UPONYAJI WA MAGONJWA.

Chanzo cha magonjwa: Magonjwa yanatokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya mtu aliyekuwa mngonjwa alimwonya akisema, “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi” Yn 5:14. Mtu akiwa amefanya dhambi anapoumwa na kupimwa ugonjwa unaonekana. Iwapo akipimwa vipomo vyote na ugonjwa hauonekani yamkini ni pepo wachafu wamemwingia. “Mara huenda akachukua pamoja naye pepo wengine walio waovu kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya” Mt 12:45.

Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili, unaotokana kukosa lishe ya mlo wa kila siku (Utapia mlo). Mapungufu katika mwili wa mwanadamu yanaweza yakawa ni kusudi la Mungu, ijapokuwa si yote. “Bwana akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani amfanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, Bwana? Kut 4:11.

Kuponywa kwa dawa.

Kwa kawaida kuna njia ambayo imekuwa ikitumika ya kutibu mangonjwa ambayo ni kutibu kwa kutumia dawa. Tiba za dawa zimekuwapo kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali. Mtu anapokuwa mgonjwa kuna hatua ya kuchukua, kwanza anaenda hospitali au kupelekwa kutona na hali yake hajiwezi. Daktari anampima na kufahamu ugonjwa alio nao, halafu anamwandikia dawa na maelekezo ya kuzitumia. Kama hatazingatia maelekezo na kuzitumia haiwezekani akapona. Hapa tunaweza kuona mgonjwa ili apone ni lazima azingatie maelekezo aliyopewa na daktari. Lakini baadhi ya magonjwa hayana tiba kama UKIMWI (HIV Aids). Hata hivyo usikate tamaa mwamini Mungu anaweza kukuponya kwa njia ya kumwomba. Atakuponya kwa neema, na rehema, kwa uwezo na nguvu zake.VIlevile kuna kanuni na maelekezo ya kufuata ili Mungu akuponye

UPONYAJI WA MUNGU. Una maelekezo na kanuni za kufuata:

1. Kutubu na kuziacha dhambi: “Azifichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema” Mit 28:13. “Twajua ya kwamba Mungu hawasikii wenye dhambi;bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake huyo humsikia” Yn 9:31.

2. Kuishi maisha ya utakatifu: Ndio maana Mungu amesema; “Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako. Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote…” Kumb 7:12, 15. Katika maandiko haya tunaona Mungu alisema na baba zetu ya kwamba kwa upande wetu tunapozishika na kuzitenda hukumu zake (Sheria zake). Na kwa upande wake yeye ndipo hutuondolea ugonjwa wote. Kwa sababu Mungu aliwaapia baba zetu akisema, nitakutimizia agano na rehema. Kwa kiapo chake anathibitisha atafanya yale aliyoahidi katika Agano alilolifanya na baba zetu. Mahali pengine tunasoma:

“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote,…Mche Bwana, ukajiepushe na uovu, Itakuwa afya mwilini pako. Na mafuta mifupani mwako. Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzishike kauli zangu. Kwa maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote”Mit 3:5,7,8.

3.Kumwamini Mungu na neno lake: Ndiyo maana Mungu alisema “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita roho yangu haina furaha naye.” Ebr 10:38. Kutokana na andiko hili, linaonyesha lazima mtu awe mwenye haki ndipo aweze kuishi kwa imani. Pia lazima kwanza kuamini moyoni na kuwa na uhakika Mungu atakuponya kama neno linavyosema,“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana (wazi) ya mambo yasiyoonekana” Ebr 11:1
4. Kuishi maisha ya unyenyekevu: “Dhabihu za Mungu ni mioyo iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka Ee Mungu hutaudharau. “Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuwaganga jeraha zao” Zab 51:17; 147:3. Mungu anahitaji watu waliovunjika na kupondeka moyo ili awaponye. Maana ya kuvunjika na kupondeka moyo ni kunyenyekea chini ya Mungu na kujua yeye ni mwenye uwezo na nguvu zote; kutokuwa na kiburi na kujiona wewe ni bora kuliko wengine, kutokuonee na kunyanyasa wengine, kutokujivunia ulivyo nayo na kujisifia kwa yale unayoyafanya na kutokudharau wengine au kuwapuuza. “Amdharauye mwenzake afanya dhambi;…” Mit 14:21. Yesu Kristo yeye ni mfano kwetu, alikuwa ni mnyenyekevu aliacha enzi na mamlaka aliyokuwa nayo mbinguni akaja duniani kwa namna ya mtumwa hakutaka makuu na fahari, alimtii Mungu.

5. Kuomba kwa imani: “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa , tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba”Yoh 5:14-15. Haya maandiko yanafundisha ni muhimu kujua kwamba tunapomwomba Mungu anatuskia, tunapoomba sawaswa na mapenzi yake (neno lake). Pia kujua tulichoomba tunacho tayari. Kama umemwomba Mungu akuponye unajua umepona, hii ni imani katika Mungu. Ndiyo maana Yesu alifundisha akisema, “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaoombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” Mk 11:24.

6. Kuomba kwa bidii: Kuomba kwa bidii bila kukata tamaa hadi Bwana akuponye kabisa. Iwapo umeomba lakini bado Bwana hajakuponya, endelea kunyenyeke na kumlilia tena na tena mpaka Bwana akuponye. Kuomba kwa bidii ni mfano wa mwanariadha anayeshindana na wanariadha kwa kukimbia. Mwanariada anayeshinda ni kwa sababu amekimbia kwa bidii na kupewa zawadi. Kuna mifano ya kufuata ya watumishi wa Mungu waliomwomba Mungu kwa bidii tena na tena wakajibiwa, mmojapo ni Eliya;
“Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi; akainama uso mpaka magotini. Akamwambia mtumishi wake, kwea sasa ukatazame upande wa bahari. Akakwea na kutazama, akasema, hakuna kitu. Naye akanena, enenda tena mara saba. Ikawa mara ya saba akasema, tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. … Ikawa muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikawa mvua nyingi…” 1Fal 18:42-45. Hapa maandiko yanaonyesha jinsi Eliya alimwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili, wingu la mvua halikutokea lakini hakukata tamaa aliendelea kuomba mpaka mara ya saba wingu likaonekana na mvua ikanyesha. Na mwingine aliyeomba kwa bidii na kujibiwa ni Elisha baada ya kumtuma Gehazi mtumishi wake kumfufua mtoto.

“Na Gehazi akawatagulia, akaiweka ile fimbo juu ya mtoto; lakini hapakuwa na sauti wala majibu. Basi Elisha alipofika nyumbani, tazama, mtoto amekwisha kufa, amelazwa kitandani pake. Basi akaingia ndani akajifungia mlango, yeye na Yule mtoto wote wawili, akamwomba Bwana... Kisha akarudi, akatembea nyumbani, huko Na huko mara moja; akapanda akajinyoosha juu yake; Na Yule mtoto akapiga chafya mara Saba, Na mtoto akafumbua macho yake.” 2 Fal 4:31-35. Elisha naye alimtuma mtumishi wake Gehazi akaiweke fimbo juu mtoto abaye alikuwa amekufa ili afufuke, wala hakufufuka, lakini Elisha hakukata tamaa alikwenda mwenyewe akamwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili na mtoto akafufuka.

7. Kumshukuru Mungu: “Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” 1The 5:18. Katika maisha yetu ni muhimu tumshukuru Mungu kwa ajili ya mema yote anayotutende kila siku.

Mungu ni mwaminifu.
Yale yote aliyoyaahidi katika neno lake hakika atayafanya kama alivyosema; “Mimi sitalihalifu agano langu, sitalibadili Neno lililotoka midomoni mwangu.” Zab 89:34. “Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu” Kut 20:6. “Maana Kama vile mvua ishukavyo, Na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; Bali huinywesha ardhi, Na kuizalisha Na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, Na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure Bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma” Isa 55:10-11.

USHUHUDA. Hapa ninatoa ushuhuda wa mtu ambaye Bwana amemponya mara nyingi kwa magonjwa tofauti. Siri ya uponyaji wake ni kwamba yeye ni mtakatifu amejilinda na kuepuka dhambi. kumbuka dhambi ni kizuizi cha uponyaji wa Mungu kwako. Amekuwa ni mwenye imani na unyenyekevu, amevunjika na kupondeka moyo. Wakati mwingine anapomwomba Mungu huanguka kifulifuli akimsihi Mungu. Hakika mtu kama huyu atasikilizwa kwa sababu anao ujasiri, hana dhambi inayomhukumu ndani ya moyo wake.

Ndio maana imeandikwa “Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri (bila dhambi), ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.” Ebr 4:16. Mtu anapodumu katika maisha ya kumpendeza Mungu anapata neema au upendeleo kujibiwa maombi. Wakati mwingine hata kabla ya kuomba hujibiwa. “Na itakuwa kwamba, kabla ya kuomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.” Isa 65:24. “….maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.” Mt 6:8.
UPONYAJI WA MAGONJWA. Chanzo cha magonjwa: Magonjwa yanatokana na mtu kufanya dhambi. Ndiyo maana Yesu alipomponya mtu aliyekuwa mngonjwa alimwonya akisema, “…Angalia umekuwa mzima; usitende dhambi tena, lisije likakupata jambo lililo baya zaidi” Yn 5:14. Mtu akiwa amefanya dhambi anapoumwa na kupimwa ugonjwa unaonekana. Iwapo akipimwa vipomo vyote na ugonjwa hauonekani yamkini ni pepo wachafu wamemwingia. “Mara huenda akachukua pamoja naye pepo wengine walio waovu kuliko yeye mwenyewe nao huingia na kukaa humo; na mtu Yule hali yake huwa mbaya kuliko ya kwanza. Ndivyo itakavyokuwa kwa kizazi hiki kilicho kibaya” Mt 12:45. Wakati mwingine sii kila mtu anayeumwa amefanya dhambi, bali ni matokeo ya ugonjwa katika mwili, unaotokana kukosa lishe ya mlo wa kila siku (Utapia mlo). Mapungufu katika mwili wa mwanadamu yanaweza yakawa ni kusudi la Mungu, ijapokuwa si yote. “Bwana akamwambia, Ni nani aliyekifanya kinywa cha mwanadamu? Au ni nani amfanyaye mtu kuwa bubu au kiziwi, au mwenye kuona, au kuwa kipofu? Si mimi, Bwana? Kut 4:11. Kuponywa kwa dawa. Kwa kawaida kuna njia ambayo imekuwa ikitumika ya kutibu mangonjwa ambayo ni kutibu kwa kutumia dawa. Tiba za dawa zimekuwapo kwa ajili ya kutibu magonjwa mbalimbali. Mtu anapokuwa mgonjwa kuna hatua ya kuchukua, kwanza anaenda hospitali au kupelekwa kutona na hali yake hajiwezi. Daktari anampima na kufahamu ugonjwa alio nao, halafu anamwandikia dawa na maelekezo ya kuzitumia. Kama hatazingatia maelekezo na kuzitumia haiwezekani akapona. Hapa tunaweza kuona mgonjwa ili apone ni lazima azingatie maelekezo aliyopewa na daktari. Lakini baadhi ya magonjwa hayana tiba kama UKIMWI (HIV Aids). Hata hivyo usikate tamaa mwamini Mungu anaweza kukuponya kwa njia ya kumwomba. Atakuponya kwa neema, na rehema, kwa uwezo na nguvu zake.VIlevile kuna kanuni na maelekezo ya kufuata ili Mungu akuponye UPONYAJI WA MUNGU. Una maelekezo na kanuni za kufuata: 1. Kutubu na kuziacha dhambi: “Azifichaye dhambi zake hatafanikiwa; Bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema” Mit 28:13. “Twajua ya kwamba Mungu hawasikii wenye dhambi;bali mtu akiwa ni mcha Mungu, na kuyafanya mapenzi yake huyo humsikia” Yn 9:31. 2. Kuishi maisha ya utakatifu: Ndio maana Mungu amesema; “Na itakuwa, kwa sababu mwazisikiza hukumu hizi, na kuzishika na kuzitenda, basi Bwana, Mungu wako, atakutimizia agano na rehema aliyowaapia baba zako. Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote…” Kumb 7:12, 15. Katika maandiko haya tunaona Mungu alisema na baba zetu ya kwamba kwa upande wetu tunapozishika na kuzitenda hukumu zake (Sheria zake). Na kwa upande wake yeye ndipo hutuondolea ugonjwa wote. Kwa sababu Mungu aliwaapia baba zetu akisema, nitakutimizia agano na rehema. Kwa kiapo chake anathibitisha atafanya yale aliyoahidi katika Agano alilolifanya na baba zetu. Mahali pengine tunasoma: “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote,…Mche Bwana, ukajiepushe na uovu, Itakuwa afya mwilini pako. Na mafuta mifupani mwako. Mwanangu, sikiliza maneno yangu; Tega sikio lako, uzishike kauli zangu. Kwa maana ni uhai kwa wale wazipatao, Na afya ya mwili wao wote”Mit 3:5,7,8. 3.Kumwamini Mungu na neno lake: Ndiyo maana Mungu alisema “Lakini mwenye haki wangu ataishi kwa imani; Naye akisita-sita roho yangu haina furaha naye.” Ebr 10:38. Kutokana na andiko hili, linaonyesha lazima mtu awe mwenye haki ndipo aweze kuishi kwa imani. Pia lazima kwanza kuamini moyoni na kuwa na uhakika Mungu atakuponya kama neno linavyosema,“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana (wazi) ya mambo yasiyoonekana” Ebr 11:1 4. Kuishi maisha ya unyenyekevu: “Dhabihu za Mungu ni mioyo iliyovunjika; Moyo uliovunjika na kupondeka Ee Mungu hutaudharau. “Huwaponya waliopondeka moyo, Na kuwaganga jeraha zao” Zab 51:17; 147:3. Mungu anahitaji watu waliovunjika na kupondeka moyo ili awaponye. Maana ya kuvunjika na kupondeka moyo ni kunyenyekea chini ya Mungu na kujua yeye ni mwenye uwezo na nguvu zote; kutokuwa na kiburi na kujiona wewe ni bora kuliko wengine, kutokuonee na kunyanyasa wengine, kutokujivunia ulivyo nayo na kujisifia kwa yale unayoyafanya na kutokudharau wengine au kuwapuuza. “Amdharauye mwenzake afanya dhambi;…” Mit 14:21. Yesu Kristo yeye ni mfano kwetu, alikuwa ni mnyenyekevu aliacha enzi na mamlaka aliyokuwa nayo mbinguni akaja duniani kwa namna ya mtumwa hakutaka makuu na fahari, alimtii Mungu. 5. Kuomba kwa imani: “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa , tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba”Yoh 5:14-15. Haya maandiko yanafundisha ni muhimu kujua kwamba tunapomwomba Mungu anatuskia, tunapoomba sawaswa na mapenzi yake (neno lake). Pia kujua tulichoomba tunacho tayari. Kama umemwomba Mungu akuponye unajua umepona, hii ni imani katika Mungu. Ndiyo maana Yesu alifundisha akisema, “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaoombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu” Mk 11:24. 6. Kuomba kwa bidii: Kuomba kwa bidii bila kukata tamaa hadi Bwana akuponye kabisa. Iwapo umeomba lakini bado Bwana hajakuponya, endelea kunyenyeke na kumlilia tena na tena mpaka Bwana akuponye. Kuomba kwa bidii ni mfano wa mwanariadha anayeshindana na wanariadha kwa kukimbia. Mwanariada anayeshinda ni kwa sababu amekimbia kwa bidii na kupewa zawadi. Kuna mifano ya kufuata ya watumishi wa Mungu waliomwomba Mungu kwa bidii tena na tena wakajibiwa, mmojapo ni Eliya; “Naye Eliya akapanda juu mpaka kilele cha Karmeli; akasujudu kifudifudi; akainama uso mpaka magotini. Akamwambia mtumishi wake, kwea sasa ukatazame upande wa bahari. Akakwea na kutazama, akasema, hakuna kitu. Naye akanena, enenda tena mara saba. Ikawa mara ya saba akasema, tazama, wingu linatoka katika bahari, nalo ni dogo kama mkono wa mtu. … Ikawa muda si muda, mbingu zikawa nyeusi kwa mawingu na upepo, ikawa mvua nyingi…” 1Fal 18:42-45. Hapa maandiko yanaonyesha jinsi Eliya alimwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili, wingu la mvua halikutokea lakini hakukata tamaa aliendelea kuomba mpaka mara ya saba wingu likaonekana na mvua ikanyesha. Na mwingine aliyeomba kwa bidii na kujibiwa ni Elisha baada ya kumtuma Gehazi mtumishi wake kumfufua mtoto. “Na Gehazi akawatagulia, akaiweka ile fimbo juu ya mtoto; lakini hapakuwa na sauti wala majibu. Basi Elisha alipofika nyumbani, tazama, mtoto amekwisha kufa, amelazwa kitandani pake. Basi akaingia ndani akajifungia mlango, yeye na Yule mtoto wote wawili, akamwomba Bwana... Kisha akarudi, akatembea nyumbani, huko Na huko mara moja; akapanda akajinyoosha juu yake; Na Yule mtoto akapiga chafya mara Saba, Na mtoto akafumbua macho yake.” 2 Fal 4:31-35. Elisha naye alimtuma mtumishi wake Gehazi akaiweke fimbo juu mtoto abaye alikuwa amekufa ili afufuke, wala hakufufuka, lakini Elisha hakukata tamaa alikwenda mwenyewe akamwomba Mungu mara ya kwanza na mara ya pili na mtoto akafufuka. 7. Kumshukuru Mungu: “Shukuruni kwa kila jambo; maana hayo ni mapenzi ya Mungu kwenu katika Kristo Yesu.” 1The 5:18. Katika maisha yetu ni muhimu tumshukuru Mungu kwa ajili ya mema yote anayotutende kila siku. Mungu ni mwaminifu. Yale yote aliyoyaahidi katika neno lake hakika atayafanya kama alivyosema; “Mimi sitalihalifu agano langu, sitalibadili Neno lililotoka midomoni mwangu.” Zab 89:34. “Nami nawarehemu maelfu elfu wanipendao, na kuzishika amri zangu” Kut 20:6. “Maana Kama vile mvua ishukavyo, Na theluji, kutoka mbinguni, wala hairudi huko; Bali huinywesha ardhi, Na kuizalisha Na kuichipuza, ikampa mtu apandaye mbegu, Na mtu alaye chakula; ndivyo litakavyokuwa neno langu, litokalo katika kinywa changu; halitanirudia bure Bali litatimiza mapenzi yangu, nalo litafanikiwa katika mambo yale niliyolituma” Isa 55:10-11. USHUHUDA. Hapa ninatoa ushuhuda wa mtu ambaye Bwana amemponya mara nyingi kwa magonjwa tofauti. Siri ya uponyaji wake ni kwamba yeye ni mtakatifu amejilinda na kuepuka dhambi. kumbuka dhambi ni kizuizi cha uponyaji wa Mungu kwako. Amekuwa ni mwenye imani na unyenyekevu, amevunjika na kupondeka moyo. Wakati mwingine anapomwomba Mungu huanguka kifulifuli akimsihi Mungu. Hakika mtu kama huyu atasikilizwa kwa sababu anao ujasiri, hana dhambi inayomhukumu ndani ya moyo wake. Ndio maana imeandikwa “Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri (bila dhambi), ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.” Ebr 4:16. Mtu anapodumu katika maisha ya kumpendeza Mungu anapata neema au upendeleo kujibiwa maombi. Wakati mwingine hata kabla ya kuomba hujibiwa. “Na itakuwa kwamba, kabla ya kuomba, nitajibu; na wakiwa katika kunena, nitasikia.” Isa 65:24. “….maana Baba yenu anajua mnayohitaji kabla ninyi hamjamwomba.” Mt 6:8.
Love
1
0 Kommentare 2 Geteilt 9KB Ansichten 0 Bewertungen