa ulimwengu mpya. Malaika akimfahamisha Danieli kuhusu mambo haya alisema,

    Danieli 7:27 “Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.”

    Danieli 7:22 “hata akaja huyo mzee wa siku, nao watakatifu wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia watakatifu waumiliki ufalme.”

    Danieli 7:28 “Huu ndio mwisho wa jambo lile. Nami, Danieli, fikira zangu zilinifadhaisha, na uso wangu ulinibadilika; lakini naliliweka jambo hilo moyoni mwangu.”

    Je ni upendo gani ambao Mungu ametupa kwa kutufunulia nyakati na majira ya mwisho wa ulimwengu? Hata kwa wale ambao hawaamini wanaweza kufunguliwa macho yao ili waone ni jinsi gani Yesu Kristo ni kweli na hakika, na kwamba nini tutakosa kama tusipomwamini Yeye. Leo ndiyo wakati wa kumtafuta Bwana kwa moyo wote, akili zote, na nguvu zote ili giza lisije kufika na kutukuta hatusitahili kuuingia ufalme wa Mungu. Ushauri wa Yesu ni kwamba, “kesheni na kuomba.”huku tukidumu katika utakatifu kwani tafsiri halisi ya kukesha maana yake tuwe macho kwakila jambo shetani asije akatuvamia tukaanguka dhambini hivyo jitenge na uovu.Haiwezekani kumuona Mungu pasipo utakatifu kwani utakatifu ndiyo njia tutakayopitia,ndiyo tiketi yakuingia katika ufalme wa Mungu.Isaya 35:8,Kumbuka Mungu anazuia mabaya yasiipate dunia na utawala mpinga Kristo kwaajili yakutukamilisha na kutupiga muhuri wake na muhuri huo ni wokovu kumpokea yeye na kumuamini na kumkiri yeye peke yake kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha yako.naye atakupa kipawa cha Roho mtakatifu atakaye kuwezesha kuishi kwa utakatifu hadi atakapo kuja.KUMBUKA HAKUNA MNYAMA MKUBWA NA WAKUTISHA KAMA DHAMBI RUMI YAKO YA LEO NI MOYO WAKO MWENYEWE,HIVYO ONDOA PICHA ZA KATOLIKI AKILINI MWAKO WEKA IMANI JUU YA YESU KRISTO KAMA UKISIKIA LEO ANABISHA BASI FUNGUA MOYO WAKO AINGIE NAYE ATAKUPA ZAWADI YA ROHO MTAKATIFU NA UZIMA WA MILELE UFUNUO 3:19-20.TAFUTA UBATIZO SAHIHI UKAZALIWE NA KUFUFULIWA NA KRISTO KIROHHO NA UKATISHWE NAYE MBINGUNI KWAANZIA SASA KIROHO.WAKOLOSAI 3:1-4,EFESO 2:4-7

    MUNGU AKUBARIKI SANA WEWE UTAKAYE SOMA UJUMBE HUU

    EV.GIDION LAIZER.
    NURU YA UPENDO ARUSHA

    Wanyama wanne wa Danieli 7 Karibu tujifunze kitabu hiki cha Daniel sura ya 7 ili tupate kujua BWANA ALIMFUNULIA NINI DANIEL KATIKA NDOTO NA KWETU SISI INATUFUNULIA NINI.Basi andaa moyo wako kujifunza karibu sana Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danieli aliona ndoto na maono kuhusu wanyama wanne ambao ni falme au mataifa manne. Aliona pepo nne za mbinguni zikivuma juu ya bahari kubwa, kisha wanyama wanne wakubwa wenye sifa tofauti tofauti walitokea juu bahari. Baadaye, Danieli alitamani sana kujua maono hayo yalimaanisha nini, hivyo alimkaribia malaika Gabrieli aliyekuwa amesimama karibu naye ili amfahamishe ukweli wa maono hayo. Naye malaika akamfahamisha. Danieli 7:2 “Danieli akanena, akisema, Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa.” “Pepo” katika unabii hutumika kuwakirisha vita, tufani, au ghasia. Yeremia 25:32 inasema, “BWANA wa majeshi asema hivi, Tazama, uovu utatokea toka taifa hata taifa, na tufani kuu itainuliwa toka pande za mwisho wa dunia.” Katika Ufunuo 7:1-3 tunaona malaika wameamuriwa kuzishikilia “pepo” nne; yaani kuzuia vita hata Mungu atakapomaliza kuwatia mhuri watu wake. Hivyo upepo katika unabii = vita, tufani au dhoruba. “Bahari” au maji katika unabii hutumika kuwakilisha mataifa na watu, Ufunuo 7:15 inasema, “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.” [angalia pia Isaya 8:7]. Danieli 7:3 “Ndipo wanyama wanne wakatokea baharini wote wa namna mbalimbali.” “Mnyama” katika unabii hutumika kuwakilisha taifa au ufalme, malaika katika Danieli 7:17 alipomfahamisha Danieli kuhusu maono haya, alisema, “Wanyama hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani.” Hivyo, wale wanyama wanne wa Danieli 7:3 wanaotokea baharini ni wafalme wanne watakaotokea miongoni mwa mataifa na watu (duniani). Bahari = watu. Danieli 7:4 “Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu.” Mnyama wa kwanza aliye kama simba kwa hakika ni ufalme wa Babeli, ambao ulikuwa ukitawala wakati wa nabii Danieli. Sifa za mnyama huyo za kuwa kama simba, na kuwa na mabawa kama ya tai, zinawakilisha kuwa ufalme huo ungekuwa na nguvu nyingi na mwepesi katika kufanya vita, hii ni sawa na ufalme wa Babeli wakati wa mfalme Nebukandreza. Yeremia alipotabiri juu ya Yerusalemu kuhusuliwa na Babeli, alitaja sifa za Babeli kama tai. Yeremia 4:7, 13 inasema, “Simba ametoka katika kichaka chake, ndiye aangamizaye mataifa;…Tazama atapanda juu kama mawingu, na magari yake ya vita yatakuwa kama kisulisuli; farasi zake ni wepesi kuliko tai…” Pia Habakuki 1:6, 8 inasema, “Kwa maana, angalieni, nawaondokeshea Wakalidayo, taifa lile kali, lenye haraka kupita kiasi; wapitao katikati ya dunia, ili wayamiliki makao yasiyo yao…wapanda farasi wao watoka mbali sana; huruka kama tai afanyaye haraka ale.” Hivyo, yule mnyama wa kwanza anawakilisha ufalme wa Babeli. Danieli 7:4 juu ya mnyama wa kwanza inasema, “…naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi…naye akapewa moyo wa kibinadamu.” Badiliko hili lililotokea la mabawa yake kufutuka manyoya na kupewa roho ya kibinaadamu, linawakilisha kupungua kwa nguvu na wepesi wa ufalme wa Babeli, kitu ambacho kilitokea baada ya mfalme Nebukandreza kupita, na ufalme ukawa dhaifu na usio na nguvu wakati wa utawala wa wafalme; Nabonadius and Belshaza. Danieli 7:5 “Na tazama, mnyama mwingine, wa pili, kama dubu, naye aliinuliwa upande mmoja, na mifupa mitatu ya mbavu ilikuwamo kinywani mwake katika meno yake; wakamwambia mnyama huyo hivi, Inuka, ule nyama tele.” Mnyama wa pili kwa hakika anawakilisha ufalme wa Umedi na Uajemi, ambao ulifuata baada ya ufalme wa Babeli kuanguka. Mnyama huyu aliye kama dubu, tena ameinuliwa upande mmoja, kwa hakika, ni ufalme uliokuwa na pande mbili “Umedi na Uajemi” ambapo upande mmoja wa Uajemi uliinuliwa zaidi kwa ukuu kuliko upande mwingine wa uamedi katika ufalme wa “Umedi&Uajemi. Zile mbavu tatu zilizo katika kinywa cha dubu, zinawakilisha nchi tatu Babeli, Lydia, na Misri ambazo zilihusuliwa na ufalme wa Umedi na uajemi. Danieli 7:6 “Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.” Mnyama wa tatu anawakilisha ufalme wa Ugiriki/Uyunani, ambao ulifuata baada ya ufalme wa Umedi na Uajemi kuanguka. Tafadhari kumbuka kuwa mnyama huyu wa tatu aliye kama chui, tena ana mabawa manne; angewakilisha taifa ambalo ni jepesi na la haraka zaidi kuliko taifa la Babeli ambalo lilikuwa na mabawa mawili pekee. Hii inawakilisha vizuri zaidi ufalme wa Ugiriki wakati ulipokuwa chini ya utawala wa Alexander, ufalme huo ulikuwa mwepesi na wa haraka sana katika kuhusuru miji, na uliyapanga majeshi yake kwa jinsi ambayo kamwe haifanani na nyakati zilizokuwa zimepita. Vile vichwa vinne vinawakilisha sehemu nne ambazo ufalme huo uligawanyika baada ya mfalme Alexander. Danieli 7:7 “Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.” Malaika Gabrieli katika Danieli 7:23 akimfafanulia Danieli ukweli kuhusu mnyama huyu wa nne alisema, “…Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia, utakaokuwa mbali na falme zile zote, nao utakula dunia yote, na kuikanyaga, na kuivunja vipande vipande.” Mnyama huyu wa nne anawakilisha ufalme wa Roma, uliofuta baada ya ufalme wa Ugiriki kuanguka. Ufalme huu unafananishwa na “chuma” ikimaanisha Jeshi lake ni katili na lenye nguvu nyingi sana. Danieli 7:7 inasema kuwa, ufalme huu wa Roma uko mbali/tofauti na falme zile tatu za Babeli, Umedi na Uajemi, na Ugiriki; Utofauti huo ni kwamba falme zile tatu zilikuwa falme za kipagani tu, lakini ufalme huu wa Roma ni mchanganyiko wa upagani na ukristo kwa wakati mmoja: yaan, upapa. Mnyama huyu wa nne ana pembe kumi kama Danieli 7:7 inavyomwelezea. Pembe katika unabii pia hutumika kuwakilisha ufalme au taifa, malaika Gabrieli katika Danieli 7:24 alipokuwa anamfahamisha Danieli ukweli kuhusu zile pembe kumi za yule mnyama wa nne, alisema, “Na habali za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.” Hivyo, zile pembe kumi za yule mnyama wa nne ambaye tumegundua kuwa ni Roma, pembe hizo ni mataifa kumi ambayo yapo katika ufalme wa Roma. Baada ya ufalme wa Roma ya kipagani kuanguka, katika mwaka 351 hadi 476 BK uligawanyika katika mataifa(pembe) kumi ambayo katika historia yamekuwa yakijulikana kama mataifa kumi ya Ulaya ya magharibi. Danieli 7:8 “Nikaziangalia sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang’olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu.” Malaika Gabrieli akifafanua kuhusu pembe hiyo ndogo itakayoinuka katika zile pembe kumi, katika Danieli 7:24 alisema, “Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.” Huko nyuma tumegundua kuwa zile pembe kumi za mnyama wa nne, zilizoorodheshwa katika Danieli 7:7 ni mataifa kumi ya Ulaya ya magharibi ambayo yaligawanyika katika ufalme wa Roma. Sasa katika Danieli 7:8 pembe nyingine ndogo ikainuka na ikang’oa pembe tatu katika zile pembe kumi. Katika Danieli 7:24 malaika akafafanua kuwa, ile pembe ndogo ni ufalme au taifa jingine dogo ambalo litatokea ndani ya ufalme huo wa Roma katika mataifa yale kumi au pembe kumi. Kisha taifa hilo dogo au pembe ndogo baada ya kutokea litaangusha mataifa matatu katika yale mataifa kumi ya mwanzo. Kwa hakika taifa hili dogo (au pembe ndogo) ni taifa dogo la Vatican(upapa) ambalo liliinuka baada ya mataifa yale kumi. Taifa dogo la Vatican(upapa) liliinuka kutoka katika taifa la Italia, na taifa la Italia ni moja wapo katika yale mataifa kumi ( pembe 10). Baada ya taifa la Vatican kuinuka liliyaondoa mataifa matatu katika yale mataifa kumi ya mwanzo, hii inaweza kufananishwa vizuri na ile pembe ndogo inayong’oa pembe tatu katika zile pembe kumi za mwanzo. Sababu ya taifa dogo la Vatican kuyaondoa mataifa matatu katika yale kumi ya mwanzo ni kwamba, taifa la Upapa(vatican) lilitaka kuyatawala yale mataifa kumi yote, lakini mataifa matatu yalikataa kujiweka chini ya utawala wa upapa, hivyo upapa ukafanya vita juu ya mataifa hayo matatu na kuyaondoa kabisa hata yasiwepo. Mataifa matatu yaliyoondolewa ni Heruli, liling’olewa na upapa mwaka 493 B.K. Vandal, liling’olewa na upapa mwaka 534 B.K. Ostrogoth, liling’olewa upapa mwaka 538 B.K. Ifuatayo ni orodha ya mataifa 10 ya ufalme wa Roma (au pembe 10 za mnyama), huku mataifa mataifa 3 yakiwa yameondolewa (au pembe tatu zikiwa zimeng’olewa) na utawala wa upapa (pembe ndogo). Saxon, kwa sasa ni taifa la Uingereza. Frank, kwa sasa ni taifa la Ufaransa. Alamanni, kwa sasa ni taifa la Ujerumani. Visigoth, kwa sasa ni taifa la Uhispania. Suevi, kwa sasa ni taifa la Ureno. Lombard, kwa sasa ni taifa la Italia. Burgundia, kwa sasa ni taifa la Uswidi. Heruli, liling’olewa na pembe ndogo 493 B.K. Vandal, liling’olewa na pembe ndogo 534 B.K. Ostrogoth, liling’olewa na pembe ndogo 538 B.K Ushahidi mwingine unaothibitisha kuwa ile pembe ndogo ya Daniel 7:8 ni utawala upapa, ni ushahidi unaopatikana katika Danieli 7:25 ambapo inasema, Danieli 7:25 “Naye (pembe ndogo) atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.” Hapa ushahidi usioweza kupingika ni swala la kubadili majira na sheria za Mungu, ni mamlaka ya upapa pekee ndiyo iliyobadili sheria za Mungu, Sabato kutoka siku ya saba(Jumamosi) kwenda siku ya kwanza (Jumapili). “Bila shaka kanisa la katoliki hudai kuwa badiliko, (la Sabato Jumamosi kwenda Jumapili) ilikuwa ni kitendo chake…na kitendo hicho ni ALAMA ya mamlaka yake katika mambo ya kidini.” –-H.F. Thomas, Chancellor of Cardinal Gibbons “Jumapili ni ALAMA yetu ya mamlaka…kanisa liko juu ya Biblia, na uhamishaji huu wa utunzaji wa Sabato ni ushahidi wa jambo hilo la ukweli.” -–Catholic Record of London, Ontario Sept 1, 1923. Pia Danieli 7:25 inasema, pembe ndogo atawadhoofisha watakatifu wa Mungu, nao watatiwa mikononi mwake kwa muda wa wakati mmoja, na nyakati mbili, na nusu wakati. Wakati mmoja = mwaka 1, nyakati mbili = miaka 2, na nusu wakati = nusu mwaka, (hivyo, 1+2+05=3.5 miaka 3 na nusu). Miaka 3 na nusu = miezi 42 au siku 1260. Katika unabii siku moja = mwaka 1, Ezekieli 4:6 inasema, “…siku arobaini, siku moja kwa mwaka mmoja, nimekuagiza.” Hesabu 14:34 pia inasema, “…siku arobaini kila siku kuhesabiwa mwaka…” Hivyo, kutokana na Ezekieli 4:6 na Hesabu 14:34, ni hakika kwamba siku 1260 ni sawa na miaka 1260 ambayo Upapa ungetawala na kuwadhofisha watakatifu. Historia inathibitisha kuwa Upapa ulipata nguvu kabisa kuanzia mwaka 538BK, baada ya kumaliza kuyang’oa mataifa 3, hivyo utawala rasmi wa upapa ulianza mwaka 538. “Vigillius…alikalia kiti cha upapa (538 B.K.) chini ya ulinzi wa jeshi la Belisarius.” –History of the Christian Church, Vol. 3, p. 327 Hivyo, ukijumlisha ile miaka 1260 ambayo upapa ungewadhoofisha watakatifu katika mwaka 538BK, utapata mwaka 1798BK (538+1260=1798). Kwa hiyo upapa ungewadhoofisha watakatifu kuanzia mwaka 538BK, hadi 1798BK. Historia inathibitisha kabisa kuwa upapa uliwadhoofisha watakatifu tangu mwaka 538bk hadi 1798bk ambapo upapa ulipata jeraha la mauti. “Katika mwaka 1798 Jemedari Berthier aliingia Roma, akauondoa kabisa utawala wa upapa, na kuanzisha mwingine.” –Encyclopedia Britannica 1941 edition Upapa ulipoondolewa madarakani katika mwaka 1798BK, hapo ndipo mateso ya wakristo yalikoma vile vile kama Danieli 7:25 inavyosema. Kwa hakika hii ni miaka halisi 1260 au miaka ya kiunabii 3.5, au wakati, nyakati mbili, na nusu wakati ya Danieli 7:25. Historia inasema wazi kuwa Upapa uliwadhoofisha watakatifu kwa miaka 1260, hata kanisa la Romani Katoliki linakubali kuwa liliwatesa wakristo wakati huo wa zama za giza, na papa Yohane II mwaka 2000 alitubu dhambi ya kanisa ya kuua Wakristo zaidi ya milioni 100. Kifuatacho ni baadhi ya ushahidi unaothibitisha kuwa kanisa Katoliki liliua wtakatifu kama Danieli 7:25 inavyosema. “Kwa sababu ya kufundisha imani kinyume na mafundisho ya Roma, historia inaonyesha vifo vya wafia dini zaidi ya milioni 100” –Brief Bible Readings, p 16. “Katoliki ana baadhi ya sababu kwa upande wake wakati anapotoa adhabu kwa waasi wa kidini, kwa maana anajidaia jina la Ukristo kwake mwenyewe kwa kuzuia, na anajidai kufundisha kwamba uwepo wa Roho wa Mungu kamwe hautaondoka kwake…Siyo kosa zaidi kumuua mtu kwa sababu ya uasi wa kidini, kuliko kwa sababu ya uuaji,…[na] katika mambo mengi mateso kwa maoni ya kidini siyo tu kwamba yanaruhusiwa, lakini ni ya busara na ya lazima.” –The Lawfulnees of Persecution” in the Rambler, 4, June, 1849, pp 119, 126. (“The Rambler” lilikuwa ni gazeti la kila siku la Romani Katoliki lililochapishwa kuanzia mwaka 1848 hadi 1862). “Chini ya mawazo na desturi za kijerumani, mateso yalitumiwa kidogo kuanzia karne ya 9 hadi karne ya 12, lakini kwa uhuikaji wa sheria ya Romani mateso yalianzishwa tena katika karne ya 12…Katika mwaka 1252 (Papa) Innocent IV aliruhusu adhabu ya mateso juu ya waasi wa kidini kwa kutumia mamlaka ya kiserikali, na mateso yakaja kuwa na mahali palipojulikana katika utaribu wa mahakama ya kiuchunguzi.” –New Catholic Encyclopedia, arts. “Inquisition”, “Auto-da-Fe’,” na “Massacre of St Bartholomew’s Day.” Hukumu na ufalme wa watakatifu. Danieli 7:9 “Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mmoja wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao.” Danieli 7:10 “Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.” Hukumu ambayo inatajwa hapo ni hukumu ya upelelezi ambayo ilianza tarehe 22 Octoba 1844 mwishoni mwa Siku 2300 za kiunabii za Danieli 8:14. Katika mwaka 1844 ambapo Yesu alimaliza kazi yake ya Ukuhani katika chumba cha Patakatifu, na akahamia chumba cha Patakatifu mno kwa ajili ya kazi yake ya Upatanisho, vitabu vilifunuliwa kwa ajili ya kuanza hukumu. Na hukumu hiyo ilianza kwa waliokufa na itaendelea hata kwa walio hai ambao wamekuwa na nuru kuu lakini wakashindwa kuenenda katika nuru. Ukisoma vizuri katika Danieli 7:11, 26 utaona kuwa hukumu imethibitishwa juu ya mfumo wa Upapa na utawala wake wote wa Roma. Danieli 7:11 “Nikatazama wakati huo; kwa sababu ya sauti ya yale maneno makubwa iliyoyasema ile pembe(upapa); nalitazama hata mnyama(Roma) yule akauawa, mwili wake ukaharibiwa, akatolewa ateketezwe kwa moto.” Wakati malaika akimfahamisha Danieli juu ya hukumu itakayokuja juu ya upapa na juu ya dola na ufalme wote wa Roma, katika Danieli 7:26 alisema, “Lakini hukumu itawekwa, nao watamwondolea(pembe ndogo[upapa]) mamlaka yake, kuipoteza na kuiangamiza, hata milele.” Lakini kuhusu wale wanyama wengine watatu unabii unasema, Danieli 7:12 “Na kwa habari za wale wanyama wengine, walinyang’anywa mamlaka yao; walakini maisha yao yalidumishwa kwa wakati na majira.” Wanyama wale watatu walinyang’anywa mamlaka yao na mnyama wa nne ambaye ni ufalme wa Roma, lakini maisha yao yaliendelea kuwepo; kwa mfano, taifa la Babeli liliendelea kuishi mpaka sasa linajulikana kama taifa la Irak (Al Hillah), vile vile kwa Umedi na Uajemi, na Ugiriki. Mataifa haya yanaishi hata sasa lakini mamlaka yao walinyanganywa na dola la Roma. Tukiangalia wanyama wote wanne tunaona kama ifuatavyo: Mnyama=Ufalme.1.Babeli.2.Umedi/Uajemi.3.Ugiriki.4.Roma Mnyama wa nne ni ufalme wa nne na wa mwisho katika historia ya dunia, na ufalme huo ni Roma, una pembe kumi ambazo ni mataifa yake kumi, pia una pembe ndogo ambayo ni upapa. Je unapita muda mrefu kabla dunia haijaisha? Tuko katika nyakati za mwishoni kabisa za mnyama wa nne na wa mwisho. Na hivi karibuni Yesu atakuja na kuziangamiza falme zote na upapa, na kisha ataanzisha ufalme wake pamoja na watakatifu katika ulimwengu mpya, ambao hautakuwa na mwisho. Ni Yerusalemu mpya utakaoshuka kutoka juu mbinguni. Danieli 7:13 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu(Mwana wa Adamu) akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye.” Danieli 7:14 “Naye(Mwana wa Adam) akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.” Wakati umekaribia, naam, wakati umefika ambao Yesu atarudi duniani kuwachukua watakatifu wake, nao watatawala katika ufalme wake wa amani ambao uzuri wake hakuna mtu anayeweza kuuelezea, ni ufalme ambao si wa dunia hii bali wa ulimwengu mpya. Malaika akimfahamisha Danieli kuhusu mambo haya alisema, Danieli 7:27 “Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.” Danieli 7:22 “hata akaja huyo mzee wa siku, nao watakatifu wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia watakatifu waumiliki ufalme.” Danieli 7:28 “Huu ndio mwisho wa jambo lile. Nami, Danieli, fikira zangu zilinifadhaisha, na uso wangu ulinibadilika; lakini naliliweka jambo hilo moyoni mwangu.” Je ni upendo gani ambao Mungu ametupa kwa kutufunulia nyakati na majira ya mwisho wa ulimwengu? Hata kwa wale ambao hawaamini wanaweza kufunguliwa macho yao ili waone ni jinsi gani Yesu Kristo ni kweli na hakika, na kwamba nini tutakosa kama tusipomwamini Yeye. Leo ndiyo wakati wa kumtafuta Bwana kwa moyo wote, akili zote, na nguvu zote ili giza lisije kufika na kutukuta hatusitahili kuuingia ufalme wa Mungu. Ushauri wa Yesu ni kwamba, “kesheni na kuomba.”huku tukidumu katika utakatifu kwani tafsiri halisi ya kukesha maana yake tuwe macho kwakila jambo shetani asije akatuvamia tukaanguka dhambini hivyo jitenge na uovu.Haiwezekani kumuona Mungu pasipo utakatifu kwani utakatifu ndiyo njia tutakayopitia,ndiyo tiketi yakuingia katika ufalme wa Mungu.Isaya 35:8,Kumbuka Mungu anazuia mabaya yasiipate dunia na utawala mpinga Kristo kwaajili yakutukamilisha na kutupiga muhuri wake na muhuri huo ni wokovu kumpokea yeye na kumuamini na kumkiri yeye peke yake kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha yako.naye atakupa kipawa cha Roho mtakatifu atakaye kuwezesha kuishi kwa utakatifu hadi atakapo kuja.KUMBUKA HAKUNA MNYAMA MKUBWA NA WAKUTISHA KAMA DHAMBI RUMI YAKO YA LEO NI MOYO WAKO MWENYEWE,HIVYO ONDOA PICHA ZA KATOLIKI AKILINI MWAKO WEKA IMANI JUU YA YESU KRISTO KAMA UKISIKIA LEO ANABISHA BASI FUNGUA MOYO WAKO AINGIE NAYE ATAKUPA ZAWADI YA ROHO MTAKATIFU NA UZIMA WA MILELE UFUNUO 3:19-20.TAFUTA UBATIZO SAHIHI UKAZALIWE NA KUFUFULIWA NA KRISTO KIROHHO NA UKATISHWE NAYE MBINGUNI KWAANZIA SASA KIROHO.WAKOLOSAI 3:1-4,EFESO 2:4-7 MUNGU AKUBARIKI SANA WEWE UTAKAYE SOMA UJUMBE HUU EV.GIDION LAIZER. NURU YA UPENDO ARUSHA
    Like
    4
    2 التعليقات 0 المشاركات 71كيلو بايت مشاهدة 0 معاينة
  • JE YESU WA WAKRISTO NDIYE YULE ISA WA WAISLAM?

    Mara kwa mara, unaweza kuwasikia Waislamu wakisema kuwa Isa a.s. kama anavyotajwa ndani ya Qur’an tukufu, ndiye Yesu Kristo wa Nazareti, kama anavyotajwa ndani ya Biblia Takatifu. Wanafanya hivyo kwa kulinganisha baadhi ya aya zilizomo ndani ya Biblia Takatifu, na zile zilizomo ndani ya Qur’an.

    Kwa mfano, wanasema kwa mujibu wa Biblia mama yake Yesu Kristo anaitwa Mariamu. Wanasoma katika Injili ya Marko 6:3-4“Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose na Yuda na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake” . Wanafananisha aya hiyo na ile iliyomo ndani ya Qur’an katika Suratul Al-Maidah, 5:75 “ Masih bin Maryam si chochote ila ni mtume tu……”,

    Hoja nyingine wanayoitumia ni kusema kwamba eti jina Isa ni katika lugha ya Kiarabu. Jambo hilo siyo kweli. Kwa sababu katika lugha ya Kiarabu, Yesu anaitwa Yasu’a siyo Isa. Na ikumbukwe kuwa Biblia ndicho kitabu kilichotangulia kuwepo duniani miaka ipatayo 1500 kabla ya Qur’an. Hoja yetu kwa Waislamu ni hii nani aliyebadilisha jina Yasu’a kuwa Isa?.

    Jina Yasu’a linashabihiana zaidi na Jina Yehoshua ambalo hilo ni katika lugha ya Kiebrania, na katika Kiyunani lugha iliyotumika kuandika Agano Jipya anaitwa Iesous (tamka Yesu) tafsiri ya maneno hayo kwa lugha ya Kiswahili ni Mwokozi. Tunasoma hayo katika Math 1:21-23 “ Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana yeye ndiye atakaye waokoa watu wake na dhambi zao.

    Hayo yote yamekuwa ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa Nabii akisema Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.” Hoja yetu Je Isa a.s naye ni Mwokozi na Imanueli kama alivyo Yesu Kristo? Jambo jingine tunalopaswa kulizingatia tunapoangalia tofauti zao ni kuhusu mama zao. Mama yake Yesu Kristo ni Mariam anayetoka katika ukoo wa Yuda. Tunasoma hayo katika kitabu cha Mwanzo 49:10 “ Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake,Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki,Ambaye mataifa watamtii”. Unabii huu umetimia kwa Yesu Kristo.

    Tunasoma hayo katika Waebrania 7:14 “Maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika Yuda, kabila ambayo Musa hakunena neno lolote juu yake katika mambo ya ukuhani” Lakini tusomapo habari za Isa, yeye mama yake anatoka ukoo wa Imrani. Ambaye ni baba yao Haruni, Miriamu na Musa. Tunayasoma hayo katika Suratul Al-Maryam 19:28 “Ewe dada yake Haruni. Baba yako hakuwa mtu mbaya. Wala mama yako hakuwa hasharati”.

    fafanuzi unaoifafanua aya hii ya 19:28 uliyomo ndani ya Qur’an, tafsiri ya King Fahd uk. 405, unasomeka hivi “ This Harun (Aaron) is not the brother of Musa (Moses), but he was another pious man at the time of Maryam (Mary)” Tafsiri “Huyu Harun siyo ndugu yake Musa, bali alikuwa ni mtu mwingine tu mcha Mungu, aliyeishi wakati wa kipindi cha Maryam” Kwa mujibu wa Biblia, Haruni ni mtoto wa mzee Amran na mama yao anaitwa Yekobedi na kwao wamezaliwa watoto watatu Haruni, Miriam na mdogo wao Musa. Tunasoma hayo katika kitabu cha Hesabu 26:59 “Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi binti wa Lawi ,ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amram Haruni,na Musa,na Miriamu umbu lao” Tofauti nyingine ni kuumbwa kwao:

    1) ISSA KAUMBWA. Qur’an Suratul Imran, 3:59 “ Bila shaka hali ya Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama hali ya Adam; alimwumba kwa udongo kisha akamwambia: “Kuwa”; basi akawa” Lakini tusomapo kumhusu YESU, YEYE HAKUUMBWA BALI NI NENO LA MUNGU. Yoh 1 : 1,14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu naye Neno alikuwa Mungu……..Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu…….” Mika 5:2 “ Bali wewe, Bethlehem Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israel; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele” Yoh: 8:58 “ Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahim asijakuwako, mimi niko”. Zaidi ya hayo Biblia inatujulisha kuwa yeye ndiye Muumbaji mwenyewe Yoh 1:3 “Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika” Kol 1:16-17 “ Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana ; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake”

    2) (A) ISSA A.S : BAADA YA KUONDOKA KWAKE, (KAMA WAISLAMU WANAVYOAMINI), HAJAWAHI KUTOKEA KWA NAMNA YOYOTE ILE. (B) YESU KRISTO: BAADA YA KUONDOKA KWAKE ALIMTOKEA PAUL (SAUL). Mdo 9:4 “ Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Saul, Saul, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema , Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe”

    3) (A) ISSA A.S: ALITABIRI KUJA KWA MUHAMMAD Quran Suratul As Saff , 61:6 “Na (wakumbushe) aliposema (Nabii) Isa bin Maryamu (kuwaambia mayahudi) enyi wana wa Israili! mimi ni mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu. Nisadikishaye yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati. Na kutoa habari njema ya mtume atakayewajia nyuma yangu ambaye jina lake litakuwa Ahmad(Muhammad). Na maana ya majina mawili yote haya ni moja. Maana yake Mwenye kushukuriwa kwa maneno yake mazuri na vitendo vyake vizuri na kila chake kwani vyake vyote ni vizuri).Lakini alipowajia kwa hoja zilizowazi walisema: “ Huu ni udanganyifu uliyo dhahiri”. (B)YESU KRISTO ALIMTUMA ROHO MTAKATIFU KATIKA SIKU YA PENTEKOSTE. Yoh: 14:26 “.Lakini huyo Msaidizi,huyo Roho Mtakatifu,ambaye Baba atampeleka kwa jina langu,atawafundisha yote,na kuwakumbusha yote niliyowaambia”. Katka Kiyunani anaitwa “Paracletos” yaani msaidizi au mfariji Yoh 15:26 “ Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia” Yoh 16:7 “Lakini mimi ninawaambia iliyo kweli; yawafaa nyinyi mimi niondoke,kwa maana mimi nisipoondoka huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu nitampeleka kwenu”.

    4) (A) ISSA A.S : JINA LAKE HALINA NGUVU WALA UWEZO WA KUOKOA BALI NI RANGI MBILI Katika Al-Lu’lu’war-Marjani, Juzuu na1, Hadithi na104 uk. 64 “ Hadithi ya Ibn Abbas (r.a) kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema, “Nilimuona Musa (a.s) katika usiku wa Al-Isra, niliopelekwa,naye ni mtu mrefu, mwenye nywele za hudhurungi zimejikunjakunja kama mtu wa Shanua.Na nilimuona Isa (a.s), naye ni mtu wa wastani wa umbo, unaelekea kwenye wekundu na weupe, ana nywele zilizonyooka……” (B) YESU KRISTO: JINA LAKE NI WOKOVU. Mdo 4:9-10,12 “ kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu,jinsi alivyoponywa, jueni nyinyi nyote na watu wote wa Israel ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye nyinyi mlimsulubisha, na Mungu alimfufua katika wafu kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu…………………….Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo” Baadhi ya aya ndani ya Qur’an zinaeleza kuwa Isa a.s aliwaponya wenye upofu. Ni akina nani hao tutajiwe angalau mmoja? Yesu alimponya kipofu Batromayo. Aya zingine zinasema Isa a.s alifufua wafu. Ni akina nani hao? Yesu alimfufua Lazaro. Jina tulilopewa ni jina moja tu lenye wokovu la Yesu Kristo. Jina la Isa a.s lisilo na wokovu limehusishwaje na jina la Yesu Kristo wa Nazareth lenye wokovu? Mdo 16:31 “ Wakamwambia , Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka wewe pamoja na nyumba yako.”

    5) (A) ISSA.A.S : YEYE SIYO MWANA WA MUNGU. Qur’ani Suratul Al An-Am,6:101 “Yeye ndiye Mwumba wa mbingu na ardhi. inamkinikanaje awe na mwana, hali hana mke. Naye ndiye aliye umba kila kitu (sio baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu”. Qurani Suratul At-Tawba (Kutubu), 9:30 “Na Mayahudi wanasema “Uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu” na “Wakristo wanasema “Masihi ni Mwana wa Mwenyezi Mungu” Haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasi na kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale waliokufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa! Fundisho la Uwana wa Mungu kama Biblia inavyofundisha, halimo katika mafundisho na itikadi ya dini ya Kiislamu kwa hiyo Isa a.s siyo mwana wa Mungu. (B) YESU KRISTO: YEYE NI MWANA WA MUNGU. Luka 1:30-31,35 “Malaika akamwambia usiogope Mariamu,kwa maana umepata neema kwa Mungu.Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Malaika akajibu akamwambia,Roho Mtakatifu atakujilia juu yako,na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli;kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu Mwana wa Mungu. Hivyo Isa siyo Mwana Mungu lakini Yesu ni mwana wa Mungu. Kwa hivyo Yesu siyo Isa. 6) (A) ISSA A.S: YEYE SIYO MUNGU ALIYEFANYIKA MWILI. Suratul Al- Maidah,(meza), 5:72-73 Bila ya shaka wamekufuru wale waliosema, “ Mwenyezi Mungu ni Masih (issa)bin Maryam”.(Na hali ya kuwa)Masihi alisema “Enyi wana wa Israel! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wenu. Kwani anayemshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahali pake (patakuwa) ni Motoni. Na madhalimu hawatakuwa na wasaidizi (wa kuwasaidia siku ya Kiama) “Kwa hakika wamekufuru wale waliosema mwenyenzi Mungu ni mmoja katika (wale waungu) watatu (yeye ndiye watatu wao ) hali hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu mmoja ( tu peke yake) na kama hawataacha hayo wasemayo kwa yakini itawakamata wale wanaoendelea na ukafiri miongoni mwao adhabu iumizayo”. (B)YESU YEYE NI NENO LA MUNGU LILILOFANYIKA MWILI: Yoh 1 : 1,14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu naye Neno alikuwa Mungu……..Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu…….”

    7) (A) ISSA A.S YEYE HAJAWAHI KUSULUBIWA WALA KUUWAWA Qurani Suratul An-Nisaa (Wanawake) 4:157-158 “Na kwa (ajili ya )kusema kwao sisi tumemuua masihi Isa mwana wa Maryamu, mtume wa Mungu. Hali hawakumuua wala hawakumsulubu bali walibabaishiwa (mtu mwingine wakamdhani nabii Isa.) Na kwa hakika wale waliokhitalifiana katika (hakika)hiyo (ya kumuua nabii Isa) wamo katika shaka nalo (jambo hilo kusema kauwawa]. Wao (kabisa) hawana yakini juu ya (jambo)hili (la kuwa kweli wamemuua nabii isa) isipokuwa wanafuata dhana tu.Na kwa yakini hawakumuua. Bali mwenyenzi Mungu alimnyanyua kwake. Na mwenyenzi Mungu ni mwenye nguvu (na)mwenye hikima. (B)YESU KRISTO: YEYE ALISULUBIWA MSALABANI Yohana 19:18,31,33 “Wakamsulibisha huko,na wengine wawili pamoja,mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati.Basi Wayahudi, kwa sababu ni Maandalio, miili isikae juu ya misalaba siku ya sabato(maana sabato ile ilikuwa siku kubwa), walimwomba Pilato miguu yao ivunjwe,wakaondolewe. Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa,hawakumvunja miguu”.

    8) (A) ISSA A.S HANA HADHI YA KUABUDIWA NA BINADAMU YEYOTE. Qur’an, Suratul Al-Maidah, 5:116 “ Na (kumbukeni) Mwnyezi Mungu atakaposema: “Ewe Isa bin Maryam! Je ,wewe uliwaambia watu: ‘Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu’?” Aseme (Nabii Isa): “Wewe umetakasika na kuwa na mshirika, hainijuzii mimi kusema ambayo si haki yangu (kuyasema, kwa kuwa ni ya uongo), kama ningalisema bila shaka ungalijua ; unayajua yaliyomo nafsini mwangu, lakini mimi siyajui yaliyomo nafsini mwako; hakika Wewe ndiye ujuaye mambo ya ghaibu. B) YESU ANASTAHILI KUABUDIWA NA WANADAMU NA MALAIKA Math 2: 2 “yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? kwa maana tuliiona nyota yake mashariki nasi tumekuja kumsujudia.” Yoh 9: 35 “ Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu? Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini? Yesu akamwambia Umemwona, naye anayesema nawe ndiye. Akasema, naamini, Bwana, akamsujudia.” Filipi 2:10-11 “ili kwa Jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.” Ebr 1:6 “ Hata tena amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu Malaika wote wa Mungu.

    9) (A) ISA HASTAHILI KUWA MWOMBEZI WA WATU KWA MUNGU Sahih Al-Bukhari, vol.6 ,Hadithi no 3, The Noble Qur’an, English Translation uk. 8 “…….Nenda kwa Musa, mtumishi wa Allah ambaye Allah alizungumza naye uso kwa uso na alimpa Torati. Hivyo watakwenda kwake naye atasema ‘ Mimi sistahili kwa jukumu hilo la uombezi, na atataja mauaji aliyoyafanya kwa mtu ambaye si muuaji, na hivyo atajisikia aibu mbele ya Mola wake, naye atasema nendeni kwa Isa, mtumishi wa Allah, Mjumbe wake neno lake na roho iliyotoka kwake. Isa atasema sistahili mimi kubeba jukumu la uombezi…….” B) YESU ANASTAHILI KUWA MWOMBEZI WA WANADAMU KWA MUNGU 1 Tim 2:5 “ Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;” Ebr 7:24-25 “ bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.Naye, kwa sababu hii , aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu Hai siku zote ili awaombee.

    10) (a) ISA NI NABII MWINGINE TU ASIYE TOFAUTI NA WENGINE Qur’an Suratul Baqarah, (ng’ombe)2:136 “ “Semeni nyinyi (Waislamu waambiwe Mayahudi na Manasara; waambieni): “Tumemwamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa, na yale yaliyoteremshwa kwa Ibrahimu na Ismail na Is-haqa na Yaaqubu na kizazi (chake Yaaqubu); na waliyopewa Musa na Isa na pia yale waliyopewa Manabii (wengine) kutoka kwa Mola wao; hatutofautishi baina ya yoyote katika hao. (Wote tunawaamini); na sisi tumenyenyekea Kwake.” b) YESU YEYE YU JUU KULIKO VITU VYOTE Efeso 1:20-23 “ aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na malaika, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya Kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.”

    11) (a) ISA ATAKAPORUDI, ATAOA NA KUZAA WATOTO Mishkat Al- Masabih, vol 2 uk.1159, Sahih Muslim, vol. 1 uk 92 “ Isa atakaporudi ataishi miaka arobaini (40), muda ambao atakuwa ameoa na kuzaa watoto, na atafanya ibada ya hija.” b) YESU ATAKAPORUDI ATAKUJA KULINYAKUA KANISA, YAANI BIBI ARUSI Efeso 5:25-26, 32-33 “ Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, Uf 19:7 “ Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana Kondoo imekuja na mkewe amejiweka tayari.akajitoa kwa ajili yake, ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;…..Siri hiyo ni kubwa ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mmewe.”

    12)(a) ISA ATAKUFA BAADA YA KUISHI MIAKA AROBAINI (40) Mishkat Al- Masabih, vol 2 uk. 1159,Sunan Abu Dawud, Hadithi 4310, Sahih Muslim, vol.1, uk.92 , “Isa atakaporudi ataondosha dini zote zisiwepo isipokuwa Uislamu. Atamharibu Masih Dajjal, na ataishi duniani miaka arobaini (40) na kisha atakufa. Na baada ya kufa atazikwa pembeni mwa kaburi la Muhammad.” B) YESU BAADA YA KUFUFUKA YU HAI SIKU ZOTE HAFI TENA Rum 6:9 “ tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena.” Ebr 7:24-25 “ bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.Naye, kwa sababu hii , aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu Hai siku zote ili awaombee.” Uf 1:17-18 “ Nami nilipomwona nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, mimi ni wa kwanza na wa mwisho, aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama , ni hai hata milele na milele nami ninazo funguo za mauti na za kuzimu.”

    13)(a) ISA ALIPOZALIWA SAUTI YA FARAJA ILITOKA CHINI YA ARDHI Qur’an Suratul Maryam,19:23-24 “ Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, (akawa anazaa na huku) anasema: “ Laiti ningekufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa.” Mara ikamfikia sauti kutoka chini yake (inamwambia): usihuzunike. Hakika Mola wako amejaalia (ameweka) kijito cha maji chini yako;” Mafundisho ya Kiislamu yanaeleza kuwa huko chini ya ardhi kuna mnyama. Na huyo mnyama anazijua aya za Qur’an. Qur’an katika Suratul Al-Naml, 27:82 “Na kauli (ya kuja kiyama) itakapowathibitikia Tutawatolea mnyama katika ardhi atakayewasemeza kwa sababu watu walikuwa hawaziyakinishi Aya Zetu” b) ALIPOZALIWA YESU SAUTI ZA MALAIKA ZILITOKA JUU Luka 2:13-16 “ Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Ikawa malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika alilotujulisha Bwana. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini”

    (14)(a) ISA HANA UFAHAMU WA MAMBO MBALIMBALI katika Al-Lu’lu’ war- Marjan,kitabu cha 3 Hadithi na 1528 uk.883 “Hadithi ya Abu Huraira (r.a) kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema “Issa Ibn Mariam (a,s) alimwona mtu anaiba akamuuliza umeiba? akasema hapana ,Naapa kwa Allah ambaye hakuna mola isipokuwa yeye .Issa (a.s) akasema nimemuamini Allah na limeniongopea jicho langu”. b) YESU ANAYAJUA YOTE Yohana 1:47-48 “ Basi Yesu akamwona Nathanael anakuja kwake, akanena habari zake “Tazama Mwizraeli kweli kweli hamna hila ndani yake. Nathaeli akamwambia umepataje kunitambua? Yesu akajibu akamwambia, Kabla Filipo hajakuita ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona” Yoh 2:24-25 “ Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe aliyajua yaliyomo ndani ya mwanadamu”

    15) (a) ISA A.S MAMA YAKE ALIKUTWA PEMBEZONI MWA MSIKITI ALIPOLETEWA HABARI ZA KUZALIWA KWAKE. Qur’an Suratul Maryam,19:16-17 “ Na mtaje Mariamu kitabuni humu. Alipojitenga na jamaa zake, (akenda) mahali upande wa mashariki (wa msikiti) na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea muhuisha Sharia Yetu (Jibrili)- akajimithilisha kwake (kwa sura ya) binadamu aliye kamili b) YESU KRISTO, MAMA YAKE ALIKUTWA NYUMBANI KWAO NAZARETI Luka 1:26-28 “Mwezi wa sita malaika Gabriel alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti. Kwa mwana mwali Bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yusufu wa mbari ya Daudi. Na jina lake Bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, salamu uliyepewa neema Bwana yu pamoja nawe.”

    16)(a) MIMBA YA ISA ILIKUWA NI YA SIKU MOJA Qur’an Suratul Maryam,19:21-22 “ (Malaika) akasema: “ Nikama hivyo (unavyosema; lakini) Mola wako amesema ‘Haya ni sahali Kwangu, na ili Tumfanye muujiza kwa wanaasamu na rehema itokayo Kwetu (ndiyo Tumefanya hivi);’ Na hili ni jambo lililokwisha kuhukumiwa.” Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali” b) MIMBA YA YESU SIKU ZILITIMIA. Luka 2:6-7 “ ikawa, katika kukaa huko, siku zake za kuzaa zikatimia, akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika hori ya kulia ng’ombe kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni” NB: Mwezi wa sita uliotajwa katika Luka 1:26 ni mwezi wenye kuelezea umri wa mimba ya Yohana ndani ya tumbo la Elizabethi. Luka 1: 36 “ Tena tazama jamaa yako Elizabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa” NB: Hori iliyotajwa hapa,ina maana ya chombo cha kulishia wanyama kinachokuwa ndani ya zizi. Kwa Kiyunani (Kigiriki) ambayo ndiyo lugha iliyotumika kuandikia Agano Jipya ,chombo hicho kinaitwa “Fatne” kwa Kiingereza kinaitwa “a manger”

    17)ISA (A.S) ATAKAPORUDI ATAKUJA KUVUNJA MISALABA NA KUUA NGURUWE Mkweli Mwaminifu, Juzuu 3-4, uk.20, Hadithi na. 753 “ Haisimami saa ya (kiyama) mpaka akuteremkieni nabii Isa (a.s) mwana wa Maryamu atahukumu (kwa sheria ya Kiislamu) (na) muadilifu, basi atavunja misalaba (ya Wakristo Makanisani) na ataua nguruwe, na ataondosha fedheha au (aibu), na mali itazidi kuwa nyingi sana mpaka hataikubali (ataikataa) mtu (kwa kuogopa kiyama)” .Soma pia katika Sahihi Bukhar, vol. 3, Hadithi na 425,. Al-Lu’lu’war-Marjan, juzuu ya 1,Hadithi na 95 uk.51. The Noble Qur’an uk.757 b)YESU KRISTO ATAKAPORUDI ATAWATUMA MALAIKA ZAKE KUWAKUSANYA WATAKATIFU Luka 24:30-31 “ ndipo itakapoonekana ishara ya mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi, naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu.” ONYO LA YESU KRISTO WA NAZARETH Math 24:24 “ kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini hata walio wateule.” (Angalia pia Marko 13:22) Yoh 8:24 “ Kwa hiyo naliwambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye mtakufa katika dhambi zenu.”

    WEWE MTEULE JE UTADANGANYWA NA KUDANGANYIKA KUWA KWELI ISA A.S NDIYE YESU KRISTO? UKIAMINI HIVYO UTAKUWA UMEDANGANYIKA NA UTAKOSA WOKOVU WA MWENYEZI MUNGU!!!!!!!!!! YESU KRISTO, YEYE NI IMMANUEL, MSHAURI WA AJABU, MUNGU MWENYE NGUVU, BABA WA MILELE, MFALME WA AMANI!!!! (ISAYA 9:6, MATH 1:23) HIZI SIYO SIFA ZA Shkhê Êdén Hãzãrd kwa Max Shimba Ministries
    JE YESU WA WAKRISTO NDIYE YULE ISA WA WAISLAM? Mara kwa mara, unaweza kuwasikia Waislamu wakisema kuwa Isa a.s. kama anavyotajwa ndani ya Qur’an tukufu, ndiye Yesu Kristo wa Nazareti, kama anavyotajwa ndani ya Biblia Takatifu. Wanafanya hivyo kwa kulinganisha baadhi ya aya zilizomo ndani ya Biblia Takatifu, na zile zilizomo ndani ya Qur’an. Kwa mfano, wanasema kwa mujibu wa Biblia mama yake Yesu Kristo anaitwa Mariamu. Wanasoma katika Injili ya Marko 6:3-4“Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose na Yuda na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake” . Wanafananisha aya hiyo na ile iliyomo ndani ya Qur’an katika Suratul Al-Maidah, 5:75 “ Masih bin Maryam si chochote ila ni mtume tu……”, Hoja nyingine wanayoitumia ni kusema kwamba eti jina Isa ni katika lugha ya Kiarabu. Jambo hilo siyo kweli. Kwa sababu katika lugha ya Kiarabu, Yesu anaitwa Yasu’a siyo Isa. Na ikumbukwe kuwa Biblia ndicho kitabu kilichotangulia kuwepo duniani miaka ipatayo 1500 kabla ya Qur’an. Hoja yetu kwa Waislamu ni hii nani aliyebadilisha jina Yasu’a kuwa Isa?. Jina Yasu’a linashabihiana zaidi na Jina Yehoshua ambalo hilo ni katika lugha ya Kiebrania, na katika Kiyunani lugha iliyotumika kuandika Agano Jipya anaitwa Iesous (tamka Yesu) tafsiri ya maneno hayo kwa lugha ya Kiswahili ni Mwokozi. Tunasoma hayo katika Math 1:21-23 “ Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana yeye ndiye atakaye waokoa watu wake na dhambi zao. Hayo yote yamekuwa ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa Nabii akisema Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.” Hoja yetu Je Isa a.s naye ni Mwokozi na Imanueli kama alivyo Yesu Kristo? Jambo jingine tunalopaswa kulizingatia tunapoangalia tofauti zao ni kuhusu mama zao. Mama yake Yesu Kristo ni Mariam anayetoka katika ukoo wa Yuda. Tunasoma hayo katika kitabu cha Mwanzo 49:10 “ Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake,Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki,Ambaye mataifa watamtii”. Unabii huu umetimia kwa Yesu Kristo. Tunasoma hayo katika Waebrania 7:14 “Maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika Yuda, kabila ambayo Musa hakunena neno lolote juu yake katika mambo ya ukuhani” Lakini tusomapo habari za Isa, yeye mama yake anatoka ukoo wa Imrani. Ambaye ni baba yao Haruni, Miriamu na Musa. Tunayasoma hayo katika Suratul Al-Maryam 19:28 “Ewe dada yake Haruni. Baba yako hakuwa mtu mbaya. Wala mama yako hakuwa hasharati”. fafanuzi unaoifafanua aya hii ya 19:28 uliyomo ndani ya Qur’an, tafsiri ya King Fahd uk. 405, unasomeka hivi “ This Harun (Aaron) is not the brother of Musa (Moses), but he was another pious man at the time of Maryam (Mary)” Tafsiri “Huyu Harun siyo ndugu yake Musa, bali alikuwa ni mtu mwingine tu mcha Mungu, aliyeishi wakati wa kipindi cha Maryam” Kwa mujibu wa Biblia, Haruni ni mtoto wa mzee Amran na mama yao anaitwa Yekobedi na kwao wamezaliwa watoto watatu Haruni, Miriam na mdogo wao Musa. Tunasoma hayo katika kitabu cha Hesabu 26:59 “Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi binti wa Lawi ,ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amram Haruni,na Musa,na Miriamu umbu lao” Tofauti nyingine ni kuumbwa kwao: 1) ISSA KAUMBWA. Qur’an Suratul Imran, 3:59 “ Bila shaka hali ya Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama hali ya Adam; alimwumba kwa udongo kisha akamwambia: “Kuwa”; basi akawa” Lakini tusomapo kumhusu YESU, YEYE HAKUUMBWA BALI NI NENO LA MUNGU. Yoh 1 : 1,14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu naye Neno alikuwa Mungu……..Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu…….” Mika 5:2 “ Bali wewe, Bethlehem Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israel; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele” Yoh: 8:58 “ Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahim asijakuwako, mimi niko”. Zaidi ya hayo Biblia inatujulisha kuwa yeye ndiye Muumbaji mwenyewe Yoh 1:3 “Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika” Kol 1:16-17 “ Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana ; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake” 2) (A) ISSA A.S : BAADA YA KUONDOKA KWAKE, (KAMA WAISLAMU WANAVYOAMINI), HAJAWAHI KUTOKEA KWA NAMNA YOYOTE ILE. (B) YESU KRISTO: BAADA YA KUONDOKA KWAKE ALIMTOKEA PAUL (SAUL). Mdo 9:4 “ Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Saul, Saul, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema , Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe” 3) (A) ISSA A.S: ALITABIRI KUJA KWA MUHAMMAD Quran Suratul As Saff , 61:6 “Na (wakumbushe) aliposema (Nabii) Isa bin Maryamu (kuwaambia mayahudi) enyi wana wa Israili! mimi ni mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu. Nisadikishaye yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati. Na kutoa habari njema ya mtume atakayewajia nyuma yangu ambaye jina lake litakuwa Ahmad(Muhammad). Na maana ya majina mawili yote haya ni moja. Maana yake Mwenye kushukuriwa kwa maneno yake mazuri na vitendo vyake vizuri na kila chake kwani vyake vyote ni vizuri).Lakini alipowajia kwa hoja zilizowazi walisema: “ Huu ni udanganyifu uliyo dhahiri”. (B)YESU KRISTO ALIMTUMA ROHO MTAKATIFU KATIKA SIKU YA PENTEKOSTE. Yoh: 14:26 “.Lakini huyo Msaidizi,huyo Roho Mtakatifu,ambaye Baba atampeleka kwa jina langu,atawafundisha yote,na kuwakumbusha yote niliyowaambia”. Katka Kiyunani anaitwa “Paracletos” yaani msaidizi au mfariji Yoh 15:26 “ Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia” Yoh 16:7 “Lakini mimi ninawaambia iliyo kweli; yawafaa nyinyi mimi niondoke,kwa maana mimi nisipoondoka huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu nitampeleka kwenu”. 4) (A) ISSA A.S : JINA LAKE HALINA NGUVU WALA UWEZO WA KUOKOA BALI NI RANGI MBILI Katika Al-Lu’lu’war-Marjani, Juzuu na1, Hadithi na104 uk. 64 “ Hadithi ya Ibn Abbas (r.a) kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema, “Nilimuona Musa (a.s) katika usiku wa Al-Isra, niliopelekwa,naye ni mtu mrefu, mwenye nywele za hudhurungi zimejikunjakunja kama mtu wa Shanua.Na nilimuona Isa (a.s), naye ni mtu wa wastani wa umbo, unaelekea kwenye wekundu na weupe, ana nywele zilizonyooka……” (B) YESU KRISTO: JINA LAKE NI WOKOVU. Mdo 4:9-10,12 “ kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu,jinsi alivyoponywa, jueni nyinyi nyote na watu wote wa Israel ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye nyinyi mlimsulubisha, na Mungu alimfufua katika wafu kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu…………………….Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo” Baadhi ya aya ndani ya Qur’an zinaeleza kuwa Isa a.s aliwaponya wenye upofu. Ni akina nani hao tutajiwe angalau mmoja? Yesu alimponya kipofu Batromayo. Aya zingine zinasema Isa a.s alifufua wafu. Ni akina nani hao? Yesu alimfufua Lazaro. Jina tulilopewa ni jina moja tu lenye wokovu la Yesu Kristo. Jina la Isa a.s lisilo na wokovu limehusishwaje na jina la Yesu Kristo wa Nazareth lenye wokovu? Mdo 16:31 “ Wakamwambia , Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka wewe pamoja na nyumba yako.” 5) (A) ISSA.A.S : YEYE SIYO MWANA WA MUNGU. Qur’ani Suratul Al An-Am,6:101 “Yeye ndiye Mwumba wa mbingu na ardhi. inamkinikanaje awe na mwana, hali hana mke. Naye ndiye aliye umba kila kitu (sio baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu”. Qurani Suratul At-Tawba (Kutubu), 9:30 “Na Mayahudi wanasema “Uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu” na “Wakristo wanasema “Masihi ni Mwana wa Mwenyezi Mungu” Haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasi na kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale waliokufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa! Fundisho la Uwana wa Mungu kama Biblia inavyofundisha, halimo katika mafundisho na itikadi ya dini ya Kiislamu kwa hiyo Isa a.s siyo mwana wa Mungu. (B) YESU KRISTO: YEYE NI MWANA WA MUNGU. Luka 1:30-31,35 “Malaika akamwambia usiogope Mariamu,kwa maana umepata neema kwa Mungu.Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Malaika akajibu akamwambia,Roho Mtakatifu atakujilia juu yako,na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli;kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu Mwana wa Mungu. Hivyo Isa siyo Mwana Mungu lakini Yesu ni mwana wa Mungu. Kwa hivyo Yesu siyo Isa. 6) (A) ISSA A.S: YEYE SIYO MUNGU ALIYEFANYIKA MWILI. Suratul Al- Maidah,(meza), 5:72-73 Bila ya shaka wamekufuru wale waliosema, “ Mwenyezi Mungu ni Masih (issa)bin Maryam”.(Na hali ya kuwa)Masihi alisema “Enyi wana wa Israel! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wenu. Kwani anayemshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahali pake (patakuwa) ni Motoni. Na madhalimu hawatakuwa na wasaidizi (wa kuwasaidia siku ya Kiama) “Kwa hakika wamekufuru wale waliosema mwenyenzi Mungu ni mmoja katika (wale waungu) watatu (yeye ndiye watatu wao ) hali hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu mmoja ( tu peke yake) na kama hawataacha hayo wasemayo kwa yakini itawakamata wale wanaoendelea na ukafiri miongoni mwao adhabu iumizayo”. (B)YESU YEYE NI NENO LA MUNGU LILILOFANYIKA MWILI: Yoh 1 : 1,14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu naye Neno alikuwa Mungu……..Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu…….” 7) (A) ISSA A.S YEYE HAJAWAHI KUSULUBIWA WALA KUUWAWA Qurani Suratul An-Nisaa (Wanawake) 4:157-158 “Na kwa (ajili ya )kusema kwao sisi tumemuua masihi Isa mwana wa Maryamu, mtume wa Mungu. Hali hawakumuua wala hawakumsulubu bali walibabaishiwa (mtu mwingine wakamdhani nabii Isa.) Na kwa hakika wale waliokhitalifiana katika (hakika)hiyo (ya kumuua nabii Isa) wamo katika shaka nalo (jambo hilo kusema kauwawa]. Wao (kabisa) hawana yakini juu ya (jambo)hili (la kuwa kweli wamemuua nabii isa) isipokuwa wanafuata dhana tu.Na kwa yakini hawakumuua. Bali mwenyenzi Mungu alimnyanyua kwake. Na mwenyenzi Mungu ni mwenye nguvu (na)mwenye hikima. (B)YESU KRISTO: YEYE ALISULUBIWA MSALABANI Yohana 19:18,31,33 “Wakamsulibisha huko,na wengine wawili pamoja,mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati.Basi Wayahudi, kwa sababu ni Maandalio, miili isikae juu ya misalaba siku ya sabato(maana sabato ile ilikuwa siku kubwa), walimwomba Pilato miguu yao ivunjwe,wakaondolewe. Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa,hawakumvunja miguu”. 8) (A) ISSA A.S HANA HADHI YA KUABUDIWA NA BINADAMU YEYOTE. Qur’an, Suratul Al-Maidah, 5:116 “ Na (kumbukeni) Mwnyezi Mungu atakaposema: “Ewe Isa bin Maryam! Je ,wewe uliwaambia watu: ‘Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu’?” Aseme (Nabii Isa): “Wewe umetakasika na kuwa na mshirika, hainijuzii mimi kusema ambayo si haki yangu (kuyasema, kwa kuwa ni ya uongo), kama ningalisema bila shaka ungalijua ; unayajua yaliyomo nafsini mwangu, lakini mimi siyajui yaliyomo nafsini mwako; hakika Wewe ndiye ujuaye mambo ya ghaibu. B) YESU ANASTAHILI KUABUDIWA NA WANADAMU NA MALAIKA Math 2: 2 “yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? kwa maana tuliiona nyota yake mashariki nasi tumekuja kumsujudia.” Yoh 9: 35 “ Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu? Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini? Yesu akamwambia Umemwona, naye anayesema nawe ndiye. Akasema, naamini, Bwana, akamsujudia.” Filipi 2:10-11 “ili kwa Jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.” Ebr 1:6 “ Hata tena amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu Malaika wote wa Mungu. 9) (A) ISA HASTAHILI KUWA MWOMBEZI WA WATU KWA MUNGU Sahih Al-Bukhari, vol.6 ,Hadithi no 3, The Noble Qur’an, English Translation uk. 8 “…….Nenda kwa Musa, mtumishi wa Allah ambaye Allah alizungumza naye uso kwa uso na alimpa Torati. Hivyo watakwenda kwake naye atasema ‘ Mimi sistahili kwa jukumu hilo la uombezi, na atataja mauaji aliyoyafanya kwa mtu ambaye si muuaji, na hivyo atajisikia aibu mbele ya Mola wake, naye atasema nendeni kwa Isa, mtumishi wa Allah, Mjumbe wake neno lake na roho iliyotoka kwake. Isa atasema sistahili mimi kubeba jukumu la uombezi…….” B) YESU ANASTAHILI KUWA MWOMBEZI WA WANADAMU KWA MUNGU 1 Tim 2:5 “ Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;” Ebr 7:24-25 “ bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.Naye, kwa sababu hii , aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu Hai siku zote ili awaombee. 10) (a) ISA NI NABII MWINGINE TU ASIYE TOFAUTI NA WENGINE Qur’an Suratul Baqarah, (ng’ombe)2:136 “ “Semeni nyinyi (Waislamu waambiwe Mayahudi na Manasara; waambieni): “Tumemwamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa, na yale yaliyoteremshwa kwa Ibrahimu na Ismail na Is-haqa na Yaaqubu na kizazi (chake Yaaqubu); na waliyopewa Musa na Isa na pia yale waliyopewa Manabii (wengine) kutoka kwa Mola wao; hatutofautishi baina ya yoyote katika hao. (Wote tunawaamini); na sisi tumenyenyekea Kwake.” b) YESU YEYE YU JUU KULIKO VITU VYOTE Efeso 1:20-23 “ aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na malaika, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya Kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.” 11) (a) ISA ATAKAPORUDI, ATAOA NA KUZAA WATOTO Mishkat Al- Masabih, vol 2 uk.1159, Sahih Muslim, vol. 1 uk 92 “ Isa atakaporudi ataishi miaka arobaini (40), muda ambao atakuwa ameoa na kuzaa watoto, na atafanya ibada ya hija.” b) YESU ATAKAPORUDI ATAKUJA KULINYAKUA KANISA, YAANI BIBI ARUSI Efeso 5:25-26, 32-33 “ Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, Uf 19:7 “ Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana Kondoo imekuja na mkewe amejiweka tayari.akajitoa kwa ajili yake, ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;…..Siri hiyo ni kubwa ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mmewe.” 12)(a) ISA ATAKUFA BAADA YA KUISHI MIAKA AROBAINI (40) Mishkat Al- Masabih, vol 2 uk. 1159,Sunan Abu Dawud, Hadithi 4310, Sahih Muslim, vol.1, uk.92 , “Isa atakaporudi ataondosha dini zote zisiwepo isipokuwa Uislamu. Atamharibu Masih Dajjal, na ataishi duniani miaka arobaini (40) na kisha atakufa. Na baada ya kufa atazikwa pembeni mwa kaburi la Muhammad.” B) YESU BAADA YA KUFUFUKA YU HAI SIKU ZOTE HAFI TENA Rum 6:9 “ tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena.” Ebr 7:24-25 “ bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.Naye, kwa sababu hii , aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu Hai siku zote ili awaombee.” Uf 1:17-18 “ Nami nilipomwona nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, mimi ni wa kwanza na wa mwisho, aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama , ni hai hata milele na milele nami ninazo funguo za mauti na za kuzimu.” 13)(a) ISA ALIPOZALIWA SAUTI YA FARAJA ILITOKA CHINI YA ARDHI Qur’an Suratul Maryam,19:23-24 “ Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, (akawa anazaa na huku) anasema: “ Laiti ningekufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa.” Mara ikamfikia sauti kutoka chini yake (inamwambia): usihuzunike. Hakika Mola wako amejaalia (ameweka) kijito cha maji chini yako;” Mafundisho ya Kiislamu yanaeleza kuwa huko chini ya ardhi kuna mnyama. Na huyo mnyama anazijua aya za Qur’an. Qur’an katika Suratul Al-Naml, 27:82 “Na kauli (ya kuja kiyama) itakapowathibitikia Tutawatolea mnyama katika ardhi atakayewasemeza kwa sababu watu walikuwa hawaziyakinishi Aya Zetu” b) ALIPOZALIWA YESU SAUTI ZA MALAIKA ZILITOKA JUU Luka 2:13-16 “ Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Ikawa malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika alilotujulisha Bwana. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini” (14)(a) ISA HANA UFAHAMU WA MAMBO MBALIMBALI katika Al-Lu’lu’ war- Marjan,kitabu cha 3 Hadithi na 1528 uk.883 “Hadithi ya Abu Huraira (r.a) kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema “Issa Ibn Mariam (a,s) alimwona mtu anaiba akamuuliza umeiba? akasema hapana ,Naapa kwa Allah ambaye hakuna mola isipokuwa yeye .Issa (a.s) akasema nimemuamini Allah na limeniongopea jicho langu”. b) YESU ANAYAJUA YOTE Yohana 1:47-48 “ Basi Yesu akamwona Nathanael anakuja kwake, akanena habari zake “Tazama Mwizraeli kweli kweli hamna hila ndani yake. Nathaeli akamwambia umepataje kunitambua? Yesu akajibu akamwambia, Kabla Filipo hajakuita ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona” Yoh 2:24-25 “ Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe aliyajua yaliyomo ndani ya mwanadamu” 15) (a) ISA A.S MAMA YAKE ALIKUTWA PEMBEZONI MWA MSIKITI ALIPOLETEWA HABARI ZA KUZALIWA KWAKE. Qur’an Suratul Maryam,19:16-17 “ Na mtaje Mariamu kitabuni humu. Alipojitenga na jamaa zake, (akenda) mahali upande wa mashariki (wa msikiti) na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea muhuisha Sharia Yetu (Jibrili)- akajimithilisha kwake (kwa sura ya) binadamu aliye kamili b) YESU KRISTO, MAMA YAKE ALIKUTWA NYUMBANI KWAO NAZARETI Luka 1:26-28 “Mwezi wa sita malaika Gabriel alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti. Kwa mwana mwali Bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yusufu wa mbari ya Daudi. Na jina lake Bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, salamu uliyepewa neema Bwana yu pamoja nawe.” 16)(a) MIMBA YA ISA ILIKUWA NI YA SIKU MOJA Qur’an Suratul Maryam,19:21-22 “ (Malaika) akasema: “ Nikama hivyo (unavyosema; lakini) Mola wako amesema ‘Haya ni sahali Kwangu, na ili Tumfanye muujiza kwa wanaasamu na rehema itokayo Kwetu (ndiyo Tumefanya hivi);’ Na hili ni jambo lililokwisha kuhukumiwa.” Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali” b) MIMBA YA YESU SIKU ZILITIMIA. Luka 2:6-7 “ ikawa, katika kukaa huko, siku zake za kuzaa zikatimia, akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika hori ya kulia ng’ombe kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni” NB: Mwezi wa sita uliotajwa katika Luka 1:26 ni mwezi wenye kuelezea umri wa mimba ya Yohana ndani ya tumbo la Elizabethi. Luka 1: 36 “ Tena tazama jamaa yako Elizabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa” NB: Hori iliyotajwa hapa,ina maana ya chombo cha kulishia wanyama kinachokuwa ndani ya zizi. Kwa Kiyunani (Kigiriki) ambayo ndiyo lugha iliyotumika kuandikia Agano Jipya ,chombo hicho kinaitwa “Fatne” kwa Kiingereza kinaitwa “a manger” 17)ISA (A.S) ATAKAPORUDI ATAKUJA KUVUNJA MISALABA NA KUUA NGURUWE Mkweli Mwaminifu, Juzuu 3-4, uk.20, Hadithi na. 753 “ Haisimami saa ya (kiyama) mpaka akuteremkieni nabii Isa (a.s) mwana wa Maryamu atahukumu (kwa sheria ya Kiislamu) (na) muadilifu, basi atavunja misalaba (ya Wakristo Makanisani) na ataua nguruwe, na ataondosha fedheha au (aibu), na mali itazidi kuwa nyingi sana mpaka hataikubali (ataikataa) mtu (kwa kuogopa kiyama)” .Soma pia katika Sahihi Bukhar, vol. 3, Hadithi na 425,. Al-Lu’lu’war-Marjan, juzuu ya 1,Hadithi na 95 uk.51. The Noble Qur’an uk.757 b)YESU KRISTO ATAKAPORUDI ATAWATUMA MALAIKA ZAKE KUWAKUSANYA WATAKATIFU Luka 24:30-31 “ ndipo itakapoonekana ishara ya mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi, naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu.” ONYO LA YESU KRISTO WA NAZARETH Math 24:24 “ kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini hata walio wateule.” (Angalia pia Marko 13:22) Yoh 8:24 “ Kwa hiyo naliwambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye mtakufa katika dhambi zenu.” WEWE MTEULE JE UTADANGANYWA NA KUDANGANYIKA KUWA KWELI ISA A.S NDIYE YESU KRISTO? UKIAMINI HIVYO UTAKUWA UMEDANGANYIKA NA UTAKOSA WOKOVU WA MWENYEZI MUNGU!!!!!!!!!! YESU KRISTO, YEYE NI IMMANUEL, MSHAURI WA AJABU, MUNGU MWENYE NGUVU, BABA WA MILELE, MFALME WA AMANI!!!! (ISAYA 9:6, MATH 1:23) HIZI SIYO SIFA ZA Shkhê Êdén Hãzãrd kwa Max Shimba Ministries
    0 التعليقات 0 المشاركات 13كيلو بايت مشاهدة 0 معاينة
  • QURAN YAMKIRI YESU KUWA NI MUNGU WA KWELI

    Mwandishi Abel Suleiman Shiriwa


    Katika vitu ambavyo waislamu huwasumbua vichwa na akili zao, ni kuhusu Uungu wa Yesu, sema vitu vyote lakini ukifika hapo kwenye Uungu wa Bwana Yesu basi mnapotezana, na kitu ambacho kinawafanya waislamu washindwe kukubali kuwa yeye ni Mungu, ni ukosefu wao wa ROHO MTAKATIFU, maana mtu hawezi kukiri kuwa Yesu ni Bwana (Mungu) kama hana ROHO MTAKATIFU, kama yasemavyo maandiko.
    2 Korintho 12: 3 Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu.


    Kwa hivyo Ndugu yangu Mkristo unapojadiliana na Muislamu kuhusu Habari za Uungu wa Yesu, kamwe hawezi kukubali mpaka ROHO MTAKATIFU auhusike, kinyume na hapao itakuwa ni sawa na kumpigia mbuzi Gitaa, kwa hivyo hoja zake zote zitaegemea katika hali ya Kuutazama mwili kama ambavyo Elisabeti, alimtazama Yesu kama mtu wa kawaida sana ambaye atazaliwa na Mariam, lakini mara baada ya kujazwa na Roho Matakatifu, ndipo alipokiri kuwa Yesu ni Bwana yaani Mungu wake.


    Luka 1: 39 Basi, Mariamu akaondoka siku hizo, akaenda hata nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda,

    40 akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti.
    41 Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu;
    42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa.
    43 Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?


    Hapo tumeona ni namna gani Umuhimu wa ROHO MATAKATIFU, katika kumjua Yesu kuwa ni Mungu, kwa kuwa Waislamu hawana Roho Mtakatifu, kazi yao hasa ni kumtaza Yesu alipoutwaa Mwili wa Kibinadamu, na kuwa na asili ya mtu, na kuuficha Uungu wake katika mwili, ndo maana akawa akiijita Mtume, Mwana, Kuhani, na hata Nabii, sasa leo sina lengo hasa la kuueleza Uungu hasa wa Yesu, kiundani kwa Biblia, bali nataka niitazame Quran namna ambavyo imemkiri Yesu kuwa ni Mungu, kwa kueleza Sifa za Mungu, ambazo Yesu anazo, kwa hivyo nitaeleza SIFA 5 NDANI YA QURAN ambazo zinakiri UUngu wa Yesu.


    (1) Mungu ni mwenye kujua yaliyomo katika nyoyo za watu.
    رَّبُّكُمْ أَعْلَمُ بِمَا فِي نُفُوسِكُمْ إِن تَكُونُواْ صَالِحِينَ فَإِنَّهُ كَانَ لِلأَوَّابِينَ غَفُورًا
    Quran 17:25. Mola wenu anajua sana yaliyomo nyoyoni mwenu, kama mkiwa wema, basi hakika yeye ndiye Mwenye kusamehe wenye kurejea.




    Hapo Quan inatupa habari kuwa MOla au Mungu yeye ni mwenye kujua yaliyomo katika nyoyo za wanadamu, sifa hiyo inamwendea Yesu kwani ni mwenye kujua yaliyomo ndani ya mioyo ya wanadamu.
    Yohana 2: 24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote;
    25 na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu.
    Kama Waislamu wangelikuwa na Roho Matakatifu, kwa ushahidi huu basi wasingeweza kupinga kuhusu UUngu wa Yesu.


    (2) MUNGU NI NI MWENYE KUONGEZA IDADI YA UWEPO WA WATATU
    Namaanisha kuwa pakiwa na watu wawili au watatu basi Mungu anaongezeka na kuwa wanne, kwa watu watatu, au watano kwa watu wanne, kama isimemavyo Quran
    أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَى ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ وَلَا خَمْسَةٍ إِلَّا هُوَ سَادِسُهُمْ وَلَا أَدْنَى مِن ذَلِكَ وَلَا أَكْثَرَ إِلَّا هُوَ مَعَهُمْ أَيْنَ مَا كَانُوا ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُوا يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّ اللَّهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
    Quran 57:7. Je, huoni kwamba Mwenyeezi Mungu anajua viliyomo mbinguni na viliyomo ardhini? Hawashauriani kwa siri watatu ila yeye ni wa nne wao, wala watano ila yeye ni wa sita wao, wala wachache kuliko hao wala zaidi ila yeye huwa pamoja nao popote walipo. Kisha siku ya Kiyama atawaambia waliyoyatenda hakika Mwenyeezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.


    Hapo tunapewa sifa za Mungu, kwa uzuri kabisa, pakiwa na wawili Mungu wa tatu, wakiwa watatu, Mungu wanne, wakiwa wanne, Mungu wa watano, SIFA hizo zinamwendea Yesu Kristo mwenyewe kama alivyosema.


    Mathayo 18: 20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao.


    Hapa Yesu anatuambia sifa hiyo ya kuwa pamoja na watu wawili au watatu, sifa hiyo ni yake yeye mwenyewe Yesu…. Tatizo la kutokuwa na Roho Mtakatifu kwa waislamu ndiyo maana wanashindwa kutambua kuwa Yesu ni Mungu.


    (3) Mungu yeye ni Nuru ya Mbingu na Nchi.
    اللَّهُ نُورُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ مَثَلُ نُورِهِ كَمِشْكَاةٍ فِيهَا مِصْبَاحٌ الْمِصْبَاحُ فِي زُجَاجَةٍ الزُّجَاجَةُ كَأَنَّهَا كَوْكَبٌ دُرِّيٌّ يُوقَدُ مِن شَجَرَةٍ مُّبَارَكَةٍ زَيْتُونِةٍ لَّا شَرْقِيَّةٍ وَلَا غَرْبِيَّةٍ يَكَادُ زَيْتُهَا يُضِيءُ وَلَوْ لَمْ تَمْسَسْهُ نَارٌ نُّورٌ عَلَى نُورٍ يَهْدِي اللَّهُ لِنُورِهِ مَن يَشَاء وَيَضْرِبُ اللَّهُ الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ وَاللَّهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
    Quran 24: 35. Mwenyeezi Mungu ni nuru ya mbingu na ardhi, mfano wa nuru yake ni kama shubaka ndani yake mna taa. Taa ile imo katika tungi, tungi lile ni kama nyota ing'aayo inayowashwa katika mti uliobarikiwa wa mzaituni, si wa mashariki wala magharibi yanakaribia mafuta yake kung'aa ingawa moto haujayagusa, nuru juu ya nuru, Mwenyeezi Mungu humuongoza kwenye nuru yake amtakaye, na Mwenyeezi Mungu hupiga mifano kwa watu, na Mwenyeezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu.


    QURAN IMESEMA MUNGU, NI NURU YA MBINGU NA NCHI, SIFA HIYO NI YA YESU, MAANA YESU NI NURU YA ULIMWENGU.
    Yohana 8: 12 Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.


    TENA YESU NI NURU YA MBINGU.
    Matendo 26: 13 Ee Mfalme, ndipo wakati wa adhuhuri njiani naliona nuru inatoka mbinguni ipitayo mwangaza wa jua, ikinimulikia mimi, na wale waliofuatana nami pande zote.
    14 Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo.
    15 Nami nikasema, Wewe u nani, Bwana? Bwana akaniambia, Mimi ni Yesu, ambaye wewe unaniudhi.
    Sifa zote hizo za kuwa Nuru ya Mbingu na aridhi, Yesu, anazo, kwa nini Waislamu wanashindwa kutambua kuwa Yesu ni Mungu? Ni kwa sababu, hawana ROHO MTAKATIFU.


    (4) MWENYEZI MUNGU YEYE NI MWANZO NA WA MWISHO.
    Quran inatupa habari kuwa Mwenyezi Mungu sifa yake yeye ni wa kwanza na pia ni wa Mwisho.
    Quran 57: هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ
    3. Yeye ndiye wa Mwanzo na wa Mwisho, naye ni wa dhahiri, na wa siri, naye ni Mjuzi wa kila


    Hapa Quran inasema yeye, Allah hasemi, mimi ni wa kwanza na mwisho, bali yeye, kuonesha kuwa siyo muhusika wa sifa, sasa Yesu yeye ambaye ndiye Muhusika wa sifa hizo, anasema


    Ufunuo 1: 16 Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake.
    17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho,


    Yesu anasema Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, Allah yeye anasema yeye, yeye hii inamwendea Yesu, kwa kuwa ameshatangulia kusema hata kabla ya kuja Quran, kinachowafunga ni Ukosefu wa ROHO MTAKATIFU kwa waislamu.


    (5) MWENYEZI MUNGU YUKO MBINGUNI.
    Quran inaeleza kuwa Mungu yupo mbinguni,
    Quran 67: أَمْ أَمِنتُم مَّن فِي السَّمَاء أَن يُرْسِلَ عَلَيْكُمْ حَاصِبًا فَسَتَعْلَمُونَ كَيْفَ نَذِيرِ
    17. Au je, mnadhani mko salama kwa (Mwenyezi Mungu) alioko mbinguni kuwa yeye hatakuleteeni kimbunga chenye changarawe? basi karibuni mtajua lilivyo onyo langu
    Quran inatambua uwepo wa Mungu kuwepo mbinguni, kwani Allah yeye makao yake ni hapa Duniani, huko Makka ambako waislamu, huenda kuhiji huko, na pia kila swala huelekea kwake, Allah Makka kama alivyoema katika quran 7:29. Kwa hivyo Allah hawezi kuwa mbinguni kwa sababu yeye yupo Duniani, Sifa hiyo ipo kwa Yesu.


    Matendo 1:9 Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao.
    10 Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe,
    11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni?


    Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni.


    Pengine Waislamu wanaweza kujiuliza Ni vipi Yesu achukuliwe kwenda Mbinguni? Alichukuliwa na nani? Ni wingu ndilo ambalo lilimchukua, kwani Wingu ni gari la Mungu.


    Zaburi 104: 3 Na kuziweka nguzo za orofa zake majini. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, Na kwenda juu ya mabawa ya upepo,


    KWA HIVYO NIMEWEKA HIVYO VIPENGELE VICHACHE ILI ANGALAU NIWEZE KUWATOA WAISLAMU GIZANI KUHUSU UUNGU wa Yesu, japo kuwa siyo rahisi wao kukubali kuwa Yesu ni Mungu, hata kama maandiko wanayaona dhahiri, ila kwa sababu hawana ROHO MTAKATIFU, wataendelea kupinga kuwa siyo Mungu, wakati Quran imekubali, na isitoshe mungu wa dunia hii (shetani) amezifunga fahamu na akili zao kwa kumkosa ROHO MTAKATIFU, isiwazunukie Nuru ya Injili ya Kristo aliye Sura yake Mungu.
    2 Korintho 4: 3 Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea;
    4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu.


    Waislamu Mtafuteni ROHO MTAKATIFU, ili muweze kumjua Yesu na UUngu wake…. Muislamu tambua kuwa Quran imetumika tu kama kibao kukuonesha njia, yaani inakuelekeza pa kumpaa Mungu, ukifika sehemu ukakuta kibao kimekuelekeza kwa mshare, Muhumbili ni kule, wewe usikae kwenye hicho Kibao, hapo siyo Muhimbili, fuata Ramani ya Hicho kibao, utafika Muhimbili, Quran ni kibao, kinakuelekeza kwenye Biblia, huko ndo unampata Mungu wa kweli Yesu.
    QURAN YAMKIRI YESU KUWA NI MUNGU WA KWELI Mwandishi Abel Suleiman Shiriwa Katika vitu ambavyo waislamu huwasumbua vichwa na akili zao, ni kuhusu Uungu wa Yesu, sema vitu vyote lakini ukifika hapo kwenye Uungu wa Bwana Yesu basi mnapotezana, na kitu ambacho kinawafanya waislamu washindwe kukubali kuwa yeye ni Mungu, ni ukosefu wao wa ROHO MTAKATIFU, maana mtu hawezi kukiri kuwa Yesu ni Bwana (Mungu) kama hana ROHO MTAKATIFU, kama yasemavyo maandiko. 2 Korintho 12: 3 Kwa hiyo nawaarifu, ya kwamba hakuna mtu anenaye katika Roho wa Mungu, kusema, Yesu amelaaniwa; wala hawezi mtu kusema, Yesu ni Bwana, isipokuwa katika Roho Mtakatifu. Kwa hivyo Ndugu yangu Mkristo unapojadiliana na Muislamu kuhusu Habari za Uungu wa Yesu, kamwe hawezi kukubali mpaka ROHO MTAKATIFU auhusike, kinyume na hapao itakuwa ni sawa na kumpigia mbuzi Gitaa, kwa hivyo hoja zake zote zitaegemea katika hali ya Kuutazama mwili kama ambavyo Elisabeti, alimtazama Yesu kama mtu wa kawaida sana ambaye atazaliwa na Mariam, lakini mara baada ya kujazwa na Roho Matakatifu, ndipo alipokiri kuwa Yesu ni Bwana yaani Mungu wake. Luka 1: 39 Basi, Mariamu akaondoka siku hizo, akaenda hata nchi ya milimani kwa haraka mpaka mji mmoja wa Yuda, 40 akaingia nyumbani kwa Zakaria akamwamkia Elisabeti. 41 Ikawa Elisabeti aliposikia kule kuamkia kwake Mariamu, kitoto kichanga kikaruka ndani ya tumbo lake; Elisabeti akajazwa Roho Mtakatifu; 42 akapaza sauti kwa nguvu akasema, Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa. 43 Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi? Hapo tumeona ni namna gani Umuhimu wa ROHO MATAKATIFU, katika kumjua Yesu kuwa ni Mungu, kwa kuwa Waislamu hawana Roho Mtakatifu, kazi yao hasa ni kumtaza Yesu alipoutwaa Mwili wa Kibinadamu, na kuwa na asili ya mtu, na kuuficha Uungu wake katika mwili, ndo maana akawa akiijita Mtume, Mwana, Kuhani, na hata Nabii, sasa leo sina lengo hasa la kuueleza Uungu hasa wa Yesu, kiundani kwa Biblia, bali nataka niitazame Quran namna ambavyo imemkiri Yesu kuwa ni Mungu, kwa kueleza Sifa za Mungu, ambazo Yesu anazo, kwa hivyo nitaeleza SIFA 5 NDANI YA QURAN ambazo zinakiri UUngu wa Yesu. (1) Mungu ni mwenye kujua yaliyomo katika nyoyo za watu. رَّبُّكُمْ أَعْلَمُ بِمَا فِي نُفُوسِكُمْ إِن تَكُونُواْ صَالِحِينَ فَإِنَّهُ كَانَ لِلأَوَّابِينَ غَفُورًا Quran 17:25. Mola wenu anajua sana yaliyomo nyoyoni mwenu, kama mkiwa wema, basi hakika yeye ndiye Mwenye kusamehe wenye kurejea. Hapo Quan inatupa habari kuwa MOla au Mungu yeye ni mwenye kujua yaliyomo katika nyoyo za wanadamu, sifa hiyo inamwendea Yesu kwani ni mwenye kujua yaliyomo ndani ya mioyo ya wanadamu. Yohana 2: 24 Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; 25 na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe alijua yaliyomo ndani ya mwanadamu. Kama Waislamu wangelikuwa na Roho Matakatifu, kwa ushahidi huu basi wasingeweza kupinga kuhusu UUngu wa Yesu. (2) MUNGU NI NI MWENYE KUONGEZA IDADI YA UWEPO WA WATATU Namaanisha kuwa pakiwa na watu wawili au watatu basi Mungu anaongezeka na kuwa wanne, kwa watu watatu, au watano kwa watu wanne, kama isimemavyo Quran أَلَمْ تَرَ أَنَّ اللَّهَ يَعْلَمُ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ مَا يَكُونُ مِن نَّجْوَى ثَلَاثَةٍ إِلَّا هُوَ رَابِعُهُمْ وَلَا خَمْسَةٍ إِلَّا هُوَ سَادِسُهُمْ وَلَا أَدْنَى مِن ذَلِكَ وَلَا أَكْثَرَ إِلَّا هُوَ مَعَهُمْ أَيْنَ مَا كَانُوا ثُمَّ يُنَبِّئُهُم بِمَا عَمِلُوا يَوْمَ الْقِيَامَةِ إِنَّ اللَّهَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ Quran 57:7. Je, huoni kwamba Mwenyeezi Mungu anajua viliyomo mbinguni na viliyomo ardhini? Hawashauriani kwa siri watatu ila yeye ni wa nne wao, wala watano ila yeye ni wa sita wao, wala wachache kuliko hao wala zaidi ila yeye huwa pamoja nao popote walipo. Kisha siku ya Kiyama atawaambia waliyoyatenda hakika Mwenyeezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu. Hapo tunapewa sifa za Mungu, kwa uzuri kabisa, pakiwa na wawili Mungu wa tatu, wakiwa watatu, Mungu wanne, wakiwa wanne, Mungu wa watano, SIFA hizo zinamwendea Yesu Kristo mwenyewe kama alivyosema. Mathayo 18: 20 Kwa kuwa walipo wawili watatu wamekusanyika kwa jina langu, nami nipo papo hapo katikati yao. Hapa Yesu anatuambia sifa hiyo ya kuwa pamoja na watu wawili au watatu, sifa hiyo ni yake yeye mwenyewe Yesu…. Tatizo la kutokuwa na Roho Mtakatifu kwa waislamu ndiyo maana wanashindwa kutambua kuwa Yesu ni Mungu. (3) Mungu yeye ni Nuru ya Mbingu na Nchi. اللَّهُ نُورُ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ مَثَلُ نُورِهِ كَمِشْكَاةٍ فِيهَا مِصْبَاحٌ الْمِصْبَاحُ فِي زُجَاجَةٍ الزُّجَاجَةُ كَأَنَّهَا كَوْكَبٌ دُرِّيٌّ يُوقَدُ مِن شَجَرَةٍ مُّبَارَكَةٍ زَيْتُونِةٍ لَّا شَرْقِيَّةٍ وَلَا غَرْبِيَّةٍ يَكَادُ زَيْتُهَا يُضِيءُ وَلَوْ لَمْ تَمْسَسْهُ نَارٌ نُّورٌ عَلَى نُورٍ يَهْدِي اللَّهُ لِنُورِهِ مَن يَشَاء وَيَضْرِبُ اللَّهُ الْأَمْثَالَ لِلنَّاسِ وَاللَّهُ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ Quran 24: 35. Mwenyeezi Mungu ni nuru ya mbingu na ardhi, mfano wa nuru yake ni kama shubaka ndani yake mna taa. Taa ile imo katika tungi, tungi lile ni kama nyota ing'aayo inayowashwa katika mti uliobarikiwa wa mzaituni, si wa mashariki wala magharibi yanakaribia mafuta yake kung'aa ingawa moto haujayagusa, nuru juu ya nuru, Mwenyeezi Mungu humuongoza kwenye nuru yake amtakaye, na Mwenyeezi Mungu hupiga mifano kwa watu, na Mwenyeezi Mungu ni Mjuzi wa kila kitu. QURAN IMESEMA MUNGU, NI NURU YA MBINGU NA NCHI, SIFA HIYO NI YA YESU, MAANA YESU NI NURU YA ULIMWENGU. Yohana 8: 12 Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima. TENA YESU NI NURU YA MBINGU. Matendo 26: 13 Ee Mfalme, ndipo wakati wa adhuhuri njiani naliona nuru inatoka mbinguni ipitayo mwangaza wa jua, ikinimulikia mimi, na wale waliofuatana nami pande zote. 14 Tukaanguka nchi sote, nikasikia sauti ikisema nami kwa lugha ya kiebrania, Sauli! Sauli! Mbona waniudhi? Ni vigumu kwako kuupiga mateke mchokoo. 15 Nami nikasema, Wewe u nani, Bwana? Bwana akaniambia, Mimi ni Yesu, ambaye wewe unaniudhi. Sifa zote hizo za kuwa Nuru ya Mbingu na aridhi, Yesu, anazo, kwa nini Waislamu wanashindwa kutambua kuwa Yesu ni Mungu? Ni kwa sababu, hawana ROHO MTAKATIFU. (4) MWENYEZI MUNGU YEYE NI MWANZO NA WA MWISHO. Quran inatupa habari kuwa Mwenyezi Mungu sifa yake yeye ni wa kwanza na pia ni wa Mwisho. Quran 57: هُوَ الْأَوَّلُ وَالْآخِرُ وَالظَّاهِرُ وَالْبَاطِنُ وَهُوَ بِكُلِّ شَيْءٍ عَلِيمٌ 3. Yeye ndiye wa Mwanzo na wa Mwisho, naye ni wa dhahiri, na wa siri, naye ni Mjuzi wa kila Hapa Quran inasema yeye, Allah hasemi, mimi ni wa kwanza na mwisho, bali yeye, kuonesha kuwa siyo muhusika wa sifa, sasa Yesu yeye ambaye ndiye Muhusika wa sifa hizo, anasema Ufunuo 1: 16 Naye alikuwa na nyota saba katika mkono wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa chake; na uso wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake. 17 Nami nilipomwona, nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, Yesu anasema Mimi ni wa kwanza na wa mwisho, Allah yeye anasema yeye, yeye hii inamwendea Yesu, kwa kuwa ameshatangulia kusema hata kabla ya kuja Quran, kinachowafunga ni Ukosefu wa ROHO MTAKATIFU kwa waislamu. (5) MWENYEZI MUNGU YUKO MBINGUNI. Quran inaeleza kuwa Mungu yupo mbinguni, Quran 67: أَمْ أَمِنتُم مَّن فِي السَّمَاء أَن يُرْسِلَ عَلَيْكُمْ حَاصِبًا فَسَتَعْلَمُونَ كَيْفَ نَذِيرِ 17. Au je, mnadhani mko salama kwa (Mwenyezi Mungu) alioko mbinguni kuwa yeye hatakuleteeni kimbunga chenye changarawe? basi karibuni mtajua lilivyo onyo langu Quran inatambua uwepo wa Mungu kuwepo mbinguni, kwani Allah yeye makao yake ni hapa Duniani, huko Makka ambako waislamu, huenda kuhiji huko, na pia kila swala huelekea kwake, Allah Makka kama alivyoema katika quran 7:29. Kwa hivyo Allah hawezi kuwa mbinguni kwa sababu yeye yupo Duniani, Sifa hiyo ipo kwa Yesu. Matendo 1:9 Akiisha kusema hayo, walipokuwa wakitazama, akainuliwa, wingu likampokea kutoka machoni pao. 10 Walipokuwa wakikaza macho mbinguni, yeye alipokuwa akienda zake, tazama, watu wawili wakasimama karibu nao, wenye nguo nyeupe, 11 wakasema, Enyi watu wa Galilaya, mbona mmesimama mkitazama mbinguni? Huyu Yesu aliyechukuliwa kutoka kwenu kwenda juu mbinguni, atakuja jinsi iyo hiyo mlivyomwona akienda zake mbinguni. Pengine Waislamu wanaweza kujiuliza Ni vipi Yesu achukuliwe kwenda Mbinguni? Alichukuliwa na nani? Ni wingu ndilo ambalo lilimchukua, kwani Wingu ni gari la Mungu. Zaburi 104: 3 Na kuziweka nguzo za orofa zake majini. Huyafanya mawingu kuwa gari lake, Na kwenda juu ya mabawa ya upepo, KWA HIVYO NIMEWEKA HIVYO VIPENGELE VICHACHE ILI ANGALAU NIWEZE KUWATOA WAISLAMU GIZANI KUHUSU UUNGU wa Yesu, japo kuwa siyo rahisi wao kukubali kuwa Yesu ni Mungu, hata kama maandiko wanayaona dhahiri, ila kwa sababu hawana ROHO MTAKATIFU, wataendelea kupinga kuwa siyo Mungu, wakati Quran imekubali, na isitoshe mungu wa dunia hii (shetani) amezifunga fahamu na akili zao kwa kumkosa ROHO MTAKATIFU, isiwazunukie Nuru ya Injili ya Kristo aliye Sura yake Mungu. 2 Korintho 4: 3 Lakini ikiwa injili yetu imesitirika, imesitirika kwa hao wanaopotea; 4 ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikira zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu wake Kristo aliye sura yake Mungu. Waislamu Mtafuteni ROHO MTAKATIFU, ili muweze kumjua Yesu na UUngu wake…. Muislamu tambua kuwa Quran imetumika tu kama kibao kukuonesha njia, yaani inakuelekeza pa kumpaa Mungu, ukifika sehemu ukakuta kibao kimekuelekeza kwa mshare, Muhumbili ni kule, wewe usikae kwenye hicho Kibao, hapo siyo Muhimbili, fuata Ramani ya Hicho kibao, utafika Muhimbili, Quran ni kibao, kinakuelekeza kwenye Biblia, huko ndo unampata Mungu wa kweli Yesu.
    0 التعليقات 0 المشاركات 5كيلو بايت مشاهدة 0 معاينة
  • TOFAUTI KUMI NA SABA (17) KATI YA YESU WA WAKRISTO NA ISA WA WAISLAM.

    Mara kwa mara, unaweza kuwasikia Waislamu wakisema kuwa Isa a.s. kama anavyotajwa ndani ya Qur’an tukufu, ndiye Yesu Kristo wa Nazareti, kama anavyotajwa ndani ya Biblia Takatifu. Wanafanya hivyo kwa kulinganisha baadhi ya aya zilizomo ndani ya Biblia Takatifu, na zile zilizomo ndani ya Qur’an. Kwa mfano, wanasema kwa mujibu wa Biblia mama yake Yesu Kristo anaitwa Mariamu. Wanasoma katika Injili ya Marko 6:3-4“Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose na Yuda na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake” . 

    Wanafananisha aya hiyo na ile iliyomo ndani ya Qur’an katika Suratul Al-Maidah, 5:75 “ Masih bin Maryam si chochote ila ni mtume tu……”,

    Hoja nyingine wanayoitumia ni kusema kwamba eti jina Isa ni katika lugha ya Kiarabu. Jambo hilo siyo kweli. Kwa sababu katika lugha ya Kiarabu, Yesu anaitwa Yasu’a siyo Isa. Na ikumbukwe kuwa Biblia ndicho kitabu kilichotangulia kuwepo duniani miaka ipatayo 1500 kabla ya Qur’an.(Qur’an is a post Bible book).

    Hoja yetu kwa Waislamu ni hii nani aliyebadilisha jina Yasu’a kuwa Isa?. Jina Yasu’a linashabihiana zaidi na Jina Yehoshua ambalo hilo ni katika lugha ya Kiebrania, na katika Kiyunani lugha iliyotumika kuandika Agano Jipya anaitwa Iesous (tamka Yesu) tafsiri ya maneno hayo kwa lugha ya Kiswahili ni Mwokozi.

    Tunasoma hayo katika Math 1:21-23 “ Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana yeye ndiye atakaye waokoa watu wake na dhambi zao. Hayo yote yamekuwa ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa Nabii akisema Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.”

    Hoja yetu Je Isa a.s naye ni Mwokozi na Imanueli kama alivyo Yesu Kristo?.

    Jambo jingine tunalopaswa kulizingatia tunapoangalia tofauti zao ni kuhusu mama zao. Mama yake Yesu Kristo ni Mariam anayetoka katika ukoo wa Yuda. Tunasoma hayo katika kitabu cha Mwanzo 49:10 “ Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake,Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki,Ambaye mataifa watamtii”.

    Unabii huu umetimia kwa Yesu Kristo.Tunasoma hayo katika Waebrania 7:14 “Maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika Yuda, kabila ambayo Musa hakunena neno lolote juu yake katika mambo ya ukuhani”

    Lakini tusomapo habari za Isa, yeye mama yake anatoka ukoo wa Imrani. Ambaye ni baba yao Haruni, Miriamu na Musa. Tunayasoma hayo katika Suratul Al-Maryam 19:28 “Ewe dada yake Haruni. Baba yako hakuwa mtu mbaya. Wala mama yako hakuwa hasharati”.

    fafanuzi unaoifafanua aya hii ya 19:28 uliyomo ndani ya Qur’an, tafsiri ya King Fahd uk. 405, unasomeka hivi “ This Harun (Aaron) is not the brother of Musa (Moses), but he was another pious man at the time of Maryam (Mary)”

    Tafsiri “Huyu Harun siyo ndugu yake Musa, bali alikuwa ni mtu mwingine tu mcha Mungu, aliyeishi wakati wa kipindi cha Maryam”
    Kwa mujibu wa Biblia, Haruni ni mtoto wa mzee Amran na mama yao anaitwa Yekobedi na kwao wamezaliwa watoto watatu Haruni, Miriam na mdogo wao Musa. Tunasoma hayo katika kitabu cha Hesabu 26:59 “Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi binti wa Lawi ,ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amram Haruni,na Musa,na Miriamu umbu lao”

    Tofauti nyingine ni kuumbwa kwao: ISSA KAUMBWA. Qur’an Suratul Imran, 3:59 “ Bila shaka hali ya Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama hali ya Adam; alimwumba kwa udongo kisha akamwambia: “Kuwa”; basi akawa”

    Lakini tusomapo kumhusu YESU, YEYE HAKUUMBWA BALI NI NENO LA MUNGU.

    Yoh 1 : 1,14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu naye Neno alikuwa Mungu……..Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu…….”

    Mika 5:2 “ Bali wewe, Bethlehem Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israel; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele”

    Yoh: 8:58 “ Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahim asijakuwako, mimi niko”.

    Zaidi ya hayo Biblia inatujulisha kuwa yeye ndiye Muumbaji mwenyewe

    Yoh 1:3 “Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika”

    Kol 1:16-17 “ Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana ; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake”



    2) (A) ISSA A.S : BAADA YA KUONDOKA KWAKE, (KAMA WAISLAMU WANAVYOAMINI), HAJAWAHI KUTOKEA KWA NAMNA YOYOTE ILE.
    (B) YESU KRISTO: BAADA YA KUONDOKA KWAKE ALIMTOKEA PAUL (SAUL).
    Mdo 9:4 “ Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Saul, Saul, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema , Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe”



    3) (A) ISSA A.S: ALITABIRI KUJA KWA MUHAMMAD Quran Suratul As Saff , 61:6
    “Na (wakumbushe) aliposema (Nabii) Isa bin Maryamu (kuwaambia mayahudi) enyi wana wa Israili! mimi ni mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu. Nisadikishaye yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati. Na kutoa habari njema ya mtume atakayewajia nyuma yangu ambaye jina lake litakuwa Ahmad(Muhammad). Na maana ya majina mawili yote haya ni moja. Maana yake Mwenye kushukuriwa kwa maneno yake mazuri na vitendo vyake vizuri na kila chake kwani vyake vyote ni vizuri).Lakini alipowajia kwa hoja zilizowazi walisema: “ Huu ni udanganyifu uliyo dhahiri”.


    (B)YESU KRISTO ALIMTUMA ROHO MTAKATIFU KATIKA SIKU YA PENTEKOSTE.
    Yoh: 14:26 “.Lakini huyo Msaidizi,huyo Roho Mtakatifu,ambaye Baba atampeleka kwa jina langu,atawafundisha yote,na kuwakumbusha yote niliyowaambia”. Katka Kiyunani anaitwa “Paracletos” yaani msaidizi au mfariji

    Yoh 15:26 “ Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia”

    Yoh 16:7 “Lakini mimi ninawaambia iliyo kweli; yawafaa nyinyi mimi niondoke,kwa maana mimi nisipoondoka huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu nitampeleka kwenu”.



    4) (A) ISSA A.S : JINA LAKE HALINA NGUVU WALA UWEZO WA KUOKOA BALI NI RANGI MBILI
    Katika Al-Lu’lu’war-Marjani, Juzuu na1, Hadithi na104 uk. 64 “ Hadithi ya Ibn Abbas (r.a) kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema, “Nilimuona Musa (a.s) katika usiku wa Al-Isra, niliopelekwa,naye ni mtu mrefu, mwenye nywele za hudhurungi zimejikunjakunja kama mtu wa Shanua.Na nilimuona Isa (a.s), naye ni mtu wa wastani wa umbo, unaelekea kwenye wekundu na weupe, ana nywele zilizonyooka……”

    (B) YESU KRISTO: JINA LAKE NI WOKOVU. 
    Mdo 4:9-10,12 “ kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu,jinsi alivyoponywa, jueni nyinyi nyote na watu wote wa Israel ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye nyinyi mlimsulubisha, na Mungu alimfufua katika wafu kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu…………………….Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo”

    Baadhi ya aya ndani ya Qur’an zinaeleza kuwa Isa a.s aliwaponya wenye upofu. Ni akina nani hao tutajiwe angalau mmoja? Yesu alimponya kipofu Batromayo.

    Aya zingine zinasema Isa a.s alifufua wafu. Ni akina nani hao? Yesu alimfufua Lazaro.

    Jina tulilopewa ni jina moja tu lenye wokovu la Yesu Kristo. Jina la Isa a.s lisilo na wokovu limehusishwaje na jina la Yesu Kristo wa Nazareth lenye wokovu?

    Mdo 16:31 “ Wakamwambia , Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka wewe pamoja na nyumba yako.”



    5) (A) ISSA.A.S : YEYE SIYO MWANA WA MUNGU. 
    Qur’ani Suratul Al An-Am,6:101 “Yeye ndiye Mwumba wa mbingu na ardhi. inamkinikanaje awe na mwana, hali hana mke. Naye ndiye aliye umba kila kitu (sio baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu”.

    Qurani Suratul At-Tawba (Kutubu), 9:30 “Na Mayahudi wanasema “Uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu” na “Wakristo wanasema “Masihi ni Mwana wa Mwenyezi Mungu” Haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasi na kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale waliokufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa!

    Fundisho la Uwana wa Mungu kama Biblia inavyofundisha, halimo katika mafundisho na itikadi ya dini ya Kiislamu kwa hiyo Isa a.s siyo mwana wa Mungu.

    (B) YESU KRISTO: YEYE NI MWANA WA MUNGU. Luka 1:30-31,35
    “Malaika akamwambia usiogope Mariamu,kwa maana umepata neema kwa Mungu.Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Malaika akajibu akamwambia,Roho Mtakatifu atakujilia juu yako,na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli;kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu Mwana wa Mungu.

    Hivyo Isa siyo Mwana Mungu lakini Yesu ni mwana wa Mungu. Kwa hivyo Yesu siyo Isa.



    6) (A) ISSA A.S: YEYE SIYO MUNGU ALIYEFANYIKA MWILI. 
    Suratul Al- Maidah,(meza), 5:72-73 Bila ya shaka wamekufuru wale waliosema, “ Mwenyezi Mungu ni Masih (issa)bin Maryam”.(Na hali ya kuwa)Masihi alisema “Enyi wana wa Israel! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wenu. Kwani anayemshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahali pake (patakuwa) ni Motoni. Na madhalimu hawatakuwa na wasaidizi (wa kuwasaidia siku ya Kiama) “Kwa hakika wamekufuru wale waliosema mwenyenzi Mungu ni mmoja katika (wale waungu) watatu (yeye ndiye watatu wao ) hali hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu mmoja ( tu peke yake) na kama hawataacha hayo wasemayo kwa yakini itawakamata wale wanaoendelea na ukafiri miongoni mwao adhabu iumizayo”.

    (B)YESU YEYE NI NENO LA MUNGU LILILOFANYIKA MWILI:
    Yoh 1 : 1,14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu naye Neno alikuwa Mungu……..Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu…….”



    7) (A) ISSA A.S YEYE HAJAWAHI KUSULUBIWA WALA KUUWAWA
    Qurani Suratul An-Nisaa (Wanawake) 4:157-158

    “Na kwa (ajili ya )kusema kwao sisi tumemuua masihi Isa mwana wa Maryamu, mtume wa Mungu. Hali hawakumuua wala hawakumsulubu bali walibabaishiwa (mtu mwingine wakamdhani nabii Isa.) Na kwa hakika wale waliokhitalifiana katika (hakika)hiyo (ya kumuua nabii Isa) wamo katika shaka nalo (jambo hilo kusema kauwawa]. Wao (kabisa) hawana yakini juu ya (jambo)hili (la kuwa kweli wamemuua nabii isa) isipokuwa wanafuata dhana tu.Na kwa yakini hawakumuua. Bali mwenyenzi Mungu alimnyanyua kwake. Na mwenyenzi Mungu ni mwenye nguvu (na)mwenye hikima.

    (B)YESU KRISTO: YEYE ALISULUBIWA MSALABANI 
    Yohana 19:18,31,33 “Wakamsulibisha huko,na wengine wawili pamoja,mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati.Basi Wayahudi, kwa sababu ni Maandalio, miili isikae juu ya misalaba siku ya sabato(maana sabato ile ilikuwa siku kubwa), walimwomba Pilato miguu yao ivunjwe,wakaondolewe. Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa,hawakumvunja miguu”.



    8) (A) ISSA A.S HANA HADHI YA KUABUDIWA NA BINADAMU YEYOTE.
    Qur’an, Suratul Al-Maidah, 5:116 “ Na (kumbukeni) Mwnyezi Mungu atakaposema: “Ewe Isa bin Maryam! Je ,wewe uliwaambia watu: ‘Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu’?” Aseme (Nabii Isa): “Wewe umetakasika na kuwa na mshirika, hainijuzii mimi kusema ambayo si haki yangu (kuyasema, kwa kuwa ni ya uongo), kama ningalisema bila shaka ungalijua ; unayajua yaliyomo nafsini mwangu, lakini mimi siyajui yaliyomo nafsini mwako; hakika Wewe ndiye ujuaye mambo ya ghaibu.

    B) YESU ANASTAHILI KUABUDIWA NA WANADAMU NA MALAIKA
    Math 2: 2 “yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? kwa maana tuliiona nyota yake mashariki nasi tumekuja kumsujudia.”

    Yoh 9: 35 “ Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu? Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini? Yesu akamwambia Umemwona, naye anayesema nawe ndiye. Akasema, naamini, Bwana, akamsujudia.”

    Filipi 2:10-11 “ili kwa Jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.”

    Ebr 1:6 “ Hata tena amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu Malaika wote wa Mungu.





    9) (A) ISA HASTAHILI KUWA MWOMBEZI WA WATU KWA MUNGU
    Sahih Al-Bukhari, vol.6 ,Hadithi no 3, The Noble Qur’an, English Translation uk. 8

    “…….Nenda kwa Musa, mtumishi wa Allah ambaye Allah alizungumza naye uso kwa uso na alimpa Torati. Hivyo watakwenda kwake naye atasema ‘ Mimi sistahili kwa jukumu hilo la uombezi, na atataja mauaji aliyoyafanya kwa mtu ambaye si muuaji, na hivyo atajisikia aibu mbele ya Mola wake, naye atasema nendeni kwa Isa, mtumishi wa Allah, Mjumbe wake neno lake na roho iliyotoka kwake. Isa atasema sistahili mimi kubeba jukumu la uombezi…….”

    B) YESU ANASTAHILI KUWA MWOMBEZI WA WANADAMU KWA MUNGU
    1 Tim 2:5 “ Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;”
    Ebr 7:24-25 “ bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.Naye, kwa sababu hii , aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu Hai siku zote ili awaombee.



    10) (a) ISA NI NABII MWINGINE TU ASIYE TOFAUTI NA WENGINE
    Qur’an Suratul Baqarah, (ng’ombe)2:136 “ “Semeni nyinyi (Waislamu waambiwe Mayahudi na Manasara; waambieni): “Tumemwamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa, na yale yaliyoteremshwa kwa Ibrahimu na Ismail na Is-haqa na Yaaqubu na kizazi (chake Yaaqubu); na waliyopewa Musa na Isa na pia yale waliyopewa Manabii (wengine) kutoka kwa Mola wao; hatutofautishi baina ya yoyote katika hao. (Wote tunawaamini); na sisi tumenyenyekea Kwake.”

    b) YESU YEYE YU JUU KULIKO VITU VYOTE
    Efeso 1:20-23 “ aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na malaika, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya Kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.”



    11) (a) ISA ATAKAPORUDI, ATAOA NA KUZAA WATOTO
    Mishkat Al- Masabih, vol 2 uk.1159, Sahih Muslim, vol. 1 uk 92 “ Isa atakaporudi ataishi miaka arobaini (40), muda ambao atakuwa ameoa na kuzaa watoto, na atafanya ibada ya hija.”

    b) YESU ATAKAPORUDI ATAKUJA KULINYAKUA KANISA, YAANI BIBI ARUSI
    Efeso 5:25-26, 32-33 “ Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, Uf 19:7 “ Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana Kondoo imekuja na mkewe amejiweka tayari.akajitoa kwa ajili yake, ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;…..Siri hiyo ni kubwa ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mmewe.”


    12)(a) ISA ATAKUFA BAADA YA KUISHI MIAKA AROBAINI (40)
    Mishkat Al- Masabih, vol 2 uk. 1159,Sunan Abu Dawud, Hadithi 4310, Sahih Muslim, vol.1, uk.92 , “Isa atakaporudi ataondosha dini zote zisiwepo isipokuwa Uislamu. Atamharibu Masih Dajjal, na ataishi duniani miaka arobaini (40) na kisha atakufa. Na baada ya kufa atazikwa pembeni mwa kaburi la Muhammad.”

    B) YESU BAADA YA KUFUFUKA YU HAI SIKU ZOTE HAFI TENA
    Rum 6:9 “ tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena.”

    Ebr 7:24-25 “ bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.Naye, kwa sababu hii , aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu Hai siku zote ili awaombee.”

    Uf 1:17-18 “ Nami nilipomwona nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, mimi ni wa kwanza na wa mwisho, aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama , ni hai hata milele na milele nami ninazo funguo za mauti na za kuzimu.”



    13)(a) ISA ALIPOZALIWA SAUTI YA FARAJA ILITOKA CHINI YA ARDHI
    Qur’an Suratul Maryam,19:23-24 “ Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, (akawa anazaa na huku) anasema: “ Laiti ningekufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa.” Mara ikamfikia sauti kutoka chini yake (inamwambia): usihuzunike. Hakika Mola wako amejaalia (ameweka) kijito cha maji chini yako;”

    Mafundisho ya Kiislamu yanaeleza kuwa huko chini ya ardhi kuna mnyama. Na huyo mnyama anazijua aya za Qur’an.

    Qur’an katika Suratul Al-Naml, 27:82 “Na kauli (ya kuja kiyama) itakapowathibitikia Tutawatolea mnyama katika ardhi atakayewasemeza kwa sababu watu walikuwa hawaziyakinishi Aya Zetu”

    b) ALIPOZALIWA YESU SAUTI ZA MALAIKA ZILITOKA JUU
    Luka 2:13-16 “ Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Ikawa malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika alilotujulisha Bwana. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini”



    (14)(a) ISA HANA UFAHAMU WA MAMBO MBALIMBALI 
    katika Al-Lu’lu’ war- Marjan,kitabu cha 3 Hadithi na 1528 uk.883 “Hadithi ya Abu Huraira (r.a) kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema “Issa Ibn Mariam (a,s) alimwona mtu anaiba akamuuliza umeiba? akasema hapana ,Naapa kwa Allah ambaye hakuna mola isipokuwa yeye .Issa (a.s) akasema nimemuamini Allah na limeniongopea jicho langu”.

    b) YESU ANAYAJUA YOTE
    Yohana 1:47-48 “ Basi Yesu akamwona Nathanael anakuja kwake, akanena habari zake “Tazama Mwizraeli kweli kweli hamna hila ndani yake. Nathaeli akamwambia umepataje kunitambua? Yesu akajibu akamwambia, Kabla Filipo hajakuita ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona”

    Yoh 2:24-25 “ Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe aliyajua yaliyomo ndani ya mwanadamu”



    15) (a) ISA A.S MAMA YAKE ALIKUTWA PEMBEZONI MWA MSIKITI ALIPOLETEWA HABARI ZA KUZALIWA KWAKE.
    Qur’an Suratul Maryam,19:16-17 “ Na mtaje Mariamu kitabuni humu. Alipojitenga na jamaa zake, (akenda) mahali upande wa mashariki (wa msikiti) na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea muhuisha Sharia Yetu (Jibrili)- akajimithilisha kwake (kwa sura ya) binadamu aliye kamili


    b) YESU KRISTO, MAMA YAKE ALIKUTWA NYUMBANI KWAO NAZARETI
    Luka 1:26-28 “Mwezi wa sita malaika Gabriel alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti. Kwa mwana mwali Bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yusufu wa mbari ya Daudi. Na jina lake Bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, salamu uliyepewa neema Bwana yu pamoja nawe.”



    16)(a) MIMBA YA ISA ILIKUWA NI YA SIKU MOJA
    Qur’an Suratul Maryam,19:21-22 “ (Malaika) akasema: “ Nikama hivyo (unavyosema; lakini) Mola wako amesema ‘Haya ni sahali Kwangu, na ili Tumfanye muujiza kwa wanaasamu na rehema itokayo Kwetu (ndiyo Tumefanya hivi);’ Na hili ni jambo lililokwisha kuhukumiwa.” Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali”


    b) MIMBA YA YESU SIKU ZILITIMIA.
    Luka 2:6-7 “ ikawa, katika kukaa huko, siku zake za kuzaa zikatimia, akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika hori ya kulia ng’ombe kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni”


    NB: Mwezi wa sita uliotajwa katika Luka 1:26 ni mwezi wenye kuelezea umri wa mimba ya Yohana ndani ya tumbo la Elizabethi. Luka 1: 36 “ Tena tazama jamaa yako Elizabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa”

    NB: Hori iliyotajwa hapa,ina maana ya chombo cha kulishia wanyama kinachokuwa ndani ya zizi. Kwa Kiyunani (Kigiriki) ambayo ndiyo lugha iliyotumika kuandikia Agano Jipya ,chombo hicho kinaitwa “Fatne” kwa Kiingereza kinaitwa “a manger”



    17)ISA (A.S) ATAKAPORUDI ATAKUJA KUVUNJA MISALABA NA KUUA NGURUWE
    Mkweli Mwaminifu, Juzuu 3-4, uk.20, Hadithi na. 753 “ Haisimami saa ya (kiyama) mpaka akuteremkieni nabii Isa (a.s) mwana wa Maryamu atahukumu (kwa sheria ya Kiislamu) (na) muadilifu, basi atavunja misalaba (ya Wakristo Makanisani) na ataua nguruwe, na ataondosha fedheha au (aibu), na mali itazidi kuwa nyingi sana mpaka hataikubali (ataikataa) mtu (kwa kuogopa kiyama)” .Soma pia katika Sahihi Bukhar, vol. 3, Hadithi na 425,. Al-Lu’lu’war-Marjan, juzuu ya 1,Hadithi na 95 uk.51. The Noble Qur’an uk.757

    b)YESU KRISTO ATAKAPORUDI ATAWATUMA MALAIKA ZAKE KUWAKUSANYA WATAKATIFU 
    Luka 24:30-31 “ ndipo itakapoonekana ishara ya mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi, naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu.”


    ONYO LA YESU KRISTO WA NAZARETH
    Math 24:24 “ kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini hata walio wateule.” (Angalia pia Marko 13:22)

    Yoh 8:24 “ Kwa hiyo naliwambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye mtakufa katika dhambi zenu.”


    WEWE MTEULE JE UTADANGANYWA NA KUDANGANYIKA KUWA KWELI ISA A.S NDIYE YESU KRISTO? UKIAMINI HIVYO UTAKUWA UMEDANGANYIKA NA UTAKOSA WOKOVU WA MWENYEZI MUNGU!!!!!!!!!!


    YESU KRISTO, YEYE NI IMMANUEL, MSHAURI WA AJABU, MUNGU MWENYE NGUVU, BABA WA MILELE, MFALME WA AMANI!!!! (ISAYA 9:6, MATH 1:23)
    TOFAUTI KUMI NA SABA (17) KATI YA YESU WA WAKRISTO NA ISA WA WAISLAM. Mara kwa mara, unaweza kuwasikia Waislamu wakisema kuwa Isa a.s. kama anavyotajwa ndani ya Qur’an tukufu, ndiye Yesu Kristo wa Nazareti, kama anavyotajwa ndani ya Biblia Takatifu. Wanafanya hivyo kwa kulinganisha baadhi ya aya zilizomo ndani ya Biblia Takatifu, na zile zilizomo ndani ya Qur’an. Kwa mfano, wanasema kwa mujibu wa Biblia mama yake Yesu Kristo anaitwa Mariamu. Wanasoma katika Injili ya Marko 6:3-4“Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose na Yuda na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake” .  Wanafananisha aya hiyo na ile iliyomo ndani ya Qur’an katika Suratul Al-Maidah, 5:75 “ Masih bin Maryam si chochote ila ni mtume tu……”, Hoja nyingine wanayoitumia ni kusema kwamba eti jina Isa ni katika lugha ya Kiarabu. Jambo hilo siyo kweli. Kwa sababu katika lugha ya Kiarabu, Yesu anaitwa Yasu’a siyo Isa. Na ikumbukwe kuwa Biblia ndicho kitabu kilichotangulia kuwepo duniani miaka ipatayo 1500 kabla ya Qur’an.(Qur’an is a post Bible book). Hoja yetu kwa Waislamu ni hii nani aliyebadilisha jina Yasu’a kuwa Isa?. Jina Yasu’a linashabihiana zaidi na Jina Yehoshua ambalo hilo ni katika lugha ya Kiebrania, na katika Kiyunani lugha iliyotumika kuandika Agano Jipya anaitwa Iesous (tamka Yesu) tafsiri ya maneno hayo kwa lugha ya Kiswahili ni Mwokozi. Tunasoma hayo katika Math 1:21-23 “ Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana yeye ndiye atakaye waokoa watu wake na dhambi zao. Hayo yote yamekuwa ili litimie neno lililonenwa na Bwana kwa ujumbe wa Nabii akisema Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, Mungu pamoja nasi.” Hoja yetu Je Isa a.s naye ni Mwokozi na Imanueli kama alivyo Yesu Kristo?. Jambo jingine tunalopaswa kulizingatia tunapoangalia tofauti zao ni kuhusu mama zao. Mama yake Yesu Kristo ni Mariam anayetoka katika ukoo wa Yuda. Tunasoma hayo katika kitabu cha Mwanzo 49:10 “ Fimbo ya enzi haitaondoka katika Yuda, Wala mfanya sheria kati ya miguu yake,Hata atakapokuja Yeye, mwenye milki,Ambaye mataifa watamtii”. Unabii huu umetimia kwa Yesu Kristo.Tunasoma hayo katika Waebrania 7:14 “Maana ni dhahiri kwamba Bwana wetu alitoka katika Yuda, kabila ambayo Musa hakunena neno lolote juu yake katika mambo ya ukuhani” Lakini tusomapo habari za Isa, yeye mama yake anatoka ukoo wa Imrani. Ambaye ni baba yao Haruni, Miriamu na Musa. Tunayasoma hayo katika Suratul Al-Maryam 19:28 “Ewe dada yake Haruni. Baba yako hakuwa mtu mbaya. Wala mama yako hakuwa hasharati”. fafanuzi unaoifafanua aya hii ya 19:28 uliyomo ndani ya Qur’an, tafsiri ya King Fahd uk. 405, unasomeka hivi “ This Harun (Aaron) is not the brother of Musa (Moses), but he was another pious man at the time of Maryam (Mary)” Tafsiri “Huyu Harun siyo ndugu yake Musa, bali alikuwa ni mtu mwingine tu mcha Mungu, aliyeishi wakati wa kipindi cha Maryam” Kwa mujibu wa Biblia, Haruni ni mtoto wa mzee Amran na mama yao anaitwa Yekobedi na kwao wamezaliwa watoto watatu Haruni, Miriam na mdogo wao Musa. Tunasoma hayo katika kitabu cha Hesabu 26:59 “Na jina la mke wa Amramu aliitwa Yokebedi binti wa Lawi ,ambaye alizaliwa kwake Lawi huko Misri; na huyo Yokebedi akamzalia Amram Haruni,na Musa,na Miriamu umbu lao” Tofauti nyingine ni kuumbwa kwao: ISSA KAUMBWA. Qur’an Suratul Imran, 3:59 “ Bila shaka hali ya Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama hali ya Adam; alimwumba kwa udongo kisha akamwambia: “Kuwa”; basi akawa” Lakini tusomapo kumhusu YESU, YEYE HAKUUMBWA BALI NI NENO LA MUNGU. Yoh 1 : 1,14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu naye Neno alikuwa Mungu……..Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu…….” Mika 5:2 “ Bali wewe, Bethlehem Efrata, uliye mdogo kuwa miongoni mwa elfu za Yuda; kutoka kwako wewe atanitokea mmoja atakayekuwa mtawala katika Israel; ambaye matokeo yake yamekuwa tangu zamani za kale, tangu milele” Yoh: 8:58 “ Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahim asijakuwako, mimi niko”. Zaidi ya hayo Biblia inatujulisha kuwa yeye ndiye Muumbaji mwenyewe Yoh 1:3 “Vyote vilifanyika kwa huyo; wala pasipo yeye hakikufanyika chochote kilichofanyika” Kol 1:16-17 “ Kwa kuwa katika yeye vitu vyote viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana ; ikiwa ni vitu vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia yake na kwa ajili yake” 2) (A) ISSA A.S : BAADA YA KUONDOKA KWAKE, (KAMA WAISLAMU WANAVYOAMINI), HAJAWAHI KUTOKEA KWA NAMNA YOYOTE ILE. (B) YESU KRISTO: BAADA YA KUONDOKA KWAKE ALIMTOKEA PAUL (SAUL). Mdo 9:4 “ Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Saul, Saul, mbona waniudhi? Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema , Mimi ndimi Yesu unayeniudhi wewe” 3) (A) ISSA A.S: ALITABIRI KUJA KWA MUHAMMAD Quran Suratul As Saff , 61:6 “Na (wakumbushe) aliposema (Nabii) Isa bin Maryamu (kuwaambia mayahudi) enyi wana wa Israili! mimi ni mtume wa Mwenyezi Mungu kwenu. Nisadikishaye yaliyo kuwa kabla yangu katika Taurati. Na kutoa habari njema ya mtume atakayewajia nyuma yangu ambaye jina lake litakuwa Ahmad(Muhammad). Na maana ya majina mawili yote haya ni moja. Maana yake Mwenye kushukuriwa kwa maneno yake mazuri na vitendo vyake vizuri na kila chake kwani vyake vyote ni vizuri).Lakini alipowajia kwa hoja zilizowazi walisema: “ Huu ni udanganyifu uliyo dhahiri”. (B)YESU KRISTO ALIMTUMA ROHO MTAKATIFU KATIKA SIKU YA PENTEKOSTE. Yoh: 14:26 “.Lakini huyo Msaidizi,huyo Roho Mtakatifu,ambaye Baba atampeleka kwa jina langu,atawafundisha yote,na kuwakumbusha yote niliyowaambia”. Katka Kiyunani anaitwa “Paracletos” yaani msaidizi au mfariji Yoh 15:26 “ Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia” Yoh 16:7 “Lakini mimi ninawaambia iliyo kweli; yawafaa nyinyi mimi niondoke,kwa maana mimi nisipoondoka huyo Msaidizi hatakuja kwenu; bali mimi nikienda zangu nitampeleka kwenu”. 4) (A) ISSA A.S : JINA LAKE HALINA NGUVU WALA UWEZO WA KUOKOA BALI NI RANGI MBILI Katika Al-Lu’lu’war-Marjani, Juzuu na1, Hadithi na104 uk. 64 “ Hadithi ya Ibn Abbas (r.a) kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema, “Nilimuona Musa (a.s) katika usiku wa Al-Isra, niliopelekwa,naye ni mtu mrefu, mwenye nywele za hudhurungi zimejikunjakunja kama mtu wa Shanua.Na nilimuona Isa (a.s), naye ni mtu wa wastani wa umbo, unaelekea kwenye wekundu na weupe, ana nywele zilizonyooka……” (B) YESU KRISTO: JINA LAKE NI WOKOVU.  Mdo 4:9-10,12 “ kama tukiulizwa leo habari ya jambo jema alilofanyiwa yule mtu dhaifu,jinsi alivyoponywa, jueni nyinyi nyote na watu wote wa Israel ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye nyinyi mlimsulubisha, na Mungu alimfufua katika wafu kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu…………………….Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo” Baadhi ya aya ndani ya Qur’an zinaeleza kuwa Isa a.s aliwaponya wenye upofu. Ni akina nani hao tutajiwe angalau mmoja? Yesu alimponya kipofu Batromayo. Aya zingine zinasema Isa a.s alifufua wafu. Ni akina nani hao? Yesu alimfufua Lazaro. Jina tulilopewa ni jina moja tu lenye wokovu la Yesu Kristo. Jina la Isa a.s lisilo na wokovu limehusishwaje na jina la Yesu Kristo wa Nazareth lenye wokovu? Mdo 16:31 “ Wakamwambia , Mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka wewe pamoja na nyumba yako.” 5) (A) ISSA.A.S : YEYE SIYO MWANA WA MUNGU.  Qur’ani Suratul Al An-Am,6:101 “Yeye ndiye Mwumba wa mbingu na ardhi. inamkinikanaje awe na mwana, hali hana mke. Naye ndiye aliye umba kila kitu (sio baadhi yake kavizaa). Naye ni mjuzi wa kila kitu”. Qurani Suratul At-Tawba (Kutubu), 9:30 “Na Mayahudi wanasema “Uzeri ni mwana wa Mwenyezi Mungu” na “Wakristo wanasema “Masihi ni Mwana wa Mwenyezi Mungu” Haya ndiyo wasemayo kwa vinywa vyao (pasi na kuyapima). Wanayaiga maneno ya wale waliokufuru kabla yao, Mwenyezi Mungu awaangamize. Wanageuzwa namna gani hawa! Fundisho la Uwana wa Mungu kama Biblia inavyofundisha, halimo katika mafundisho na itikadi ya dini ya Kiislamu kwa hiyo Isa a.s siyo mwana wa Mungu. (B) YESU KRISTO: YEYE NI MWANA WA MUNGU. Luka 1:30-31,35 “Malaika akamwambia usiogope Mariamu,kwa maana umepata neema kwa Mungu.Tazama utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Malaika akajibu akamwambia,Roho Mtakatifu atakujilia juu yako,na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli;kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu Mwana wa Mungu. Hivyo Isa siyo Mwana Mungu lakini Yesu ni mwana wa Mungu. Kwa hivyo Yesu siyo Isa. 6) (A) ISSA A.S: YEYE SIYO MUNGU ALIYEFANYIKA MWILI.  Suratul Al- Maidah,(meza), 5:72-73 Bila ya shaka wamekufuru wale waliosema, “ Mwenyezi Mungu ni Masih (issa)bin Maryam”.(Na hali ya kuwa)Masihi alisema “Enyi wana wa Israel! Mwabuduni Mwenyezi Mungu, Mola wenu. Kwani anayemshirikisha Mwenyezi Mungu, hakika Mwenyezi Mungu atamharimishia Pepo, na mahali pake (patakuwa) ni Motoni. Na madhalimu hawatakuwa na wasaidizi (wa kuwasaidia siku ya Kiama) “Kwa hakika wamekufuru wale waliosema mwenyenzi Mungu ni mmoja katika (wale waungu) watatu (yeye ndiye watatu wao ) hali hakuna mungu ila Mwenyezi Mungu mmoja ( tu peke yake) na kama hawataacha hayo wasemayo kwa yakini itawakamata wale wanaoendelea na ukafiri miongoni mwao adhabu iumizayo”. (B)YESU YEYE NI NENO LA MUNGU LILILOFANYIKA MWILI: Yoh 1 : 1,14 “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu naye Neno alikuwa Mungu……..Naye Neno alifanyika mwili akakaa kwetu…….” 7) (A) ISSA A.S YEYE HAJAWAHI KUSULUBIWA WALA KUUWAWA Qurani Suratul An-Nisaa (Wanawake) 4:157-158 “Na kwa (ajili ya )kusema kwao sisi tumemuua masihi Isa mwana wa Maryamu, mtume wa Mungu. Hali hawakumuua wala hawakumsulubu bali walibabaishiwa (mtu mwingine wakamdhani nabii Isa.) Na kwa hakika wale waliokhitalifiana katika (hakika)hiyo (ya kumuua nabii Isa) wamo katika shaka nalo (jambo hilo kusema kauwawa]. Wao (kabisa) hawana yakini juu ya (jambo)hili (la kuwa kweli wamemuua nabii isa) isipokuwa wanafuata dhana tu.Na kwa yakini hawakumuua. Bali mwenyenzi Mungu alimnyanyua kwake. Na mwenyenzi Mungu ni mwenye nguvu (na)mwenye hikima. (B)YESU KRISTO: YEYE ALISULUBIWA MSALABANI  Yohana 19:18,31,33 “Wakamsulibisha huko,na wengine wawili pamoja,mmoja huku na mmoja huku, na Yesu katikati.Basi Wayahudi, kwa sababu ni Maandalio, miili isikae juu ya misalaba siku ya sabato(maana sabato ile ilikuwa siku kubwa), walimwomba Pilato miguu yao ivunjwe,wakaondolewe. Lakini walipomjia Yesu na kuona ya kuwa amekwisha kufa,hawakumvunja miguu”. 8) (A) ISSA A.S HANA HADHI YA KUABUDIWA NA BINADAMU YEYOTE. Qur’an, Suratul Al-Maidah, 5:116 “ Na (kumbukeni) Mwnyezi Mungu atakaposema: “Ewe Isa bin Maryam! Je ,wewe uliwaambia watu: ‘Nifanyeni mimi na mama yangu kuwa waungu badala ya Mwenyezi Mungu’?” Aseme (Nabii Isa): “Wewe umetakasika na kuwa na mshirika, hainijuzii mimi kusema ambayo si haki yangu (kuyasema, kwa kuwa ni ya uongo), kama ningalisema bila shaka ungalijua ; unayajua yaliyomo nafsini mwangu, lakini mimi siyajui yaliyomo nafsini mwako; hakika Wewe ndiye ujuaye mambo ya ghaibu. B) YESU ANASTAHILI KUABUDIWA NA WANADAMU NA MALAIKA Math 2: 2 “yuko wapi yeye aliyezaliwa mfalme wa Wayahudi? kwa maana tuliiona nyota yake mashariki nasi tumekuja kumsujudia.” Yoh 9: 35 “ Yesu akasikia kwamba wamemtoa nje; naye alipomwona alisema, Wewe wamwamini Mwana wa Mungu? Naye akajibu akasema, Ni nani, Bwana, nipate kumwamini? Yesu akamwambia Umemwona, naye anayesema nawe ndiye. Akasema, naamini, Bwana, akamsujudia.” Filipi 2:10-11 “ili kwa Jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI BWANA, kwa utukufu wa Mungu Baba.” Ebr 1:6 “ Hata tena amletapo mzaliwa wa kwanza ulimwenguni, asema, Na wamsujudu Malaika wote wa Mungu. 9) (A) ISA HASTAHILI KUWA MWOMBEZI WA WATU KWA MUNGU Sahih Al-Bukhari, vol.6 ,Hadithi no 3, The Noble Qur’an, English Translation uk. 8 “…….Nenda kwa Musa, mtumishi wa Allah ambaye Allah alizungumza naye uso kwa uso na alimpa Torati. Hivyo watakwenda kwake naye atasema ‘ Mimi sistahili kwa jukumu hilo la uombezi, na atataja mauaji aliyoyafanya kwa mtu ambaye si muuaji, na hivyo atajisikia aibu mbele ya Mola wake, naye atasema nendeni kwa Isa, mtumishi wa Allah, Mjumbe wake neno lake na roho iliyotoka kwake. Isa atasema sistahili mimi kubeba jukumu la uombezi…….” B) YESU ANASTAHILI KUWA MWOMBEZI WA WANADAMU KWA MUNGU 1 Tim 2:5 “ Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu;” Ebr 7:24-25 “ bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.Naye, kwa sababu hii , aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu Hai siku zote ili awaombee. 10) (a) ISA NI NABII MWINGINE TU ASIYE TOFAUTI NA WENGINE Qur’an Suratul Baqarah, (ng’ombe)2:136 “ “Semeni nyinyi (Waislamu waambiwe Mayahudi na Manasara; waambieni): “Tumemwamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa, na yale yaliyoteremshwa kwa Ibrahimu na Ismail na Is-haqa na Yaaqubu na kizazi (chake Yaaqubu); na waliyopewa Musa na Isa na pia yale waliyopewa Manabii (wengine) kutoka kwa Mola wao; hatutofautishi baina ya yoyote katika hao. (Wote tunawaamini); na sisi tumenyenyekea Kwake.” b) YESU YEYE YU JUU KULIKO VITU VYOTE Efeso 1:20-23 “ aliotenda katika Kristo alipomfufua katika wafu, akamweka mkono wake wa kuume katika ulimwengu wa roho; juu sana kuliko ufalme wote, na malaika, na nguvu, na usultani, na kila jina litajwalo, wala si ulimwenguni humu tu, bali katika ule ujao pia; akavitia vitu vyote chini ya miguu yake akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya Kanisa; ambalo ndilo mwili wake, ukamilifu wake anayekamilika kwa vyote katika vyote.” 11) (a) ISA ATAKAPORUDI, ATAOA NA KUZAA WATOTO Mishkat Al- Masabih, vol 2 uk.1159, Sahih Muslim, vol. 1 uk 92 “ Isa atakaporudi ataishi miaka arobaini (40), muda ambao atakuwa ameoa na kuzaa watoto, na atafanya ibada ya hija.” b) YESU ATAKAPORUDI ATAKUJA KULINYAKUA KANISA, YAANI BIBI ARUSI Efeso 5:25-26, 32-33 “ Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, Uf 19:7 “ Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu wake; kwa kuwa arusi ya Mwana Kondoo imekuja na mkewe amejiweka tayari.akajitoa kwa ajili yake, ili makusudi alitakase na kulisafisha kwa maji katika neno;…..Siri hiyo ni kubwa ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa. Lakini kila mtu ampende mke wake kama nafsi yake mwenyewe; wala mke asikose kumstahi mmewe.” 12)(a) ISA ATAKUFA BAADA YA KUISHI MIAKA AROBAINI (40) Mishkat Al- Masabih, vol 2 uk. 1159,Sunan Abu Dawud, Hadithi 4310, Sahih Muslim, vol.1, uk.92 , “Isa atakaporudi ataondosha dini zote zisiwepo isipokuwa Uislamu. Atamharibu Masih Dajjal, na ataishi duniani miaka arobaini (40) na kisha atakufa. Na baada ya kufa atazikwa pembeni mwa kaburi la Muhammad.” B) YESU BAADA YA KUFUFUKA YU HAI SIKU ZOTE HAFI TENA Rum 6:9 “ tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena.” Ebr 7:24-25 “ bali yeye, kwa kuwa akaa milele, anao ukuhani wake usioondoka.Naye, kwa sababu hii , aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu Hai siku zote ili awaombee.” Uf 1:17-18 “ Nami nilipomwona nalianguka miguuni pake kama mtu aliyekufa. Akaweka mkono wake wa kuume juu yangu, akisema, Usiogope, mimi ni wa kwanza na wa mwisho, aliye hai; nami nalikuwa nimekufa, na tazama , ni hai hata milele na milele nami ninazo funguo za mauti na za kuzimu.” 13)(a) ISA ALIPOZALIWA SAUTI YA FARAJA ILITOKA CHINI YA ARDHI Qur’an Suratul Maryam,19:23-24 “ Kisha uchungu ukampeleka katika shina la mtende, (akawa anazaa na huku) anasema: “ Laiti ningekufa kabla ya haya, na ningekuwa niliyesahaulika kabisa.” Mara ikamfikia sauti kutoka chini yake (inamwambia): usihuzunike. Hakika Mola wako amejaalia (ameweka) kijito cha maji chini yako;” Mafundisho ya Kiislamu yanaeleza kuwa huko chini ya ardhi kuna mnyama. Na huyo mnyama anazijua aya za Qur’an. Qur’an katika Suratul Al-Naml, 27:82 “Na kauli (ya kuja kiyama) itakapowathibitikia Tutawatolea mnyama katika ardhi atakayewasemeza kwa sababu watu walikuwa hawaziyakinishi Aya Zetu” b) ALIPOZALIWA YESU SAUTI ZA MALAIKA ZILITOKA JUU Luka 2:13-16 “ Mara walikuwapo pamoja na huyo malaika, wingi wa jeshi la mbinguni, wakimsifu Mungu na kusema, Atukuzwe Mungu juu mbinguni na duniani iwe amani kwa watu aliowaridhia. Ikawa malaika hao walipoondoka kwenda zao mbinguni, wale wachungaji waliambiana, Haya na twendeni mpaka Bethlehemu, tukalione hilo lililofanyika alilotujulisha Bwana. Wakaenda kwa haraka wakamkuta Mariamu na Yusufu, na yule mtoto mchanga amelala horini” (14)(a) ISA HANA UFAHAMU WA MAMBO MBALIMBALI  katika Al-Lu’lu’ war- Marjan,kitabu cha 3 Hadithi na 1528 uk.883 “Hadithi ya Abu Huraira (r.a) kutoka kwa Mtume (s.a.w) amesema “Issa Ibn Mariam (a,s) alimwona mtu anaiba akamuuliza umeiba? akasema hapana ,Naapa kwa Allah ambaye hakuna mola isipokuwa yeye .Issa (a.s) akasema nimemuamini Allah na limeniongopea jicho langu”. b) YESU ANAYAJUA YOTE Yohana 1:47-48 “ Basi Yesu akamwona Nathanael anakuja kwake, akanena habari zake “Tazama Mwizraeli kweli kweli hamna hila ndani yake. Nathaeli akamwambia umepataje kunitambua? Yesu akajibu akamwambia, Kabla Filipo hajakuita ulipokuwapo chini ya mtini nilikuona” Yoh 2:24-25 “ Lakini Yesu hakujiaminisha kwao; kwa kuwa yeye aliwajua wote; na kwa sababu hakuwa na haja ya mtu kushuhudia habari za mwanadamu; kwa maana yeye mwenyewe aliyajua yaliyomo ndani ya mwanadamu” 15) (a) ISA A.S MAMA YAKE ALIKUTWA PEMBEZONI MWA MSIKITI ALIPOLETEWA HABARI ZA KUZALIWA KWAKE. Qur’an Suratul Maryam,19:16-17 “ Na mtaje Mariamu kitabuni humu. Alipojitenga na jamaa zake, (akenda) mahali upande wa mashariki (wa msikiti) na akaweka pazia kujikinga nao. Tukampelekea muhuisha Sharia Yetu (Jibrili)- akajimithilisha kwake (kwa sura ya) binadamu aliye kamili b) YESU KRISTO, MAMA YAKE ALIKUTWA NYUMBANI KWAO NAZARETI Luka 1:26-28 “Mwezi wa sita malaika Gabriel alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti. Kwa mwana mwali Bikira aliyekuwa ameposwa na mtu jina lake Yusufu wa mbari ya Daudi. Na jina lake Bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, salamu uliyepewa neema Bwana yu pamoja nawe.” 16)(a) MIMBA YA ISA ILIKUWA NI YA SIKU MOJA Qur’an Suratul Maryam,19:21-22 “ (Malaika) akasema: “ Nikama hivyo (unavyosema; lakini) Mola wako amesema ‘Haya ni sahali Kwangu, na ili Tumfanye muujiza kwa wanaasamu na rehema itokayo Kwetu (ndiyo Tumefanya hivi);’ Na hili ni jambo lililokwisha kuhukumiwa.” Basi akachukua mimba yake, na akaondoka nayo mpaka mahali pa mbali” b) MIMBA YA YESU SIKU ZILITIMIA. Luka 2:6-7 “ ikawa, katika kukaa huko, siku zake za kuzaa zikatimia, akamzaa mwanawe, kifungua mimba, akamvika nguo za kitoto, akamlaza katika hori ya kulia ng’ombe kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni” NB: Mwezi wa sita uliotajwa katika Luka 1:26 ni mwezi wenye kuelezea umri wa mimba ya Yohana ndani ya tumbo la Elizabethi. Luka 1: 36 “ Tena tazama jamaa yako Elizabeti naye amechukua mimba ya mtoto mwanamume katika uzee wake; na mwezi huu ni wa sita kwake yeye aliyeitwa tasa” NB: Hori iliyotajwa hapa,ina maana ya chombo cha kulishia wanyama kinachokuwa ndani ya zizi. Kwa Kiyunani (Kigiriki) ambayo ndiyo lugha iliyotumika kuandikia Agano Jipya ,chombo hicho kinaitwa “Fatne” kwa Kiingereza kinaitwa “a manger” 17)ISA (A.S) ATAKAPORUDI ATAKUJA KUVUNJA MISALABA NA KUUA NGURUWE Mkweli Mwaminifu, Juzuu 3-4, uk.20, Hadithi na. 753 “ Haisimami saa ya (kiyama) mpaka akuteremkieni nabii Isa (a.s) mwana wa Maryamu atahukumu (kwa sheria ya Kiislamu) (na) muadilifu, basi atavunja misalaba (ya Wakristo Makanisani) na ataua nguruwe, na ataondosha fedheha au (aibu), na mali itazidi kuwa nyingi sana mpaka hataikubali (ataikataa) mtu (kwa kuogopa kiyama)” .Soma pia katika Sahihi Bukhar, vol. 3, Hadithi na 425,. Al-Lu’lu’war-Marjan, juzuu ya 1,Hadithi na 95 uk.51. The Noble Qur’an uk.757 b)YESU KRISTO ATAKAPORUDI ATAWATUMA MALAIKA ZAKE KUWAKUSANYA WATAKATIFU  Luka 24:30-31 “ ndipo itakapoonekana ishara ya mwana wa Adamu mbinguni; ndipo mataifa yote ya ulimwengu watakapoomboleza, nao watamwona mwana wa Adamu akija juu ya mawingu ya mbinguni pamoja na nguvu na utukufu mwingi, naye atawatuma malaika zake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu.” ONYO LA YESU KRISTO WA NAZARETH Math 24:24 “ kwa maana watatokea makristo wa uongo, na manabii wa uongo nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza, kama yamkini hata walio wateule.” (Angalia pia Marko 13:22) Yoh 8:24 “ Kwa hiyo naliwambieni ya kwamba mtakufa katika dhambi zenu; kwa sababu msiposadiki ya kuwa mimi ndiye mtakufa katika dhambi zenu.” WEWE MTEULE JE UTADANGANYWA NA KUDANGANYIKA KUWA KWELI ISA A.S NDIYE YESU KRISTO? UKIAMINI HIVYO UTAKUWA UMEDANGANYIKA NA UTAKOSA WOKOVU WA MWENYEZI MUNGU!!!!!!!!!! YESU KRISTO, YEYE NI IMMANUEL, MSHAURI WA AJABU, MUNGU MWENYE NGUVU, BABA WA MILELE, MFALME WA AMANI!!!! (ISAYA 9:6, MATH 1:23)
    0 التعليقات 0 المشاركات 13كيلو بايت مشاهدة 0 معاينة
  • UPONYAJI WA MAGONJWA.

    Chanzo cha magonjwa: Magonjwa yanatokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya mtu aliyekuwa mngonjwa alimwonya akisema, “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi” Yn 5:14. Mtu akiwa amefanya dhambi anapoumwa na kupimwa ugonjwa unaonekana. Iwapo akipimwa vipomo vyote na ugonjwa hauonekani yamkini ni pepo wachafu wamemwingia. “Mara huenda akachukua pamoja naye pepo wengine walio waovu kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya” Mt 12:45.

    Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili, unaotokana kukosa lishe ya mlo wa kila siku (Utapia mlo). Mapungufu katika mwili wa mwanadamu yanaweza yakawa ni kusudi la Mungu, ijapokuwa si yote. “Bwana akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani amfanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, Bwana? Kut 4:11.

    Kuponywa kwa dawa.

    Kwa kawaida kuna njia ambayo imekuwa ikitumika ya kutibu mangonjwa ambayo ni kutibu kwa kutumia dawa. Tiba za dawa zimekuwapo kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali. Mtu anapokuwa mgonjwa kuna hatua ya kuchukua, kwanza anaenda hospitali au kupelekwa kutona na hali yake hajiwezi. Daktari anampima na kufahamu ugonjwa alio nao, halafu anamwandikia dawa na maelekezo ya kuzitumia. Kama hatazingatia maelekezo na kuzitumia haiwezekani akapona. Hapa tunaweza kuona mgonjwa ili apone ni lazima azingatie maelekezo aliyopewa na daktari. Lakini baadhi ya magonjwa hayana tiba kama UKIMWI (HIV Aids). Hata hivyo usikate tamaa mwamini Mungu anaweza kukuponya kwa njia ya kumwomba. Atakuponya kwa neema, na rehema, kwa uwezo na nguvu zake.VIlevile kuna kanuni na maelekezo ya kufuata ili Mungu akuponye

    UPONYAJI WA MUNGU. Una maelekezo na kanuni za kufuata:

    1. Kutubu na kuziacha dhambi: “Azifichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema” Mit 28:13. “Twajua ya kwamba Mungu hawasikii wenye dhambi;bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake huyo humsikia” Yn 9:31.

    2. Kuishi maisha ya utakatifu: Ndio maana Mungu amesema; “Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako. Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote…” Kumb 7:12, 15. Katika maandiko haya tunaona Mungu alisema na baba zetu ya kwamba kwa upande wetu tunapozishika na kuzitenda hukumu zake (Sheria zake). Na kwa upande wake yeye ndipo hutuondolea ugonjwa wote. Kwa sababu Mungu aliwaapia baba zetu akisema, nitakutimizia agano na rehema. Kwa kiapo chake anathibitisha atafanya yale aliyoahidi katika Agano alilolifanya na baba zetu. Mahali pengine tunasoma:

    “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote,…Mche Bwana, ukajiepushe na uovu, Itakuwa afya mwilini pako. Na mafuta mifupani mwako. Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzishike kauli zangu. Kwa maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote”Mit 3:5,7,8.

    3.Kumwamini Mungu na neno lake: Ndiyo maana Mungu alisema “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita roho yangu haina furaha naye.” Ebr 10:38. Kutokana na andiko hili, linaonyesha lazima mtu awe mwenye haki ndipo aweze kuishi kwa imani. Pia lazima kwanza kuamini moyoni na kuwa na uhakika Mungu atakuponya kama neno linavyosema,“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana (wazi) ya mambo yasiyoonekana” Ebr 11:1
    4. Kuishi maisha ya unyenyekevu: “Dhabihu za Mungu ni mioyo iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka Ee Mungu hutaudharau. “Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuwaganga jeraha zao” Zab 51:17; 147:3. Mungu anahitaji watu waliovunjika na kupondeka moyo ili awaponye. Maana ya kuvunjika na kupondeka moyo ni kunyenyekea chini ya Mungu na kujua yeye ni mwenye uwezo na nguvu zote; kutokuwa na kiburi na kujiona wewe ni bora kuliko wengine, kutokuonee na kunyanyasa wengine, kutokujivunia ulivyo nayo na kujisifia kwa yale unayoyafanya na kutokudharau wengine au kuwapuuza. “Amdharauye mwenzake afanya dhambi;…” Mit 14:21. Yesu Kristo yeye ni mfano kwetu, alikuwa ni mnyenyekevu aliacha enzi na mamlaka aliyokuwa nayo mbinguni akaja duniani kwa namna ya mtumwa hakutaka makuu na fahari, alimtii Mungu.

    5. Kuomba kwa imani: “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa , tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba”Yoh 5:14-15. Haya maandiko yanafundisha ni muhimu kujua kwamba tunapomwomba Mungu anatuskia, tunapoomba sawaswa na mapenzi yake (neno lake). Pia kujua tulichoomba tunacho tayari. Kama umemwomba Mungu akuponye unajua umepona, hii ni imani katika Mungu. Ndiyo maana Yesu alifundisha akisema, “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaoombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” Mk 11:24.

    6. Kuomba kwa bidii: Kuomba kwa bidii bila kukata tamaa hadi Bwana akuponye kabisa. Iwapo umeomba lakini bado Bwana hajakuponya, endelea kunyenyeke na kumlilia tena na tena mpaka Bwana akuponye. Kuomba kwa bidii ni mfano wa mwanariadha anayeshindana na wanariadha kwa kukimbia. Mwanariada anayeshinda ni kwa sababu amekimbia kwa bidii na kupewa zawadi. Kuna mifano ya kufuata ya watumishi wa Mungu waliomwomba Mungu kwa bidii tena na tena wakajibiwa, mmojapo ni Eliya;
    “Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi; akainama uso mpaka magotini. Akamwambia mtumishi wake, kwea sasa ukatazame upande wa bahari. Akakwea na kutazama, akasema, hakuna kitu. Naye akanena, enenda tena mara saba. Ikawa mara ya saba akasema, tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. … Ikawa muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikawa mvua nyingi…” 1Fal 18:42-45. Hapa maandiko yanaonyesha jinsi Eliya alimwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili, wingu la mvua halikutokea lakini hakukata tamaa aliendelea kuomba mpaka mara ya saba wingu likaonekana na mvua ikanyesha. Na mwingine aliyeomba kwa bidii na kujibiwa ni Elisha baada ya kumtuma Gehazi mtumishi wake kumfufua mtoto.

    “Na Gehazi akawatagulia, akaiweka ile fimbo juu ya mtoto; lakini hapakuwa na sauti wala majibu. Basi Elisha alipofika nyumbani, tazama, mtoto amekwisha kufa, amelazwa kitandani pake. Basi akaingia ndani akajifungia mlango, yeye na Yule mtoto wote wawili, akamwomba Bwana... Kisha akarudi, akatembea nyumbani, huko Na huko mara moja; akapanda akajinyoosha juu yake; Na Yule mtoto akapiga chafya mara Saba, Na mtoto akafumbua macho yake.” 2 Fal 4:31-35. Elisha naye alimtuma mtumishi wake Gehazi akaiweke fimbo juu mtoto abaye alikuwa amekufa ili afufuke, wala hakufufuka, lakini Elisha hakukata tamaa alikwenda mwenyewe akamwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili na mtoto akafufuka.

    7. Kumshukuru Mungu: “Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” 1The 5:18. Katika maisha yetu ni muhimu tumshukuru Mungu kwa ajili ya mema yote anayotutende kila siku.

    Mungu ni mwaminifu.
    Yale yote aliyoyaahidi katika neno lake hakika atayafanya kama alivyosema; “Mimi sitalihalifu agano langu, sitalibadili Neno lililotoka midomoni mwangu.” Zab 89:34. “Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu” Kut 20:6. “Maana Kama vile mvua ishukavyo, Na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; Bali huinywesha ardhi, Na kuizalisha Na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, Na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure Bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma” Isa 55:10-11.

    USHUHUDA. Hapa ninatoa ushuhuda wa mtu ambaye Bwana amemponya mara nyingi kwa magonjwa tofauti. Siri ya uponyaji wake ni kwamba yeye ni mtakatifu amejilinda na kuepuka dhambi. kumbuka dhambi ni kizuizi cha uponyaji wa Mungu kwako. Amekuwa ni mwenye imani na unyenyekevu, amevunjika na kupondeka moyo. Wakati mwingine anapomwomba Mungu huanguka kifulifuli akimsihi Mungu. Hakika mtu kama huyu atasikilizwa kwa sababu anao ujasiri, hana dhambi inayomhukumu ndani ya moyo wake.

    Ndio maana imeandikwa “Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri (bila dhambi), ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.” Ebr 4:16. Mtu anapodumu katika maisha ya kumpendeza Mungu anapata neema au upendeleo kujibiwa maombi. Wakati mwingine hata kabla ya kuomba hujibiwa. “Na itakuwa kwamba, kabla ya kuomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.” Isa 65:24. “….maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.” Mt 6:8.
    UPONYAJI WA MAGONJWA. Chanzo cha magonjwa: Magonjwa yanatokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya mtu aliyekuwa mngonjwa alimwonya akisema, “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi” Yn 5:14. Mtu akiwa amefanya dhambi anapoumwa na kupimwa ugonjwa unaonekana. Iwapo akipimwa vipomo vyote na ugonjwa hauonekani yamkini ni pepo wachafu wamemwingia. “Mara huenda akachukua pamoja naye pepo wengine walio waovu kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya” Mt 12:45. Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili, unaotokana kukosa lishe ya mlo wa kila siku (Utapia mlo). Mapungufu katika mwili wa mwanadamu yanaweza yakawa ni kusudi la Mungu, ijapokuwa si yote. “Bwana akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani amfanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, Bwana? Kut 4:11. Kuponywa kwa dawa. Kwa kawaida kuna njia ambayo imekuwa ikitumika ya kutibu mangonjwa ambayo ni kutibu kwa kutumia dawa. Tiba za dawa zimekuwapo kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali. Mtu anapokuwa mgonjwa kuna hatua ya kuchukua, kwanza anaenda hospitali au kupelekwa kutona na hali yake hajiwezi. Daktari anampima na kufahamu ugonjwa alio nao, halafu anamwandikia dawa na maelekezo ya kuzitumia. Kama hatazingatia maelekezo na kuzitumia haiwezekani akapona. Hapa tunaweza kuona mgonjwa ili apone ni lazima azingatie maelekezo aliyopewa na daktari. Lakini baadhi ya magonjwa hayana tiba kama UKIMWI (HIV Aids). Hata hivyo usikate tamaa mwamini Mungu anaweza kukuponya kwa njia ya kumwomba. Atakuponya kwa neema, na rehema, kwa uwezo na nguvu zake.VIlevile kuna kanuni na maelekezo ya kufuata ili Mungu akuponye UPONYAJI WA MUNGU. Una maelekezo na kanuni za kufuata: 1. Kutubu na kuziacha dhambi: “Azifichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema” Mit 28:13. “Twajua ya kwamba Mungu hawasikii wenye dhambi;bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake huyo humsikia” Yn 9:31. 2. Kuishi maisha ya utakatifu: Ndio maana Mungu amesema; “Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako. Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote…” Kumb 7:12, 15. Katika maandiko haya tunaona Mungu alisema na baba zetu ya kwamba kwa upande wetu tunapozishika na kuzitenda hukumu zake (Sheria zake). Na kwa upande wake yeye ndipo hutuondolea ugonjwa wote. Kwa sababu Mungu aliwaapia baba zetu akisema, nitakutimizia agano na rehema. Kwa kiapo chake anathibitisha atafanya yale aliyoahidi katika Agano alilolifanya na baba zetu. Mahali pengine tunasoma: “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote,…Mche Bwana, ukajiepushe na uovu, Itakuwa afya mwilini pako. Na mafuta mifupani mwako. Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzishike kauli zangu. Kwa maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote”Mit 3:5,7,8. 3.Kumwamini Mungu na neno lake: Ndiyo maana Mungu alisema “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita roho yangu haina furaha naye.” Ebr 10:38. Kutokana na andiko hili, linaonyesha lazima mtu awe mwenye haki ndipo aweze kuishi kwa imani. Pia lazima kwanza kuamini moyoni na kuwa na uhakika Mungu atakuponya kama neno linavyosema,“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana (wazi) ya mambo yasiyoonekana” Ebr 11:1 4. Kuishi maisha ya unyenyekevu: “Dhabihu za Mungu ni mioyo iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka Ee Mungu hutaudharau. “Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuwaganga jeraha zao” Zab 51:17; 147:3. Mungu anahitaji watu waliovunjika na kupondeka moyo ili awaponye. Maana ya kuvunjika na kupondeka moyo ni kunyenyekea chini ya Mungu na kujua yeye ni mwenye uwezo na nguvu zote; kutokuwa na kiburi na kujiona wewe ni bora kuliko wengine, kutokuonee na kunyanyasa wengine, kutokujivunia ulivyo nayo na kujisifia kwa yale unayoyafanya na kutokudharau wengine au kuwapuuza. “Amdharauye mwenzake afanya dhambi;…” Mit 14:21. Yesu Kristo yeye ni mfano kwetu, alikuwa ni mnyenyekevu aliacha enzi na mamlaka aliyokuwa nayo mbinguni akaja duniani kwa namna ya mtumwa hakutaka makuu na fahari, alimtii Mungu. 5. Kuomba kwa imani: “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa , tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba”Yoh 5:14-15. Haya maandiko yanafundisha ni muhimu kujua kwamba tunapomwomba Mungu anatuskia, tunapoomba sawaswa na mapenzi yake (neno lake). Pia kujua tulichoomba tunacho tayari. Kama umemwomba Mungu akuponye unajua umepona, hii ni imani katika Mungu. Ndiyo maana Yesu alifundisha akisema, “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaoombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” Mk 11:24. 6. Kuomba kwa bidii: Kuomba kwa bidii bila kukata tamaa hadi Bwana akuponye kabisa. Iwapo umeomba lakini bado Bwana hajakuponya, endelea kunyenyeke na kumlilia tena na tena mpaka Bwana akuponye. Kuomba kwa bidii ni mfano wa mwanariadha anayeshindana na wanariadha kwa kukimbia. Mwanariada anayeshinda ni kwa sababu amekimbia kwa bidii na kupewa zawadi. Kuna mifano ya kufuata ya watumishi wa Mungu waliomwomba Mungu kwa bidii tena na tena wakajibiwa, mmojapo ni Eliya; “Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi; akainama uso mpaka magotini. Akamwambia mtumishi wake, kwea sasa ukatazame upande wa bahari. Akakwea na kutazama, akasema, hakuna kitu. Naye akanena, enenda tena mara saba. Ikawa mara ya saba akasema, tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. … Ikawa muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikawa mvua nyingi…” 1Fal 18:42-45. Hapa maandiko yanaonyesha jinsi Eliya alimwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili, wingu la mvua halikutokea lakini hakukata tamaa aliendelea kuomba mpaka mara ya saba wingu likaonekana na mvua ikanyesha. Na mwingine aliyeomba kwa bidii na kujibiwa ni Elisha baada ya kumtuma Gehazi mtumishi wake kumfufua mtoto. “Na Gehazi akawatagulia, akaiweka ile fimbo juu ya mtoto; lakini hapakuwa na sauti wala majibu. Basi Elisha alipofika nyumbani, tazama, mtoto amekwisha kufa, amelazwa kitandani pake. Basi akaingia ndani akajifungia mlango, yeye na Yule mtoto wote wawili, akamwomba Bwana... Kisha akarudi, akatembea nyumbani, huko Na huko mara moja; akapanda akajinyoosha juu yake; Na Yule mtoto akapiga chafya mara Saba, Na mtoto akafumbua macho yake.” 2 Fal 4:31-35. Elisha naye alimtuma mtumishi wake Gehazi akaiweke fimbo juu mtoto abaye alikuwa amekufa ili afufuke, wala hakufufuka, lakini Elisha hakukata tamaa alikwenda mwenyewe akamwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili na mtoto akafufuka. 7. Kumshukuru Mungu: “Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” 1The 5:18. Katika maisha yetu ni muhimu tumshukuru Mungu kwa ajili ya mema yote anayotutende kila siku. Mungu ni mwaminifu. Yale yote aliyoyaahidi katika neno lake hakika atayafanya kama alivyosema; “Mimi sitalihalifu agano langu, sitalibadili Neno lililotoka midomoni mwangu.” Zab 89:34. “Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu” Kut 20:6. “Maana Kama vile mvua ishukavyo, Na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; Bali huinywesha ardhi, Na kuizalisha Na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, Na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure Bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma” Isa 55:10-11. USHUHUDA. Hapa ninatoa ushuhuda wa mtu ambaye Bwana amemponya mara nyingi kwa magonjwa tofauti. Siri ya uponyaji wake ni kwamba yeye ni mtakatifu amejilinda na kuepuka dhambi. kumbuka dhambi ni kizuizi cha uponyaji wa Mungu kwako. Amekuwa ni mwenye imani na unyenyekevu, amevunjika na kupondeka moyo. Wakati mwingine anapomwomba Mungu huanguka kifulifuli akimsihi Mungu. Hakika mtu kama huyu atasikilizwa kwa sababu anao ujasiri, hana dhambi inayomhukumu ndani ya moyo wake. Ndio maana imeandikwa “Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri (bila dhambi), ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.” Ebr 4:16. Mtu anapodumu katika maisha ya kumpendeza Mungu anapata neema au upendeleo kujibiwa maombi. Wakati mwingine hata kabla ya kuomba hujibiwa. “Na itakuwa kwamba, kabla ya kuomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.” Isa 65:24. “….maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.” Mt 6:8.
    Love
    1
    0 التعليقات 2 المشاركات 9كيلو بايت مشاهدة 0 معاينة
إعلان مُمول
[Repenting + Holiness = Entering Heaven / Kutubu + Utakatifu = Kuingia Mbinguni].