Yesu Kristo hajaumbwa bali alikuwepo tangu milele yote

0
5K

Ni kweli kabisa kwamba Yesu alikuwepo tangu milele yote kabla ya kuumbwa kitu cho chote kile. Bwana Yesu kwa kauli ya kinywa chake mwenyewe anasema kwamba:

“Na sasa, Baba, unitukuze Mimi pamoja Nawe, kwa utukufu ule Mimi niliokuwa nao pamoja Nawe kabla ya ulimwengu kuwako.” (Yohana 17:5)

Neno “UTUKUFU” maana yake ni heshima, uweza, uzuri, umaarufu, nguvu, sifa na mamlaka. Mambo hayo yote Yesu alikuwa nayo kabla hata ulimwengu haujaumbwa. Yesu Kristo alikuwapo hata kabla ya kuzaliwa na Mariamu; jambo hili pia Yesu Kristo kwa kinywa Chake Yeye mwenyewe ametuthibitishia alipokuwa akiwaambia Wayahudi kwamba:

 

“Yeye aliye wa Mungu huyasikia maneno ya Mungu; hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa Mungu.

 

Wayahudi wakajibu, wakamwambia, Je! Sisi hatusemi vema ya kwamba wewe u Msamaria, nawe una pepo?

 

Yesu akajibu, Mimi sina pepo; lakini Mimi namheshimu Baba yangu, na ninyi mwanivunjia heshima Yangu. Wala mimi siutafuti utukufu Wangu; Yuko mwenye kutafuta na kuhukumu. Amin, amin, nawaambia, Mtu akilishika neno langu, hataona mauti milele. Basi Wayahudi wakamwambia, Sasa tumeng’amua ya kuwa una pepo. Ibrahimu amekufa, na manabii wamekufa; nawe wasema, Mtu akuilishika neno langu, hataonja mauti milele. Wewe u mkuu kuliko baba yetu Ibrahimu, ambaye amekufa? Nao manabii wamekufa. Wajifanya u nani? Yesu akajibu, Nikijitukuza mwenyewe, utukufu wangu si situ; anitukuzaye ni Baba Yangu, ambaye ninyi mwanena kuwa ni Mungu wenu. Wala ninyi hamkumjua; lakini mimi namjua. Nikisema ya kwamba simjui, nitakuwa mwongo kama ninyi; lakini namjua, na neno lake nalishika. Ibrahimu baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.

 

Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe haujapata bado miaka hamsini, nawe umemona Ibrahimu? Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, Mimi niko.” (Yohana 8:47-58)

 

Katika kisa tulichokisoma katika maandiko hayo (Yohana 8:47-57) tunajifunza mambo kadhaa hapo. Tumeona dhahiri jinsi ambavyo hata baadhi ya Wayahudi ilivyo wawia vigumu sana kumwelewa huyu Yesu ni nani; hata wakadiriki kusema kuwa Yesu anayo mapepo (mashetani). Hawakumwelewa kwa sababu walimtazama Yesu kibinadamu kama jinsi wao walivyo, lakini hawakujua kuwa Yesu ni alikuwepo hata kabla ya Yeye kuzaliwa na Mariamu. Huyo Ibrahimu anayeongelewa hapo ni yule ambaye habari zake tunazisoma katika kitabu cha MWANZO cha Biblia (Ibrahimu baba yake Isaka na Ishmaili). Wayahudi walishangaa; Inawezekanaje huyu Yesu aseme alimwona Ibrahimu aliyeishi na kufa miaka mingi tena zaidi ya elfu moja iliyopita, wakati huyu Yesu tumemwona utotoni mwake na hata sasa bado hajatimiza umri wa miaka hamsini? Hayo yalikuwa ni mawazo ya kibinadamu; tena inaezekana hata wewe ukawa ni miongoni mwa waliokuwa wanawaza hivyo; lakini, Yesu mwenyewe anatuthibitishia kwa kinywa Chake kwa kusema:

“...Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, Mimi niko.” (Yohana 8:58)

Pia Yesu amewaambia Wayahudi kuwa huyo ambaye wao wanamwita Mungu (YEHOVA), Yeye ndiye Baba wa Yesu; tena Yesu anamjua ingawa hao Wayahudi hawamju (Yohana 8:54,55). Vile vile tusomapo kitabu cha MITHALI tunaona habari zinazo mhusu huyu Yesu; imeandikwa kwamba:

 

“BWANA alikuwa nami katika mwanzo wa njia yake. Kabla ya matendo Yake ya kale. Nalitukuka tokea milele, tangu awali, Kabla haijawako dunia. Wakati visipokuwapo vilindi nalijidhihirisha... (...I was brought forth... – NKJV)...” (Mithali 8:22-24)

Usomapo Biblia ya Kiswahili; hapo nilipoandika “...Wakati visipokuwapo vilindi NALIJIDHIHIRISHA...” utaona baadhi ya Biblia za Kiswahili zimeandika “...NALIZALIWA...” lakini maana halisi hapo ni “...I was brought forth...” ambayo tafsiri yake ni “...NALIJITOKEZA...” au “...NALIJIDHIHIRISHA...”

 

Kumbuka kuwa Wayahudi walimtambua Mungu kwa jina "YEHOVA" ambalo mara nyingi walitamka kwa kusema "BWANA." Hapo Biblia Takatifu inamtaja huyu Yesu likuwa pamoja na YEHOVA katika mwanzo wa njia za YEHOVA. Kabla ya YEHOVA kuumba cho chote (...matendo ya kale...) huyu Yesu alikuwepo. Hivyo basi; huyu Yesu alikuwapo “...tokea milele, tangu awali, Kabla haijawako dunia.” (Mithali 8:23) Neno “MILELE” maana yake ni wakati ambao hauna mwanzo wala mwisho; ni wakati usioweza kuhesabika.

 

Upo ushahidi mwingi sana ndani ya Biblia Takatifu unaotuthibitishia kuwa Yesu alikuwepo hata kabla ya kuumbwa kitu cho chote kile; kwani nao manabii pia walitabiri ujio wa Yesu ambaye alikuwepo tangu milele yote, na tena manabii hao walisema wazi wazi kuwa huyu Yesu ni Mungu. 

Tafuta
Vitengo
Soma Zaidi
GENESIS
Verse by verse explanation of Genesis 16
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 28 questions at the...
Kwa THE HOLY BIBLE 2022-01-21 04:52:01 0 5K
NDOA KIBIBLIA
JIFUNZE KUFIKIRI KABLA HUJACHUKUA UAMUZI WA KUOA AU KUOLEWA
Nawasalimu kwa jina la Yesu . Leo katika nyanja hii ya vijana, nimeona ni vema tukashirikishana...
Kwa GOSPEL PREACHER 2021-11-23 07:13:49 0 6K
Injili Ya Yesu Kristo
MJUE MWIGIZAJI WA FILAMU YA YESU AMBAYE BAADHI YA WATU HUDHANI KWAMBA NI YESU.
BRIAN DEACON ndio jina lake mwigizaji huyo ambaye ni mwingereza aliyezaliwa mnamo tarehe...
Kwa GOSPEL PREACHER 2021-11-19 05:33:52 0 5K
OTHERS
KAMA YESU ALIKUWA NI MUNGU, JE ALIKUWA ANAMWOMBA NANI?
Swali la Yesu ni Mungu na nani alikuwa anamwomba, huwa linaleta utatanishi mkubwa sana na kama...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 06:21:06 0 5K
Injili Ya Yesu Kristo
YESU NI MUNGU AMBAYE ANAPONYA MAGONJWA YOTE
Yesu alisema kwamba ishara moja itakayofuatana na waaminio ni kwamba wataweka mikono juu ya...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-22 03:16:57 0 5K