• VITU VITAKAVYOKUWEZESHA KUTUMIA VIZURI MALAKA ULIYOPEWA NA MUNGU

    Marko 11: 27-28 ‘’ 27

    Wakafika tena Yerusalemu, wakati Yesu akitembea hekaluni, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wakamjia.
    Wakamwuliza, “UNAFANYA MAMBO HAYA KWA MAMLAKA GANI? Naye ni nani aliyekupa MAMLAKA YA KUFANYA HAYO?​

    Matendo ya Mitume 4:5-7 ‘’ 5

    Siku ya pili yake viongozi wa Kiyahudi, wazee na waandishi wa sheria wakakusanyika Yerusalemu,
    6walikuwepo Kuhani Mkuu Anasi, Kayafa, Yohana, Iskanda na wengi wa jamaa ya Kuhani Mkuu.
    7Wakiisha kuwasimamisha Petro na Yohana katikati yao, wakawauliza, “Ni kwa UWEZO GANI AU KWA JINA LA NANI mmefanya jambo hili?”’’​


    Yesu aliulizwa swali hili kuwa ni kwa mamlaka ya nani unafanya jambo hili. Hata wanafuzni wa Yesu pia waliulizwa swali hili. Maana kwa akati ule viongozi wa dini hawakujua kuwa walifanya kwa mamlaka ya nani na ni nani aliwepa mamlaka kwa sababu hawakuwahi ona. Maana wangejua wasingeuliza. Pointi ni kuwa si vile vinavyofanyika unapokuwa na mamlaka bali ni VITU GANI vitakuwezesha kutumia mamlaka uliyopewa na Mungu.
    MAANA YA MAMLAKA-- ni haki ya kisheria inayompa mtu uwezo wa kuamua na kusimamia utii juu ya kile alichokiamua.
    Kwa hiyo kwa kujua maana hii utajua ni kwanini wale viongozi wa dini waliomuuliza Yesu lile swali na walilowauliza akina Petro na wanafunzi ili wajue kuwa ni mamlaka ipi ndiyo waliyokuwa nayo na ni nani aliyesimamia utii wa kile walichofanya maana wakuu wa dini walijua vizuri sana sharia.
    LEO TUTAPITIA MAMLAKA AINA 11 AMBAZO YESU AMETUPA.
    1. MAMLAKA JUU YA UUMBAJI NA MUNGU.

    Mwanzo 1: 24-27 , Mungu katupa mamlaka ya kutawala kila kitu alichokiumba Yeye. Na ona sasa ugomvi wa Musa na Farao na wale waganga na wachawi ulikuwa kwenye viumbe. Ndio maana utaona Musa aligeuza fimbo yake ikawa nyoka na ikameza zingine za wale wachawi. Ivi unajua wachawi wanapigana vita kwa kutumia viumbe mfano Paka, Panya,Nyoka,Mbwa, bundi n.k
    Musa alisema kama mimi ni mtumishi wa Mungu na tuone kinachowatokea na ghafla ardi ikafumbua kinywa chake na ikawameza. Yoshua alipojua kuwa maadui zake walikuwa wanapigana nae kutoka kwenye nguvu zilizokuwa kwenye jua na yeye akaamua kulisimamisha jua. Nae Shetani aliamua kutumia mawambi na upepo ili kupigana na Yesu na wanafunzi wa Yesu hawakujua cha kufanya lakini Yesu alijua cha kufanya.​

    2. MAMLAKA JUU YA PEPO NA MARADHI.

    Luka 9:1 ‘’ Yesu akiisha kuwaita wale kumi na wawili pamoja, aliwapa mamalaka na uwezo wa kutoa pepo wachafu wote na kuponya magonjwa yote,’’
    Kuwa na mamlaka haimaanishi kuwa unaweza kuitumia sawasawa kama Mungu anavyotaka bali kwa hiyo unahitaji sana kuomba sana ili Mungu akupe maarifa vizuri namna ya kutumia mamlaka hii uliyopewa na Mungu.​

    3. MAMLAKA JUU YA MFUMO WA UTAWALA WA GIZA/ SHETANI.

    Waefeso 6:12 ‘’ wamba mweze kuzipinga hila za Shetani. 12Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho’’
    Mamlaka ya hapa ni tofauti na ile mamlaka ya kwenye Luka 9:1 , kwa mfano mamlaka juu ya Tanzania na mamlaka ya juu ya watanzania ni tofauti kwa sababu Mamlaka juu ya Tanzania ni juu ya mfumo bali mamalaka juu ya watanzania ni juu ya watu. Kwa hiyo mfano Tanzania kiongozi akifa, watu watahuzunika afu baadae watateua mwingine maana nafasi ile ipo kisheria. Kwa maana hiyo huwezi tumia mamlaka juu ya pepo ili kuja kushughulikia falme. Hizi ni mamlaka unahitaji kujua.​

    4. MAMLAKA JUU YA UFALME WA MBINGUNI.

    Mathayo 16:19 ‘’ 19Nitakupa funguo za Ufalme wa Mbinguni na lo lote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, lo lote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.’’
    Kwa hiyo jua kuwa mamlaka zina mipaka, kwa hiyo ili jambo lifunguliwa Duniani ndipo linafunguliwa na mbinguni. Lakini order intoka Duniani.
    Pia Mungu ametupa kufungua vitu vingine. Kwa hiyo ujio wa Dhambi Duniani iliondoa ufalme wa Mungu. Hata wale waliofungwa na kuzimu unaweza wafungua. Kwa hali hii ni hatari sana kwa Mtu aliyeokoka kutokaa kwenye mamlaka ya ufalme wa Mungu. Hivyo Mungu anaweka watu kwenye mamlaka ili waweze kuzisimamia. Mtu yeyote anapookoka anahamishwa kutoka ufalme wa giza na kuletwa kwenye ufalme wa Mungu.​

    5. MAMLAKA JUU YA DHAMBI.

    Warumi 6:12-14 ‘’ 12Kwa hiyo, msiruhusu dhambi itawale ndani ya miili yenu, ipatikanayo na kufa, ili kuwafanya mzitii tamaa mbaya. 13Wala msivitoe viungo vya miili yenu vitumike kama vyombo vya uovu vya kutenda dhambi, bali jitoeni kwa Mungu, kama watu waliotolewa kutoka mautini kuingia uzimani. Nanyi vitoeni viungo vya miili yenu Kwake kama vyombo vya haki. 14Kwa maana dhambi haitakuwa na mamlaka juu yenu, kwa sababu hampo chini ya sheria, bali chini ya neema.
    Warumi 7:15-24 ‘’14

    Kwa maana tunajua kwamba sheria ni ya kiroho, lakini mimi ni wa kimwili nikiwa nimeuzwa kwenye utumwa wa dhambi.
    15Sielewi nitendalo, kwa maana lile ninalotaka kulitenda, silitendi, lakini ninatenda lile ninalolichukia.
    16Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, ni kwamba ninakubali kuwa sheria ni njema.
    17Lakini, kwa kweli si mimi tena nitendaye lile nisilotaka bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.
    18Kwa maana ninafahamu kwamba hakuna jema lo lote likaalo ndani yangu, yaani, katika asili yangu ya dhambi. Kwa kuwa nina shauku ya kutenda lililo jema, lakini siwezi kulitenda.
    19Sitendi lile jema nitakalo kutenda bali lile baya nisilolitaka, ndilo nitendalo. 20Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, si mimi tena nifanyaye hivyo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu.
    21Hivyo naiona sheria ikitenda kazi. Ninapotaka kutenda jema, jambo baya liko papo hapo.
    22Kwa maana katika utu wangu wa ndani naifurahia sheria ya Mungu.
    23Lakini ninaona kuna sheria nyingine inayotenda kazi katika viungo vya mwili wangu inayopigana vita dhidi ya ile sheria ya akili yangu.Sheria hii inanifanya mateka wa ile sheria ya dhambi inayofanya kazi katika viungo vya mwili wangu.
    24Ole wangu, mimi maskini! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?.’’​

    Kwa hiyo tulitegemea hapa Paulo aliposema kuwa Dhambi isitawale maishani mwenu na tulitegema Yeye asiwe na dhambi lakini tunachokiona hapa ni kuwa Pualo anakiri kuwa anadhambi, Kwa hiyo haikukugurantee wewe kuwa na upako kama Paulo na usiwe na dhambi. Na Tafsri ya dhambi ni Uasi lakini hii nayo uhalali wa dhambi kututawala bali sisi tushinde dhambi.
    Utajiuliza ni Kitu gani kilikuwa kinamkwamisha Paulo jibu lake ni hili ni MWILI, hata siku moja jaribu kumuuliza Yesu kuwa ni kitu gani kilikuwa kinakukwamisha kwenda msalabani na ulilia sana pale Getsamen atakuambia ni Mwili ndio maana alisema roho I radhi ila mwili ni dhaifu.
    Nia na Mwili ni Mauti , maana mwwili hauendi mbinguni na mwili hautiii cha Mungu.
    Kwa hiyo ile wewe kuwa na mamlaka juu ya pepo wabaya au maradhi haikupi kibali cha kwenda mbinguni maana Yesu alisema watasema mbona tulitoa unabii, pepo kwa jin lako lakini yeye atawaambia kuwa sikuwajua ninyi. Na ndio maana aliwaambia wanafunzi wake msifurahi kwa kuwa pepo wanawatii bali furahini kwa kuwa majina Yenu yameandikwa mbinguni.
    Kwa hiyo mamlaka hizi zinatupa namna ya kutembea hapa Duniani na sio kwenda mbinguni. Suala la kwenda mbinguni ni suala jingine kabisa. Ukiwa na mamlaka iiswe sababu ya wewe kuoandisha mabega na kumsahau Mungu wako.
    Lengo la kukuonesha utofauti wa mamlaka hizi ni kujua namna ya kwenda nazo maana kila mlango unafunguo zake maana huwezi tumia funguo za Bedroom ili kufungulia stoo uwe na uhakika hazitafungua.
    Yakobo 5:15 Biblia inasema kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana akiomba kwa bidii maana maombi kama hayo yanaweza mfungua mgonjwa na kumponya magonjwa yake na kusamehewa dhambi zake. Kwa hiyo unaweza kumuombea Mtu hata kama hana mpango wa kutubu ila kwa sababu wewe umeomb Mungu anamsamehe kabisa.
    Ndio maana Mungu anatumia kuhani na kuwaombea watu au kufanya upatanisho na namna ya kufanya toba ili Mungu aje na atengeze hapo mahali ambapo pana dhambi.Unahitaji kujua sana siri hii ya kufanya maombi ambayo yatashughulika na chanzo cha maradhi au magonjwa mabacho ni dhambi.​

    6: MAMLAKA JUU YA MALANGO YA ADUI.

    Mwanzo 22:17 Uzao wako utamiliki malango ya adui. Galatia 3:13,14,29 Biblia inasema amelaaniwa yuke angakue juu ya mti, na Yesu alifanyika laana ili kwa ajili yake ili sisi tupate neema ya kufikiwa na Braka za Ibrahimu ambazo Mungu alituahidi kwa watu wa Duniani kote.​

    7: MAMLAKA JUU YA MIJI.

    Luka 19:16-19 Habari za Yule kabaila au kwa lugha ya sasa tungemwita Mwekezaji na wale watu walipewa yale mafungu ya fedha.
    Mafungu 10 alileta faida mara 10 na akapewa mamlaka juu ya miji kumi.
    Mafungu 5 alileta faida mara 5 na akapewa mamlaka juu ya miji mitano.
    fungu 1 alileta Hakuleta faida yoyote bali alirudisha fedha tu na haikuwa na faida na akinyimwa mamlaka juu ya miji.
    Uaminifu juu ya fedha hauleti mamlaka bali uaminifu juu ya matumizi ya fedha ndio unaleta mamlaka juu ya miji.Mwekezaji anaanza kuheshimika kwenye jamii au mji aliopo kwa sababu ya kuwa na fedha. Kwa hiyo hata dini yake nayo inapata sauti kila mtu ataanza kuiheshumu. Usijulize hili ni swala la ulimwengu wa Roho.​

    8: MAMLAKA JUU YA MIFUMO YA KIUTAWALA YA WANADAMU.

    Waefeso 2:6. 6Mungu alitufufua pamoja na Kristo na kutuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu
    Waefeso 1:20-23 20ambayo aliitumia alipomfufua Kristo kutoka kwa wafu, akamketisha mkono Wake wa kuume katika mbingu, 21juu sana kuliko falme zote na mamlaka, enzi na milki na juu ya kila jina litajwalo, si katika ulimwengu huu tu, bali na katika ule ujao pia. 22Naye Mungu ameweka vitu vyote viwe chini ya miguu Yake na amemfanya Yeye awe kichwa cha vitu vyote kwa ajili ya Kanisa, 23ambalo ndilo mwili Wake, ukamilifu Wake Yeye aliye yote katika yote.
    Ufalme wa wadamu umetambulishwa kama NGUVU AU USULTANI lakini vyote ni ufalme wa wanadamu.
    Soma Ufunuo 17:1-2​

    9: MAMLAKA JUU YA MAENEO MUHIMU YENYE MAKUSNYIKO YA WATU.

    Ufunuo 5: 9-12 Wanamiliki juu ya
    i) Kabila
    ii) Lugha
    iii) Jamaa/ukoo
    iv) Taifa.
    Ufunuo 17:15-
    Ndio maanampinga kristo anafuatilia juu ya soko yaani kuuza na kununua kila sehemu yeye anafuatilia hasi kwenye mitandao. Soma Ufunuo 13.​

    10: MAMLAKA JUU YA KILA FIKRA.

    2Wakorintho 10:3-5 3Ingawa tunaishi duniani lakini hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo. 4Silaha za vita vyetu si za mwili, Bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome. 5Tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo
    Jiulize swali hili je kuna fikra ngapi ambazo hazimtii kristo na je sisi tumechukua hatia gani ili kuzifanya zimtii kristo. Chukua hatua kushughulika na kila fikra isyomtii kristo na iweze kumtii kristo.​

    11: MAMLAKA JUU YA ULIMI NA KINYWA CHAKO.

    Yakobo 3:1-12 Mtu Yupo kama meli, mtu atakula matunda ya kinywa chake. Kwa hiyo hata ndoa nyingi huvunjika kwa sababu ya maneno na hadi hufika hatua ya kusambaratika kabisa.
    Ulimi ni Karamu na Roho Mtakatifu ni wino. Kwa hiyo kuwa makini sana na matumizi ya ulimi wako.

     

    Marko 11: 27-28 ‘’ 27

    Wakafika tena Yerusalemu, wakati Yesu akitembea hekaluni, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wakamjia.28Wakamwuliza, “UNAFANYA MAMBO HAYA KWA MAMLAKA GANI? Naye ni nani aliyekupa MAMLAKA YA KUFANYA HAYO?​

    Matendo ya Mitume 4:5-7 ‘’ 5

    Siku ya pili yake viongozi wa Kiyahudi, wazee na waandishi wa sheria wakakusanyika Yerusalemu, 6walikuwepo Kuhani Mkuu Anasi, Kayafa, Yohana, Iskanda na wengi wa jamaa ya Kuhani Mkuu. 7Wakiisha kuwasimamisha Petro na Yohana katikati yao, wakawauliza, “Ni kwa UWEZO GANI AU KWA JINA LA NANI mmefanya jambo hili?”’’
    Ile kuwa tu na mamlaka haitoshi bali leo nataka tuangalie Zaidi kuwa hizo mamlaka nilizokufundisha jana utazitumiaje.
    Leo tunaangalie VITU VITAKAVYOKUWEZESHA UITUMIE IPASAVYO MAMLAKA ULIYOPEWA NA MUNGU​


    Mwanzo 1:28 ‘’ 28

    Mungu AKAWABARIKI na akawaambia, “Zaeni na mkaongezeke, mkaijaze tena dunia b na kuitiisha. Mkatawale samaki wa baharini, ndege wa angani na kila kiumbe hai kiendacho juu ya ardhi.’
    Neno AKAWABARIKIA maana yake ni kuwa akawapa vitu ambavyo vitawawezesha kufanya yale ambayo Mungu aliwaagiza kufanya. Na ukiangalia vizuri utaona kuwa Mungu aliwabariki kabla ya kuwaingiza kazini au kuwapaagizo la kuwa zaeni mkaongezeke na kuijaza nchi na kuitisha.​


    KAZI YA BARAKA.
    Kazi ya Baraka ni kukuwezesha kuwa kama Mungu anavyotaka uwe au anavyotaka ufanye kama vile yeye anavyotaka.

    MAANA YA KUITISHA, ni kumiliki kwa amri au mamalaka hata kama nchi haitaki.
    Kwa hiyo msisitizo wa Somo kuwa tu na mamlaka bali ni kujua namna ya kuitumia.

    POINTI YA 1 . MUNGU AKUPE KUJUA YA KUWA MAMLAKA ALIYOKUPA KATIKA KRISTO NI MAMLAKA AMBAYO CHIMBUKO LAKE NI ULIMWENGU WA ROHO.

    Leo natakata twende kwa mifano ili tuweze kuelewana katika somo hili.

    Tuangalie mamlaka amabayo Mungu amaetupa katika uumbaji wake

    Mwanzo 1 :24-28 Katika kitabu cha mwanzo utaona uumbaji wa Mungu na Mungu kuwabarikia watu wake. Kumbuka kuwa Mtu ni Roho anayo nafsi anaishi katika mwili.

    Na ukisoma katika Mwanzo sura ya 1 na 2, tunaona Sura ya 1 roho ya mwanadamu ikiumbwa na baadae kaika sura ya pili ndio tunoana mwili kuumbwa na kuweka pumzi na kuwa nafsi hai.Hivyo Mwanaume na Mwanamke waliumbwa wote kwenye sura ya kwanza ila miili yao ndio imekuja kuumbwa kwenye sura ya pili.

    Suala la Mwanamke ni kuzaa au kutozaa ni sauala la ulimwengu wa roho kabla halijawa suala la kimwili.

    MFANO: Kuna mwanamke mmoja katika mkoa mmoja nilikukokwa nafanya semina na alikuwa na tatizo la kupata mimba maana kila akipata mimba zinakaa miezi miwili tu na huwa zinatoka. Na yapata mimba kama 6 ivi zilikuwa tayari zimeshatoka. Na akaja na tukaomba Mungu lile tatizo liondoke na kweli baada ya Muda akaja akapata mimba na hiyo mimba nayo ikatoka. Na alipokuja tena kwangu nikamuuliza kwanini umetoa mimba.

    Akaanza kujitetea kuwa Mwakasege mimi sijatoa mimba imetoka yenyewe, bali mimi nikamuuliza jibu swali kwa nini umetoa mimba. Ilikuwa ni ngumu sana kwa yule mama kunielewa ila nikamuuliza kuwa ivi je maiti huwa inapata mimba. Akasema hapa ni kasema kwa hiyo kipi kinapata mimba ni roho au mwili wako? Na akasema ni roho kwa hiyo nikamuambia ukipata mimba nyingine tena isemeshe kuwa usitoke hadi miezi tisa itakapotimia. Tukaomba nikamuacha.

    Baada ya Muda akaja akapata mimba tena na baada ya miezi miwili dalili za kutoka mimba zikaanza tena na akaanza kutatufuta kila mahali na Mungu alituficha kila akija mahali tulipo anatukosa mara utasikia tumeondoka na kwenda mahali pengine. Baada ya kutukosa akarudi kwake na kuanza kusoma yale tuliyomfundisha. Na alipoanza kikiri ile mistari mara ile hali ikakoma na akapata mtoto wa kwanza na wa pili na wa tatu …. Ooh haleluya haleluya.

    Hapa nataka uone jinsi Mungu alivyomfundisha Imani na hakika Mungu alimsaidia. Jifunze sana juu ya kutumia mamlaka ambazo Mungu ametupa.

    Kutoka 10:21-23 21

    Kisha BWANA akamwambia Musa, “Nyosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.’’ 22Kwa hiyo Musa akaunyosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu. 23Hakuna mtu ye yote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Wasraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi
    Hapa tunaona wana wa Israel wakiwa na Nuru na Wamisri wakiwa na giza na ili uelewe vizuri mamlaka hii aliyoitumia Musa kuingilia mfumo wa Nuru inabidi uone kilichoandikwa kwenye kitabu cha​


    Mwanzo 1:14-15

    ‘’ Mungu akasema, “Iwepo mianga kwenye nafasi ya anga ili itenganishe mchana na usiku, nayo iwe alama ya kutambulisha majira mbali mbali, siku na miaka, 15nayo iwe ndiyo mianga kwenye nafasi ya anga itoe nuru juu ya dunia.’’ ​


    Ikawa hivyo
    Kazi ya Jua ni kutawala mchana na mwezi utawale usiku. Lakini Musa alipewa mamlaka ya kuweza kuingilia mfumo wa jua na kukata mwanga wa wamisri na kuweka mwanga kwa wana wa Israel.

    Yaani ina maana wamisri walikuwa hata wakiwa na taa zilikuwa hazitoi mwanga. Suala la giza na nuru kabla halijawa suala la kimwili limekuwa suala la kwanza kabisa katika ulimwengu wa roho.

    Chanzo cha kusoma haya ni kutokana na hali iliyokuwa ikinusumbua sana ya mvua kunyesha kila mahali ukiweka hema hii ya kwetu mvua ilikuwa inaanza kunyesha au hata me mwenyewe nikenda mahali utakuta mvua tu inaaanza hata kama sio majira yake. Ndio nikaanza kutafuta majibu kwenye biblia. Na ndipo Mungu aliponifundisha namna ya kuingilia majira na namna ya kuidhibiti mvua.

    MFANO WA MOROGORO.

    Nakumbuka mwaka mmoja tulikuwa tunaandaa semina ya Morogoro na nikawauliza wenyeji wakasema mvua kwa sasa imeisha na tukapeleka hema na sku ile tunafunga hema mvua kubwa ikawa inanyesha na wenzutu walijenga hema katikati ya mvua na semina nayo ilianza kwenye mvua kama siku tatu ivi mvua ilikuwa inanyesha na watu walikuwa wanakuja wengi na miamvuli. Hapo nikaona sasa hii mvua itatuharibia utaratibu na utulivu nikaomba Mungu mvua ile iache kunyesha hadi tutakopamaliza semina. Na nilikuwa nakaa kwenye hoteli karibu na milima ya uluguru. Na mvua ikaanza kunyesha milimani nilikuwa nainyoshea kidole kuwa ewe mvua usije huku mjini hadi nimalize semina. Na baada ya hapo unaona wingu linaondoka na mvua inakoma kabisa.


    Basi siku ile ya mwisho tunamaliza semina nikawaambia wakazi wa Morogoro kuwa samahani jamani nilimaisha mvua ili tuwe na semina ila kuanzia kesho saa kumi mvua itarudi (baada ya kuwaambia wenzangu kuwa hema litaanuliwa kabla ya saa kumi na kuweka kwenye gari tayari kwa safari). Basi mtu mmoja alisema haya anayoyasema yakitokea me ntaokoka.

    Baada ya saa kumaliza semina ile kesho yake tulimtembelea mtu mmoja Morogoro tukawa tunamsalimia na ilipofika saa kumi baada ya kuwasiliana na wenzangu kuwa hema na ila kitu tayari wamepakia kwenye lori la kwetu na manyunyu ya mvua yakaanza taratibu, na mkwe wangu akanikumbusha kuwa tuliiambia mvua inyeshe kuanzia saa kumi na kuendelea sisi kukaa pale ile tulikuwa tunaizuia ile mvua.

    Basi tukaaga na tulipoanza kuondoka maana tulikuwa tunaenda Dar es Salaam kwa gari. Mvua kubwa ilinyesha Morogoro usiku kucha na kesh yake ikaendelea kusnyesha na kunyesha. Watu wakampigia simu mwenyekiti wa kamati ya kwetu Morogoro ya kuwa tunaomba Mwambie mwakasege aisimamishe mvua sasa maana inatosha sasa. Oooh haleluya haleluya…..


    Hii ni mamlaka ambayo Mungu anakupa lazima unajua kuwa ni mamlaka ya ulimwengu wa roho na inahitaji hekima sana kuitumia na usiitumie wewe utakavyo maana utaanza kuleta usumbufu kwa watu wengine.

    MAMLAKA JUU YA MFUMO WA SHETANI.
    Waefeso 6:12 ‘’ 12

    Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.​

    Waefeso 3:8-11 ’’
    8Ingawa mimi ni mdogo kuliko aliye mdogo kabisa miongoni mwa watakatifu wote, nilipewa neema hii ili niwahubirie watu Mataifa kuhusu utajiri usiopimika ulio ndani ya Kristo na 9kuweka wazi kwa kila mtu jinsi ile siri iliyokuwa imefichwa kwa nyakati zote katika Mungu aliyeumba vitu vyote.10Ili kwa njia ya Kanisa, hekima yote ya Mungu ipate kujulikana kwa watawala na WENYE MAMLAKA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO,11SAWASAWA NA KUSUDI LAKE LA MILELE KATIKA KRISTO YESU BWANA WETU. 12YEYE AMBAYE NDANI YAKE NA KWA NJIA YA IMANI KATIKA YEYE TUWEZE KUMKARIBIA MUNGU KWA UJASIRI NA KWA UHURU.13Kwa hiyo, nawaomba msikate tamaa kwa sababu ya mateso yangu kwa ajili yenu, hayo ni utukufu wenu.
    Kwa hiyo ile kuwa na mamlaka juu ya mfumo wa shetani haitoshi bali inahitajika pia kujua mamlaka juu ya mfuno wa utawala wa wanadamu.

    Angalia Waefeso 1:20 utaona neno katika Ulimwengu wa roho juu sana kuliko falme na mamlaka na kila jina litajwalo. Mungu katuweka juu sana juu ya mamlaka juu ya ufalme wa Shetani na ufalme wa Wanadamu. Hivyo ni muhimu sana kuwa na maarifa ya kushughulika na watu na mifumo yao ya kiutalawa.

    MAMLAKA JUU YA KILA FIKRA.
    2Wakorintho 10:3-5 ‘’ 3Ingawa tunaishi duniani lakini hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo. 4Silaha za vita vyetu si za mwili, Bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome. 5Tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo.
    Hapa tunaona kuwa hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili bali tunafanya kwa jinsi ya rohoni na tukiangusha mawazo na kila fikra isiyo mtii kristo na ipate kumtii kristo. Na kila kijiinuacho juu ya Elimu ya Mungu nacho kipate kumtii Mungu.

    Twende kwa Yesu tukawaangalie wanafunzi wawili yaani Yuda na Petro. Yuda alikuwa ni mpole sana na Petro kwa lugha ya sasa tungesema alikwa na kiherehere sana au msemaji sana. Petro aliposikia habari za Yesu kwenda msalabani alimwita na akaanza kumkemea na kumwambia rudi nyuma ewe shetani kwa sababu huwazi ya Mungu. Yesu alikuwa anamwambia petro umeside/ umeingiliwa na shetani saa ngapi. Bila Yesu kumkemea shetani lile pepo lingeendelea kumsumbua sana Petro. Hii ilitokana na Shetani kuomba kibali kuwa anataka awapepete kama ngano na Yesu akamwambia Petro shetani ameomba kibali ili awapepete kama ngano lakini mimi Yesu nimekuombea ili utakapoongoka uwaimarishe na dnugu zako.

    Yesu alipokuwa anazungumza na wanafuzni wake kuwa watamkibia na kumkataa ila Petro alisema mimi sitaweza, Yesu alimwambia kuwa Petro utanikana Mara tatu na Petro alimkana Yesu mara tatu na mara ya tatu alinaani kabisa. Ina maana alikuwa maejitoa kwenye uanafunzi wa Yesu.

    Ndio maana Yesu alipofufuka aliwaambia waambieni wanafunzi wangu na Petro ile neno Na Petro ina maana petro hakuwa mwanafunzi tena. Na ndio maana Yesu alipokuwa nazngumza nao alimwambia Petro mata tatu kuwa je wanipenda, hii ilikuwa ni kumsaidia Petro maan aalimkana Yesu mara tatu.

    MFANO. Wangapi hapa wanajua kuendesha baiskeli, na je unaweza kuacha kuandesha baiskeli, jibu ni hapana. Maana yake ni kuwa kitu kimeingia kwenye mfumo wako wa fahamu na halitoki. Hata kama haumkumbuki aliyekufundisha kuendesha baiskeli ila hautakauja ushahau kuendesha baiskeli.
    Kwa hiyo kumkemea pepo tu haitoshi maana huwezi jua kuwa ni kitu gani kaweka kwenye fikra za mu huyo. Hivyo pia kuomba matengenezo kutoka kwa Mungu juu ya mtu ambaye umekea lile pepo limtoke ili mfumo wake wa fikra urudi kama Mungu alivyoagiza.

    Luka 22:1-6 Hapa tunaona Shetani akimwingia Yuda na kumfanya amsaliti Yesu, na Yuda aliwaambia wakuu wa makuhani kuwa yeye ndiye aliyekuwa karibu sana na Yesu na akawapa na mbinu za namna ya kumkamata na jinsi atavyofanikisha ndipo akapewa rushwa ya vipande thelathini vya fedha.
    Shetani nae alikamata fikra za Yuda hadi hukumu ilipoingia ndani ya Yuda na aksahau hadi kumwamini MUngu ili kuwa anawezakumsamehe maana Mungu anasema dhambi yako ijapokuwa nyekundu kama damu itakuwa nyeupe kama theluji, ila Yuda alisahauna hadi akajinyonga. Hata kama umemkosea Mungu namna gani rudi kwa Mungu na Mungu atakusamehe, usiogope rudi kwa Bwana maana huko kwingine hakuna msaada na usije fanya maamuzi kama Yuda, Njoo kwa Yesu ndio maana alikufia msalabali rudi rudi kwa Bwana.

    Elimu ni suala la kiroho kabla halijawa la kimwili na ona maarifa ambayo watu wanapewa baada ya Muda utakuja kuona watu wanaanza kujitenga na Yesu na kuanza kukaa mbali na uso wa Mungu. Kwa hiyo ni muhimu sana kuombea elimu ambazo watu wanapewa ili ziwe za Elimu ya Mungu na sio zingine maana shetani nae ana elimu yake inayomnfanya amkatae Mungu.
    Ili kujinaua hapo mahali Fanya maombi ya aina tatu.
    1: OMBA KWA MUNGU MACHO YAKO YATIWE NURU.
    Waefeso1:17-23 ndio maana Paulo aliwaombea watu wa efeso japo walikuwa wameokoka lakini aliwaombea maombi haya. Na mimi ni sala yangu ya kila siku huwa najiombe maombi haya mara kwa mara.na wewe chukua sala hii ni ya kwako jiombee kila siku kila siku na iwe ni utaratibu wa maisha yako ya kila siku
    2: OMBA MUNGU AKUPE KUTAFSIRI KWA JINSI YA ROHONI KWA MANENO YA ROHONI.
    1Wakorintho 10:10-14 na Waebrania 11:3 Kwa Imani twafahamu kuwa ulimwengu uliumbwa kwa vitu visivyooneka, na katika warumi 10:17 imani huja kwa kusikia na katika ulimwengu war oho inatupa kufahamu.
    3: OMBA MUNGU AKUSAIDIE KUKUA KIROHO.
    Wagalatia 4:1-2 Lakini nalisema nanyi kama watoto. Mrithi ajapokuwa mtoto huwa kama mtu hadi pale wakati ule ulioamriwa na Bwana wake. Kwa hiyo lazima ukue kiroho ili ukue kiroho na ndipo vitu vingine utaweza kuvitumia.
    Mfano: Ukiwa na mtoto wako mwenye miaka 10 ukamnunulia gari na ukampa kuwa uwe ni urithi wake, hata kama anajua kuendesha sharia ya nchi haimruhusu kuanza kuendesha gari kwa sababu hajatimiza miaka 18. Kwa hiyo ukubwa (ukomavu) ni muhimu sana katika ulimwengu wa roho.

    Ikiwa bado hujampokea Bwana Yesu pamoja na vipawa vya Roho mtakatifu tafadhali wasiliana nasi kwa namba zifuatazo.0695540999/0789001312UBATIZO SAHIHI NI KWA JINA LA YESU KWAHIYO KAMA HUJABATIZWA UBATIZO SAHIHI BASI TAFUTA KANISA LINALOBATIZA KWA MAJI MENGI NA KWA JINA LA YESU.KAMA UKIHITAJI KUJIFUNZA ZAIDI WASILIANA NASI KWA HIZO NAMBA HAPO JUU PIA TUNA GROUP LA WHATSAPP LA KUJIFUNZA TU BIBLIA HIVYO NYOTE MNAKARIBISHWA.

    Ubarikiwe sana Bwana
    Ev.Gidion laizer

    NURU YA UPENDO ARUSHA



    VITU VITAKAVYOKUWEZESHA KUTUMIA VIZURI MALAKA ULIYOPEWA NA MUNGU Marko 11: 27-28 ‘’ 27 Wakafika tena Yerusalemu, wakati Yesu akitembea hekaluni, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wakamjia. Wakamwuliza, “UNAFANYA MAMBO HAYA KWA MAMLAKA GANI? Naye ni nani aliyekupa MAMLAKA YA KUFANYA HAYO?​ Matendo ya Mitume 4:5-7 ‘’ 5 Siku ya pili yake viongozi wa Kiyahudi, wazee na waandishi wa sheria wakakusanyika Yerusalemu, 6walikuwepo Kuhani Mkuu Anasi, Kayafa, Yohana, Iskanda na wengi wa jamaa ya Kuhani Mkuu. 7Wakiisha kuwasimamisha Petro na Yohana katikati yao, wakawauliza, “Ni kwa UWEZO GANI AU KWA JINA LA NANI mmefanya jambo hili?”’’​ Yesu aliulizwa swali hili kuwa ni kwa mamlaka ya nani unafanya jambo hili. Hata wanafuzni wa Yesu pia waliulizwa swali hili. Maana kwa akati ule viongozi wa dini hawakujua kuwa walifanya kwa mamlaka ya nani na ni nani aliwepa mamlaka kwa sababu hawakuwahi ona. Maana wangejua wasingeuliza. Pointi ni kuwa si vile vinavyofanyika unapokuwa na mamlaka bali ni VITU GANI vitakuwezesha kutumia mamlaka uliyopewa na Mungu. MAANA YA MAMLAKA-- ni haki ya kisheria inayompa mtu uwezo wa kuamua na kusimamia utii juu ya kile alichokiamua. Kwa hiyo kwa kujua maana hii utajua ni kwanini wale viongozi wa dini waliomuuliza Yesu lile swali na walilowauliza akina Petro na wanafunzi ili wajue kuwa ni mamlaka ipi ndiyo waliyokuwa nayo na ni nani aliyesimamia utii wa kile walichofanya maana wakuu wa dini walijua vizuri sana sharia. LEO TUTAPITIA MAMLAKA AINA 11 AMBAZO YESU AMETUPA. 1. MAMLAKA JUU YA UUMBAJI NA MUNGU. Mwanzo 1: 24-27 , Mungu katupa mamlaka ya kutawala kila kitu alichokiumba Yeye. Na ona sasa ugomvi wa Musa na Farao na wale waganga na wachawi ulikuwa kwenye viumbe. Ndio maana utaona Musa aligeuza fimbo yake ikawa nyoka na ikameza zingine za wale wachawi. Ivi unajua wachawi wanapigana vita kwa kutumia viumbe mfano Paka, Panya,Nyoka,Mbwa, bundi n.k Musa alisema kama mimi ni mtumishi wa Mungu na tuone kinachowatokea na ghafla ardi ikafumbua kinywa chake na ikawameza. Yoshua alipojua kuwa maadui zake walikuwa wanapigana nae kutoka kwenye nguvu zilizokuwa kwenye jua na yeye akaamua kulisimamisha jua. Nae Shetani aliamua kutumia mawambi na upepo ili kupigana na Yesu na wanafunzi wa Yesu hawakujua cha kufanya lakini Yesu alijua cha kufanya.​ 2. MAMLAKA JUU YA PEPO NA MARADHI. Luka 9:1 ‘’ Yesu akiisha kuwaita wale kumi na wawili pamoja, aliwapa mamalaka na uwezo wa kutoa pepo wachafu wote na kuponya magonjwa yote,’’ Kuwa na mamlaka haimaanishi kuwa unaweza kuitumia sawasawa kama Mungu anavyotaka bali kwa hiyo unahitaji sana kuomba sana ili Mungu akupe maarifa vizuri namna ya kutumia mamlaka hii uliyopewa na Mungu.​ 3. MAMLAKA JUU YA MFUMO WA UTAWALA WA GIZA/ SHETANI. Waefeso 6:12 ‘’ wamba mweze kuzipinga hila za Shetani. 12Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho’’ Mamlaka ya hapa ni tofauti na ile mamlaka ya kwenye Luka 9:1 , kwa mfano mamlaka juu ya Tanzania na mamlaka ya juu ya watanzania ni tofauti kwa sababu Mamlaka juu ya Tanzania ni juu ya mfumo bali mamalaka juu ya watanzania ni juu ya watu. Kwa hiyo mfano Tanzania kiongozi akifa, watu watahuzunika afu baadae watateua mwingine maana nafasi ile ipo kisheria. Kwa maana hiyo huwezi tumia mamlaka juu ya pepo ili kuja kushughulikia falme. Hizi ni mamlaka unahitaji kujua.​ 4. MAMLAKA JUU YA UFALME WA MBINGUNI. Mathayo 16:19 ‘’ 19Nitakupa funguo za Ufalme wa Mbinguni na lo lote utakalolifunga duniani litakuwa limefungwa Mbinguni, lo lote utakalofungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni.’’ Kwa hiyo jua kuwa mamlaka zina mipaka, kwa hiyo ili jambo lifunguliwa Duniani ndipo linafunguliwa na mbinguni. Lakini order intoka Duniani. Pia Mungu ametupa kufungua vitu vingine. Kwa hiyo ujio wa Dhambi Duniani iliondoa ufalme wa Mungu. Hata wale waliofungwa na kuzimu unaweza wafungua. Kwa hali hii ni hatari sana kwa Mtu aliyeokoka kutokaa kwenye mamlaka ya ufalme wa Mungu. Hivyo Mungu anaweka watu kwenye mamlaka ili waweze kuzisimamia. Mtu yeyote anapookoka anahamishwa kutoka ufalme wa giza na kuletwa kwenye ufalme wa Mungu.​ 5. MAMLAKA JUU YA DHAMBI. Warumi 6:12-14 ‘’ 12Kwa hiyo, msiruhusu dhambi itawale ndani ya miili yenu, ipatikanayo na kufa, ili kuwafanya mzitii tamaa mbaya. 13Wala msivitoe viungo vya miili yenu vitumike kama vyombo vya uovu vya kutenda dhambi, bali jitoeni kwa Mungu, kama watu waliotolewa kutoka mautini kuingia uzimani. Nanyi vitoeni viungo vya miili yenu Kwake kama vyombo vya haki. 14Kwa maana dhambi haitakuwa na mamlaka juu yenu, kwa sababu hampo chini ya sheria, bali chini ya neema. Warumi 7:15-24 ‘’14 Kwa maana tunajua kwamba sheria ni ya kiroho, lakini mimi ni wa kimwili nikiwa nimeuzwa kwenye utumwa wa dhambi. 15Sielewi nitendalo, kwa maana lile ninalotaka kulitenda, silitendi, lakini ninatenda lile ninalolichukia. 16Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, ni kwamba ninakubali kuwa sheria ni njema. 17Lakini, kwa kweli si mimi tena nitendaye lile nisilotaka bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 18Kwa maana ninafahamu kwamba hakuna jema lo lote likaalo ndani yangu, yaani, katika asili yangu ya dhambi. Kwa kuwa nina shauku ya kutenda lililo jema, lakini siwezi kulitenda. 19Sitendi lile jema nitakalo kutenda bali lile baya nisilolitaka, ndilo nitendalo. 20Basi kama ninatenda lile nisilotaka kutenda, si mimi tena nifanyaye hivyo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu. 21Hivyo naiona sheria ikitenda kazi. Ninapotaka kutenda jema, jambo baya liko papo hapo. 22Kwa maana katika utu wangu wa ndani naifurahia sheria ya Mungu. 23Lakini ninaona kuna sheria nyingine inayotenda kazi katika viungo vya mwili wangu inayopigana vita dhidi ya ile sheria ya akili yangu.Sheria hii inanifanya mateka wa ile sheria ya dhambi inayofanya kazi katika viungo vya mwili wangu. 24Ole wangu, mimi maskini! Ni nani atakayeniokoa na mwili huu wa mauti?.’’​ Kwa hiyo tulitegemea hapa Paulo aliposema kuwa Dhambi isitawale maishani mwenu na tulitegema Yeye asiwe na dhambi lakini tunachokiona hapa ni kuwa Pualo anakiri kuwa anadhambi, Kwa hiyo haikukugurantee wewe kuwa na upako kama Paulo na usiwe na dhambi. Na Tafsri ya dhambi ni Uasi lakini hii nayo uhalali wa dhambi kututawala bali sisi tushinde dhambi. Utajiuliza ni Kitu gani kilikuwa kinamkwamisha Paulo jibu lake ni hili ni MWILI, hata siku moja jaribu kumuuliza Yesu kuwa ni kitu gani kilikuwa kinakukwamisha kwenda msalabani na ulilia sana pale Getsamen atakuambia ni Mwili ndio maana alisema roho I radhi ila mwili ni dhaifu. Nia na Mwili ni Mauti , maana mwwili hauendi mbinguni na mwili hautiii cha Mungu. Kwa hiyo ile wewe kuwa na mamlaka juu ya pepo wabaya au maradhi haikupi kibali cha kwenda mbinguni maana Yesu alisema watasema mbona tulitoa unabii, pepo kwa jin lako lakini yeye atawaambia kuwa sikuwajua ninyi. Na ndio maana aliwaambia wanafunzi wake msifurahi kwa kuwa pepo wanawatii bali furahini kwa kuwa majina Yenu yameandikwa mbinguni. Kwa hiyo mamlaka hizi zinatupa namna ya kutembea hapa Duniani na sio kwenda mbinguni. Suala la kwenda mbinguni ni suala jingine kabisa. Ukiwa na mamlaka iiswe sababu ya wewe kuoandisha mabega na kumsahau Mungu wako. Lengo la kukuonesha utofauti wa mamlaka hizi ni kujua namna ya kwenda nazo maana kila mlango unafunguo zake maana huwezi tumia funguo za Bedroom ili kufungulia stoo uwe na uhakika hazitafungua. Yakobo 5:15 Biblia inasema kuomba kwake mwenye haki kwafaa sana akiomba kwa bidii maana maombi kama hayo yanaweza mfungua mgonjwa na kumponya magonjwa yake na kusamehewa dhambi zake. Kwa hiyo unaweza kumuombea Mtu hata kama hana mpango wa kutubu ila kwa sababu wewe umeomb Mungu anamsamehe kabisa. Ndio maana Mungu anatumia kuhani na kuwaombea watu au kufanya upatanisho na namna ya kufanya toba ili Mungu aje na atengeze hapo mahali ambapo pana dhambi.Unahitaji kujua sana siri hii ya kufanya maombi ambayo yatashughulika na chanzo cha maradhi au magonjwa mabacho ni dhambi.​ 6: MAMLAKA JUU YA MALANGO YA ADUI. Mwanzo 22:17 Uzao wako utamiliki malango ya adui. Galatia 3:13,14,29 Biblia inasema amelaaniwa yuke angakue juu ya mti, na Yesu alifanyika laana ili kwa ajili yake ili sisi tupate neema ya kufikiwa na Braka za Ibrahimu ambazo Mungu alituahidi kwa watu wa Duniani kote.​ 7: MAMLAKA JUU YA MIJI. Luka 19:16-19 Habari za Yule kabaila au kwa lugha ya sasa tungemwita Mwekezaji na wale watu walipewa yale mafungu ya fedha. Mafungu 10 alileta faida mara 10 na akapewa mamlaka juu ya miji kumi. Mafungu 5 alileta faida mara 5 na akapewa mamlaka juu ya miji mitano. fungu 1 alileta Hakuleta faida yoyote bali alirudisha fedha tu na haikuwa na faida na akinyimwa mamlaka juu ya miji. Uaminifu juu ya fedha hauleti mamlaka bali uaminifu juu ya matumizi ya fedha ndio unaleta mamlaka juu ya miji.Mwekezaji anaanza kuheshimika kwenye jamii au mji aliopo kwa sababu ya kuwa na fedha. Kwa hiyo hata dini yake nayo inapata sauti kila mtu ataanza kuiheshumu. Usijulize hili ni swala la ulimwengu wa Roho.​ 8: MAMLAKA JUU YA MIFUMO YA KIUTAWALA YA WANADAMU. Waefeso 2:6. 6Mungu alitufufua pamoja na Kristo na kutuketisha pamoja naye katika ulimwengu wa roho katika Kristo Yesu Waefeso 1:20-23 20ambayo aliitumia alipomfufua Kristo kutoka kwa wafu, akamketisha mkono Wake wa kuume katika mbingu, 21juu sana kuliko falme zote na mamlaka, enzi na milki na juu ya kila jina litajwalo, si katika ulimwengu huu tu, bali na katika ule ujao pia. 22Naye Mungu ameweka vitu vyote viwe chini ya miguu Yake na amemfanya Yeye awe kichwa cha vitu vyote kwa ajili ya Kanisa, 23ambalo ndilo mwili Wake, ukamilifu Wake Yeye aliye yote katika yote. Ufalme wa wadamu umetambulishwa kama NGUVU AU USULTANI lakini vyote ni ufalme wa wanadamu. Soma Ufunuo 17:1-2​ 9: MAMLAKA JUU YA MAENEO MUHIMU YENYE MAKUSNYIKO YA WATU. Ufunuo 5: 9-12 Wanamiliki juu ya i) Kabila ii) Lugha iii) Jamaa/ukoo iv) Taifa. Ufunuo 17:15- Ndio maanampinga kristo anafuatilia juu ya soko yaani kuuza na kununua kila sehemu yeye anafuatilia hasi kwenye mitandao. Soma Ufunuo 13.​ 10: MAMLAKA JUU YA KILA FIKRA. 2Wakorintho 10:3-5 3Ingawa tunaishi duniani lakini hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo. 4Silaha za vita vyetu si za mwili, Bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome. 5Tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo Jiulize swali hili je kuna fikra ngapi ambazo hazimtii kristo na je sisi tumechukua hatia gani ili kuzifanya zimtii kristo. Chukua hatua kushughulika na kila fikra isyomtii kristo na iweze kumtii kristo.​ 11: MAMLAKA JUU YA ULIMI NA KINYWA CHAKO. Yakobo 3:1-12 Mtu Yupo kama meli, mtu atakula matunda ya kinywa chake. Kwa hiyo hata ndoa nyingi huvunjika kwa sababu ya maneno na hadi hufika hatua ya kusambaratika kabisa. Ulimi ni Karamu na Roho Mtakatifu ni wino. Kwa hiyo kuwa makini sana na matumizi ya ulimi wako.   Marko 11: 27-28 ‘’ 27 Wakafika tena Yerusalemu, wakati Yesu akitembea hekaluni, viongozi wa makuhani, walimu wa sheria pamoja na wazee wakamjia.28Wakamwuliza, “UNAFANYA MAMBO HAYA KWA MAMLAKA GANI? Naye ni nani aliyekupa MAMLAKA YA KUFANYA HAYO?​ Matendo ya Mitume 4:5-7 ‘’ 5 Siku ya pili yake viongozi wa Kiyahudi, wazee na waandishi wa sheria wakakusanyika Yerusalemu, 6walikuwepo Kuhani Mkuu Anasi, Kayafa, Yohana, Iskanda na wengi wa jamaa ya Kuhani Mkuu. 7Wakiisha kuwasimamisha Petro na Yohana katikati yao, wakawauliza, “Ni kwa UWEZO GANI AU KWA JINA LA NANI mmefanya jambo hili?”’’ Ile kuwa tu na mamlaka haitoshi bali leo nataka tuangalie Zaidi kuwa hizo mamlaka nilizokufundisha jana utazitumiaje. Leo tunaangalie VITU VITAKAVYOKUWEZESHA UITUMIE IPASAVYO MAMLAKA ULIYOPEWA NA MUNGU​ Mwanzo 1:28 ‘’ 28 Mungu AKAWABARIKI na akawaambia, “Zaeni na mkaongezeke, mkaijaze tena dunia b na kuitiisha. Mkatawale samaki wa baharini, ndege wa angani na kila kiumbe hai kiendacho juu ya ardhi.’ Neno AKAWABARIKIA maana yake ni kuwa akawapa vitu ambavyo vitawawezesha kufanya yale ambayo Mungu aliwaagiza kufanya. Na ukiangalia vizuri utaona kuwa Mungu aliwabariki kabla ya kuwaingiza kazini au kuwapaagizo la kuwa zaeni mkaongezeke na kuijaza nchi na kuitisha.​ KAZI YA BARAKA. Kazi ya Baraka ni kukuwezesha kuwa kama Mungu anavyotaka uwe au anavyotaka ufanye kama vile yeye anavyotaka. MAANA YA KUITISHA, ni kumiliki kwa amri au mamalaka hata kama nchi haitaki. Kwa hiyo msisitizo wa Somo kuwa tu na mamlaka bali ni kujua namna ya kuitumia. POINTI YA 1 . MUNGU AKUPE KUJUA YA KUWA MAMLAKA ALIYOKUPA KATIKA KRISTO NI MAMLAKA AMBAYO CHIMBUKO LAKE NI ULIMWENGU WA ROHO. Leo natakata twende kwa mifano ili tuweze kuelewana katika somo hili. Tuangalie mamlaka amabayo Mungu amaetupa katika uumbaji wake Mwanzo 1 :24-28 Katika kitabu cha mwanzo utaona uumbaji wa Mungu na Mungu kuwabarikia watu wake. Kumbuka kuwa Mtu ni Roho anayo nafsi anaishi katika mwili. Na ukisoma katika Mwanzo sura ya 1 na 2, tunaona Sura ya 1 roho ya mwanadamu ikiumbwa na baadae kaika sura ya pili ndio tunoana mwili kuumbwa na kuweka pumzi na kuwa nafsi hai.Hivyo Mwanaume na Mwanamke waliumbwa wote kwenye sura ya kwanza ila miili yao ndio imekuja kuumbwa kwenye sura ya pili. Suala la Mwanamke ni kuzaa au kutozaa ni sauala la ulimwengu wa roho kabla halijawa suala la kimwili. MFANO: Kuna mwanamke mmoja katika mkoa mmoja nilikukokwa nafanya semina na alikuwa na tatizo la kupata mimba maana kila akipata mimba zinakaa miezi miwili tu na huwa zinatoka. Na yapata mimba kama 6 ivi zilikuwa tayari zimeshatoka. Na akaja na tukaomba Mungu lile tatizo liondoke na kweli baada ya Muda akaja akapata mimba na hiyo mimba nayo ikatoka. Na alipokuja tena kwangu nikamuuliza kwanini umetoa mimba. Akaanza kujitetea kuwa Mwakasege mimi sijatoa mimba imetoka yenyewe, bali mimi nikamuuliza jibu swali kwa nini umetoa mimba. Ilikuwa ni ngumu sana kwa yule mama kunielewa ila nikamuuliza kuwa ivi je maiti huwa inapata mimba. Akasema hapa ni kasema kwa hiyo kipi kinapata mimba ni roho au mwili wako? Na akasema ni roho kwa hiyo nikamuambia ukipata mimba nyingine tena isemeshe kuwa usitoke hadi miezi tisa itakapotimia. Tukaomba nikamuacha. Baada ya Muda akaja akapata mimba tena na baada ya miezi miwili dalili za kutoka mimba zikaanza tena na akaanza kutatufuta kila mahali na Mungu alituficha kila akija mahali tulipo anatukosa mara utasikia tumeondoka na kwenda mahali pengine. Baada ya kutukosa akarudi kwake na kuanza kusoma yale tuliyomfundisha. Na alipoanza kikiri ile mistari mara ile hali ikakoma na akapata mtoto wa kwanza na wa pili na wa tatu …. Ooh haleluya haleluya. Hapa nataka uone jinsi Mungu alivyomfundisha Imani na hakika Mungu alimsaidia. Jifunze sana juu ya kutumia mamlaka ambazo Mungu ametupa. Kutoka 10:21-23 21 Kisha BWANA akamwambia Musa, “Nyosha mkono wako kuelekea angani ili giza litande katika nchi ya Misri, giza ambalo watu wanaweza kulipapasa na kulihisi.’’ 22Kwa hiyo Musa akaunyosha mkono wake kuelekea angani, na giza nene likafunika pote katika nchi ya Misri kwa muda wa siku tatu. 23Hakuna mtu ye yote aliyeweza kumwona mwenzake, wala kuondoka mahali alipokuwa kwa muda wa siku tatu. Lakini Wasraeli wote walikuwa na mwanga katika maeneo yao waliyokuwa wanaishi Hapa tunaona wana wa Israel wakiwa na Nuru na Wamisri wakiwa na giza na ili uelewe vizuri mamlaka hii aliyoitumia Musa kuingilia mfumo wa Nuru inabidi uone kilichoandikwa kwenye kitabu cha​ Mwanzo 1:14-15 ‘’ Mungu akasema, “Iwepo mianga kwenye nafasi ya anga ili itenganishe mchana na usiku, nayo iwe alama ya kutambulisha majira mbali mbali, siku na miaka, 15nayo iwe ndiyo mianga kwenye nafasi ya anga itoe nuru juu ya dunia.’’ ​ Ikawa hivyo Kazi ya Jua ni kutawala mchana na mwezi utawale usiku. Lakini Musa alipewa mamlaka ya kuweza kuingilia mfumo wa jua na kukata mwanga wa wamisri na kuweka mwanga kwa wana wa Israel. Yaani ina maana wamisri walikuwa hata wakiwa na taa zilikuwa hazitoi mwanga. Suala la giza na nuru kabla halijawa suala la kimwili limekuwa suala la kwanza kabisa katika ulimwengu wa roho. Chanzo cha kusoma haya ni kutokana na hali iliyokuwa ikinusumbua sana ya mvua kunyesha kila mahali ukiweka hema hii ya kwetu mvua ilikuwa inaanza kunyesha au hata me mwenyewe nikenda mahali utakuta mvua tu inaaanza hata kama sio majira yake. Ndio nikaanza kutafuta majibu kwenye biblia. Na ndipo Mungu aliponifundisha namna ya kuingilia majira na namna ya kuidhibiti mvua. MFANO WA MOROGORO. Nakumbuka mwaka mmoja tulikuwa tunaandaa semina ya Morogoro na nikawauliza wenyeji wakasema mvua kwa sasa imeisha na tukapeleka hema na sku ile tunafunga hema mvua kubwa ikawa inanyesha na wenzutu walijenga hema katikati ya mvua na semina nayo ilianza kwenye mvua kama siku tatu ivi mvua ilikuwa inanyesha na watu walikuwa wanakuja wengi na miamvuli. Hapo nikaona sasa hii mvua itatuharibia utaratibu na utulivu nikaomba Mungu mvua ile iache kunyesha hadi tutakopamaliza semina. Na nilikuwa nakaa kwenye hoteli karibu na milima ya uluguru. Na mvua ikaanza kunyesha milimani nilikuwa nainyoshea kidole kuwa ewe mvua usije huku mjini hadi nimalize semina. Na baada ya hapo unaona wingu linaondoka na mvua inakoma kabisa. Basi siku ile ya mwisho tunamaliza semina nikawaambia wakazi wa Morogoro kuwa samahani jamani nilimaisha mvua ili tuwe na semina ila kuanzia kesho saa kumi mvua itarudi (baada ya kuwaambia wenzangu kuwa hema litaanuliwa kabla ya saa kumi na kuweka kwenye gari tayari kwa safari). Basi mtu mmoja alisema haya anayoyasema yakitokea me ntaokoka. Baada ya saa kumaliza semina ile kesho yake tulimtembelea mtu mmoja Morogoro tukawa tunamsalimia na ilipofika saa kumi baada ya kuwasiliana na wenzangu kuwa hema na ila kitu tayari wamepakia kwenye lori la kwetu na manyunyu ya mvua yakaanza taratibu, na mkwe wangu akanikumbusha kuwa tuliiambia mvua inyeshe kuanzia saa kumi na kuendelea sisi kukaa pale ile tulikuwa tunaizuia ile mvua. Basi tukaaga na tulipoanza kuondoka maana tulikuwa tunaenda Dar es Salaam kwa gari. Mvua kubwa ilinyesha Morogoro usiku kucha na kesh yake ikaendelea kusnyesha na kunyesha. Watu wakampigia simu mwenyekiti wa kamati ya kwetu Morogoro ya kuwa tunaomba Mwambie mwakasege aisimamishe mvua sasa maana inatosha sasa. Oooh haleluya haleluya….. Hii ni mamlaka ambayo Mungu anakupa lazima unajua kuwa ni mamlaka ya ulimwengu wa roho na inahitaji hekima sana kuitumia na usiitumie wewe utakavyo maana utaanza kuleta usumbufu kwa watu wengine. MAMLAKA JUU YA MFUMO WA SHETANI. Waefeso 6:12 ‘’ 12 Kwa maana kushindana kwetu si juu ya nyama na damu, bali dhidi ya falme, mamlaka, dhidi ya wakuu wa giza na majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.​ Waefeso 3:8-11 ’’ 8Ingawa mimi ni mdogo kuliko aliye mdogo kabisa miongoni mwa watakatifu wote, nilipewa neema hii ili niwahubirie watu Mataifa kuhusu utajiri usiopimika ulio ndani ya Kristo na 9kuweka wazi kwa kila mtu jinsi ile siri iliyokuwa imefichwa kwa nyakati zote katika Mungu aliyeumba vitu vyote.10Ili kwa njia ya Kanisa, hekima yote ya Mungu ipate kujulikana kwa watawala na WENYE MAMLAKA KATIKA ULIMWENGU WA ROHO,11SAWASAWA NA KUSUDI LAKE LA MILELE KATIKA KRISTO YESU BWANA WETU. 12YEYE AMBAYE NDANI YAKE NA KWA NJIA YA IMANI KATIKA YEYE TUWEZE KUMKARIBIA MUNGU KWA UJASIRI NA KWA UHURU.13Kwa hiyo, nawaomba msikate tamaa kwa sababu ya mateso yangu kwa ajili yenu, hayo ni utukufu wenu. Kwa hiyo ile kuwa na mamlaka juu ya mfumo wa shetani haitoshi bali inahitajika pia kujua mamlaka juu ya mfuno wa utawala wa wanadamu. Angalia Waefeso 1:20 utaona neno katika Ulimwengu wa roho juu sana kuliko falme na mamlaka na kila jina litajwalo. Mungu katuweka juu sana juu ya mamlaka juu ya ufalme wa Shetani na ufalme wa Wanadamu. Hivyo ni muhimu sana kuwa na maarifa ya kushughulika na watu na mifumo yao ya kiutalawa. MAMLAKA JUU YA KILA FIKRA. 2Wakorintho 10:3-5 ‘’ 3Ingawa tunaishi duniani lakini hatupigani vita kama ulimwengu ufanyavyo. 4Silaha za vita vyetu si za mwili, Bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome. 5Tukiangusha mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinuacho juu ya elimu ya Mungu na tukiteka nyara kila fikira ipate kumtii Kristo. Hapa tunaona kuwa hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili bali tunafanya kwa jinsi ya rohoni na tukiangusha mawazo na kila fikra isiyo mtii kristo na ipate kumtii kristo. Na kila kijiinuacho juu ya Elimu ya Mungu nacho kipate kumtii Mungu. Twende kwa Yesu tukawaangalie wanafunzi wawili yaani Yuda na Petro. Yuda alikuwa ni mpole sana na Petro kwa lugha ya sasa tungesema alikwa na kiherehere sana au msemaji sana. Petro aliposikia habari za Yesu kwenda msalabani alimwita na akaanza kumkemea na kumwambia rudi nyuma ewe shetani kwa sababu huwazi ya Mungu. Yesu alikuwa anamwambia petro umeside/ umeingiliwa na shetani saa ngapi. Bila Yesu kumkemea shetani lile pepo lingeendelea kumsumbua sana Petro. Hii ilitokana na Shetani kuomba kibali kuwa anataka awapepete kama ngano na Yesu akamwambia Petro shetani ameomba kibali ili awapepete kama ngano lakini mimi Yesu nimekuombea ili utakapoongoka uwaimarishe na dnugu zako. Yesu alipokuwa anazungumza na wanafuzni wake kuwa watamkibia na kumkataa ila Petro alisema mimi sitaweza, Yesu alimwambia kuwa Petro utanikana Mara tatu na Petro alimkana Yesu mara tatu na mara ya tatu alinaani kabisa. Ina maana alikuwa maejitoa kwenye uanafunzi wa Yesu. Ndio maana Yesu alipofufuka aliwaambia waambieni wanafunzi wangu na Petro ile neno Na Petro ina maana petro hakuwa mwanafunzi tena. Na ndio maana Yesu alipokuwa nazngumza nao alimwambia Petro mata tatu kuwa je wanipenda, hii ilikuwa ni kumsaidia Petro maan aalimkana Yesu mara tatu. MFANO. Wangapi hapa wanajua kuendesha baiskeli, na je unaweza kuacha kuandesha baiskeli, jibu ni hapana. Maana yake ni kuwa kitu kimeingia kwenye mfumo wako wa fahamu na halitoki. Hata kama haumkumbuki aliyekufundisha kuendesha baiskeli ila hautakauja ushahau kuendesha baiskeli. Kwa hiyo kumkemea pepo tu haitoshi maana huwezi jua kuwa ni kitu gani kaweka kwenye fikra za mu huyo. Hivyo pia kuomba matengenezo kutoka kwa Mungu juu ya mtu ambaye umekea lile pepo limtoke ili mfumo wake wa fikra urudi kama Mungu alivyoagiza. Luka 22:1-6 Hapa tunaona Shetani akimwingia Yuda na kumfanya amsaliti Yesu, na Yuda aliwaambia wakuu wa makuhani kuwa yeye ndiye aliyekuwa karibu sana na Yesu na akawapa na mbinu za namna ya kumkamata na jinsi atavyofanikisha ndipo akapewa rushwa ya vipande thelathini vya fedha. Shetani nae alikamata fikra za Yuda hadi hukumu ilipoingia ndani ya Yuda na aksahau hadi kumwamini MUngu ili kuwa anawezakumsamehe maana Mungu anasema dhambi yako ijapokuwa nyekundu kama damu itakuwa nyeupe kama theluji, ila Yuda alisahauna hadi akajinyonga. Hata kama umemkosea Mungu namna gani rudi kwa Mungu na Mungu atakusamehe, usiogope rudi kwa Bwana maana huko kwingine hakuna msaada na usije fanya maamuzi kama Yuda, Njoo kwa Yesu ndio maana alikufia msalabali rudi rudi kwa Bwana. Elimu ni suala la kiroho kabla halijawa la kimwili na ona maarifa ambayo watu wanapewa baada ya Muda utakuja kuona watu wanaanza kujitenga na Yesu na kuanza kukaa mbali na uso wa Mungu. Kwa hiyo ni muhimu sana kuombea elimu ambazo watu wanapewa ili ziwe za Elimu ya Mungu na sio zingine maana shetani nae ana elimu yake inayomnfanya amkatae Mungu. Ili kujinaua hapo mahali Fanya maombi ya aina tatu. 1: OMBA KWA MUNGU MACHO YAKO YATIWE NURU. Waefeso1:17-23 ndio maana Paulo aliwaombea watu wa efeso japo walikuwa wameokoka lakini aliwaombea maombi haya. Na mimi ni sala yangu ya kila siku huwa najiombe maombi haya mara kwa mara.na wewe chukua sala hii ni ya kwako jiombee kila siku kila siku na iwe ni utaratibu wa maisha yako ya kila siku 2: OMBA MUNGU AKUPE KUTAFSIRI KWA JINSI YA ROHONI KWA MANENO YA ROHONI. 1Wakorintho 10:10-14 na Waebrania 11:3 Kwa Imani twafahamu kuwa ulimwengu uliumbwa kwa vitu visivyooneka, na katika warumi 10:17 imani huja kwa kusikia na katika ulimwengu war oho inatupa kufahamu. 3: OMBA MUNGU AKUSAIDIE KUKUA KIROHO. Wagalatia 4:1-2 Lakini nalisema nanyi kama watoto. Mrithi ajapokuwa mtoto huwa kama mtu hadi pale wakati ule ulioamriwa na Bwana wake. Kwa hiyo lazima ukue kiroho ili ukue kiroho na ndipo vitu vingine utaweza kuvitumia. Mfano: Ukiwa na mtoto wako mwenye miaka 10 ukamnunulia gari na ukampa kuwa uwe ni urithi wake, hata kama anajua kuendesha sharia ya nchi haimruhusu kuanza kuendesha gari kwa sababu hajatimiza miaka 18. Kwa hiyo ukubwa (ukomavu) ni muhimu sana katika ulimwengu wa roho. Ikiwa bado hujampokea Bwana Yesu pamoja na vipawa vya Roho mtakatifu tafadhali wasiliana nasi kwa namba zifuatazo.0695540999/0789001312UBATIZO SAHIHI NI KWA JINA LA YESU KWAHIYO KAMA HUJABATIZWA UBATIZO SAHIHI BASI TAFUTA KANISA LINALOBATIZA KWA MAJI MENGI NA KWA JINA LA YESU.KAMA UKIHITAJI KUJIFUNZA ZAIDI WASILIANA NASI KWA HIZO NAMBA HAPO JUU PIA TUNA GROUP LA WHATSAPP LA KUJIFUNZA TU BIBLIA HIVYO NYOTE MNAKARIBISHWA. Ubarikiwe sana Bwana Ev.Gidion laizer NURU YA UPENDO ARUSHA
    Like
    3
    4 Commentarios 0 Acciones 15K Views 0 Vista previa


  • Wanyama wanne wa Danieli 7

    Karibu tujifunze kitabu hiki cha Daniel sura ya 7 ili tupate kujua BWANA ALIMFUNULIA NINI DANIEL KATIKA NDOTO NA KWETU SISI INATUFUNULIA NINI.Basi andaa moyo wako kujifunza karibu sana

    Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danieli aliona ndoto na maono kuhusu wanyama wanne ambao ni falme au mataifa manne. Aliona pepo nne za mbinguni zikivuma juu ya bahari kubwa, kisha wanyama wanne wakubwa wenye sifa tofauti tofauti walitokea juu bahari. Baadaye, Danieli alitamani sana kujua maono hayo yalimaanisha nini, hivyo alimkaribia malaika Gabrieli aliyekuwa amesimama karibu naye ili amfahamishe ukweli wa maono hayo. Naye malaika akamfahamisha.

    Danieli 7:2 “Danieli akanena, akisema, Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa.”

    “Pepo” katika unabii hutumika kuwakirisha vita, tufani, au ghasia. Yeremia 25:32 inasema, “BWANA wa majeshi asema hivi, Tazama, uovu utatokea toka taifa hata taifa, na tufani kuu itainuliwa toka pande za mwisho wa dunia.” Katika Ufunuo 7:1-3 tunaona malaika wameamuriwa kuzishikilia “pepo” nne; yaani kuzuia vita hata Mungu atakapomaliza kuwatia mhuri watu wake. Hivyo upepo katika unabii = vita, tufani au dhoruba.

    “Bahari” au maji katika unabii hutumika kuwakilisha mataifa na watu, Ufunuo 7:15 inasema, “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.” [angalia pia Isaya 8:7].

    Danieli 7:3 “Ndipo wanyama wanne wakatokea baharini wote wa namna mbalimbali.”

    “Mnyama” katika unabii hutumika kuwakilisha taifa au ufalme, malaika katika Danieli 7:17 alipomfahamisha Danieli kuhusu maono haya, alisema, “Wanyama hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani.” Hivyo, wale wanyama wanne wa Danieli 7:3 wanaotokea baharini ni wafalme wanne watakaotokea miongoni mwa mataifa na watu (duniani). Bahari = watu.

    Danieli 7:4 “Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu.”

    Mnyama wa kwanza aliye kama simba kwa hakika ni ufalme wa Babeli, ambao ulikuwa ukitawala wakati wa nabii Danieli. Sifa za mnyama huyo za kuwa kama simba, na kuwa na mabawa kama ya tai, zinawakilisha kuwa ufalme huo ungekuwa na nguvu nyingi na mwepesi katika kufanya vita, hii ni sawa na ufalme wa Babeli wakati wa mfalme Nebukandreza. Yeremia alipotabiri juu ya Yerusalemu kuhusuliwa na Babeli, alitaja sifa za Babeli kama tai. Yeremia 4:7, 13 inasema, “Simba ametoka katika kichaka chake, ndiye aangamizaye mataifa;…Tazama atapanda juu kama mawingu, na magari yake ya vita yatakuwa kama kisulisuli; farasi zake ni wepesi kuliko tai…” Pia Habakuki 1:6, 8 inasema, “Kwa maana, angalieni, nawaondokeshea Wakalidayo, taifa lile kali, lenye haraka kupita kiasi; wapitao katikati ya dunia, ili wayamiliki makao yasiyo yao…wapanda farasi wao watoka mbali sana; huruka kama tai afanyaye haraka ale.” Hivyo, yule mnyama wa kwanza anawakilisha ufalme wa Babeli.

    Danieli 7:4 juu ya mnyama wa kwanza inasema, “…naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi…naye akapewa moyo wa kibinadamu.” Badiliko hili lililotokea la mabawa yake kufutuka manyoya na kupewa roho ya kibinaadamu, linawakilisha kupungua kwa nguvu na wepesi wa ufalme wa Babeli, kitu ambacho kilitokea baada ya mfalme Nebukandreza kupita, na ufalme ukawa dhaifu na usio na nguvu wakati wa utawala wa wafalme; Nabonadius and Belshaza.

    Danieli 7:5 “Na tazama, mnyama mwingine, wa pili, kama dubu, naye aliinuliwa upande mmoja, na mifupa mitatu ya mbavu ilikuwamo kinywani mwake katika meno yake; wakamwambia mnyama huyo hivi, Inuka, ule nyama tele.”

    Mnyama wa pili kwa hakika anawakilisha ufalme wa Umedi na Uajemi, ambao ulifuata baada ya ufalme wa Babeli kuanguka. Mnyama huyu aliye kama dubu, tena ameinuliwa upande mmoja, kwa hakika, ni ufalme uliokuwa na pande mbili “Umedi na Uajemi” ambapo upande mmoja wa Uajemi uliinuliwa zaidi kwa ukuu kuliko upande mwingine wa uamedi katika ufalme wa “Umedi&Uajemi. Zile mbavu tatu zilizo katika kinywa cha dubu, zinawakilisha nchi tatu Babeli, Lydia, na Misri ambazo zilihusuliwa na ufalme wa Umedi na uajemi.

    Danieli 7:6 “Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.”

    Mnyama wa tatu anawakilisha ufalme wa Ugiriki/Uyunani, ambao ulifuata baada ya ufalme wa Umedi na Uajemi kuanguka. Tafadhari kumbuka kuwa mnyama huyu wa tatu aliye kama chui, tena ana mabawa manne; angewakilisha taifa ambalo ni jepesi na la haraka zaidi kuliko taifa la Babeli ambalo lilikuwa na mabawa mawili pekee. Hii inawakilisha vizuri zaidi ufalme wa Ugiriki wakati ulipokuwa chini ya utawala wa Alexander, ufalme huo ulikuwa mwepesi na wa haraka sana katika kuhusuru miji, na uliyapanga majeshi yake kwa jinsi ambayo kamwe haifanani na nyakati zilizokuwa zimepita. Vile vichwa vinne vinawakilisha sehemu nne ambazo ufalme huo uligawanyika baada ya mfalme Alexander.

    Danieli 7:7 “Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.”

    Malaika Gabrieli katika Danieli 7:23 akimfafanulia Danieli ukweli kuhusu mnyama huyu wa nne alisema, “…Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia, utakaokuwa mbali na falme zile zote, nao utakula dunia yote, na kuikanyaga, na kuivunja vipande vipande.” Mnyama huyu wa nne anawakilisha ufalme wa Roma, uliofuta baada ya ufalme wa Ugiriki kuanguka. Ufalme huu unafananishwa na “chuma” ikimaanisha Jeshi lake ni katili na lenye nguvu nyingi sana. Danieli 7:7 inasema kuwa, ufalme huu wa Roma uko mbali/tofauti na falme zile tatu za Babeli, Umedi na Uajemi, na Ugiriki; Utofauti huo ni kwamba falme zile tatu zilikuwa falme za kipagani tu, lakini ufalme huu wa Roma ni mchanganyiko wa upagani na ukristo kwa wakati mmoja: yaan, upapa.

    Mnyama huyu wa nne ana pembe kumi kama Danieli 7:7 inavyomwelezea. Pembe katika unabii pia hutumika kuwakilisha ufalme au taifa, malaika Gabrieli katika Danieli 7:24 alipokuwa anamfahamisha Danieli ukweli kuhusu zile pembe kumi za yule mnyama wa nne, alisema, “Na habali za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.” Hivyo, zile pembe kumi za yule mnyama wa nne ambaye tumegundua kuwa ni Roma, pembe hizo ni mataifa kumi ambayo yapo katika ufalme wa Roma. Baada ya ufalme wa Roma ya kipagani kuanguka, katika mwaka 351 hadi 476 BK uligawanyika katika mataifa(pembe) kumi ambayo katika historia yamekuwa yakijulikana kama mataifa kumi ya Ulaya ya magharibi.

    Danieli 7:8 “Nikaziangalia sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang’olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu.”

    Malaika Gabrieli akifafanua kuhusu pembe hiyo ndogo itakayoinuka katika zile pembe kumi, katika Danieli 7:24 alisema, “Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.” Huko nyuma tumegundua kuwa zile pembe kumi za mnyama wa nne, zilizoorodheshwa katika Danieli 7:7 ni mataifa kumi ya Ulaya ya magharibi ambayo yaligawanyika katika ufalme wa Roma. Sasa katika Danieli 7:8 pembe nyingine ndogo ikainuka na ikang’oa pembe tatu katika zile pembe kumi.

    Katika Danieli 7:24 malaika akafafanua kuwa, ile pembe ndogo ni ufalme au taifa jingine dogo ambalo litatokea ndani ya ufalme huo wa Roma katika mataifa yale kumi au pembe kumi. Kisha taifa hilo dogo au pembe ndogo baada ya kutokea litaangusha mataifa matatu katika yale mataifa kumi ya mwanzo. Kwa hakika taifa hili dogo (au pembe ndogo) ni taifa dogo la Vatican(upapa) ambalo liliinuka baada ya mataifa yale kumi. Taifa dogo la Vatican(upapa) liliinuka kutoka katika taifa la Italia, na taifa la Italia ni moja wapo katika yale mataifa kumi ( pembe 10). Baada ya taifa la Vatican kuinuka liliyaondoa mataifa matatu katika yale mataifa kumi ya mwanzo, hii inaweza kufananishwa vizuri na ile pembe ndogo inayong’oa pembe tatu katika zile pembe kumi za mwanzo.

    Sababu ya taifa dogo la Vatican kuyaondoa mataifa matatu katika yale kumi ya mwanzo ni kwamba, taifa la Upapa(vatican) lilitaka kuyatawala yale mataifa kumi yote, lakini mataifa matatu yalikataa kujiweka chini ya utawala wa upapa, hivyo upapa ukafanya vita juu ya mataifa hayo matatu na kuyaondoa kabisa hata yasiwepo. Mataifa matatu yaliyoondolewa ni Heruli, liling’olewa na
    upapa mwaka 493 B.K.
    Vandal, liling’olewa na
    upapa mwaka 534 B.K.
    Ostrogoth, liling’olewa upapa mwaka 538 B.K.

    Ifuatayo ni orodha ya mataifa 10 ya ufalme wa Roma (au pembe 10 za mnyama), huku mataifa mataifa 3 yakiwa yameondolewa (au pembe tatu zikiwa zimeng’olewa) na utawala wa upapa (pembe ndogo).

    Saxon, kwa sasa ni
    taifa la Uingereza.

    Frank, kwa sasa ni
    taifa la Ufaransa.

    Alamanni, kwa sasa ni
    taifa la Ujerumani.

    Visigoth, kwa sasa ni
    taifa la Uhispania.

    Suevi, kwa sasa ni taifa
    la Ureno.

    Lombard, kwa sasa ni
    taifa la Italia.

    Burgundia, kwa sasa
    ni taifa la Uswidi.

    Heruli, liling’olewa na
    pembe ndogo 493 B.K.

    Vandal, liling’olewa na
    pembe ndogo 534 B.K.

    Ostrogoth,
    liling’olewa na pembe
    ndogo 538 B.K

    Ushahidi mwingine unaothibitisha kuwa ile pembe ndogo ya Daniel 7:8 ni utawala upapa, ni ushahidi unaopatikana katika Danieli 7:25 ambapo inasema,

    Danieli 7:25 “Naye (pembe ndogo) atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.”

    Hapa ushahidi usioweza kupingika ni swala la kubadili majira na sheria za Mungu, ni mamlaka ya upapa pekee ndiyo iliyobadili sheria za Mungu, Sabato kutoka siku ya saba(Jumamosi) kwenda siku ya kwanza (Jumapili).

    “Bila shaka kanisa la katoliki hudai kuwa badiliko, (la Sabato Jumamosi kwenda Jumapili) ilikuwa ni kitendo chake…na kitendo hicho ni ALAMA ya mamlaka yake katika mambo ya kidini.” –-H.F. Thomas, Chancellor of Cardinal Gibbons

    “Jumapili ni ALAMA yetu ya mamlaka…kanisa liko juu ya Biblia, na uhamishaji huu wa utunzaji wa Sabato ni ushahidi wa jambo hilo la ukweli.” -–Catholic Record of London, Ontario Sept 1, 1923.

    Pia Danieli 7:25 inasema, pembe ndogo atawadhoofisha watakatifu wa Mungu, nao watatiwa mikononi mwake kwa muda wa wakati mmoja, na nyakati mbili, na nusu wakati. Wakati mmoja = mwaka 1, nyakati mbili = miaka 2, na nusu wakati = nusu mwaka, (hivyo, 1+2+05=3.5 miaka 3 na nusu). Miaka 3 na nusu = miezi 42 au siku 1260.

    Katika unabii siku moja = mwaka 1, Ezekieli 4:6 inasema, “…siku arobaini, siku moja kwa mwaka mmoja, nimekuagiza.” Hesabu 14:34 pia inasema, “…siku arobaini kila siku kuhesabiwa mwaka…” Hivyo, kutokana na Ezekieli 4:6 na Hesabu 14:34, ni hakika kwamba siku 1260 ni sawa na miaka 1260 ambayo Upapa ungetawala na kuwadhofisha watakatifu.

    Historia inathibitisha kuwa Upapa ulipata nguvu kabisa kuanzia mwaka 538BK, baada ya kumaliza kuyang’oa mataifa 3, hivyo utawala rasmi wa upapa ulianza mwaka 538.

    “Vigillius…alikalia kiti cha upapa (538 B.K.) chini ya ulinzi wa jeshi la Belisarius.” –History of the Christian Church, Vol. 3, p. 327

    Hivyo, ukijumlisha ile miaka 1260 ambayo upapa ungewadhoofisha watakatifu katika mwaka 538BK, utapata mwaka 1798BK (538+1260=1798). Kwa hiyo upapa ungewadhoofisha watakatifu kuanzia mwaka 538BK, hadi 1798BK. Historia inathibitisha kabisa kuwa upapa uliwadhoofisha watakatifu tangu mwaka 538bk hadi 1798bk ambapo upapa ulipata jeraha la mauti.

    “Katika mwaka 1798 Jemedari Berthier aliingia Roma, akauondoa kabisa utawala wa upapa, na kuanzisha mwingine.” –Encyclopedia Britannica 1941 edition

    Upapa ulipoondolewa madarakani katika mwaka 1798BK, hapo ndipo mateso ya wakristo yalikoma vile vile kama Danieli 7:25 inavyosema. Kwa hakika hii ni miaka halisi 1260 au miaka ya kiunabii 3.5, au wakati, nyakati mbili, na nusu wakati ya Danieli 7:25.

    Historia inasema wazi kuwa Upapa uliwadhoofisha watakatifu kwa miaka 1260, hata kanisa la Romani Katoliki linakubali kuwa liliwatesa wakristo wakati huo wa zama za giza, na papa Yohane II mwaka 2000 alitubu dhambi ya kanisa ya kuua Wakristo zaidi ya milioni 100. Kifuatacho ni baadhi ya ushahidi unaothibitisha kuwa kanisa Katoliki liliua wtakatifu kama Danieli 7:25 inavyosema.

    “Kwa sababu ya kufundisha imani kinyume na mafundisho ya Roma, historia inaonyesha vifo vya wafia dini zaidi ya milioni 100” –Brief Bible Readings, p 16.

    “Katoliki ana baadhi ya sababu kwa upande wake wakati anapotoa adhabu kwa waasi wa kidini, kwa maana anajidaia jina la Ukristo kwake mwenyewe kwa kuzuia, na anajidai kufundisha kwamba uwepo wa Roho wa Mungu kamwe hautaondoka kwake…Siyo kosa zaidi kumuua mtu kwa sababu ya uasi wa kidini, kuliko kwa sababu ya uuaji,…[na] katika mambo mengi mateso kwa maoni ya kidini siyo tu kwamba yanaruhusiwa, lakini ni ya busara na ya lazima.” –The Lawfulnees of Persecution” in the Rambler, 4, June, 1849, pp 119, 126. (“The Rambler” lilikuwa ni gazeti la kila siku la Romani Katoliki lililochapishwa kuanzia mwaka 1848 hadi 1862).

    “Chini ya mawazo na desturi za kijerumani, mateso yalitumiwa kidogo kuanzia karne ya 9 hadi karne ya 12, lakini kwa uhuikaji wa sheria ya Romani mateso yalianzishwa tena katika karne ya 12…Katika mwaka 1252 (Papa) Innocent IV aliruhusu adhabu ya mateso juu ya waasi wa kidini kwa kutumia mamlaka ya kiserikali, na mateso yakaja kuwa na mahali palipojulikana katika utaribu wa mahakama ya kiuchunguzi.” –New Catholic Encyclopedia, arts. “Inquisition”, “Auto-da-Fe’,” na “Massacre of St Bartholomew’s Day.”

    Hukumu na ufalme wa watakatifu.

    Danieli 7:9 “Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mmoja wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao.”

    Danieli 7:10 “Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.”

    Hukumu ambayo inatajwa hapo ni hukumu ya upelelezi ambayo ilianza tarehe 22 Octoba 1844 mwishoni mwa Siku 2300 za kiunabii za Danieli 8:14. Katika mwaka 1844 ambapo Yesu alimaliza kazi yake ya Ukuhani katika chumba cha Patakatifu, na akahamia chumba cha Patakatifu mno kwa ajili ya kazi yake ya Upatanisho, vitabu vilifunuliwa kwa ajili ya kuanza hukumu. Na hukumu hiyo ilianza kwa waliokufa na itaendelea hata kwa walio hai ambao wamekuwa na nuru kuu lakini wakashindwa kuenenda katika nuru. Ukisoma vizuri katika Danieli 7:11, 26 utaona kuwa hukumu imethibitishwa juu ya mfumo wa Upapa na utawala wake wote wa Roma.

    Danieli 7:11 “Nikatazama wakati huo; kwa sababu ya sauti ya yale maneno makubwa iliyoyasema ile pembe(upapa); nalitazama hata mnyama(Roma) yule akauawa, mwili wake ukaharibiwa, akatolewa ateketezwe kwa moto.”

    Wakati malaika akimfahamisha Danieli juu ya hukumu itakayokuja juu ya upapa na juu ya dola na ufalme wote wa Roma, katika Danieli 7:26 alisema, “Lakini hukumu itawekwa, nao watamwondolea(pembe ndogo[upapa]) mamlaka yake, kuipoteza na kuiangamiza, hata milele.” Lakini kuhusu wale wanyama wengine watatu unabii unasema,

    Danieli 7:12 “Na kwa habari za wale wanyama wengine, walinyang’anywa mamlaka yao; walakini maisha yao yalidumishwa kwa wakati na majira.”

    Wanyama wale watatu walinyang’anywa mamlaka yao na mnyama wa nne ambaye ni ufalme wa Roma, lakini maisha yao yaliendelea kuwepo; kwa mfano, taifa la Babeli liliendelea kuishi mpaka sasa linajulikana kama taifa la Irak (Al Hillah), vile vile kwa Umedi na Uajemi, na Ugiriki. Mataifa haya yanaishi hata sasa lakini mamlaka yao walinyanganywa na dola la Roma.

    Tukiangalia wanyama wote wanne tunaona kama ifuatavyo:

    Mnyama=Ufalme.1.Babeli.2.Umedi/Uajemi.3.Ugiriki.4.Roma

    Mnyama wa nne ni ufalme wa nne na wa mwisho katika historia ya dunia, na ufalme huo ni Roma, una pembe kumi ambazo ni mataifa yake kumi, pia una pembe ndogo ambayo ni upapa. Je unapita muda mrefu kabla dunia haijaisha? Tuko katika nyakati za mwishoni kabisa za mnyama wa nne na wa mwisho. Na hivi karibuni Yesu atakuja na kuziangamiza falme zote na upapa, na kisha ataanzisha ufalme wake pamoja na watakatifu katika ulimwengu mpya, ambao hautakuwa na mwisho. Ni Yerusalemu mpya utakaoshuka kutoka juu mbinguni.

    Danieli 7:13 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu(Mwana wa Adamu) akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye.”

    Danieli 7:14 “Naye(Mwana wa Adam) akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.”

    Wakati umekaribia, naam, wakati umefika ambao Yesu atarudi duniani kuwachukua watakatifu wake, nao watatawala katika ufalme wake wa amani ambao uzuri wake hakuna mtu anayeweza kuuelezea, ni ufalme ambao si wa dunia hii bali wa ulimwengu mpya. Malaika akimfahamisha Danieli kuhusu mambo haya alisema,

    Danieli 7:27 “Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.”

    Danieli 7:22 “hata akaja huyo mzee wa siku, nao watakatifu wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia watakatifu waumiliki ufalme.”

    Danieli 7:28 “Huu ndio mwisho wa jambo lile. Nami, Danieli, fikira zangu zilinifadhaisha, na uso wangu ulinibadilika; lakini naliliweka jambo hilo moyoni mwangu.”

    Je ni upendo gani ambao Mungu ametupa kwa kutufunulia nyakati na majira ya mwisho wa ulimwengu? Hata kwa wale ambao hawaamini wanaweza kufunguliwa macho yao ili waone ni jinsi gani Yesu Kristo ni kweli na hakika, na kwamba nini tutakosa kama tusipomwamini Yeye. Leo ndiyo wakati wa kumtafuta Bwana kwa moyo wote, akili zote, na nguvu zote ili giza lisije kufika na kutukuta hatusitahili kuuingia ufalme wa Mungu. Ushauri wa Yesu ni kwamba, “kesheni na kuomba.”huku tukidumu katika utakatifu kwani tafsiri halisi ya kukesha maana yake tuwe macho kwakila jambo shetani asije akatuvamia tukaanguka dhambini hivyo jitenge na uovu.Haiwezekani kumuona Mungu pasipo utakatifu kwani utakatifu ndiyo njia tutakayopitia,ndiyo tiketi yakuingia katika ufalme wa Mungu.Isaya 35:8,Kumbuka Mungu anazuia mabaya yasiipate dunia na utawala mpinga Kristo kwaajili yakutukamilisha na kutupiga muhuri wake na muhuri huo ni wokovu kumpokea yeye na kumuamini na kumkiri yeye peke yake kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha yako.naye atakupa kipawa cha Roho mtakatifu atakaye kuwezesha kuishi kwa utakatifu hadi atakapo kuja.KUMBUKA HAKUNA MNYAMA MKUBWA NA WAKUTISHA KAMA DHAMBI RUMI YAKO YA LEO NI MOYO WAKO MWENYEWE,HIVYO ONDOA PICHA ZA KATOLIKI AKILINI MWAKO WEKA IMANI JUU YA YESU KRISTO KAMA UKISIKIA LEO ANABISHA BASI FUNGUA MOYO WAKO AINGIE NAYE ATAKUPA ZAWADI YA ROHO MTAKATIFU NA UZIMA WA MILELE UFUNUO 3:19-20.TAFUTA UBATIZO SAHIHI UKAZALIWE NA KUFUFULIWA NA KRISTO KIROHHO NA UKATISHWE NAYE MBINGUNI KWAANZIA SASA KIROHO.WAKOLOSAI 3:1-4,EFESO 2:4-7

    MUNGU AKUBARIKI SANA WEWE UTAKAYE SOMA UJUMBE HUU

    EV.GIDION LAIZER.
    NURU YA UPENDO ARUSHA

    Wanyama wanne wa Danieli 7 Karibu tujifunze kitabu hiki cha Daniel sura ya 7 ili tupate kujua BWANA ALIMFUNULIA NINI DANIEL KATIKA NDOTO NA KWETU SISI INATUFUNULIA NINI.Basi andaa moyo wako kujifunza karibu sana Katika mwaka wa kwanza wa Belshaza, mfalme wa Babeli, Danieli aliona ndoto na maono kuhusu wanyama wanne ambao ni falme au mataifa manne. Aliona pepo nne za mbinguni zikivuma juu ya bahari kubwa, kisha wanyama wanne wakubwa wenye sifa tofauti tofauti walitokea juu bahari. Baadaye, Danieli alitamani sana kujua maono hayo yalimaanisha nini, hivyo alimkaribia malaika Gabrieli aliyekuwa amesimama karibu naye ili amfahamishe ukweli wa maono hayo. Naye malaika akamfahamisha. Danieli 7:2 “Danieli akanena, akisema, Naliona katika maono yangu wakati wa usiku; na tazama, hizo pepo nne za mbinguni zilivuma kwa nguvu juu ya bahari kubwa.” “Pepo” katika unabii hutumika kuwakirisha vita, tufani, au ghasia. Yeremia 25:32 inasema, “BWANA wa majeshi asema hivi, Tazama, uovu utatokea toka taifa hata taifa, na tufani kuu itainuliwa toka pande za mwisho wa dunia.” Katika Ufunuo 7:1-3 tunaona malaika wameamuriwa kuzishikilia “pepo” nne; yaani kuzuia vita hata Mungu atakapomaliza kuwatia mhuri watu wake. Hivyo upepo katika unabii = vita, tufani au dhoruba. “Bahari” au maji katika unabii hutumika kuwakilisha mataifa na watu, Ufunuo 7:15 inasema, “Kisha akaniambia, Yale maji uliyoyaona, hapo aketipo yule kahaba, ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.” [angalia pia Isaya 8:7]. Danieli 7:3 “Ndipo wanyama wanne wakatokea baharini wote wa namna mbalimbali.” “Mnyama” katika unabii hutumika kuwakilisha taifa au ufalme, malaika katika Danieli 7:17 alipomfahamisha Danieli kuhusu maono haya, alisema, “Wanyama hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani.” Hivyo, wale wanyama wanne wa Danieli 7:3 wanaotokea baharini ni wafalme wanne watakaotokea miongoni mwa mataifa na watu (duniani). Bahari = watu. Danieli 7:4 “Wa kwanza alikuwa kama simba, naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi, akasimamishwa juu kwa miguu miwili kama mwanadamu; naye akapewa moyo wa kibinadamu.” Mnyama wa kwanza aliye kama simba kwa hakika ni ufalme wa Babeli, ambao ulikuwa ukitawala wakati wa nabii Danieli. Sifa za mnyama huyo za kuwa kama simba, na kuwa na mabawa kama ya tai, zinawakilisha kuwa ufalme huo ungekuwa na nguvu nyingi na mwepesi katika kufanya vita, hii ni sawa na ufalme wa Babeli wakati wa mfalme Nebukandreza. Yeremia alipotabiri juu ya Yerusalemu kuhusuliwa na Babeli, alitaja sifa za Babeli kama tai. Yeremia 4:7, 13 inasema, “Simba ametoka katika kichaka chake, ndiye aangamizaye mataifa;…Tazama atapanda juu kama mawingu, na magari yake ya vita yatakuwa kama kisulisuli; farasi zake ni wepesi kuliko tai…” Pia Habakuki 1:6, 8 inasema, “Kwa maana, angalieni, nawaondokeshea Wakalidayo, taifa lile kali, lenye haraka kupita kiasi; wapitao katikati ya dunia, ili wayamiliki makao yasiyo yao…wapanda farasi wao watoka mbali sana; huruka kama tai afanyaye haraka ale.” Hivyo, yule mnyama wa kwanza anawakilisha ufalme wa Babeli. Danieli 7:4 juu ya mnyama wa kwanza inasema, “…naye alikuwa na mabawa ya tai; nikatazama, hata mabawa yake yakafutuka manyoya, akainuliwa katika nchi…naye akapewa moyo wa kibinadamu.” Badiliko hili lililotokea la mabawa yake kufutuka manyoya na kupewa roho ya kibinaadamu, linawakilisha kupungua kwa nguvu na wepesi wa ufalme wa Babeli, kitu ambacho kilitokea baada ya mfalme Nebukandreza kupita, na ufalme ukawa dhaifu na usio na nguvu wakati wa utawala wa wafalme; Nabonadius and Belshaza. Danieli 7:5 “Na tazama, mnyama mwingine, wa pili, kama dubu, naye aliinuliwa upande mmoja, na mifupa mitatu ya mbavu ilikuwamo kinywani mwake katika meno yake; wakamwambia mnyama huyo hivi, Inuka, ule nyama tele.” Mnyama wa pili kwa hakika anawakilisha ufalme wa Umedi na Uajemi, ambao ulifuata baada ya ufalme wa Babeli kuanguka. Mnyama huyu aliye kama dubu, tena ameinuliwa upande mmoja, kwa hakika, ni ufalme uliokuwa na pande mbili “Umedi na Uajemi” ambapo upande mmoja wa Uajemi uliinuliwa zaidi kwa ukuu kuliko upande mwingine wa uamedi katika ufalme wa “Umedi&Uajemi. Zile mbavu tatu zilizo katika kinywa cha dubu, zinawakilisha nchi tatu Babeli, Lydia, na Misri ambazo zilihusuliwa na ufalme wa Umedi na uajemi. Danieli 7:6 “Kisha nikatazama, na kumbe! Mnyama mwingine, kama chui, naye juu ya mgongo wake alikuwa na mabawa manne kama ya ndege; mnyama huyo alikuwa na vichwa vinne; akapewa mamlaka.” Mnyama wa tatu anawakilisha ufalme wa Ugiriki/Uyunani, ambao ulifuata baada ya ufalme wa Umedi na Uajemi kuanguka. Tafadhari kumbuka kuwa mnyama huyu wa tatu aliye kama chui, tena ana mabawa manne; angewakilisha taifa ambalo ni jepesi na la haraka zaidi kuliko taifa la Babeli ambalo lilikuwa na mabawa mawili pekee. Hii inawakilisha vizuri zaidi ufalme wa Ugiriki wakati ulipokuwa chini ya utawala wa Alexander, ufalme huo ulikuwa mwepesi na wa haraka sana katika kuhusuru miji, na uliyapanga majeshi yake kwa jinsi ambayo kamwe haifanani na nyakati zilizokuwa zimepita. Vile vichwa vinne vinawakilisha sehemu nne ambazo ufalme huo uligawanyika baada ya mfalme Alexander. Danieli 7:7 “Baadaye nikaona katika njozi ya usiku, na tazama, mnyama wa nne, mwenye kutisha, mwenye nguvu, mwenye uwezo mwingi, naye alikuwa na meno ya chuma, makubwa sana; alikula na kuvunja vipande vipande, na kuyakanyaga mabaki kwa miguu yake; na umbo lake lilikuwa mbali kabisa na wale wa kwanza, naye alikuwa na pembe kumi.” Malaika Gabrieli katika Danieli 7:23 akimfafanulia Danieli ukweli kuhusu mnyama huyu wa nne alisema, “…Huyo mnyama wa nne atakuwa ni ufalme wa nne juu ya dunia, utakaokuwa mbali na falme zile zote, nao utakula dunia yote, na kuikanyaga, na kuivunja vipande vipande.” Mnyama huyu wa nne anawakilisha ufalme wa Roma, uliofuta baada ya ufalme wa Ugiriki kuanguka. Ufalme huu unafananishwa na “chuma” ikimaanisha Jeshi lake ni katili na lenye nguvu nyingi sana. Danieli 7:7 inasema kuwa, ufalme huu wa Roma uko mbali/tofauti na falme zile tatu za Babeli, Umedi na Uajemi, na Ugiriki; Utofauti huo ni kwamba falme zile tatu zilikuwa falme za kipagani tu, lakini ufalme huu wa Roma ni mchanganyiko wa upagani na ukristo kwa wakati mmoja: yaan, upapa. Mnyama huyu wa nne ana pembe kumi kama Danieli 7:7 inavyomwelezea. Pembe katika unabii pia hutumika kuwakilisha ufalme au taifa, malaika Gabrieli katika Danieli 7:24 alipokuwa anamfahamisha Danieli ukweli kuhusu zile pembe kumi za yule mnyama wa nne, alisema, “Na habali za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.” Hivyo, zile pembe kumi za yule mnyama wa nne ambaye tumegundua kuwa ni Roma, pembe hizo ni mataifa kumi ambayo yapo katika ufalme wa Roma. Baada ya ufalme wa Roma ya kipagani kuanguka, katika mwaka 351 hadi 476 BK uligawanyika katika mataifa(pembe) kumi ambayo katika historia yamekuwa yakijulikana kama mataifa kumi ya Ulaya ya magharibi. Danieli 7:8 “Nikaziangalia sana pembe zake, na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang’olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu.” Malaika Gabrieli akifafanua kuhusu pembe hiyo ndogo itakayoinuka katika zile pembe kumi, katika Danieli 7:24 alisema, “Na habari za zile pembe kumi, katika ufalme huo wataondoka wafalme kumi; na mwingine ataondoka baada ya hao; naye atakuwa mbali na hao wa kwanza; naye atawashusha wafalme watatu.” Huko nyuma tumegundua kuwa zile pembe kumi za mnyama wa nne, zilizoorodheshwa katika Danieli 7:7 ni mataifa kumi ya Ulaya ya magharibi ambayo yaligawanyika katika ufalme wa Roma. Sasa katika Danieli 7:8 pembe nyingine ndogo ikainuka na ikang’oa pembe tatu katika zile pembe kumi. Katika Danieli 7:24 malaika akafafanua kuwa, ile pembe ndogo ni ufalme au taifa jingine dogo ambalo litatokea ndani ya ufalme huo wa Roma katika mataifa yale kumi au pembe kumi. Kisha taifa hilo dogo au pembe ndogo baada ya kutokea litaangusha mataifa matatu katika yale mataifa kumi ya mwanzo. Kwa hakika taifa hili dogo (au pembe ndogo) ni taifa dogo la Vatican(upapa) ambalo liliinuka baada ya mataifa yale kumi. Taifa dogo la Vatican(upapa) liliinuka kutoka katika taifa la Italia, na taifa la Italia ni moja wapo katika yale mataifa kumi ( pembe 10). Baada ya taifa la Vatican kuinuka liliyaondoa mataifa matatu katika yale mataifa kumi ya mwanzo, hii inaweza kufananishwa vizuri na ile pembe ndogo inayong’oa pembe tatu katika zile pembe kumi za mwanzo. Sababu ya taifa dogo la Vatican kuyaondoa mataifa matatu katika yale kumi ya mwanzo ni kwamba, taifa la Upapa(vatican) lilitaka kuyatawala yale mataifa kumi yote, lakini mataifa matatu yalikataa kujiweka chini ya utawala wa upapa, hivyo upapa ukafanya vita juu ya mataifa hayo matatu na kuyaondoa kabisa hata yasiwepo. Mataifa matatu yaliyoondolewa ni Heruli, liling’olewa na upapa mwaka 493 B.K. Vandal, liling’olewa na upapa mwaka 534 B.K. Ostrogoth, liling’olewa upapa mwaka 538 B.K. Ifuatayo ni orodha ya mataifa 10 ya ufalme wa Roma (au pembe 10 za mnyama), huku mataifa mataifa 3 yakiwa yameondolewa (au pembe tatu zikiwa zimeng’olewa) na utawala wa upapa (pembe ndogo). Saxon, kwa sasa ni taifa la Uingereza. Frank, kwa sasa ni taifa la Ufaransa. Alamanni, kwa sasa ni taifa la Ujerumani. Visigoth, kwa sasa ni taifa la Uhispania. Suevi, kwa sasa ni taifa la Ureno. Lombard, kwa sasa ni taifa la Italia. Burgundia, kwa sasa ni taifa la Uswidi. Heruli, liling’olewa na pembe ndogo 493 B.K. Vandal, liling’olewa na pembe ndogo 534 B.K. Ostrogoth, liling’olewa na pembe ndogo 538 B.K Ushahidi mwingine unaothibitisha kuwa ile pembe ndogo ya Daniel 7:8 ni utawala upapa, ni ushahidi unaopatikana katika Danieli 7:25 ambapo inasema, Danieli 7:25 “Naye (pembe ndogo) atanena maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.” Hapa ushahidi usioweza kupingika ni swala la kubadili majira na sheria za Mungu, ni mamlaka ya upapa pekee ndiyo iliyobadili sheria za Mungu, Sabato kutoka siku ya saba(Jumamosi) kwenda siku ya kwanza (Jumapili). “Bila shaka kanisa la katoliki hudai kuwa badiliko, (la Sabato Jumamosi kwenda Jumapili) ilikuwa ni kitendo chake…na kitendo hicho ni ALAMA ya mamlaka yake katika mambo ya kidini.” –-H.F. Thomas, Chancellor of Cardinal Gibbons “Jumapili ni ALAMA yetu ya mamlaka…kanisa liko juu ya Biblia, na uhamishaji huu wa utunzaji wa Sabato ni ushahidi wa jambo hilo la ukweli.” -–Catholic Record of London, Ontario Sept 1, 1923. Pia Danieli 7:25 inasema, pembe ndogo atawadhoofisha watakatifu wa Mungu, nao watatiwa mikononi mwake kwa muda wa wakati mmoja, na nyakati mbili, na nusu wakati. Wakati mmoja = mwaka 1, nyakati mbili = miaka 2, na nusu wakati = nusu mwaka, (hivyo, 1+2+05=3.5 miaka 3 na nusu). Miaka 3 na nusu = miezi 42 au siku 1260. Katika unabii siku moja = mwaka 1, Ezekieli 4:6 inasema, “…siku arobaini, siku moja kwa mwaka mmoja, nimekuagiza.” Hesabu 14:34 pia inasema, “…siku arobaini kila siku kuhesabiwa mwaka…” Hivyo, kutokana na Ezekieli 4:6 na Hesabu 14:34, ni hakika kwamba siku 1260 ni sawa na miaka 1260 ambayo Upapa ungetawala na kuwadhofisha watakatifu. Historia inathibitisha kuwa Upapa ulipata nguvu kabisa kuanzia mwaka 538BK, baada ya kumaliza kuyang’oa mataifa 3, hivyo utawala rasmi wa upapa ulianza mwaka 538. “Vigillius…alikalia kiti cha upapa (538 B.K.) chini ya ulinzi wa jeshi la Belisarius.” –History of the Christian Church, Vol. 3, p. 327 Hivyo, ukijumlisha ile miaka 1260 ambayo upapa ungewadhoofisha watakatifu katika mwaka 538BK, utapata mwaka 1798BK (538+1260=1798). Kwa hiyo upapa ungewadhoofisha watakatifu kuanzia mwaka 538BK, hadi 1798BK. Historia inathibitisha kabisa kuwa upapa uliwadhoofisha watakatifu tangu mwaka 538bk hadi 1798bk ambapo upapa ulipata jeraha la mauti. “Katika mwaka 1798 Jemedari Berthier aliingia Roma, akauondoa kabisa utawala wa upapa, na kuanzisha mwingine.” –Encyclopedia Britannica 1941 edition Upapa ulipoondolewa madarakani katika mwaka 1798BK, hapo ndipo mateso ya wakristo yalikoma vile vile kama Danieli 7:25 inavyosema. Kwa hakika hii ni miaka halisi 1260 au miaka ya kiunabii 3.5, au wakati, nyakati mbili, na nusu wakati ya Danieli 7:25. Historia inasema wazi kuwa Upapa uliwadhoofisha watakatifu kwa miaka 1260, hata kanisa la Romani Katoliki linakubali kuwa liliwatesa wakristo wakati huo wa zama za giza, na papa Yohane II mwaka 2000 alitubu dhambi ya kanisa ya kuua Wakristo zaidi ya milioni 100. Kifuatacho ni baadhi ya ushahidi unaothibitisha kuwa kanisa Katoliki liliua wtakatifu kama Danieli 7:25 inavyosema. “Kwa sababu ya kufundisha imani kinyume na mafundisho ya Roma, historia inaonyesha vifo vya wafia dini zaidi ya milioni 100” –Brief Bible Readings, p 16. “Katoliki ana baadhi ya sababu kwa upande wake wakati anapotoa adhabu kwa waasi wa kidini, kwa maana anajidaia jina la Ukristo kwake mwenyewe kwa kuzuia, na anajidai kufundisha kwamba uwepo wa Roho wa Mungu kamwe hautaondoka kwake…Siyo kosa zaidi kumuua mtu kwa sababu ya uasi wa kidini, kuliko kwa sababu ya uuaji,…[na] katika mambo mengi mateso kwa maoni ya kidini siyo tu kwamba yanaruhusiwa, lakini ni ya busara na ya lazima.” –The Lawfulnees of Persecution” in the Rambler, 4, June, 1849, pp 119, 126. (“The Rambler” lilikuwa ni gazeti la kila siku la Romani Katoliki lililochapishwa kuanzia mwaka 1848 hadi 1862). “Chini ya mawazo na desturi za kijerumani, mateso yalitumiwa kidogo kuanzia karne ya 9 hadi karne ya 12, lakini kwa uhuikaji wa sheria ya Romani mateso yalianzishwa tena katika karne ya 12…Katika mwaka 1252 (Papa) Innocent IV aliruhusu adhabu ya mateso juu ya waasi wa kidini kwa kutumia mamlaka ya kiserikali, na mateso yakaja kuwa na mahali palipojulikana katika utaribu wa mahakama ya kiuchunguzi.” –New Catholic Encyclopedia, arts. “Inquisition”, “Auto-da-Fe’,” na “Massacre of St Bartholomew’s Day.” Hukumu na ufalme wa watakatifu. Danieli 7:9 “Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye mmoja wa siku ameketi; mavazi yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa chake kama sufu safi; kiti chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu zake moto uwakao.” Danieli 7:10 “Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele zake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele zake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.” Hukumu ambayo inatajwa hapo ni hukumu ya upelelezi ambayo ilianza tarehe 22 Octoba 1844 mwishoni mwa Siku 2300 za kiunabii za Danieli 8:14. Katika mwaka 1844 ambapo Yesu alimaliza kazi yake ya Ukuhani katika chumba cha Patakatifu, na akahamia chumba cha Patakatifu mno kwa ajili ya kazi yake ya Upatanisho, vitabu vilifunuliwa kwa ajili ya kuanza hukumu. Na hukumu hiyo ilianza kwa waliokufa na itaendelea hata kwa walio hai ambao wamekuwa na nuru kuu lakini wakashindwa kuenenda katika nuru. Ukisoma vizuri katika Danieli 7:11, 26 utaona kuwa hukumu imethibitishwa juu ya mfumo wa Upapa na utawala wake wote wa Roma. Danieli 7:11 “Nikatazama wakati huo; kwa sababu ya sauti ya yale maneno makubwa iliyoyasema ile pembe(upapa); nalitazama hata mnyama(Roma) yule akauawa, mwili wake ukaharibiwa, akatolewa ateketezwe kwa moto.” Wakati malaika akimfahamisha Danieli juu ya hukumu itakayokuja juu ya upapa na juu ya dola na ufalme wote wa Roma, katika Danieli 7:26 alisema, “Lakini hukumu itawekwa, nao watamwondolea(pembe ndogo[upapa]) mamlaka yake, kuipoteza na kuiangamiza, hata milele.” Lakini kuhusu wale wanyama wengine watatu unabii unasema, Danieli 7:12 “Na kwa habari za wale wanyama wengine, walinyang’anywa mamlaka yao; walakini maisha yao yalidumishwa kwa wakati na majira.” Wanyama wale watatu walinyang’anywa mamlaka yao na mnyama wa nne ambaye ni ufalme wa Roma, lakini maisha yao yaliendelea kuwepo; kwa mfano, taifa la Babeli liliendelea kuishi mpaka sasa linajulikana kama taifa la Irak (Al Hillah), vile vile kwa Umedi na Uajemi, na Ugiriki. Mataifa haya yanaishi hata sasa lakini mamlaka yao walinyanganywa na dola la Roma. Tukiangalia wanyama wote wanne tunaona kama ifuatavyo: Mnyama=Ufalme.1.Babeli.2.Umedi/Uajemi.3.Ugiriki.4.Roma Mnyama wa nne ni ufalme wa nne na wa mwisho katika historia ya dunia, na ufalme huo ni Roma, una pembe kumi ambazo ni mataifa yake kumi, pia una pembe ndogo ambayo ni upapa. Je unapita muda mrefu kabla dunia haijaisha? Tuko katika nyakati za mwishoni kabisa za mnyama wa nne na wa mwisho. Na hivi karibuni Yesu atakuja na kuziangamiza falme zote na upapa, na kisha ataanzisha ufalme wake pamoja na watakatifu katika ulimwengu mpya, ambao hautakuwa na mwisho. Ni Yerusalemu mpya utakaoshuka kutoka juu mbinguni. Danieli 7:13 “Nikaona katika njozi za usiku, na tazama, mmoja aliye mfano wa mwanadamu(Mwana wa Adamu) akaja pamoja na mawingu ya mbingu akamkaribia huyo mzee wa siku, wakamleta karibu naye.” Danieli 7:14 “Naye(Mwana wa Adam) akapewa mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme wake ni ufalme usioweza kuangamizwa.” Wakati umekaribia, naam, wakati umefika ambao Yesu atarudi duniani kuwachukua watakatifu wake, nao watatawala katika ufalme wake wa amani ambao uzuri wake hakuna mtu anayeweza kuuelezea, ni ufalme ambao si wa dunia hii bali wa ulimwengu mpya. Malaika akimfahamisha Danieli kuhusu mambo haya alisema, Danieli 7:27 “Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu wake Aliye juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.” Danieli 7:22 “hata akaja huyo mzee wa siku, nao watakatifu wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia watakatifu waumiliki ufalme.” Danieli 7:28 “Huu ndio mwisho wa jambo lile. Nami, Danieli, fikira zangu zilinifadhaisha, na uso wangu ulinibadilika; lakini naliliweka jambo hilo moyoni mwangu.” Je ni upendo gani ambao Mungu ametupa kwa kutufunulia nyakati na majira ya mwisho wa ulimwengu? Hata kwa wale ambao hawaamini wanaweza kufunguliwa macho yao ili waone ni jinsi gani Yesu Kristo ni kweli na hakika, na kwamba nini tutakosa kama tusipomwamini Yeye. Leo ndiyo wakati wa kumtafuta Bwana kwa moyo wote, akili zote, na nguvu zote ili giza lisije kufika na kutukuta hatusitahili kuuingia ufalme wa Mungu. Ushauri wa Yesu ni kwamba, “kesheni na kuomba.”huku tukidumu katika utakatifu kwani tafsiri halisi ya kukesha maana yake tuwe macho kwakila jambo shetani asije akatuvamia tukaanguka dhambini hivyo jitenge na uovu.Haiwezekani kumuona Mungu pasipo utakatifu kwani utakatifu ndiyo njia tutakayopitia,ndiyo tiketi yakuingia katika ufalme wa Mungu.Isaya 35:8,Kumbuka Mungu anazuia mabaya yasiipate dunia na utawala mpinga Kristo kwaajili yakutukamilisha na kutupiga muhuri wake na muhuri huo ni wokovu kumpokea yeye na kumuamini na kumkiri yeye peke yake kuwa ni Bwana na mwokozi wa maisha yako.naye atakupa kipawa cha Roho mtakatifu atakaye kuwezesha kuishi kwa utakatifu hadi atakapo kuja.KUMBUKA HAKUNA MNYAMA MKUBWA NA WAKUTISHA KAMA DHAMBI RUMI YAKO YA LEO NI MOYO WAKO MWENYEWE,HIVYO ONDOA PICHA ZA KATOLIKI AKILINI MWAKO WEKA IMANI JUU YA YESU KRISTO KAMA UKISIKIA LEO ANABISHA BASI FUNGUA MOYO WAKO AINGIE NAYE ATAKUPA ZAWADI YA ROHO MTAKATIFU NA UZIMA WA MILELE UFUNUO 3:19-20.TAFUTA UBATIZO SAHIHI UKAZALIWE NA KUFUFULIWA NA KRISTO KIROHHO NA UKATISHWE NAYE MBINGUNI KWAANZIA SASA KIROHO.WAKOLOSAI 3:1-4,EFESO 2:4-7 MUNGU AKUBARIKI SANA WEWE UTAKAYE SOMA UJUMBE HUU EV.GIDION LAIZER. NURU YA UPENDO ARUSHA
    Like
    4
    2 Commentarios 0 Acciones 71K Views 0 Vista previa
  • Jaman mama yake tabitha,kaja kunisalimia nyumbani.ila tokea nimeolewa hajawa mama yangu tena bali wa Mume Wangu,Mungu akubariki kwa kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi maishani mwako
    Jaman mama yake tabitha,kaja kunisalimia nyumbani.ila tokea nimeolewa hajawa mama yangu tena bali wa Mume Wangu,Mungu akubariki kwa kumpokea Yesu kuwa Bwana na mwokozi maishani mwako
    Like
    Love
    4
    5 Commentarios 0 Acciones 926 Views 0 Vista previa
  • the leading cause of fueling various diseases. The spectrum typically starts from inflammation to cardiovascular problems or and sometimes ends with certain types of cancer.Often there is no time to focus on healthy eating or exercise as you reach the end of your working age. Your career, family, http://jorttweewielers.nl/guestbook
    https://chouchkette.paroledemamans.com/pate-a-tartiner-fait-maison-avec-amour-et-sans-huile-de-palme
    https://www.partitadelsabato.it/Commenti.aspx?Id=138
    the leading cause of fueling various diseases. The spectrum typically starts from inflammation to cardiovascular problems or and sometimes ends with certain types of cancer.Often there is no time to focus on healthy eating or exercise as you reach the end of your working age. Your career, family, http://jorttweewielers.nl/guestbook https://chouchkette.paroledemamans.com/pate-a-tartiner-fait-maison-avec-amour-et-sans-huile-de-palme https://www.partitadelsabato.it/Commenti.aspx?Id=138
    0 Commentarios 0 Acciones 1K Views 0 Vista previa
  • Dhahabu njema.tupo buza kwa mama kibongea.napokea mialoko https://m.youtube.com/watch?v=jOgUSMN0J-w
    Dhahabu njema.tupo buza kwa mama kibongea.napokea mialoko https://m.youtube.com/watch?v=jOgUSMN0J-w
    Like
    Love
    2
    9 Commentarios 0 Acciones 2K Views 0 Vista previa
Patrocinados
[Repenting + Holiness = Entering Heaven / Kutubu + Utakatifu = Kuingia Mbinguni].