HASARA ZA KUFANYA TENDO LA NDOA KABLA YA NDOA.

0
9K

Andiko la Msingi ni Mithali 5:1-20.

Mungu ndiye aliyewaumba mtu mume na mtu mke, akawaweka bustanini ili wamtumikie. Mungu akamuumba mwanadamu na kumpa viungo mbalimbali katika mwili. Akawapa wanadamu maungo maalumu kwa ajili ya tendo la ndoa na kisha akaliweka tendo la ndoa kuwa takatifu, tena la halali kwa wanandoa tu, tena hasa wale waliounganishwa na yeye.

Sasa katika kizazi cha leo tunaona watu wengi hasa vijana ambao bado hawajaoana (kwa maana ya kuwa wanandoa) vijana hao wanafanya tendo hilo la ndoa (ngono) tena kwa uchafu usio wa kawaida, wanafanya kwa kuzidi mipaka ambayo Mungu amempa mwanadamu, maana yake wanatumia isivyo (mis-use) maumbile/ maungo ambayo Mungu amewapa.

Soma warumi 1:24-27.Sasa wao wanapofanya haya hawajui kwamba kuna hasara kubwa wanayoipata na wao wanafikiri ndio wanakwenda na dunia. Lengo la ujumbe huu ni kukueleza hasara za kufanya tendo la ndoa kabla ya ndoa nazo ni;

(1) Ni dhambi.
Kufanya ngono kabla ya ndoa ni dhambi na warumi 6:23a inasema mshahara wa dhambi ni mauti; na pia katika Ezekiel anasema Roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa, hivyo kwa sababu hiyo hicho kitendo kitakusababishia kifo cha kimwili na kisha utahukumiwa tu na mwisho kutupwa jehnamu

(2) Kuwashibisha wengine nguvu zako.
Mithali 5:10 Tendo la ndoa ni tendo linalohitaji mtu atumie nguvu, hivyo kadri mtu (hasa mwanume) anapofanya  mara kwa mara anajipotezea nguvu zake anawashibisha wengine nguvu zake na hivyo dhoruba itamkuta katika ndoa yake pindi atakapooa kwa sababu hatakua na nguvu tena kama awali. 

(3) Utavunjiwa heshima.
Mithali 5:7, Siku zote yule unayefanya naye tendo la ndoa kwanza atakuona wewe ni mpumpavu kwa sababu anajua afanyaye tendo hilo hana akili kabisa (mithali 6:32) kwa hivyo atakudharau, zaidi atakutangaza kwa wengine na wewe mwenyewe pindi utapooa au kuolewa kwa kuwa nguvu zako uliwashibisha wengine basi utavunjiwa heshima na huyo mwenzi wako.

(4) Unafanya jambo litakaloiangamiza nafsi yako.
Mithali 6:32. Nafsi kwa kiyunani inaitwa Psuche, ndani yake kuna hisia, akili na maamuzi ya mtu. Hivyo kuiangamiza nafsi yako ni kuangamiza future yako na mipango yako uliyokuwa umejiwekea ya mbele.

(5) Unajitengenezea majeraha na fedheha maishani .
 Mithali 6:33. Sikiliza katika ngono unaweza ukapata kilema cha maisha, na magonjwa ya hatari kama vile kaswende, ukimwi n.k. Haya magonjwa yatapelekea nyama na mwili wako kuangamia utashindwa kufikia malengo uliyojipagia, utabakia kujuta tu na watu watakufanyia fedheha na wakati huo upo kitandani hujiwezi.

(6) Kuwapa wengine miaka yako.
  Mithali 5:9 , Uchunguzi chunguzi unaonyesha kwa mtu anayependelea kufanya ngono mara kwa mara hasa anapoanza kabla ya ndoa mara nyingi hawezi kuishi kwa muda mrefu si hivyo tu lakini pia tumeona mara nyingi vijana wakijiua/wakiuana /wakifa kwa ajili ya mapenzi, wengine wanaugua hadi wanakufa wadogo na kupatwa na magonjwa mabaya, na hivyo muda waliostahili waishi hapa duniani na hivyo wanakuwa wamewapa wengine miaka yao.

(7) Kuvamiwa na maroho machafu.
 Katika kufanya ngono, wengine wanaenda hadi kwa waganga wa kienyeji na wachawi na huko wengine wanapewa madawa ya ajabu ambayo yanapelekea kuwamiwa na mapepo ya ajabu, na wengine kwa kupenda ngono wamefanya ngono na majini bila wao kujua na tayari yamesha wamiliki na hawaji watatokaje kwenye kifungo hicho.

Mimi nimekuonyesha hasara zile za kibiblia tu, sasa zipo za kijamii, kitaifa, kifamilia nk. Naamini baada ya kuwa umesoma ujumbe huu, kama bado unafanya ngono basi utabadili tabia yako na kuacha ngono mpaka wakati utakapo fika na kama haujaokoka nakusihi uokoke ili Yesu akupe nguvu za kushinda hiyo dhambi.

Bwana Mungu akulinde na kukutunza.

Tafuta
Vitengo
Soma Zaidi
SPIRITUAL EDUCATION
JEHANAMU YA MOTO IPO NA ITAFANYA KAZI SIKU YA HUKUMU KUU. MATHAYO 13:40-50
JEHANAMU YA MOTO IPO NA ITAFANYA KAZI SIKU YA HUKUMU KUU. MATHAYO 13:40-50
Kwa Martin Laizer 2024-01-22 10:52:31 0 6K
DANIEL
DANIELI 11
Mungu wetu MKUU YESU KRISTO, asifiwe. Karibu katika mwendelezo wa kitabu cha Danieli, kama...
Kwa GOSPEL PREACHER 2021-11-08 01:50:31 0 7K
LEVITICUS
Verse by verse explanation of Leviticus 4
Praise the Lord Jesus Christ, please study this chapter and then answer all 84 questions at the...
Kwa THE HOLY BIBLE 2022-01-24 08:55:38 0 5K
OTHERS
NANI ALIYE TOLEWA KAFARA, ISHMAEL AU ISAKA?
Kwenye Mwanzo 22:1-18, je inawezekana kuwa mvulana ambaye Abraham alikaribia kumtoa kafara awe ni...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 22:41:15 0 5K
HOLY BIBLE
Do you have to be baptized to be filled with the Holy Spirit?
No, you do not have to be baptized to be filled with the Holy Spirit. To prove this all we have...
Kwa MAX SHIMBA MINISTRIES 2021-12-24 05:39:59 0 5K